-
[Matayarisho:
Nani huamua ninachoona mtandaoni?]
-
Hujambo, jina langu ni Taylor.
-
Natafiti intaneti na uandishi wa habari,
-
na jinsi sisi kama raia tunapokea taarifa kuhusu dunia.
-
Katika siku za zamani wakati watu walipokea taarifa,
-
mara nyingi iliamuliwa na watu.
-
Kuna wanadamu ambao waliamua mambo ambayo tulihitaji kujua.
-
Kwa hivyo tulipofungua gazeti au kutazama habari za jioni,
-
ni mtu aliyeamua tulichosikia na kutazama.
-
Matokeo ya hayo ni kwambo sote tulifahamu mambo yanayofanana.
-
Sasa mtandao umebadilisha kila kitu.
-
Unapoingia mtandaoni, unapofungua programu,
-
unachoona hakibainishwi na mtu
-
lakini na mashine.
-
Na hili ni nzuri kwa njia nyingi:
-
Inakuruhusu utumie Ramani za Google;
-
Inakuruhusu uagize chakula mtandaoni;
-
Inakuruhusu uwasiliane na marafiki kote duniani
-
na kushiriki maelezo...
-
Lakini kuna vipengele vya mashine hii
-
ambavyo tunahitaji kufikiri kwa makini kuvihusu
-
kwa sababu vinabainisha maelezo ambayo sote tunayapokea
-
kama raia katika jamii na katika demokrasia.
-
Kwa hivyo unapofungua programu
-
na unaonyeshwa picha katika mipasho yako ya Snapchat,
-
maelezo hayo yote yamebainisha na mashine hii,
-
na mashine hiyo inaendeshwa na marupurupu ya kampuni
-
ambayo inamiliki tovuti au inamiliki programu.
-
Na marupurupu hayo ni kwa ajili yako kutumia mara nyingi uwezavyo
-
katika programu hiyo.
-
Kwa hivyo wanafanya mambo yanayokufanya uhisi vizuri kuhusu kuwa hapo.
-
Wanaruhusu watu kupenda picha zako.
-
Wanakuonyesha maudhui ambayo wanafikiri ungependa kuyaona
-
ambayo huenda yatakufanya ufurahie zaidi au ukasirike zaidi
-
ambayo yatasababisha msukumo wa hisia kutoka kwako ili usiondoke hapo.
-
Hii ni kwa sababu wanataka kukuonyesha matangazo mengi zaidi iwezekanavyo
-
ukiwa mahali pale
-
kwa kuwa huo ndio muundo wao wa biashara.
-
Pia wanachukua fursa hio hio ya wewe kutumia programu yao
-
kukusanya data kukuhusu.
-
Na wanatumia data hii
-
kubuni wasifu wa kina wa maisha na tabia yako,
-
na kisha wasifu hizi zinaweza kutumiwa
-
kukuonyesha matangazo zaidi,
-
na kisha hilo hubainisha unachoona pia.
-
Lakini haya yote hayahusu tu muundo wa biashara wa kampuni hizi,
-
ina athari kwa demokrasia yetu
-
kwa sababu tunachoona mtandaoni imebadilishwa kutufaa sisi,
-
tunachopenda
-
tunachoamini,
-
kwa tunachotaka kuona au kuamini.
-
Ni hiyo inamaanisha kuwa kama jamii,
-
sote hatupati maarifa au maelezo sawa
-
ambayo ni ngumu kwa demokrasia inayotuhitaji
-
tufanye kazi kwa pamoja na kufahamu mambo yanayofanana
-
ili kufanya uamuzi unaohusu maisha yetu pamoja.
-
Sote tunapojua mambo tofauti
-
na sote tunatengwa katika vifungu vyetu vidogo vya maelezo,
-
ni vigumu kwetu kuelewana.
-
Hatuna hali au maarifa yanayofanana.
-
Nafikiri ni muhimu zaidi tufikiri kwa umakini
-
kuhusu maelezo tunayopokea mtandaoni,
-
na kuhusu kampuni na miundo inayobainisha
-
tunachoona mtandoani.
-
[NewsWise ni mradi wa CIVIX& Shirika la Uandishi wa Habari la Kanada]
-
Manukuu yametolewa na Claudia Contreras
Ukaguzi umefanywa na Carol Wang