-
-
Nina piza nzima hapa, na tuchukulie
-
kwamba ninatakiwa niikate kwenye vipande viwili vilivyo sawa.
-
Naikata hapa vipande viwili vilivyo sawa.
-
Na tuseme nimekula moja ya vipande 2 sawa.
-
Tuchukulie nimekula sehemu hii hapa.
-
Je, ni sehemu gani ya piza niliyokula?
-
Nimechukua nzima na kuigawanya
-
vipande viwili vilivyo sawa, kisha nikala moja ya vipande hivyo.
-
-
Hivyo nilikula nusu ya piza.
-
Hebu tuchukulie kwamba, badala ya kukata piza kwenye
-
vipande 2 sawa, tuchukulie
-
kwamba tumeikata kwenye vipande 4 vilivyosawa.
-
Hebu tuchore.
-
Kwa hiyo vipande 4 vilivyo sawa.
-
Kwa hiyo nitakata mara moja namna hii na kisha,
-
nitakata mara moja kama hivi.
-
Hivyo nina vipande 4 vilivyo sawa.
-
-
Lakini ninataka kula kiasi kilekile cha piza.
-
Je, nitakula vipande vingapi kati ya hivi vipande 4 sawa?
-
Ninakushauri usimamishe video na kufikiria.
-
Nitakula kula kipande hiki.
-
Chukulia nitakula kipande hiki na kipande hiki
-
hapa.
-
Nimekula sehemu ileile ya piza.
-
Kila moja ya vipande hivi imekatwa katika sehemu mbili
-
nilipokata piza namna hii.
-
Hivyo natakiwa nile vipande 2 kati ya 4,
-
tofauti na kipande 1 kati ya 2.
-
Kwa hiyo nimekula vipande 2 kati ya 4
-
-
Natumia namba tofauti hapa.
-
Hapa natumia 1 kwenye kiasi
-
na 2 kwenye asili.
-
Hapa, natumia 2 kwenye kiasi
-
na 4 kwenye asili.
-
Hizi sehemu mbili zinawakilisha kitu kile kile.
-
Nimekula kiasi kilekile cha piza.
-
Kama nimekula 2/4 ya piza, kama nimekula vipande 2 kati ya 4,
-
hiyo ni sehemu ileile ya piza
-
kama nimekula kipande 1 kati ya 2.
-
Kwa hiyo tunaweza kusema hizi mbili
-
ni sehemu sawa.
-
Hebu tufanye mfano mwingine.
-
Badala ya kugawanya katika vipande 4 vilivyo sawa,
-
hebu nigawanye katika vipande 8 vilivyo sawa.
-
-
Kwa hiyo sasa tutakata mara moja kama hivi.
-
Sasa tuna vipande viwili vilivyo sawa.
-
Kata mara moja kama hivi.
-
Sasa tuna vipande vinne vilivyo sawa.
-
Halafu gawanya kila moja ya hivyo vipande 4 kuwa vipande 2.
-
Kwa hiyo kata--
-
Nataka kupata vipande sawa.
-
Hivyo havionekani sawa kama ninavyotaka
-
Hivyo vinaonekana sawa.
-
Hivyo nina vipande vingapi vilivyosawa?
-
Nina vipande 8 sawa.
-
-
Tuchukulie ninataka kula sehemu ileile ya piza.
-
Kwa hiyo nitakula vipande vyote hivi hapa.
-
Vipande vingapi kati ya hivyo vipande sawa 8 nimekula?
-
Nimekula 1, 2, 3, 4 ya vipande sawa 8.
-
Kwa mara nyingine, sehemu hii, 4 ya 8 au 4/8,
-
ni sawa 2/4, ambayo ni sawa na 1/2.
-
Na unaweza kuona mpangilio hapa.
-
Kutoka kwenye umbo hili kwenda kwenye umbo hili,
-
ninapata mara mbili ya vipande sawa.
-
Kwa sababu nina mara mbili ya vipande sawa
-
Ninatakiwa kula mara mbili ya idadi ya viapnde.
-
Kwa hiyo nazidisha asili kwa 2,
-
na nazidisha kiasi kwa mbili
-
Kama nikizidisha kiasi na asili
-
kawa namba ileile, sibadilishi
-
kinachowakiliswa na sehemu.
-
Na unaweza kuona hapa.
-
Kutoka vipande 4 kwenda vipande 8, nimekata kila kipande,
-
nimebadilisha kila kipande kuwa vipande viwili
-
kwa hiyo nina mara mbili ya vipande.
-
Na nikitaka kula kiasi kile kile,
-
ninatakiwa kula mara mbili ya vipande.
-
Kwa hiyo zote hizi 1/2, 2/4, 4/8 na ninaweza kuendelea.
-
Ninaweza kufanya 8/16.
-
Ninaweza kufanya 16/32.
-
Zote hizi zitakuwa sehemu sawa.
-