-
[Matayarisho:
Nani huamua ninachoona mtandaoni?]
-
Hujambo, jina langu ni Taylor.
-
Natafiti intaneti na uandishi wa habari,
-
na jinsi sisi kama raia tunapokea
taarifa kuhusu dunia.
-
Katika siku za zamani
wakati watu walipokea taarifa,
-
mara nyingi iliamuliwa na watu.
-
Kulikuwa na wanadamu walioamua
mambo ambayo tulihitaji kujua.
-
Kwa hivyo tulipofungua gazeti
au kutazama habari za jioni,
-
ni mtu aliyeamua
tulichosikia na kutazama.
-
Matokeo ya hayo ni
kwamba sote tulifahamu mambo yanayofanana.
-
Sasa mtandao umebadilisha kila kitu.
-
Unapoingia mtandaoni,
unapofungua programu,
-
unachoona hakibainishwi na mtu
-
lakini na mashine.
-
Na hili ni nzuri kwa njia nyingi:
-
Inakuruhusu utumie Ramani za Google;
-
Inakuruhusu uagize chakula mtandaoni;
-
Inakuruhusu uwasiliane
na marafiki kote duniani
-
na kushiriki maelezo...
-
Lakini kuna vipengele vya mashine hii
-
ambavyo tunahitaji
kufikiri kwa makini kuvihusu
-
kwa sababu vinabainisha
maelezo ambayo sote tunayapokea
-
kama raia katika jamii
na katika demokrasia.
-
Kwa hivyo unapofungua programu
-
na unaonyeshwa picha
katika mipasho yako ya Snapchat,
-
maelezo hayo yote
hubainishwa na mashine hii,
-
na mashine hiyo huendeshwa
na marupurupu ya kampuni
-
ambayo inamiliki tovuti
au inamiliki programu.
-
Na marupurupu hayo ni kwa ajili yako
kutumia muda mwingi iwezekanavyo
-
katika programu hiyo.
-
Kwa hivyo wanafanya mambo yanayokufanya
uhisi vizuri kuhusu kuwa hapo.
-
Wanawaruhusu watu kupenda picha zako.
-
Wanakuonyesha maudhui
ambayo wanafikiri ungependa kuyaona
-
yatakayokufanya
ufurahie zaidi au ukasirike zaidi
-
yatakayokufanya uwe na hisia
zitakazosababisha usiondoke hapo.
-
Hii ni kwa sababu wanataka
kukuonyesha matangazo mengi iwezekanavyo
-
ukiwa mahali pale
-
kwa kuwa huo ndio muundo wao wa biashara.
-
Pia wanachukua fursa hio hio
ya wewe kutumia programu yao
-
kukusanya data kukuhusu.
-
Na wanatumia data hii
-
kubuni wasifu wa kina
wa maisha na tabia yako,
-
na kisha wasifu hizi zinaweza kutumiwa
-
kukuonyesha matangazo zaidi,
-
na kisha hilo hubainisha unachoona pia.
-
Lakini haya yote hayahusu tu
muundo wa biashara wa kampuni hizi,
-
yana athari kwa demokrasia yetu
-
kwa sababu tunachoona mtandaoni
imebadilishwa kutufaa sisi,
-
tunachopenda
-
tunachoamini,
-
kwa tunachotaka kuona au kuamini.
-
Ni hiyo inamaanisha kuwa kama jamii,
-
sote hatupati maarifa au maelezo sawa
-
ambayo ni ngumu kwa demokrasia
inayotuhitaji
-
tushirikiane na kujua mambo yanayofanana
-
ili kufanya uamuzi
unaohusu maisha yetu pamoja.
-
Sote tunapojua mambo tofauti
-
na sote tunatengwa katika
vifungu vyetu vidogo vya maelezo,
-
ni vigumu zaidi kwetu kuelewana.
-
Hatuna hali au maarifa yanayofanana.
-
Nafikiri ni muhimu zaidi
tufikiri kwa umakini
-
kuhusu maelezo tunayopokea mtandaoni,
-
na kuhusu kampuni
na miundo inayobainisha
-
tunachoona mtandaoni.
-
[NewsWise ni mradi wa CIVIX&
Shirika la Uandishi wa Habari la Kanada]
-
Manukuu yametolewa na Claudia Contreras
Ukaguzi umefanywa na Carol Wang