-
Hebu tufanye baadhi ya maswali
-
kwenye mazoezi ya shule ya Khan ambayo yatatufanya
-
tuandike upya hesabu za kujumlisha ili
-
tuweze kufanya ziwe kwenye namba za kukaribisha.
-
Namba ambazo zinaweza kuwa vigawe vya 10 au vigawe vya 100
-
Ngoja tuone, nina 63 jumlisha 427,
-
na hii inaonekana kama ngumu, unajua,
-
nahisi kama natakiwa kuandika ili kueleweka,
-
lakini labda natakiwa kuchukua kutoka kwenye namba moja,
-
na kuipa namba nyingine ili zote
-
ziwe namba zilizokaribishwa, ni wazi
-
kwamba 63, nikitoa tatu nitapata 60,
-
na kama nitaipeleka hiyo tatu kwenye 427,
-
itakuwa 430, na 60 jumlisha 430
-
ni hesabu rahisi zaidi.
-
Hebu tuone swali linauliza nini.
-
Hebu tufuatilie hatua kwa hatua jinsi ya kulifanya.
-
Swali linauliza 63 jumlisha 427 ni sawa
-
na 60 jumlisha ngapi jumlisha 427.
-
Kwa hiyo 60 jumlisha ngapi, hii ni
-
sawa na 63, kwa sababu tuna
-
427 sehemu zote, kwa hiyo 63 ni 60 jumlisha tatu.
-
Hiyo inaleta maana.
-
Katika hatua inayofuata, wamebadilisha mpangilio
-
60 jumlisha tatu, na halafu ongeza 427
-
ni sawa na kufanya 60 jumlisha
-
na halafu ujumlishe tatu kwa 427 kwanza.
-
Kwa hiyo tunaichukua hii tatu
-
na kuihamisha kutoka kwa 63 kwenda kwa 427.
-
Tatu jumlisha 427, hiyo ni sawa na 430.
-
Na sasa hii hesabu ya kujumlisha imekuwa rahisi zaidi.
-
60 jumlisha 430, tunaweza kufanya kwenye vichwa vyetu.
-
Tanaongeza makumi sita kweye hii,
-
kwa hiyo itakuwa 490, na tumemaliza.
-
Hebu tufanye mifano zaidi ya hii.
-
Kwa hiyo, hapa, tunataka
-
kujumlisha hizi namba mbili,
-
na ngoja tuone kama
-
tunaweza kuzikaribisha.
-
Kwa hiyo hapa, tunazivunja
-
275 kwenye 270 na ziada.
-
Hii itakuwa 270 jumlisha tano.
-
Angalia namba nyingine bado iko vile vile,
-
jumlisha 297.
-
Sasa, kwa nini tunafanya hivyo?
-
Tukichukua 5 kutoka kwenye 275 na kuipeleka kwenye 595,
-
ambacho ndicho tunachokifanya hapa,
-
595 itakuwa 600.
-
Itafanya swali liwe rahisi
-
Kwa hiyo, kwa mara nyingine, hapa tunajumlisha
-
270 na tano kwanza, na halafu tunaongeza 595,
-
lakini tunaweza kubadilisha mpangilio wa tunavyofanya.
-
Tunaweza kujumlisha tano kwa 595 kwanza,
-
na halafu tujumlishe 270.
-
Hii ni sawa na 270 jumlisha,
-
tano jumlisha 595 ni 600, na sababu
-
kwa nini tumechukua tano kutoka kwenye 270 ni ili
-
tuweze kuijumlisha kwenye 595 na kupata 600,
-
na sasa tunaweza kufanya hili kwenye vichwa vyetu.
-
270 jumlisha mamia 6, tutakwenda kuongeza
-
mamia yetu kwa sita, kwa hiyo itakuwa 870.
-
Ngoja tufanye mifano zaidi hapa.
-
Jaza nafasi iliyoachwa wazi.
-
51 jumlisha 83 ni sawa na nafasi iliyoachwa wazi jumlisha 84.
-
Naam, wameongeza 83 kwa moja kupata 84,
-
kwa hiyo tunatakiwa kupunguza 51 kwa moja.
-
Hivyo, hii itakuwa sawa na 50 jumlisha 84.
-
Sasa kwa nini mnatakiwa kujali hili?
-
Kwa nini mjali?
-
Kwa sababu sasa ni rahisi kufanya,
-
kwa sababu sasa natakiwa niseme
-
makumi nane jumlisha mamoja manne, jumlisha, jumlisha makumi mengine matano
-
Hiyo itakuwa makumi 13 na mamoja manne, au 134.
-
Kwa hiyo, hii naiona hii rahisi zaidi,
-
lakini kitu cha muhimu ni kama tukiongeza moja kwenye namba
-
tunatakiwa tutoe kiasi hicho hicho kwenye namba nyingine.
-
ili kutokubadilisha thamani
-
ya hesabu hii ya kujumlisha, kwenye swali hili.
-
Hebu tufanye maswali zaidi.
-
138 jumlisha 710 ni sawa na sehemu iliyoachwa wazi jumlisha 700
-
Kwa hiyo tulikuw na 710, na sasa ni 700.
-
Kwa hiyo tumetoa kumi kutoka kwenye hiyo namba,
-
hivyo tunatakiwa tuipe namba nyingine.
-
Hivyo tunatakiwa kuongeza 10 kwenye 138,
-
kwa hiyo itakuwa 148.
-
Sasa, kwa nini hiyo ilikuwa muhimu?
-
Naam 148 jumlisha 700, unaweza kufanya hilo kichwani mwako.
-
Itakuwa 848, na hiyo ni rahisi kufanya
-
zaidi ya hichi tulichokuwa nacho hapa.