Hans Rosling aonyesha takwimu bora kuliko zote ulizoziona
-
0:00 - 0:04Takriban miaka 10 iliyopita, nilianza kazi ya kufundisha maendeleo ya ulimwengu
-
0:04 - 0:08kwa wanafunzi wa Kiswidishi wa shahada ya kwanza. Hii ilikuwa baada ya
-
0:08 - 0:12takriban miaka 20 ya kufanya kazi pamoja na taasisi mbalimbali za Afrika nikitafiti kuhusu njaa
-
0:12 - 0:16katika Afrika, kwa hiyo nilikuwa natarajiwa niwe najua zaidi kuhusu dunia.
-
0:16 - 0:21Na nilianzia kwenye chuo chetu cha utabibu, Taasisi ya Karolinska,
-
0:21 - 0:25kozi ya shahada ya kwanza iliyoitwa Afya ya Ulimwengu. Lakini ukipata
-
0:25 - 0:28fursa hiyo, unapata mshawasha kidogo. Nilifikiri wanafunzi hawa
-
0:28 - 0:31kuja kwetu ni lazima wana maksi za juu unazoweza kupata
-
0:31 - 0:34kwenye mfumo wa vyuo vya Sweden -- kwahiyo labda wanajua kila kitu
-
0:34 - 0:38kuhusu nitakachowafundisha. Kwa hiyo niliwapa mtihani mara tu walipokuja.
-
0:38 - 0:41Na moja wapo kati ya maswali ambayo nilijifunza mengi ni hili hapa:
-
0:41 - 0:45"Ni nchi gani kati ya hizi tano ina kiwango kikubwa cha vifo vya watoto kati ya jozi hizi tano?"
-
0:45 - 0:49Na niliziweka pamoja, ili katika kila kundi la nchi,
-
0:49 - 0:54moja ina kiwango kikubwa cha vifo vya watoto zaidi ya nyingine. Na hii inamaanisha kwamba
-
0:54 - 0:59kuna tofauti kubwa sana kuliko uhakika wa takwimu.
-
0:59 - 1:01Sitawapa mtihani hapa, lakini ni Uturuki,
-
1:01 - 1:06ambayo ina kiwango kikubwa pale, Poland, Urusi, Pakistani na Afrika Kusini.
-
1:06 - 1:09Na haya ndiyo majibu ya wanafunzi wa Kiswidishi. Nilifanya hivyo na nilipata
-
1:09 - 1:12kiwango cha imani, ambacho kilikuwa kidogo, na nilifurahi,
-
1:12 - 1:16kwa hakika: 1.8 ya jibu sahihi kati ya matano inawezekana. Hii ina maana kwamba
-
1:16 - 1:19kulikuwa kuna nafasi ya Profesa wa afya ya ulimwengu --
-
1:19 - 1:21(Kicheko) na kwa kozi yangu.
-
1:21 - 1:25Lakini usiku mmoja, wakati nilipokuwa natayarisha ripoti
-
1:25 - 1:29Niligundua uvumbuzi wangu. Nimeonyesha
-
1:29 - 1:34kuwa wanafunzi Waswidishi wenye alama za juu wanajua kidogo sana kuhusu takwimu
-
1:34 - 1:36za ulimwengu kuliko hata sokwe.
-
1:36 - 1:38(Kicheko)
-
1:38 - 1:42Kwasababu sokwe wangepata nusu iwapo ningewapa
-
1:42 - 1:45ndizi mbili zenye Sri Lanka na Uturuki. Wangekuwa sahihi kwa nusu yake.
-
1:45 - 1:49Lakini wanafunzi hawapo huko. Tatizo langu halikuwa kutokujua kwao:
-
1:49 - 1:52ilikuwa ni mawazo waliyojijengea.
-
1:52 - 1:56Pia nilifanya utafiti kinyume na maadili kwa maprofesa wa taasisi ya Karolinska
-
1:56 - 1:57(Kicheko)
-
1:57 - 1:59-- ambao wanatoa tuzo ya Nobel katika utabibu,
-
1:59 - 2:01na wao wako sawa tu na sokwe.
-
2:01 - 2:04(Kicheko)
-
2:04 - 2:08Hapa ndipo nilipogundua kwamba kuna haja ya kuwasiliana,
-
2:08 - 2:11kwasababu ya takwimu za kinachotokea duniani
-
2:11 - 2:14na afya ya mtoto katika kila nchi inajulikana.
-
2:14 - 2:19Tulitengeneza hii programu ya kompyuta ambayo inayoonyesha kama hivi: kila kiputo hapa ni nchi.
-
2:19 - 2:25Hii nchi hapa ni China. Hii ni India.
-
2:25 - 2:31Ukubwa wa kiputo ni idadi ya watu, na katika mhimili huu nimeweka kiwango cha uzazi.
-
2:31 - 2:34Kwasababu wanafunzi wangu, walichosema
-
2:34 - 2:36wakati walipoangalia dunia, na nilipowauliza,
-
2:36 - 2:38"Nini mnafikiri kuhusu dunia?"
-
2:38 - 2:42Naam, kwanza niligundua kuwa kitabu cha kiada kilikuwa Tintin, angalau.
-
2:42 - 2:43(Kicheko)
-
2:43 - 2:46Na walisema, "Dunia bado ni 'sisi' na 'wao.'
-
2:46 - 2:49Na sisi ni dunia ya Magharibi na wao ni Dunia ya Tatu."
-
2:49 - 2:52"Na una maana gani kwa kusema dunia ya magharibi?" Niliuliza.
-
2:52 - 2:57"Naam, haya ni maisha marefu na familia ndogo, na dunia ya tatu ni maisha mafupi na familia kubwa."
-
2:57 - 3:03Kwa hiyo hii ndio ninayoweza kuonyesha hapa. Niliweka kiwango cha uzazi hapa: idadi ya watoto kwa mwanamke,
-
3:03 - 3:07moja, mbili, tatu, nne, mpaka watoto nane kwa mwanamke mmoja.
-
3:07 - 3:13Tuna takwimu nzuri sana toka mwaka 1962 -- 1960 kuhusu -- ukubwa wa familia katika nchi zote.
-
3:13 - 3:16Kiwango cha makosa ni kidogo sana. Hapa naweka umri wa kuishi wakati wa kuzaliwa,
-
3:16 - 3:20kuanzia miaka 30 katika nchi nyingine mpaka karibu miaka 70.
-
3:20 - 3:23Na mwaka 1962 kulikuwa na kundi kubwa la nchi hapa,
-
3:23 - 3:28ambazo zilikuwa nchi zenye viwanda, na walikuwa na familia ndogo na maisha marefu.
-
3:28 - 3:30Na hizi zilikuwa nchi zinazoendelea:
-
3:30 - 3:33walikuwa na familia kubwa na walikuwa na maisha mafupi.
-
3:33 - 3:37Sasa nini kimetokea toka mwaka 1962? Tunataka kuona mabadiliko.
-
3:37 - 3:40Je wanafunzi wako sahihi? Bado ni aina mbili za nchi?
-
3:41 - 3:44Au hizi nchi zilizoendelea zina familia ndogo na wanaishi hapa?
-
3:44 - 3:46Au wana maisha marefu na wanaishi hapo juu?
-
3:46 - 3:49Hebu tuone. Tulisimamisha dunia wakati ule. Hizi zote ni takwimu za Umoja wa Mataifa
-
3:49 - 3:52ambazo zinapatikana. Hebu tuone. Unaweza kuona kule?
-
3:52 - 3:55Ni China kule, ikiendelea dhidi ya afya bora hapa, inaboreka kule.
-
3:55 - 3:58Nchi zote za kijani za Amerika ya Kusini zimeanza kuelekea kuwa na familia ndogo.
-
3:58 - 4:01Hizi za njano hapa ni nchi za Kiarabu,
-
4:01 - 4:05na wana familia kubwa, lakini wao -- hawana maisha marefu, lakini si familia kubwa.
-
4:05 - 4:08Waafrika ni kijani hapa chini. Bado wamebaki hapa.
-
4:08 - 4:11Hii ni India. Indonesia inaenda kwa kasi sana.
-
4:11 - 4:12(Kicheko)
-
4:12 - 4:15Na miaka ya 80 hapa, kuna Bangladesh bado iko miongoni mwa nchi za Afrika kule.
-
4:15 - 4:18Lakini sasa, Bangladesh -- ni miujiza iliyotokea miaka ya 80:
-
4:18 - 4:21Maimamu walianza kuhamasisha uzazi wa mpango.
-
4:21 - 4:26Walisogea juu kwenye ile kona. Na katika miaka ya 90, tulikuwa na janga la Ukimwi
-
4:26 - 4:29ambalo lilishusha umri wa kuishi wa nchi za Afrika
-
4:29 - 4:33na nyingine zote zilipanda kwenye ile kona,
-
4:33 - 4:37ambako tuna maisha marefu na familia ndogo, na tuna ulimwengu mpya kabisa.
-
4:37 - 4:50(Makofi)
-
4:50 - 4:55Ngoja nifananishe kati ya Marekani na Vietnam.
-
4:55 - 5:001964: Marekani ilikuwa na familia ndogo na maisha marefu;
-
5:00 - 5:04Vietnam ilikuwa na familia kubwa na maisha mafupi. Na hiki ndicho kilichotokea:
-
5:04 - 5:10takwimu wakati wa vita zilionyesha kuwa pamoja na vifo vyote,
-
5:10 - 5:13kulikuwa kuna mabadiliko katika umri wa kuishi. Mwisho wa mwaka,
-
5:13 - 5:16uzazi wa mpango ulianza Vietnam na waliamua kuwa na familia ndogo.
-
5:16 - 5:19Na Marekani pale juu wanakuwa na maisha marefu,
-
5:19 - 5:22wanabaki na ukubwa wa familia. Na miaka ya 80 sasa,
-
5:22 - 5:25waliacha mpango wa kikomunisti na wakaingia kwenye uchumi wa soko huria,
-
5:25 - 5:29na inaenda haraka hata zaidi ya maisha ya jamii. Na leo,
-
5:29 - 5:34Vietnam ina umri wa kuishi na ukubwa wa familia sawa
-
5:34 - 5:41hapa Vietnam, 2003, kama ilivyokuwa Marekani, 1974, mwishoni mwa vita.
-
5:41 - 5:45Nafikiri sote -- kama hatutaangalia vielelezo --
-
5:45 - 5:49tutapuuza mabadiliko makubwa huko Asia, ambayo yalikuwa
-
5:49 - 5:53mabadiliko ya kijamii kabla hatujaona mabadiliko ya kiuchumi.
-
5:53 - 5:58Hebu tuendelee kwingine hapa ambako tunaweza kuonyesha
-
5:58 - 6:05mgawanyo wa kipato duniani. Hii ni mgao wa kipato cha watu.
-
6:05 - 6:10Dola moja, dola 10 au dola 100 kwa siku.
-
6:10 - 6:14Hakuna pengo tena kati ya matajiri na maskini. Hii ni hali ya kufikirika
-
6:14 - 6:18Kuna kituta kidogo hapa. Lakini kuna watu kila sehemu.
-
6:19 - 6:23Na tukiangalia kipato kinapoishia -- kipato hicho --
-
6:23 - 6:29hii ni asilimia 100 ya kipato cha dunia kwa mwaka. Na asilimia 20 ya matajiri wakubwa kabisa,
-
6:29 - 6:36wanachukua karibu asilimia 74. Na asilimia 20 ya masikini zaidi,
-
6:36 - 6:41wanachukua karibu asilimia mbili. Na hii inaonyesha kwamba dhana
-
6:41 - 6:45ya nchi zinazoendelea ni ya mashaka. Tunafikiria kuhusu misaada, kama
-
6:45 - 6:50watu hawa wanatoa misaada kwa watu wale pale. Lakini katikati,
-
6:50 - 6:54tuna idadi kubwa ya watu duniani, wenye asilimia 24 ya kipato.
-
6:54 - 6:58Tuliyasikia haya kwa namna nyingine. Na hawa ni akina nani?
-
6:58 - 7:02Nchi mbalimbali ziko wapi? Naweza kukuonyesha Afrika.
-
7:02 - 7:07Hii ni Afrika. Asilimia 10 ya idadi ya watu duniani, wengi wao wako kwenye umaskini.
-
7:07 - 7:12Hii ni OECD. Nchi tajiri. Nchi za kundi la Umoja wa Mataifa.
-
7:12 - 7:17Na wapo huku upande huu. Kuna mwingiliano kati ya Afrika na OECD
-
7:17 - 7:20Hii hapa ni Amerika Kusini. Ni kila kitu katika dunia hii,
-
7:20 - 7:23kuanzia maskini zaidi mpaka matajiri, huko Amerika Kusini.
-
7:23 - 7:28Zaidi ya hayo, tunaweza kuiweka Ulaya Mashariki, Asia Mashariki,
-
7:28 - 7:33na Asia Kusini. Na ingekuwaje iwapo tungerejea nyuma,
-
7:33 - 7:38mpaka mwaka 1970? Wakati huo kulikuwa na nundu kubwa zaidi.
-
7:38 - 7:42Na waliokuwa kwenye umaskini mkubwa zaidi ni Waasia.
-
7:42 - 7:49Tatizo la dunia lilikuwa umaskini huko Asia. Na sasa kama nitaicha dunia isogee mbele,
-
7:49 - 7:52utaona kwamba wakati idadi ya watu inaongezeka, kuna
-
7:52 - 7:55mamia ya milioni huko Asia wanajikwamua kutoka umaskini na wengine
-
7:55 - 7:58wanaingia katika umaskini, na hii ndiyo hali tuliyonayo leo hii.
-
7:58 - 8:02Na makadirio mazuri kutoka Benki ya Dunia, ni kwamba haya yatatokea,
-
8:02 - 8:06na hatutakuwa na dunia iliyogawanyika. Tutakuwa na watu wengi katikati.
-
8:06 - 8:08Naam, hiki ni kipimo cha logarithm,
-
8:08 - 8:13lakini dhana yetu ya uchumi ni kukua kwa asilimia. Tunaiangalia
-
8:13 - 8:19kama ni uwezekano wa kuongezeka kwa asilimia. Kama nitabadili hii, na kuchukua
-
8:19 - 8:23GDP kwa taifa badala ya kipato cha familia, na ninabadili hivi
-
8:23 - 8:29takwimu moja moja kwenye takwimu za kanda za GDP,
-
8:29 - 8:33na ninazileta kanda hapa chini, ukubwa wa kiputo bado ni idadi ya watu.
-
8:33 - 8:36Na una OECD pale, na una Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara hapo,
-
8:36 - 8:39na tunatoa nchi za Kiarabu pale,
-
8:39 - 8:43zinatoka Afrika na Asia, na tunaziweka tofauti,
-
8:43 - 8:48na tunaweza kuukuza muhimili huu, na ninaipa vipimo vipya hapa,
-
8:48 - 8:51kwa kuongeza thamani ya ustawi wa jamii pale, uwezekano wa kusalimika mtoto.
-
8:51 - 8:56Sasa nimeweka pesa pale kwenye mhimili, na nina uwezekano wa watoto kusalimika pale.
-
8:56 - 9:00Katika baadhi ya nchi, asilimia 99.7 ya watoto wanaishi mpaka miaka mitano;
-
9:00 - 9:04wengine, mika 70 tu. Na hapa inaonekana kuna pengo
-
9:04 - 9:08kati ya OECD, Amerika Kusini, Ulaya Mashariki, Asia Mashariki,
-
9:08 - 9:12Nchi za kiarabu, Asia Kusini na Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara.
-
9:12 - 9:17Uwiano baina ya maisha ya watoto na pesa ni wa karibu sana.
-
9:17 - 9:25Lakini hebu niigawanye Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara. Afya iko hapa na afya bora iko kule.
-
9:25 - 9:30Ninaweza kwenda hapa na kuigawa Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara katika nchi tofauti.
-
9:30 - 9:35Na ikipasuka, ukubwa wa puto la nchi ni sawa na idadi ya watu.
-
9:35 - 9:39Hapa chini ni Siera Leone. Mauritus iko pale juu. Mauritius ilikuwa nchi ya kwanza
-
9:39 - 9:42kuondokana na vikwazo vya biashara, na waliweza kuuza sukari yao.
-
9:43 - 9:48Waliweza kuuza nguo kwa taratibu sawa na watu wa Ulaya na Amerika Kaskazini.
-
9:48 - 9:52Kuna tofauti kubwa sana ndani ya Afrika. Na Ghana iko hapa katikati.
-
9:52 - 9:55Huko Siera Leone, misaada ya kibinadamu.
-
9:55 - 10:00Hapa Uganda, misaada ya maendeleo. Hapa, muda wa kuwekeza, kule,
-
10:00 - 10:03unaweza kwenda kwa mapumziko. Ni tofauti kubwa sana
-
10:03 - 10:08katika Afrika ambayo mara nyingi tunaitambua -- kuwa iko sawa kwa kila kitu.
-
10:08 - 10:12Naweza kuigawa Asia Kusini hapa. India ni kiputo kikubwa cha katikati.
-
10:12 - 10:16Lakini kuna tofauti kubwa kati ya Afghanistani na Sri Lanka.
-
10:16 - 10:20Naweza kugawa nchi za Kiarabu. Wakoje? Hali ya hewa sawa, utamaduni sawa,
-
10:20 - 10:24dini sawa. Tofauti kubwa. Hata kati ya majirani.
-
10:24 - 10:29Yemen, vita vya wao kwa wao. Umoja wa Falme za Kiarabu, pesa ya kutosha ni sawa na ikatumiwa vizuri.
-
10:29 - 10:36Sio kama tunavyofikiria. Na hii inajumuisha watoto wa raia wa kigeni ambao wapo nchini.
-
10:36 - 10:40Takwimu ni bora zaidi ya unavyofikiria. Watu wengi wanasema takwimu ni mbaya.
-
10:41 - 10:43Kuna nafasi ya mashaka, lakini tunaweza kuona tofauti hapa:
-
10:43 - 10:46Cambodia, Singapore. Tofauti ni kubwa
-
10:46 - 10:49zaidi ya udhaifu wa takwimu. Ulaya Mashariki:
-
10:49 - 10:55Uchumi wa Kisovieti muda mrefu, lakini waliweza kujikwamua baada ya miaka kumi
-
10:55 - 10:58kwa utofauti sana. Na kuna Amerika Kusini.
-
10:58 - 11:02Leo, hatuna haja ya kwenda Cuba kutafuta nchi yenye afya bora Amerika Kusini.
-
11:02 - 11:07Chile itakuwa na idadi ndogo ya vifo vya watoto zaidi ya Cuba miaka michache ijayo kuanzia sasa.
-
11:07 - 11:10Na hapa tuna nchi zenye kipato kikubwa katika OECD.
-
11:10 - 11:14Na hapa tunapata mwelekeo wote wa ulimwengu,
-
11:14 - 11:19ambao ni karibu ni sawa na hali hii. Na tukiiangalia,
-
11:19 - 11:25inavyoonekana -- dunia, mwaka 1960, inaanza kusogea. 1960.
-
11:25 - 11:28Huyu ni Mao Tse-tung. Alileta afya China. Halafu akafariki.
-
11:28 - 11:33Halafu akaja Deng Xiaoping na akaleta pesa kwa China, na kuwapandisha chati tena.
-
11:33 - 11:37Na tumeona jinsi nchi zinavyosogea katika mwenendo tofauti kama hivi,
-
11:37 - 11:41kwa hiyo inakuwa vigumu kupata
-
11:41 - 11:46mfano wa nchi ambayo inaonyesha mwelekeo wa ulimwengu.
-
11:46 - 11:52Ningependa kuwarudisha nyuma mpaka karibu na mwaka 1960.
-
11:52 - 12:02Ningependa kulinganisha Korea Kusini ambayo ni hii hapa, na Brazil,
-
12:02 - 12:07ambayo ni hii hapa. Kibandiko kimetoka hapa. Na ningependa kufananisha Uganda,
-
12:07 - 12:12ambayo iko kule. Na ninaweza kuileta mbele, kama hivi.
-
12:12 - 12:21Na unaweza kuona jinsi Korea Kusini wanavyosonga mbele kwa kasi sana,
-
12:21 - 12:24wakati Brazil inakwenda polepole.
-
12:24 - 12:30Na kama tukirudi nyuma tena, hapa, na tukiweka alama juu yao, kama hivi,
-
12:30 - 12:34unaweza kuona tena kuwa kasi ya maendeleo
-
12:34 - 12:40ni tofauti sana, na nchi zinasogea sana au kidogo
-
12:40 - 12:44katika kiwango sawa na kukua kwa pesa na afya, lakini inaonekana unaweza kusogea
-
12:44 - 12:48haraka sana iwapo una afya kwanza kuliko ukiwa na pesa kwanza.
-
12:49 - 12:53na kuonyesha hii, unaweza kuweka Umoja wa Falme za Kiarabu.
-
12:53 - 12:56Walitokea hapa, nchi ya madini. Walivuna mafuta yote,
-
12:56 - 13:00walipata pesa zote, lakini afya haiwezi kununuliwa dukani.
-
13:00 - 13:04Inabidi uwekeze kwenye afya. Inabidi uwapeleke watoto shule.
-
13:04 - 13:07Inabidi kuwafunza wafanyakazi wa afya. Inabidi kuwaelimisha watu.
-
13:07 - 13:10Na Sheikh Sayed alifanya hivyo kwa namna nzuri.
-
13:10 - 13:14Pamoja na kuanguka kwa bei ya mafuta, aliipandisha nchi yake hapa juu.
-
13:14 - 13:18Kwa hiyo tumepata muelekeo wa ulimwengu,
-
13:18 - 13:20ambapo nchi zote zinatabia ya kutumia pesa zao
-
13:20 - 13:25vizuri zaidi ya walivyokuwa wakitumia huko nyuma. Naam, hivi ndivyo, zaidi au pungufu kidogo,
-
13:25 - 13:32ukiangalia wastani wa takwimu za nchi. Ziko kama hivi.
-
13:32 - 13:37Sasa hii ni hatari, kutumia wastani wa takwimu, kwasababu kuna
-
13:37 - 13:43tofauti kubwa kati ya nchi. Kwa hiyo nikienda kuangalia hapa, tunaona
-
13:43 - 13:49kuwa Uganda ya leo ni mahali ambapo Korea ya Kusnini ilikuwa mwaka 1960. Na kama nikiigawa Uganda,
-
13:49 - 13:54kuna tofauti ndani ya Uganda. Hii ni moja ya tano ya takwimu ndani ya Uganda.
-
13:54 - 13:57Asilimia 20 ya matajiri zaidi wa Uganda wako pale.
-
13:57 - 14:01Masikini zaidi wako hapa chini. Iwapo nikiigawa Afrika Kusini, iko kama hivi.
-
14:01 - 14:06Na iwapo nikiangalia Niger, ambako kulikuwa na ukame mbaya sana,
-
14:06 - 14:11mwishoni, iko kama hivi. Asilimia 20 ya masikini zaidi huko Niger wako hapa,
-
14:11 - 14:14na asilimia 20 ya matajiri zaidi wa Afrika Kusini wako kule,
-
14:14 - 14:19na bado tunatabia ya kuzungumzia kuhusu utatuzi upi unafaa kwa matatizo ya Afrika.
-
14:19 - 14:22Kila kitu kilichopo hapa duniani kinapatikana Afrika. Na hamuwezi
-
14:22 - 14:26kuongelea upatikanaji wa dawa za VVU [madawa] kwa moja ya tano hapa juu
-
14:26 - 14:30kwa mkakati sawa kama hapa chini. Maendeleo ya ulimwengu
-
14:30 - 14:35ni lazima yawekwe kwa makundi tofauti, na si lazima kuwa nayo
-
14:35 - 14:38katika ngazi ya kanda. Ni lazima tuingie ndani zaidi.
-
14:38 - 14:42Tumetambua kuwa wanafunzi wanapatwa na mshawasha wakiweza kutumia hii.
-
14:42 - 14:47Na wapanga sera na sekta binafsi zingependa kuona
-
14:47 - 14:51namna gani dunia inabadilika. Sasa, kwanini hii haitokei?
-
14:51 - 14:55Kwanini hatutumii takwimu tulizonazo? Tuna takwimu katika Umoja wa Mataifa,
-
14:55 - 14:57na katika taasisi za takwimu za nchi
-
14:57 - 15:01na katika vyuo vikuu na mashirika yasiyo ya kiserikali.
-
15:01 - 15:03Kwasababu takwimu zimefichwa kwenye masijala.
-
15:03 - 15:08Na umma uko pale, na mtandao wa Intaneti uko, lakini bado hatujautumia ipasavyo.
-
15:08 - 15:11Taarifa zote tunazoziona zikibadilika duniani
-
15:11 - 15:15hazihusishi takwimu zinazogharimiwa na umma. Kuna baadhi ya kurasa za tovuti
-
15:15 - 15:21mfano hii, kama ujuavyo, lakini zinachukua kutoka kwenye masijala ya takwimu,
-
15:21 - 15:26lakini watu wanaziwekea bei, funguo za siri na takwimu za kuchosha.
-
15:26 - 15:29(Kicheko). (Makofi).
-
15:29 - 15:33Na hii haitatusaidia. Sasa nini kinatakiwa? Tuna masijala za takwimu.
-
15:33 - 15:37Si masijala mpya ya takwimu unayoihitaji. Tuna vifaa vizuri vya ubunifu,
-
15:37 - 15:40na vingi vinaongezewa hapa. Kwa hiyo tulianzisha
-
15:40 - 15:45shirika lisilo la kibiashara ambalo tukaliita -- kuunganisha takwimu kwa ubunifu --
-
15:45 - 15:48tunaiita Gapminder, kutoka London chini ya ardhi, ambako wanakuonya,
-
15:48 - 15:51"angalia upenyo" Kwa hiyo tulifikiri Gapminder ilikuwa ni sahihi.
-
15:51 - 15:55Na tulianza kuandika programu ya kompyuta ambayo ingeweza kuunganisha takwimu kama hivi.
-
15:55 - 16:01Na haikuwa vigumu sana. Iliwachukua watu wengine miaka kadhaa, na tumetengeneza vielelezo.
-
16:01 - 16:03Unaweza kuchukua seti ya takwimu na kuiweka hapa.
-
16:03 - 16:08Tunakomboa takwimu za Umoja wa Mataifa, mashirika machache ya Umoja wa Mataifa.
-
16:08 - 16:12Nchi nyingine zinakubali takwimu zao ziwe wazi duniani,
-
16:12 - 16:15lakini tunachohitaji zaidi ni, kwa hakika, namna ya kuzichambua.
-
16:15 - 16:20Programu ya kutafuta ambayo itakuwezesha kunakili takwimu katika muundo wa kutafutika
-
16:20 - 16:23na kuiweka wazi duniani. Na nini tunasikia tuzungukapo?
-
16:23 - 16:27Nimefanya anthopolojia katika sehemu kubwa za takwimu. Kila mtu anasema,
-
16:28 - 16:32"Haiwezekani. Hii haiwezi kufanyika. Taarifa zetu ni za ovyoovyo
-
16:32 - 16:35kwa ndani, na kwahiyo haziwezi kupangiliwa zitafutike kama nyingine zinavyoweza kutafutwa.
-
16:35 - 16:40Hatuwezi kutoa takwimu bure kwa wanafunzi, bure kwa wajasiliamali wa dunia."
-
16:40 - 16:43Lakini hivi ndivyo tungependa tuone, au sio?
-
16:43 - 16:46Takwimu zilizogharimiwa na umma zipo hapa chini.
-
16:46 - 16:49Na tungependa maua yaote nje kwenye mtandao.
-
16:49 - 16:54Na jambo la muhimu zaidi ni kuzipangilia ili ziweze kutafutika, na watu waweze kuzitumia
-
16:54 - 16:56vifaa tofauti vya ubunifu kueleleza pale.
-
16:56 - 17:01Nina habari nzuri kwenu. Nina habari nzuri kwamba,
-
17:01 - 17:05Mkuu wa Kitengo cha Takwimu cha Umoja wa Mataifa, hasemi haiwezekani.
-
17:05 - 17:07Anasema, "Hatuwezi kufanya."
-
17:07 - 17:11(Kicheko)
-
17:11 - 17:13Huyu ni mtu mwenye akili, eeeh?
-
17:13 - 17:15(Kicheko)
-
17:15 - 17:19Kwa hiyo tunaona mambo mengi yakitokea kwenye takwimu katika miaka ijayo.
-
17:19 - 17:23Tutaweza kuangalia mgawanyo wa kipato katika namna mpya kabisa.
-
17:23 - 17:28Huu ni mgao wa kipato huko China, 1970,
-
17:29 - 17:34mgao wa kipato wa Marekani, 1970.
-
17:34 - 17:38Karibu hakuna mwingiliano, karibu hakuna mwingiliano. Na nini kimetokea?
-
17:38 - 17:43Kilichotokea ni hiki: China inakua, haiko sawa tena,
-
17:43 - 17:47na inatokea hapa, ikiingalia Marekani.
-
17:47 - 17:49Kama vile mzuka, au sio, eeeh?
-
17:49 - 17:51(Kicheko)
-
17:51 - 18:01Inatisha. Lakini nadhani ni muhimu sana kuwa na taarifa hizi.
-
18:01 - 18:07Tunahitaji sana kuziona. Badala ya kuangalia hii,
-
18:07 - 18:12ningependa kumalizia kwa kuwaonyesha watumiaji wa mtandao kwa kila 1,000.
-
18:12 - 18:17Katika programu hii ya kompyuta, tunaweza kupata karibu alama 500 kutoka katika nchi zote kwa urahisi.
-
18:17 - 18:21Inachukua muda kubadilika kwa hii,
-
18:21 - 18:26lakini katika mihimili, unaweza kupata alama yeyote utakayopenda kupata.
-
18:26 - 18:31Na kitu kizuri itakuwa ni kuziweka masijala za takwimu bure,
-
18:31 - 18:34kuweza kuzifanya ziweze kutafutika, na kuzipata kwa kubonyeza kwa nukta moja
-
18:34 - 18:39kwenye mfumo wa michoro majira ya nukta, ambapo utazielewa kwa urahisi.
-
18:39 - 18:42Naam, wanatakwimu hawazipendi, kwasababu wanasema kuwa hii
-
18:42 - 18:51haitaonyesha hali halisi; inabidi tuwe na mbinu za kuchambua takwimu.
-
18:51 - 18:54Lakini hii inajenga nadharia.
-
18:54 - 18:58Ninamalizia sasa na dunia. Pale, mtandao wa intaneti unakuja.
-
18:58 - 19:02Idadi ya wanaotumia mtandao inaongezeka kama hivi. Hii ni GDP per capita
-
19:02 - 19:07Na ni teknolojia mpya inayokuja, lakini cha kushangaza, ni namna ambavyo
-
19:07 - 19:12inashabihiana na hali ya uchumi wa nchi. Ndio maana
-
19:12 - 19:15kompyuta ya dola 100 itakuwa ya muhimu sana. Lakini ni muelekeo mzuri.
-
19:15 - 19:18Ni kama vile dunia inakuwa bapa. Au sio? Nchi hizi
-
19:18 - 19:21zinanyanyuka zaidi ya uchumi na itakuwa ni ya kufurahisha
-
19:21 - 19:25kufuatilia hii kwa miaka ijayo, na kama ambavyo ningependa muweze kufanya
-
19:25 - 19:27kwa kutumia takwimu zilizogharamiwa na umma. Asanteni sana.
-
19:28 - 19:31(Makofi)
- Title:
- Hans Rosling aonyesha takwimu bora kuliko zote ulizoziona
- Speaker:
- Hans Rosling
- Description:
-
Hujapata kuona takwimu zikielelezwa namna hii. Kwa ufundi na umahiri wa kuhadhiri, gwiji wa takwimu Hans Rosling anachambua mtazamo potofu uitwao "nchi zinazoendelea."
- Video Language:
- English
- Team:
closed TED
- Project:
- TEDTalks
- Duration:
- 19:33