< Return to Video

Why all the letters in Algebra?

  • 0:00 - 0:04
    Nipo hapa na Jesse ambae ni Mwalimu wa hesabu
  • 0:04 - 0:05
    kwenye chuo cha Khan
  • 0:05 - 0:08
    na una maswali mazuri au mawazo.
  • 0:08 - 0:12
    Swali ambalo wanafunzi wamekuwa wanauliza wanapojifunza algebra
  • 0:12 - 0:16
    ni kwa nini tunatumia herufi, kwa nini tuisitumie namba kwenye kila kitu?
  • 0:16 - 0:18
    Kwa nini tunatumia herufi?kwa nini tuna hizi
  • 0:18 - 0:22
    X, Y na Z na ABC tunapoanza kufanya algebra?
  • 0:22 - 0:23
    sawa.
  • 0:23 - 0:28
    Inafurahisha, tunawaacha mtafakari kwa mda kidogo.
  • 0:28 - 0:30
    Hivyo Sal, utajibuje hili swali?
  • 0:30 - 0:32
    Kwa nini tunahitaji herufi kwenye Algebra?
  • 0:32 - 0:36
    Kuna sababu naweza kuzieleza.
  • 0:36 - 0:38
    Moja ni ukiwa huna kitu.
  • 0:38 - 0:44
    Hivyo kama nikiandika X jumlisha tatu in sawa na kumi.
  • 0:44 - 0:47
    tunafanya hivi kwa sababu hatujui X ni nini
  • 0:47 - 0:48
    ni kitu kisichojulikana.
  • 0:48 - 0:50
    Hivyo tunaanza kuitafuta kwa njia tofauti.
  • 0:50 - 0:52
    Ila haitakiwi kuwa X.
  • 0:52 - 0:56
    Tunaweza kuweka nafasi wazi jumlisha tatu ni sawa na kumi.
  • 0:56 - 1:00
    Au tunaweza kuweka alama ya ulizo jumlisha tatu ni sawa na kumi.
  • 1:00 - 1:03
    Hivyo sio lazima iwe herufi, ila kinachohitajika ni alama tu.
  • 1:03 - 1:07
    Inaweza kuwekwa hata uso jumlisha tatu ni sawa na kumi.
  • 1:07 - 1:12
    Ila mpaka ufahamu, unahitaji alama kuwakilisha hiyo namba tusiyoijua.
  • 1:12 - 1:16
    Sasa tunafanya hili swali na kisha tujue hiyo alama inawakilisha nini.
  • 1:16 - 1:18
    Kama tulijua kabla ya muda, isingekuwa ni kitu tusichokifahamu.
  • 1:18 - 1:20
    Isingekuwa ni kitu tusichokifahamu.
  • 1:20 - 1:24
    Hivyo hiyo ni moja ya sababu ya kutumia herufi
  • 1:24 - 1:26
    na sehemu ambayo namba zenyewe haziwezi kusaidia.
  • 1:26 - 1:29
    Nyingine ni wakati unatazama mahusiano ya namba.
  • 1:29 - 1:32
    Hivyo nitafanya kitu kama- ninaweza kusema
  • 1:32 - 1:38
    ukinipa tatu, nitakupa nne.
  • 1:38 - 1:44
    Na naweza kusema, kama ukinipa tano, nitakupa sita.
  • 1:44 - 1:46
    Ninaweza kuendelea mpaka mwisho.
  • 1:46 - 1:52
    Ukinipa 7.1, nitakupa 8.1.
  • 1:52 - 1:54
    Ninaweza kuendelea kuainisha mpaka mwisho.
  • 1:54 - 1:57
    Unaweza kunipa namba yeyote na nitakuambia nitakupa ngapi.
  • 1:57 - 2:01
    Ila nitaishiwa na sehemu na muda kama nikiziorodhesha zote.
  • 2:01 - 2:06
    Tutafanya vizuri kama tutatumia herufi kutambua namba.
  • 2:06 - 2:11
    Pengine ulichonipa tunakiita X na ninachokupa tunakiita Y.
  • 2:11 - 2:15
    Ninaweza kuisema chochote unachonipa nitajumlisha na moja.
  • 2:15 - 2:17
    Na ndicho nitakacho kurudishia.
  • 2:17 - 2:21
    Sasa, huu ni mlinganyo mrahisi hapa
  • 2:21 - 2:25
    unaweza kugundua namba inayowakilisha mahusiano baina ya X
  • 2:25 - 2:28
    na Y.
  • 2:28 - 2:31
    Sasa inajulikana X yeyote utakayonipa
  • 2:31 - 2:35
    umenipa tatu, nina jumlisha moja na nitakupa nne.
  • 2:35 - 2:38
    Ukinipa 7.1, nitajumlisha moja na nitakupa 8.1.
  • 2:38 - 2:41
    Hakuna njia ya kuwakilisha zaidi ya kutumia alama.
  • 2:41 - 2:44
    Kwahiyo, sihitaji kutumia X na Y.
  • 2:44 - 2:47
    Hizi zimezoeleka kutumika tangu zamani
  • 2:47 - 2:50
    Ninaweza kusema ulichonipa ni nyota
  • 2:50 - 2:55
    na nilichokupa ni sura
  • 2:55 - 2:58
    na hii pia inaweza kuwa njia sahihi ya kuwakilisha.
  • 2:58 - 3:02
    Hivyo herufi ni alama tu,
    Hakuna cha ziada.
Title:
Why all the letters in Algebra?
Description:

more » « less
Video Language:
English
Team:
Khan Academy
Duration:
03:04

Swahili subtitles

Revisions