< Return to Video

Who is allowed to go to school?

  • 0:00 - 0:03
    Wanafunzi, karibuni kwenye ziara ya
    UNESCO kuhusu 'haki ya elimu'.
  • 0:03 - 0:05
    "Subiri!" huenda mnafikiri.
  • 0:05 - 0:08
    "Haki ya elimu? Hilo linamaanisha nini?"
  • 0:08 - 0:12
    Sote tulio katika chumba hiki, elimu
    ni kama jambo lingine tu la maisha.
  • 0:12 - 0:14
    Jambo rahisi, la kila siku.
  • 0:14 - 0:16
    ♪ (muziki) ♪
  • 0:16 - 0:19
    Hata hivyo, elimu haipatikani kila wakati
  • 0:19 - 0:20
    na hili si jambo tu la zamani.
  • 0:20 - 0:22
    Katika sehemu nyingi duniani,
  • 0:22 - 0:26
    mamilioni ya watu,
    hasa wasichana na wanawake,
  • 0:26 - 0:28
    hawajawahi kuingia darasani.
  • 0:28 - 0:30
    Fikiri tu kuhusu wanawake maishani mwako.
  • 0:30 - 0:34
    Fikiri akina mama,
    dada zako, walimu, wanarika
  • 0:34 - 0:38
    wakishindwa kupata elimu
    kwa sababu tu ni wanawake.
  • 0:38 - 0:40
    ♪ (muziki) ♪
  • 0:40 - 0:42
    Tangazo la Jumla la Haki za Kibinadamu
  • 0:42 - 0:47
    na UNESCO zinafafanua elimu kama
    haki ya msingi ya kila mwanaume, mwanamke
  • 0:47 - 0:50
    na mtoto. Kwa hivyo tunaposema kila mtu
  • 0:50 - 0:54
    ana haki ya kupata elimu
    hatutaji tu ukweli wa kawaida,
  • 0:54 - 0:57
    kauli hii ni ya majivuno kutokana na
    juhudi zilizofanywa miaka iliyopita
  • 0:57 - 1:00
    ili kuhakikisha kuwa elimu
    inakuwa haki ya msingi ya binadamu
  • 1:00 - 1:03
    ili kuruhusu mtu yeyote na kila mtu
  • 1:03 - 1:04
    duniani kupata elimu.
  • 1:06 - 1:09
    Kuna sababu mbili kuu za umuhimu wa
    haki ya kupata elimu.
  • 1:09 - 1:14
    Ya kwanza: elimu ni jambo moja
    ambalo linainua hadhi yako ya
  • 1:14 - 1:16
    jamii na uchumi.
  • 1:16 - 1:19
    Haijalishi iwapo
    ulizaliwa maskini au tajiri
  • 1:19 - 1:21
    kupata elimu kunaweza kukusaidia kufikia
  • 1:21 - 1:22
    malengo yako kamili.
  • 1:24 - 1:27
    Ya pili: kwa kutambua kuwa ni haki
  • 1:27 - 1:31
    elimu inakuwa jambo
    tunaloweza kutetea na kuhakikisha.
  • 1:31 - 1:36
    Hii inamaanisha mashirika kama vile UNESCO
    yanaweza kuweka viwango vya kimataifa
  • 1:36 - 1:39
    vya elimu na kufanya nchi
    ziwajibikie kuhakikisha
  • 1:39 - 1:42
    kuwa haki ya elimu inatolewa kisheria.
  • 1:44 - 1:48
    Dunia ni mahali pakubwa
    penye watu bilioni 7.6,
  • 1:48 - 1:50
    UNESCO huhakikisha vipi haki ya
  • 1:50 - 1:55
    elimu kwa watu bilioni 7.6 kwenye
    kipimo cha ulimwengu?
  • 1:55 - 1:57
    Kwanza, tunafanya mikutano
    ambako viongozi wanaweza kuja
  • 1:57 - 1:59
    pamoja ili kubuni makubaliano
  • 1:59 - 2:02
    kama vile makubaliano dhidi ya
    ubaguzi katika elimu.
  • 2:02 - 2:04
    Desturi na viwango ili kuhakikisha
  • 2:04 - 2:09
    fursa sawa katika elimu,
    kutetea haki za walimu, n.k...
  • 2:09 - 2:13
    Mikutano hii ni muhimu
    ili nchi zote zikubali na kusema
  • 2:13 - 2:16
    hivi ndivyo elimu inafaa kuwa kwa wanadamu
  • 2:16 - 2:19
    bila kujali wanakotoka.
  • 2:20 - 2:22
    Tunafuatilia jinsi nchi zinatekeleza
  • 2:22 - 2:26
    haki ya elimu kwa kila mtu na
    sheria na sera zinazotumika
  • 2:26 - 2:30
    kuhakikisha haki hii. Kila baada ya muda
    UNESCO huwasiliana na nchi washirika
  • 2:30 - 2:33
    ikiziomba kushiriki maelezo
    kuhusu jinsi wanahakikisha
  • 2:33 - 2:35
    haki ya elimu
  • 2:35 - 2:36
    na inatoa mapendekezo.
  • 2:36 - 2:39
    UNESCO pia inadumisha
    ufuatiliaji mtandaoni
  • 2:39 - 2:42
    ili kutoa maelezo kuhusu hili.
  • 2:42 - 2:44
    Mwishowe, tunatetea haki ya elimu
  • 2:44 - 2:49
    kupitia utafiti wa masuala muhimu,
    kama vile haki ya elimu kwa wakimbizi
  • 2:49 - 2:54
    au mifano ya jinsi sheria za elimu
    katika nchi mahususi hutekelezwa.
  • 2:56 - 2:58
    Katika kiwango cha karibu tunaenda
    na kuzipa nchi
  • 2:58 - 3:02
    zana zote wanazohitaji ili
    kuimarisha mfumo wao wa elimu,
  • 3:02 - 3:04
    pia tunasaidia nchi kupanga
  • 3:04 - 3:07
    marekebisho yao ya elimu
    na viwango vya kimataifa.
  • 3:07 - 3:10
    Kile hii inamaanisha ni tunahakikisha
    mifumo yao ya sheria na sera
  • 3:10 - 3:12
    inaendana na viwango
  • 3:12 - 3:15
    ambavyo mashirika kama yetu yameweka.
  • 3:15 - 3:19
    Hii ni ili nchi zitoe mifumo
    ya elimu iliyo thabiti na pana
  • 3:19 - 3:21
    kwa raia wake.
  • 3:22 - 3:27
    UNESCO ina mengi ya kufanya:
    vijana na watoto milioni 263
  • 3:27 - 3:32
    hawawezi kufikia shule, chini ya nchi
    1 kati ya 5 inaweza kutoa miaka 12
  • 3:32 - 3:34
    ya elimu bila malipo kwa raia wake.
  • 3:34 - 3:37
    Katika sehemu fulani za dunia
    kwa mfano wasichana,
  • 3:37 - 3:39
    wakimbizi na watu walio na ulemavu
  • 3:39 - 3:42
    wana wakati mgumu kutumia haki yao
    ya elimu,
  • 3:42 - 3:48
    vigezo vingi vinachangia hili kama vile
    umaskini, mizozo na majanga asili.
  • 3:49 - 3:54
    Licha ya haya sisi UNESCO tunaendelea
    kujitahidi kuhakikisha haki ya elimu
  • 3:54 - 3:57
    inaendelea kuwa kipaumbele cha kimataifa.
  • 3:57 - 3:59
    Ndiyo maana tuna maonyesho
    kama haya ili kukumbuka
  • 3:59 - 4:01
    kilichofanywa na kinachohitaji kufanywa,
  • 4:01 - 4:06
    ili watu kote duniani waweze
    kupata elimu na kutimiza ndoto zao.
  • 4:06 - 4:09
    Asante kwa kuja leo
    na furahieni ziara iliyobaki.
Title:
Who is allowed to go to school?
Description:

more » « less
Video Language:
English
Team:
Amplifying Voices
Project:
Promoting Girls Education
Duration:
04:19
Eddie Simiyu Wafulah edited Swahili subtitles for Who is allowed to go to school?
Eddie Simiyu Wafulah edited Swahili subtitles for Who is allowed to go to school?

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions