< Return to Video

JINSI YA KUEPUKA MSONGO wa KIROHO! | Maneno ya kutia moyo pamoja na Kaka Chris

  • 0:00 - 0:06
    Moyo wa maombi ni moyo wa amani
  • 0:06 - 0:11
    lakini moyo usio na maombi ni moyo usiotulia.
  • 0:13 - 0:22
    Neema na amani iwe kwenu nyote katika
    jina la ajabu la Yesu Kristo.
  • 0:22 - 0:26
    Watu wa Mungu, ni baraka ya ajabu iliyoje
  • 0:26 - 0:31
    kukuona umeunganishwa sasa hivi
    kutoka kote ulimwenguni
  • 0:31 - 0:35
    kusikia Neno Hai la Mungu.
  • 0:35 - 0:40
    Ndio maana tumekusanyika,
    tumeunganishwa, tunatazama sasa hivi -
  • 0:40 - 0:42
    kupokea Neno la Mungu.
  • 0:42 - 0:49
    Kwa sababu tunajua kwamba - bila kujali maswali ambayo maisha yanatupa,
  • 0:49 - 0:56
    majibu yapo katika Neno la Mungu siku zote.
  • 0:56 - 1:05
    Haijalishi uwongo ambao ulimwengu unachora karibu nawe, ukweli daima uko katika Neno la Mungu.
  • 1:05 - 1:09
    Kwa hiyo leo tutazingatia Neno lake, tukizingatia Maandiko.
  • 1:09 - 1:14
    Lakini bila shaka, tunaanza
    na muda wa maombi.
  • 1:14 - 1:23
    Kwa hiyo watu wa Mungu, tuombe sasa hivi katika jina hilo kuu la Yesu Kristo.
  • 1:23 - 1:36
    Bwana Yesu Kristo, tunakushukuru kwa neema hii ya ajabu kuwa katika uwepo wako.
  • 1:36 - 1:48
    Acha nguvu ya Neno lako izungumze utulivu kwa kila moyo wenye shida.
  • 1:48 - 1:59
    Acha nguvu za Neno Lako zivunje kila kizuizi kilichowekwa na mwanadamu.
  • 1:59 - 2:16
    Utupe neema ya kuelewa Neno lako takatifu na kulitumia katika maisha yetu ya kila siku.
  • 2:16 - 2:25
    Fungua mioyo yetu kwa ufunuo Wako
    mtakatifu sasa hivi.
  • 2:25 - 2:31
    Katika jina kuu la Yesu Kristo tunaomba.
  • 2:31 - 2:39
    Na watu wa Mungu wakasema, Amina!
  • 2:39 - 2:42
    Asante, Yesu Kristo.
  • 2:42 - 2:44
    Karibu tena, kila mtu.
  • 2:44 - 2:48
    Karibuni watu wa Mungu katika Ibada ya Leo ya Kutia Moyo
  • 2:48 - 2:53
    kutoka kwenye Studio ya God's Heart TV
    hapa North Wales.
  • 2:53 - 3:01
    Na kama nilivyotaja katika utangulizi mdogo - maswali yoyote ambayo maisha yanatupa,
  • 3:01 - 3:04
    majibu daima yako katika Neno la Mungu.
  • 3:04 - 3:07
    Na hii ndio tunataka kufanya hivi sasa -
  • 3:07 - 3:11
    tunataka kuchukua muda wa thamani kulipitia Neno la Mungu
  • 3:11 - 3:16
    na usikie kile ambacho Mungu anatuambia leo kupitia Neno Lake, kwa Roho Wake.
  • 3:16 - 3:22
    Kwa sababu kumbuka - nataka ujichunguze, maisha yako kwa muda.
  • 3:22 - 3:25
    Hebu fikiria hili.
  • 3:25 - 3:32
    Kiwango ambacho
    hali za maisha zinakuelemea
  • 3:32 - 3:38
    inaonyesha kiwango ambacho
    Neno la Mungu linakutawala.
  • 3:38 - 3:43
    Sisemi maswala, changamoto, hali za maisha sio sehemu ya safari yetu
  • 3:43 - 3:47
    ikiwa tuko karibu na Mungu,
    ikiwa Neno lake linatutawala.
  • 3:47 - 3:54
    Lakini majibu yako kwa hali hizo, masuala, changamoto
  • 3:54 - 3:59
    ni taswira ya mahali ulipo kiroho.
  • 3:59 - 4:10
    Ikiwa hali zinatuletea hofu, mashaka, kuomboleza, kunung'unika, kulalamika,
  • 4:10 - 4:17
    wasiwasi au mashaka - angalia moyo wako.
  • 4:17 - 4:22
    Hiyo ni taswira kwamba Neno la Mungu
    haliutawala moyo wako.
  • 4:22 - 4:29
    Kwa hiyo tafadhali, watu wa Mungu, geuka pamoja nami kwenye kifungu cha uthibitisho cha ujumbe wa leo,
  • 4:29 - 4:34
    ambayo imechukuliwa kutoka Wafilipi 4.
  • 4:34 - 4:44
    Haya ni Maandiko ya ajabu!
    Nitasoma kutoka Wafilipi 4:6-9.
  • 4:44 - 4:51
    Na nilipokuwa mahali pa maombi nikijiandaa kwa ajili ya ujumbe huu leo,
  • 4:51 - 4:57
    Nilikumbuka ujumbe wa kutia moyo sana kutoka kwa Nabii TB Joshua, mshauri wangu.
  • 4:57 - 5:01
    Alisema jambo ambalo nataka
    ulizingatie kwa sababu litatusaidia
  • 5:01 - 5:02
    kupitia ujumbe wa leo.
  • 5:02 - 5:15
    Alisema, “Unaweza kuwa na msongo wa mawazo. Unaweza kuwa na mkazo wa kihisia.
  • 5:15 - 5:25
    Lakini tafadhali, usiwe na msongo wa kiroho.
  • 5:25 - 5:37
    Kwa sababu ikiwa ndivyo, utapoteza mwelekeo kwa Mungu na kuanza kutafuta njia mbadala.”
  • 5:37 - 5:40
    Ninataka kusema tena, watu wa Mungu.
  • 5:40 - 5:43
    Unaweza kuwa na msongo wa kimwili.
  • 5:43 - 5:49
    Iwe imeunganishwa na afya,
    tumejifanyia kazi kupita kiasi, tumechoka
  • 5:49 - 5:53
    na miili yetu inaathirika -
    tunaweza kuwa na msongo wa kimwili.
  • 5:53 - 5:55
    Tunaweza kuwa na msongo wa kihisia.
  • 5:55 - 5:59
    Labda kuna mvutano au msongo katika mahusiano, mahali pa kazi - taja tu.
  • 5:59 - 6:10
    Tunaweza kuwa na mfadhaiko wa kihisia,
    lakini tafadhali usiwe na msongo wa kiroho
  • 6:10 - 6:18
    kwa sababu ukiwa hivyo, utapoteza mwelekeo kwa Mungu na kuanza kutafuta
  • 6:18 - 6:24
    njia mbadala za binadamu, njia za mkato.
  • 6:24 - 6:30
    Na nadhani ungekubaliana nami
    kutokana na uzoefu wa maisha kwamba
  • 6:30 - 6:37
    jaribio lolote la kuchukua njia ya mkato
    ili kuepuka mchakato wa Mungu
  • 6:37 - 6:41
    kwa kweli huishia kama 'njia ndefu'.
  • 6:41 - 6:43
    Haifanyi kuwa fupi zaidi.
  • 6:43 - 6:49
    Kwa kweli, bado unaishia kurudi pale ulipoanza
  • 6:49 - 6:54
    kwa sababu mchakato wa Mungu ni muhimu.
  • 6:54 - 6:57
    Hata ukipokea kitu
    bila mchakato na Mungu,
  • 6:57 - 6:59
    haitaambatana na bidhaa za Mungu.
  • 6:59 - 7:08
    Namaanisha nini? Unaweza kuwa na pesa bila mchakato wa Mungu lakini usiwe na amani.
  • 7:08 - 7:11
    Mungu pekee ndiye anayeweza kutoa amani.
  • 7:11 - 7:14
    Sasa, ninaposema 'msongo wa kiroho'...
    tunakuja kwenye Maandiko haya.
  • 7:14 - 7:17
    Ninaposema 'msongo wa kiroho',
    ninamaanisha nini?
  • 7:17 - 7:24
    Ninamaanisha nini ninaposema
    'usiwe na msongo wa kiroho'?
  • 7:24 - 7:35
    Hali yako inapokukosesha raha, pumziko la ndani,
  • 7:35 - 7:44
    ni ishara kwamba una msongo wa kiroho.
  • 7:44 - 7:49
    Wakati changamoto yako, jaribio, shida, chochote kinaweza kuwa,
  • 7:49 - 8:01
    vinapokuibia pumziko la ndani, amani ya moyo -
    moyo wako unapusumbuka, kufadhaika -
  • 8:01 - 8:06
    ni ishara ya msongo wa kiroho.
  • 8:06 - 8:13
    Wakati vita hiyo au mzigo huo
    utakapoondoa macho yako kwa Yesu,
  • 8:13 - 8:16
    unapotenganisha moyo wako
    na Yesu, kuwa mwangalifu.
  • 8:16 - 8:23
    Hiki ndicho kichwa cha ujumbe wa leo - 'Jihadhari na m=Msongo wa Kiroho'.
  • 8:23 - 8:27
    Ikiwa una mtu karibu na wewe nyumbani anayetazama hii, mwambie tu,
  • 8:27 - 8:31
    “Jihadhari na mkazo wa kiroho.”
  • 8:31 - 8:39
    Moyo uliofadhaika ni mahali pa kuzaliwa
    kwa maamuzi mabaya.
  • 8:39 - 8:44
    Sasa, twende kwenye Neno - Wafilipi 4.
  • 8:44 - 8:49
    Naamini wengi wetu tunafahamu kifungu hiki;
    ni kifungu maarufu sana.
  • 8:49 - 8:52
    Lakini ninataka kusisitiza ukweli fulani muhimu kutoka kwa kifungu hiki.
  • 8:52 - 9:01
    Wafilipi 4:6 - "Msijisumbue kwa lolote..."
  • 9:01 - 9:05
    Natumaini mnasikia Neno hili,
    watu wa Mungu.
  • 9:05 - 9:13
    “Msijisumbue kwa neno lo lote, bali katika kila neno kwa kusali na kuomba,
  • 9:13 - 9:24
    pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu;
  • 9:24 - 9:35
    na amani ya Mungu...” - amani isiyo ya kawaida kutoka kwa Mungu asiye wa kawaida -
  • 9:35 - 9:41
    “...na amani ya Mungu, ipitayo akili zote;
  • 9:41 - 9:52
    itahifadhi mioyo yenu na nia zenu
    kwa Kristo Yesu.
  • 9:52 - 9:57
    Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha;
  • 9:57 - 10:02
    yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza;
  • 10:02 - 10:05
    yo yote yenye sifa njema, kama kuna wema wo wote
  • 10:05 - 10:12
    na ikiwa kuna sifa nzuri - yatafakarini hayo.
  • 10:12 - 10:21
    Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea na kuyasikia na kuyaona kwangu, yafanyeni…”
  • 10:21 - 10:25
    Sio tu 'Yasemeni haya' lakini "yafanyeni haya" -
    iweke katika vitendo.
  • 10:25 - 10:32
    "...na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi."
  • 10:32 - 10:35
    Asante, Yesu, kwa
    Neno Hai la Mungu.
  • 10:35 - 10:42
    Ninataka tu kupitia Maandiko haya hatua kwa hatua na kutumia Maandiko haya
  • 10:42 - 10:48
    kama msingi wa kuhimiza kila mmoja wenu aliyeungana nasi hivi sasa
  • 10:48 - 10:50
    kutoka kwenye Neno la Mungu.
  • 10:50 - 11:03
    Kuanza, mstari wa sita unasema hivi:
    “Msijisumbue kwa lolote.”
  • 11:03 - 11:08
    Ninapenda jinsi taarifa hiyo ilivyo moja kwa moja.
  • 11:08 - 11:13
    Maandiko hapa hayaweki daraja
    kiwango cha hali yako.
  • 11:13 - 11:17
    'Sawa, ikiwa kuna jambo hapa, unaweza kuwa na wasiwasi kidogo kuhusu hilo.
  • 11:17 - 11:21
    Au ikiwa kuna jambo katika kazi yako,
    ambayo inatoa nafasi kwa wasiwasi kidogo.'
  • 11:21 - 11:24
    Hapana - hakuna kilichoachwa hapa.
  • 11:24 - 11:30
    Inasema, "Msijisumbue kwa kitu chochote."
  • 11:30 - 11:35
    Maandiko haya si pendekezo tu;
    ni maagizo. Ni wazi sana.
  • 11:35 - 11:41
    Kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyosema kwa usawa katika Mathayo 6:25-mwisho,
  • 11:41 - 11:46
    'Usijali kuhusu maisha yako.
    Msiwe na wasiwasi juu ya kesho.'
  • 11:46 - 11:50
    Ni maagizo ya wazi.
  • 11:50 - 11:56
    "Msiwe na wasiwasi juu ya kitu chochote."
  • 11:56 - 12:12
    Hakuna suala maishani ambapo wasiwasi ni jibu linalofaa au jibu sahihi. Hakuna.
  • 12:12 - 12:18
    Nimezungumza na watu wengine hapo awali na hili ni jambo ambalo wengi wetu hufanya -
  • 12:18 - 12:25
    tunaangalia hali zetu wenyewe na kuhitimisha kwamba zinapaswa kufikia kiwango tofauti.
  • 12:25 - 12:28
    Watu walikuwa wakiniambia kwenye
    simu ninapozungumza nao,
  • 12:28 - 12:32
    'Angalia, kaka Chris, ninaelewa unachosema lakini hujui hali yangu.
  • 12:32 - 12:34
    Hujui jinsi hali yangu ilivyo mbaya.
  • 12:34 - 12:38
    Hujui uzito
    wa changamoto yangu.'
  • 12:38 - 12:39
    Nakubaliana nawe!
  • 12:39 - 12:44
    Labda sijui, lakini haibadilishi ukweli wa kile Mungu anachokuambia leo
  • 12:44 - 12:49
    kupitia Neno Lake -
    'Msijisumbue kwa neno lolote.'
  • 12:49 - 12:53
    “Msijisumbue kwa lolote.”
  • 12:53 - 13:00
    Hakuna eneo la kijivu huko;
    ni wazi sana.
  • 13:00 - 13:09
    Ikiwa hali yako inakufanya uwe na wasiwasi,
  • 13:09 - 13:15
    inapendekeza uko kwenye
    njia mbaya kiroho.
  • 13:15 - 13:21
    Weka hilo moyoni mwako tunaposogea
    kwenye hatua inayofuata katika mstari huu.
  • 13:21 - 13:27
    "Msijisumbue kwa lolote ila katika kila jambo..."
  • 13:27 - 13:31
    Natumai utazingatia
    hilo tena - kila kitu.
  • 13:31 - 13:36
    Hakuna kiwango kwa hali tofauti.
  • 13:36 - 13:41
    Hakuna mabadiliko katika Neno la Mungu kulingana na kiwango cha jinsi tunavyohisi
  • 13:41 - 13:45
    hali yetu ni mbaya - hapana!
    Neno la Mungu liko wazi.
  • 13:45 - 13:51
    “...bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru;
  • 13:51 - 13:57
    haja zenu na zijulikane kwa Mungu…”
  • 13:57 - 14:10
    Dawa ya wasiwasi iko wazi sana -
    peleka hali yako kwa Mungu katika maombi.
  • 14:10 - 14:13
    Hili ndilo jibu, watu wa Mungu.
  • 14:13 - 14:19
    Kuwa na afya nzuri kiroho hakuondoi ukweli wa jambo.
  • 14:19 - 14:24
    Unaweza kuhudhuria ibada nzuri za kanisa,
  • 14:24 - 14:28
    kuwa sehemu ya kanisa hai ambapo unapokea Neno la Mungu kila juma
  • 14:28 - 14:30
    nakupokea maombi katika
    nguvu za Roho Mtakatifu.
  • 14:30 - 14:34
    Labda umekuwa ukihudhuria Huduma za Maombi Shirikishi kwenye TV ya Moyo wa Mungu.
  • 14:34 - 14:36
    Utukufu ni kwa Mungu!
  • 14:36 - 14:40
    Asante Mungu kwa kuweka moyoni mwako kuwa sehemu ya jumuiya hii ya ajabu ya waumini.
  • 14:40 - 14:46
    Lakini hiyo haibadilishi
    uhalisi wa hali za maisha.
  • 14:46 - 14:54
    Hali zitakuja, changamoto zitakuja, masuala ya maisha yatakuja kwa kila mtu.
  • 14:54 - 14:57
    Lakini jibu liko wazi katika Neno la Mungu.
  • 14:57 - 15:09
    Usijisumbue kwa lolote ila katika kila jambo - mpe Mungu, peleka kwenye maombi
  • 15:09 - 15:11
    Ni wazi sana!
  • 15:11 - 15:24
    Shida ikigonga kwenye moyo wako,
    acha ikuongoze kuomba.
  • 15:24 - 15:28
    Ikiwa hali yako inakusukuma kuomba,
  • 15:28 - 15:32
    shetani hawezi kuitumia kuutenganisha moyo wako na Mungu
  • 15:32 - 15:36
    na kukupeleka mahali penye msongo wa kiroho.
  • 15:36 - 15:39
    Hii ndiyo nia yake. Hili ndilo lengo lake.
  • 15:39 - 15:44
    Anataka kutenganisha mioyo yetu na Mungu,
  • 15:44 - 15:50
    ili mioyo yetu ifadhaike, ihangaishwe, ielemewe.
  • 15:50 - 15:55
    Na katika hali kama hiyo ya moyo,
    tunaweza kufanya kosa kwa urahisi,
  • 15:55 - 16:00
    kutenda kwa urahisi kutokana na mihemko,
    kuitikia uchokozi,
  • 16:00 - 16:06
    kutedenda kupitia lenzi ya kosa au kutenda kwa macho ya chuki - na mengine iyajuayo.
  • 16:06 - 16:09
    Anataka moyo wako usumbuke.
    Angalia mstari unaofuata.
  • 16:09 - 16:12
    Hebu nirukie mstari unaofuata katika hatua hii.
  • 16:12 - 16:15
    "...na amani ya Mungu..."
  • 16:15 - 16:18
    Unapopeleka hali yako kwa Mungu katika maombi, matokeo yake ni nini?
  • 16:18 - 16:24
    “...na amani ya Mungu, ipitayo akili zote;
  • 16:24 - 16:36
    itailinda mioyo yenu na nia zenu [kupitia] Kristo Yesu.”
  • 16:36 - 16:39
    Uwanja wa kweli wa vita si kwa nje.
  • 16:39 - 16:45
    Uwanja wa kweli wa vita ni moyo.
  • 16:45 - 16:52
    Ibilisi anataka kuhamisha usikivu wetu,
    mwelekeo wetu, nguvu zetu, maslahi yetu
  • 16:52 - 16:54
    kuje nje, kwennye mwili -
  • 16:54 - 17:07
    kwa hivyo tunaishia kumaliza muda, umakini na rasilimali katika kutafuta vita vibaya.
  • 17:07 - 17:16
    Uwanja wa kweli wa vita ni moyo -
    kutunza mioyo yetu, kulinda mioyo yetu.
  • 17:16 - 17:19
    Na Maandiko yako wazi kabisa.
  • 17:19 - 17:27
    Hali yako inapokusukuma kuomba, amani ya Mungu itaulinda moyo wako.
  • 17:27 - 17:32
    Sio lazima kusema amani ya Mungu itabadilisha hali yako
  • 17:32 - 17:33
    au kuondoa changamoto hiyo.
  • 17:33 - 17:36
    Baadhi ya hali, lazima tuzipitie.
  • 17:36 - 17:44
    Lakini kwa amani ya Mungu tutapita kati yake bila kutulemea.
  • 17:44 - 17:51
    kutupotosha au kutupeleka
    mahali nje ya imani yetu.
  • 17:51 - 17:55
    "... amani ya Mungu, ipitayo akili zote..."
  • 17:55 - 17:59
    Ninasema nini hapa watu wa Mungu?
  • 17:59 - 18:06
    Moyo wa maombi ni moyo wa amani
  • 18:06 - 18:15
    lakini moyo usio na maombi ni moyo usiotulia.
  • 18:15 - 18:17
    Nitasema tena - moyo wa maombi
    ni moyo wenye amani
  • 18:17 - 18:23
    Nitasema tena - moyo wa maombi
    ni moyo wenye amani
  • 18:23 - 18:29
    lakini moyo usio na maombi ni moyo usiotulia.
  • 18:29 - 18:30
    lakini moyo usio na maombi ni moyo usiotulia.
  • 18:30 - 18:36
    Shida ya kweli ni shida iliyo ndani,
    sio ile inayokuzunguka,
  • 18:36 - 18:39
    sio hali ya nje.
  • 18:39 - 18:46
    Shida ya kweli iko ndani - moyoni.
  • 18:46 - 18:56
    Ndiyo maana ni lazima tuone chochote
    tunachokabiliana nacho kama sababu ya kuomba.
  • 18:56 - 19:04
    Ikiwa hali yako inakusukuma kuomba, wewe ni zaidi ya mshindi kupitia Kristo.
  • 19:04 - 19:08
    Lakini ikiwa hali yako inakufanya uogope,
  • 19:08 - 19:14
    au hali yako inakufanya uwe na wasiwasi, ujilinganishe na wengine,
  • 19:14 - 19:22
    uanze kujihurumia, ujipime kwa viwango vyako vya kibinadamu,
  • 19:22 - 19:28
    au hali yako inakusukuma kukata tamaa,
  • 19:28 - 19:36
    kutafuta njia mbadala, kutafuta njia ya suluhu kwa njia zote zinazowezekana katika asili -
  • 19:36 - 19:45
    inaonyesha mioyo yetu haiko
    mahali pazuri pamoja na Mungu.
  • 19:45 - 19:52
    Ambapo shida yako inakusukuma ni onyesho la mahali ulipo kiroho.
  • 19:52 - 19:55
    Mwelekeo ambao shida yako inakuchukua -
  • 19:55 - 19:58
    Je, inakurudisha kwa Mungu,
    unakupelekea upige magoti?
  • 19:58 - 20:05
    Au inakupeleka kwenye chaguzi nyingine
    nje ya Mungu?
  • 20:05 - 20:10
    Sijui ikiwa umegundua kuwa mara nyingi shida inapotokea katika maisha yetu,
  • 20:10 - 20:14
    tunajaribu kwanza kulitatua sisi wenyewe
    kabla hatujaja kwa Mungu.
  • 20:14 - 20:17
    Ni baada ya kumaliza
    juhudi zetu wenyewe za kibinadamu -
  • 20:17 - 20:20
    'Haya! Hili ni zaidi yangu!
    Acha niende kwa Mungu.'
  • 20:20 - 20:23
    Hiyo sio njia ambayo
    Maandiko yanatuambia hapa.
  • 20:23 - 20:27
    Katika kila hali - ipeleke kwa Mungu kwa maombi.
  • 20:27 - 20:29
    Sasa, nataka mzingatie jambo hili.
  • 20:29 - 20:38
    Wengi wetu huenda moja kwa moja kwenye maombi
    na kuruka shukrani. Hapana!
  • 20:38 - 20:43
    Maandiko yanasema nini?
  • 20:43 - 20:49
    "Msijisumbue kwa neno lo lote, bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru..."
  • 20:49 - 20:52
    Kwa nini ninasisitiza hilo, watu wa Mungu?
  • 20:52 - 20:55
    Kwa sababu hii ni silaha
    aliyotupa Yesu Kristo,
  • 20:55 - 20:59
    silaha ambayo Mungu ametupa ambayo
    wengi wetu hatuitumii.
  • 20:59 - 21:03
    Wakati mwingine changamoto huja
    na tunalemewa sana
  • 21:03 - 21:06
    kwa sababu tunaangazia
    ukubwa wa changamoto hiyo.
  • 21:06 - 21:09
    Haijalishi changamoto yako ni kubwa kiasi gani,
    si kubwa kuliko Mungu.
  • 21:09 - 21:16
    Wakati mwingine unahitaji kuchukua hatua nyuma na fikiria tu hii.
  • 21:16 - 21:21
    Fikiria kile ambacho Mungu amekufanyia.
  • 21:21 - 21:24
    Fikiria kile Mungu amefanya ndani yako.
  • 21:24 - 21:27
    Fikiria kile Mungu amefanya kupitia wewe.
  • 21:27 - 21:31
    Na mashaka yako yataondoka.
  • 21:31 - 21:35
    Tafakari wema wa Mungu katika maisha yako.
  • 21:35 - 21:41
    Kila mtu hapa, kila mtu aliyeunganishwa
    na huduma hii sasa hivi,
  • 21:41 - 21:44
    hata kwa wakati huu ninapozungumza,
    chukua tu muda kufikiria nyuma
  • 21:44 - 21:47
    juu ya wema wa Mungu katika maisha yako.
  • 21:47 - 21:53
    Sisi sote tuna ushuhuda wa jinsi Mungu alivyotukomboa, jinsi alivyotuokoa,
  • 21:53 - 21:59
    jinsi alivyoingilia kati kimiujiza katika hali hiyo, jinsi alivyotuhifadhi.
  • 21:59 - 22:04
    Sisi sote tunatembea, tunaishi,
    ni shuhuda zinazopumua.
  • 22:04 - 22:15
    Na kukumbuka rekodi ya Mungu ni silaha ya kushinda uwongo wa mashaka.
  • 22:15 - 22:22
    Kwa sababu mashaka huzingatia tu kile kinachoonekana - ukubwa wa hali hiyo,
  • 22:22 - 22:28
    watu wanasema nini kuhusu hali hiyo, maoni ya wengine kuhusu hali hiyo.
  • 22:28 - 22:31
    Haya ndiyo mambo yanayojenga wasiwasi.
  • 22:31 - 22:34
    Chukua hatua nyuma.
  • 22:34 - 22:37
    Fikiri juu ya wema wa Mungu.
  • 22:37 - 22:40
    Thamini wema wa Mungu.
  • 22:40 - 22:42
    Tambua wema wa Mungu.
  • 22:42 - 22:53
    Hii ni dawa bora ya udanganyifu wa wasiwasi na upoozaji wa hofu.
  • 22:53 - 23:04
    Shukrani, shukrani - ni silaha ya ajabu namna gani, ambayo wengi wetu hatutumii.
  • 23:04 - 23:08
    Kwa sababu katika joto la sasa,
    hali inapojitokeza,
  • 23:08 - 23:12
    tatizo linapokuja,
    tunazidiwa kwa urahisi.
  • 23:12 - 23:14
    Kwanini ni hivyo?
  • 23:14 - 23:17
    Hapa ndipo ninapoenda katika
    aya inayofuata, watu wa Mungu.
  • 23:17 - 23:22
    Ninataka kuunganisha sehemu hizi mbili
    kwa uwazi sana.
  • 23:22 - 23:28
    Maandiko hayo katika Wafilipi 4:8 - ikiwa umelelewa katika nyumba ya Kikristo,
  • 23:28 - 23:32
    unafundishwa mstari huo kutoka
    shule ya Jumapili; tunaijua vizuri sana.
  • 23:32 - 23:38
    "Mambo yo yote yaliyo ya haki, safi, ya heshima, bora, yenye kupendeza, yenye kusifiwa -
  • 23:38 - 23:39
    fikiri juu ya mambo haya.'
  • 23:39 - 23:50
    Lakini angalia mistari inayotangulia maneno hayo yenye nguvu ambayo tumetoka kusoma.
  • 23:50 - 24:04
    Ikiwa sisi ni waaminifu, kile tunacholisha roho zetu ndicho chanzo cha msongo wetu wa kiroho.
  • 24:04 - 24:07
    Nitasema tena.
  • 24:07 - 24:15
    Ikiwa sisi ni watu wa Mungu wanyoofu,
    tunalisha roho zetu;
  • 24:15 - 24:26
    kile tunachozingatia
    ndicho kitu hasa kinachotunyima pumziko.
  • 24:26 - 24:39
    Acha kulalamikia madhara ya sumu unayojilisha nayo.
  • 24:39 - 24:45
    “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha;
  • 24:45 - 24:52
    yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza;
  • 24:52 - 24:54
    mambo yoyote yenye sifa njema,
    ukiwapo wema wo wote na
  • 24:54 - 24:59
    ikiwa kuna jambo lo lote la kusifiwa -
    yatafakarini hayo.”
  • 24:59 - 25:06
    Wengi wetu leo ​​tunazingatia,
  • 25:06 - 25:14
    tunalisha roho zetu vitu vichafu, visivyo haki,
  • 25:14 - 25:19
    mambo yasiyopendeza,
    mambo yenye sifa mbaya;
  • 25:19 - 25:23
    mambo ambayo hakuna fadhila.
  • 25:23 - 25:31
    Na tunashangaa kwa nini tunaanguka katika msongo wa kiroho mbele ya majitu yetu.
  • 25:31 - 25:36
    Kwa sababu tunatoa uangalifu wetu, tunalisha mioyo yetu na mambo yasiyofaa.
  • 25:36 - 25:40
    Kama Wakristo, tunapaswa kuwa waangalifu.
  • 25:40 - 25:44
    Kumbuka kichwa cha ujumbe huu: 'Jihadhari na Msongo wa Kiroho'.
  • 25:44 - 25:51
    Ikiwa hali yako inakufanya uwe na wasiwasi, angalia ni nini unaIlisha roho yako.
  • 25:51 - 26:00
    Ikiwa changamoto yako inakufanya uwe na wasiwasi, angalia kile unachokizingatia.
  • 26:00 - 26:03
    Ikiwa shida yako, inaweza kuwa chochote kile -
  • 26:03 - 26:08
    kuwa Mkristo hakuondoi ukweli wa changamoto hizi -
  • 26:08 - 26:16
    vyovyote iwavyo, ikiwa hali hiyo inakufanya ukate tamaa au uvunjike moyo,
  • 26:16 - 26:22
    angalia kile unachoupatia moyo wako.
  • 26:22 - 26:26
    Uko vile kulingana na unachokizingatia.
  • 26:26 - 26:29
    Wakristo, tunapaswa kuwa waangalifu.
  • 26:29 - 26:32
    Kuwa makini na kile unachotazama.
  • 26:32 - 26:36
    Kuwa mwangalifu kwa kile unachosikia, sikiliza.
  • 26:36 - 26:39
    Kuwa makini na unachosoma.
  • 26:39 - 26:45
    Kwa sababu haya huathiri mawazo yako.
  • 26:45 - 26:51
    Na vile mtu aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. ( Mithali 23:7 )
  • 26:51 - 27:01
    Ikiwa tunalisha mioyo yetu mambo yasiyopatana na Neno la Mungu,
  • 27:01 - 27:10
    usishangae kwamba mwitikio wako kwa majaribu ya maisha haupatani na Neno la Mungu.
  • 27:10 - 27:20
    Nakumbuka wimbo wa zamani sana ambao tulifundishwa tukiwa watoto katika shule ya Jumapili.
  • 27:20 - 27:23
    Sitakuimbia, usijali! Nitakupa tu maandishi.
  • 27:23 - 27:26
    Mstari mmoja wa wimbo huu unasema,
  • 27:26 - 27:35
    'Pale ukitoacho kinapozidi unachokiingiza, basi uhifadhi wako ndio utakuwa anguko lako.'
  • 27:35 - 27:40
    Sasa, huu ni wimbo wa watoto
    lakini ni ujumbe mzito sana.
  • 27:40 - 27:46
    'Wakati ukitoacho kinapozidi unachokiingiza, basi uhifadhi wako ndio utakuwa anguko lako.'
  • 27:46 - 27:52
    Ikiwa unalisha mwili wako kuliko unavyolisha roho yako,
  • 27:52 - 27:56
    usishangae
    msongo wa kiroho unapotokea.
  • 27:56 - 28:03
    Ikiwa unalisha akili zako zaidi ya moyo wako,
  • 28:03 - 28:14
    usishangae msongo wa kiroho unaposhambulia - moyo wenye shida, fadhaa, uliofadhaika.
  • 28:14 - 28:22
    Na kama nilivyowaambia, watu wa Mungu - maisha yetu wenyewe ni kioo, mfano wa hii.
  • 28:22 - 28:29
    Sisi sote tunaotazama sasa hivi, ikiwa hali itatokea na unaitikia kwa hisia
  • 28:29 - 28:34
    katika wakati huo, jiangalie -
    95% ya wakati unajutia majibu hayo.
  • 28:34 - 28:37
    Baadaye unasema, 'Lo, kwa nini nilisema hivyo?
  • 28:37 - 28:41
    Kwa nini nilienda mbali sana?
    Kwa nini niliitikia hivi?'
  • 28:41 - 28:48
    Unapaswa kuanza kuvipanga pamoja vipande ambavyo maafa yamesababishwa
  • 28:48 - 28:54
    kwa mwitikio wako uliopitiliza kwa sababu
    ya mhemuko, hisia.
  • 28:54 - 29:00
    Hiyo ni onyesho la kile
    unalisha nacho moyo wako.
  • 29:00 - 29:05
    Ikiwa mnailisha mioyo yenu mambo yasiyopatana na Neno la Mungu,
  • 29:05 - 29:12
    kuna madhara yake - inaweza kusababisha kwa urahisi msongo wa kiroho, kubadilisha malengo yako.
  • 29:12 - 29:17
    Vita yako, mzigo wako unakuondoa
    kutoka kwa Yesu.
  • 29:17 - 29:21
    Hii ndiyo sababu nilisema, watu wa Mungu,
    jihadharini na msongo wa kiroho.
  • 29:21 - 29:27
    Nilikuwa nikizungumza na wanandoa kwa simu hivi majuzi, nikiwapa neno la ushauri.
  • 29:27 - 29:31
    Ninakupa tu mfano huu mdogo kuelezea kile ninachokizungumza.
  • 29:31 - 29:37
    Nilikuwa nikizungumza na wanandoa na mume alikuwa akilalamika kuhusu mke wake.
  • 29:37 - 29:43
    Alisema, 'Yeye ni wa kushangaza sana! Kitu chochote kidogo kinachotokea nyumbani -
  • 29:43 - 29:46
    inakuwa tatizo kubwa kama nini.'
  • 29:46 - 29:48
    Na wanaanza kusimulia
    maswala yote ya zamani.
  • 29:48 - 29:51
    Kila kitu kinaonekana kuwa kama mchezo wa kuigiza.
  • 29:51 - 29:55
    Nami nikawasikiliza na kusema,
    'Naweza kumwuliza mkeo?
  • 29:55 - 30:01
    Niambie, madam - ni mambo gani unayopenda au tabia, ni aina gani ya mambo unayozingatia?'
  • 30:01 - 30:10
    Na alisema ana uraibu wa kutazama michezo ya kuigiza , tamthilia kwenye runinga.
  • 30:10 - 30:18
    Ndipo nikasema, Vema, bwana, usishangae kama mkeo amegeuza shida yake kuwa mchezo wa kuigiza
  • 30:18 - 30:23
    wakati anaulisha moyo wake kwa mchezo wa kuigiza.'
  • 30:23 - 30:29
    Unaweza kuangalia na kusema ni hoja ndogo lakini ninatoa mfano wa vitendo.
  • 30:29 - 30:32
    Unatilia maanani
    kwa mambo ambayo ni njozi.
  • 30:32 - 30:35
    Drama si halisi; sio ukweli.
  • 30:35 - 30:38
    Na kwa sababu unazingatia sana mchezo wa kuigiza,
  • 30:38 - 30:40
    changamoto zinapotokea katika maisha yako,
  • 30:40 - 30:44
    unaona ni fursa ya kutengeneza drama hiyo nyumbani kwako.
  • 30:44 - 30:53
    Na hii ni hatari kwa sababu msingi wetu ni Neno la Mungu.
  • 30:53 - 30:59
    Ni lazima tuwe waangalifu kwa kile tunachoipatia mioyo yetu, kile tunachozingatia,
  • 30:59 - 31:04
    kile tunacholisha roho zetu.
  • 31:04 - 31:05
    Huo ulikuwa ni mfano mdogo tu.
  • 31:05 - 31:12
    Najua baadhi yetu wanaweza au wasihusiane kwa njia tofauti - lakini nyote mnaweza kujiangalia.
  • 31:12 - 31:14
    Hakuna anayejua moyo wako kuliko wewe.
  • 31:14 - 31:19
    Ikiwa unazingatia mambo yasiyofaa, niambie hali ya moyo wako.
  • 31:19 - 31:22
    Moyo wako unaweza kufadhaika kwa urahisi.
  • 31:22 - 31:26
    Unatazama kitu ambacho unajua kama Mkristo hutakiwi kutazama.
  • 31:26 - 31:31
    Hakuna mtu anayeweza kukuona ukiitazama lakini moyo wako unajua kuwa umeitazama. Kwa nini?
  • 31:31 - 31:39
    Moyo wako unataabishwa,
    unahamakishwa, unafadhaishwa.
  • 31:39 - 31:45
    Na hakuna dawa kwa moyo uliofadhashwa nje ya Kristo.
  • 31:45 - 31:50
    Moyo wako ukifadhaika, ungana tena na Muumba wako. Hiyo ndiyo njia pekee.
  • 31:50 - 31:53
    Hakuna kiasi cha pesa kinaweza
    kununua amani ya moyo.
  • 31:53 - 31:57
    Hakuna kiasi cha sifa kinachoweza
    kupata amani ya moyo.
  • 31:57 - 32:00
    Kuna baadhi ya vitu Mungu pekee anaweza kutoa.
  • 32:00 - 32:13
    Waebrania 4:3 inasema kwamba moyo wako ukiamini kweli, unaingia katika raha.
  • 32:13 - 32:16
    Hiyo ndiyo ahadi ya Mwenyezi Mungu kwetu sisi waaminio.
  • 32:16 - 32:22
    kuwa na amani ndani bila kujali
    dhoruba nje.
  • 32:22 - 32:30
    Ukiweka shida zako mikononi mwa Mungu,
  • 32:30 - 32:34
    Ataweka amani yake mioyoni mwenu.
  • 32:34 - 32:44
    Katika Marko 4, tunaijua hii hadithi wakati Yesu alipokuwa kwenye dhoruba ndani ya mashua.
  • 32:44 - 32:50
    Yesu alikuwa mtulivu katika dhoruba
    kabla hajatuliza dhoruba.
  • 32:50 - 32:53
    Hiyo ndiyo ahadi ya Mungu
    kwenye maisha yetu kama Wakristo -
  • 32:53 - 32:59
    si kuondolewa kwa dhoruba au kutokuwepo kwa dhoruba, lakini utulivu ndani ya dhoruba.
  • 32:59 - 33:08
    Ni utulivu ndani, moyoni. Hivi ndivyo Mungu ametuahidi.
  • 33:08 - 33:11
    Narudia tena watu wa Mungu.
  • 33:11 - 33:19
    Ikiwa hali yako inakufanya uwe na wasiwasi, angalia ni nini unalisha roho yako.
  • 33:19 - 33:22
    Angalia kile unachokizingatia.
  • 33:22 - 33:33
    Angalia ni nini kinachoathiri mawazo yako kwa sababu hakuna mtu aliye juu ya ushawishi.
  • 33:33 - 33:33
    Angalia ni nini kinachoathiri mawazo yako kwa sababu hakuna mtu aliye juu ya ushawishi.
  • 33:33 - 33:40
    Neno la ushauri - usiyumbishwe
  • 33:40 - 33:47
    na maoni ya watu
    wasioshikilia maisha yako ya baadaye.
  • 33:47 - 33:53
    Usikengeushwe na maoni ya watu ambao hawaainishi hatima yako.
  • 33:53 - 34:00
    Kila mtu ana maoni.
    Si kila mtu ana hekima.
  • 34:00 - 34:04
    Acha nikusomee Wafilipi 4:9.
  • 34:04 - 34:14
    “Mambo mliyojifunza na kuyapokea na kuyasikia na kuyaona kwangu;
  • 34:14 - 34:24
    yafanyeni haya...” - Nimeipenda hii, watu wa Mungu!
    Ninapenda kauli hii!
  • 34:24 - 34:29
    Sisi ni kile tunachofanya,
    si tu kile tunachosema.
  • 34:29 - 34:39
    Matunda yetu ni utangulizi bora wa imani yetu na maelezo bora ya imani yetu.
  • 34:39 - 34:53
    Matunda yako - upendo, furaha, amani, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi,
  • 34:53 - 34:59
    "Kwa matunda yao tutawatambua." ( Mathayo 7:20 )
  • 34:59 - 35:04
    Kwa nini ninasisitiza hili?
    Kwa sababu Mtume Paulo anasema hapa,
  • 35:04 - 35:08
    'Angalia, mambo uliyoyasikia,
    yale ambayo umesoma hapo sasa -yatendeni.'
  • 35:08 - 35:14
    Kitendo huongea zaidi kuliko maneno.
  • 35:14 - 35:17
    Ukienda kanisani,
    unahudhuria kanisani,
  • 35:17 - 35:20
    na kisha baada ya kanisa
    unarudi kusengenya,
  • 35:20 - 35:24
    usitegemee amani itawale moyoni mwako.
  • 35:24 - 35:27
    Kutoka kanisani hadi kwenye uchoyo - usitarajie amani.
  • 35:27 - 35:31
    Kutoka kanisani hadi kwenye tamaa - usitarajie amani.
  • 35:31 - 35:37
    Kwenda kanisani
    hakutufanyi sisi kuwa Wakristo -
  • 35:37 - 35:43
    si zaidi ya kuvaa shati la mpira wa miguu
    wa Manchester United,
  • 35:43 - 35:48
    haimaanishi kuwa nachezea
    Manchester United.
  • 35:48 - 35:59
    Ni tendo letu, tabia yetu inayoshuhudia ukweli wa maungamo yetu.
  • 35:59 - 36:05
    'Yafanyeni haya, na
    Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.'
  • 36:05 - 36:10
    Hii ndiyo ahadi ya Mungu.
    Aliahidi kuwa pamoja nasi.
  • 36:10 - 36:15
    Aliahidi kamwe
    hatatuacha au kututelekeza.
  • 36:15 - 36:23
    Aliahidi kuwa nasi kupitia yeyote yaletwayo na maisha na kutupa amani yake.
  • 36:23 - 36:34
    Ukikosa amani, suala si
    Mungu kuwa mbali na wewe.
  • 36:34 - 36:38
    Labda ni wewe kutokuwa karibu Naye.
  • 36:38 - 36:42
    Yuko pamoja nawe. Je, tuko pamoja Naye?
  • 36:42 - 36:53
    Je, tumeunganishwa Naye, tumejitoa Kwake, daima katika uhusiano wetu Naye?
  • 36:53 - 36:58
    "...Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi."
  • 36:58 - 37:01
    Aliahidi kuwa pamoja nasi.
  • 37:01 - 37:05
    Yeye yu pamoja nasi kupitia Neno Lake, kwa Roho Wake.
  • 37:05 - 37:13
    Lakini ikiwa hali yako inakunyima kupumzika,
    ni ishara kwamba una msongo wa kiroho.
  • 37:13 - 37:17
    Na sababu ya msongo wetu wa kiroho,
    napendekeza kwenu watu wa Mungu,
  • 37:17 - 37:23
    haiko mbali sana na yale tunayoruhusu mioyoni mwetu,
  • 37:23 - 37:25
    kile tunacholisha roho zetu.
  • 37:25 - 37:31
    Huu ni utiaji moyo wangu kwenu nyote leo - jihadharini na msongo wa kiroho
  • 37:31 - 37:39
    Ikiwa kitu kinakusumbua,
    acha kikushawishi kuomba.
  • 37:39 - 37:44
    Suala lolote - lipeleke kwa Mungu.
    Suala lolote - kipeleke kwenye maombi.
  • 37:44 - 37:48
    Hilo ndilo jibu. Hiyo ndiyo
    dawa ya wasiwasi, ya mashaka,
  • 37:48 - 37:52
    kwa zana za shetani zilikusudia kutenganisha mioyo yetu na Mungu.
  • 37:52 - 37:54
    Jibu - zirudishe Kwake.
  • 37:54 - 37:59
    Nenda kwenye maombi - utapata amani ipitayo akili zote
  • 37:59 - 38:03
    ambayo itakutegemeza katika hali hiyo.
  • 38:03 - 38:09
    Sio lazima uiondoe,
    bali ikutegemeze kupitia kwayo.
  • 38:09 - 38:17
    Nataka kuhitimisha ujumbe huu kwa kusisitiza tena na kuwakumbusha
  • 38:17 - 38:25
    kuhusu ushauri nilioutoa
    kutuingiza katika Mwaka Mpya wa 2024.
  • 38:25 - 38:29
    Mwishoni mwa ujumbe huo,
    nilitoa ushauri wa vitendo.
  • 38:29 - 38:34
    Kwa sababu tunasikia Neno na
    Neno hugusa mioyo yetu.
  • 38:34 - 38:35
    Kwa wengi wetu, tunaposikia ujumbe huu sasa,
  • 38:35 - 38:40
    dhamiri zetu zinathibitisha ukweli wa ujumbe huu.
  • 38:40 - 38:43
    'Ni kweli! Ninahitaji kuwa na maombi zaidi.
  • 38:43 - 38:45
    Ninahitaji kuwa makini zaidi katika uhusiano wangu na Mungu.
  • 38:45 - 38:48
    Ninahitaji kuwa mwangalifu kwa kile
    ninachozingatia.'
  • 38:48 - 38:58
    Nzuri. Sasa, hisia za ujumbe huu kwa wakati huu zitafifia hivi karibuni
  • 38:58 - 39:01
    na masuala ya maisha yanarudi haraka.
  • 39:01 - 39:06
    Kilicho muhimu sasa ni kujenga tabia za kimungu ambazo zitakusaidia
  • 39:06 - 39:11
    kwa sababu roho i radhi
    lakini mwili ni dhaifu.
  • 39:11 - 39:13
    Kwa hivyo, hapa kuna ushauri ambao
    ninataka kusisitiza tena.
  • 39:13 - 39:26
    Ninashauri kila mtu - nyumbani kwako,
    tenga mahali pa maombi.
  • 39:26 - 39:30
    Ninataka kusisitiza tena -
    maombi yanaweza kuwa popote.
  • 39:30 - 39:33
    Sisemi hapo ndipo
    mahali pekee unapoweza kusali
  • 39:33 - 39:36
    na hupaswi kuomba popote pengine. Hapana! Moyo wetu ni chumba cha maombi.
  • 39:36 - 39:40
    Hata ninapotoa ujumbe huu sasa hivi,
    tunapaswa kuomba, kuwa katika hali ya maombi.
  • 39:40 - 39:48
    Maombi hayatokani na eneo la asili, bali kuwa na mahali palipotengwa nyumbani kwako
  • 39:48 - 39:56
    kwa ajili ya maombi kunaweza kuwa chanzo kikuu cha kutia moyo
  • 39:56 - 40:04
    ili kutukumbusha kanuni hizi -
    kwa sababu mwili ni dhaifu.
  • 40:04 - 40:07
    Wakati mwingine suala limetokea.
  • 40:07 - 40:09
    Labda watoto wetu wamekosa adabu.
  • 40:09 - 40:12
    Tunachokozwa au hamakishwa.
  • 40:12 - 40:17
    Labda kumekuwa na changamoto kazini au habari mbaya imekuja.
  • 40:17 - 40:21
    Unaweza kujua pale moyo wako unapofadhaika.
  • 40:21 - 40:25
    Wakati mwingine unahitaji mahali fulani
    kwa nje ambapo unaweza kwenda
  • 40:25 - 40:29
    kuungana tena na Mungu,
    kuungana tena na Muumba wako,
  • 40:29 - 40:31
    rudisha moyo wako kwenye mambo ya Roho.
  • 40:31 - 40:34
    Na kisha unaenda na kukabiliana na chochote unachohitaji kukabiliana nacho.
  • 40:34 - 40:36
    Huiahirishi au kuichelewesha; unakabiliana nayo.
  • 40:36 - 40:39
    Lakini unakabiliana nayo kwa hali thabiti ya moyo.
  • 40:39 - 40:42
    Changamoto kuu ambayo
    wengi wetu tunakabiliana nayo leo
  • 40:42 - 40:47
    ni kwa sababu tunashughulikia masuala
    kutoka mahali pa fujo.
  • 40:47 - 40:51
    Moyo uliofadhaika ni mahali pa kuzaliwa
    kwa maamuzi mabaya.
  • 40:51 - 40:55
    Moyo wako ukifadhaika, moyo wako hauna amani;
  • 40:55 - 40:58
    unaweza kwa urahisi sana kuchukua hatua mbaya
  • 40:58 - 41:05
    kwa sababu umezidiwa na hisia, hali, uchochezi - yote uyajuayo.
  • 41:05 - 41:06
    Na tunachukua hatua mbaya.
  • 41:06 - 41:10
    Wakati mwingine, unahitaji kupiga hatua nyuma na kwenda mahali pako pa maombi.
  • 41:10 - 41:12
    Kuwa na nafasi katika nyumba yako
    iliyotengwa kwa ajili ya maombi.
  • 41:12 - 41:14
    Nenda ukaombe huko.
    Nendeni mkamwabudu Mungu.
  • 41:14 - 41:18
    Vaeni muziki wa kuabudu na kuabudu.
    Nendeni mkamshukuru Mungu!
  • 41:18 - 41:25
    Kumbuka nilichosema kuhusu shukrani.
    Usiruke tu moja kwa moja kwenye ombi.
  • 41:25 - 41:29
    Wakati fulani baada ya kutoa shukrani, hutahitaji hata kuombea suala hilo tena
  • 41:29 - 41:32
    kwa sababu shukrani imeweka upya mtazamo wako, imeweka upya moyo wako.
  • 41:32 - 41:39
    Na unajua - Mungu ambaye amefanya hivyo kabla atafanya tena. Yeye ni mwaminifu!
  • 41:39 - 41:44
    Huu ni ushauri wangu kwenu, watu wa Mungu,
    kuwaimarisha kiroho.
  • 41:44 - 41:47
    Adui hataacha kamwe
    kushambulia mioyo yetu.
  • 41:47 - 41:52
    Uwanja wa kweli wa vita uko ndani.
  • 41:52 - 41:56
    Basi linda moyo wako.
    Linda moyo wako.
  • 41:56 - 42:02
    Suala lolote, changamoto, shida -
    ipeleke kwa Mungu, ipeleke kwa maombi.
  • 42:02 - 42:11
    Huu ni utumainishaji wangu kwenu nyote siku ya leo, na tunamshukuru Mungu kwa Neno lake.
  • 42:11 - 42:15
    Tunamshukuru Mungu kwa nafasi hii ya kupokea Neno lake.
  • 42:15 - 42:26
    Na ninaamini Neno
    limeingia kwenye mioyo iliyo wazi,
  • 42:26 - 42:35
    mioyo ambayo iko tayari kutenda Neno na kulifanya litende kazi kama Mungu anavyolifanya kuwa zuri.
Title:
JINSI YA KUEPUKA MSONGO wa KIROHO! | Maneno ya kutia moyo pamoja na Kaka Chris
Description:

Ikiwa unatamani kukua katika uhusiano wako na Mungu, ujumbe huu ni kwa ajili yako! Jifunze kutoruhusu mfadhaiko wa kihisia au kimwili kuwa msongo wa kiroho unapotazama neno hili la kutia moyo kutoka kwa Kaka Chris lenye jina la ‘Jihadhari na Msongo wa Kiroho’.

➡️ Pata kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Saidia TV ya Moyo wa Mungu kifedha - https://godsheart.tv/financial/
➡️ Habari kuhusu Maombi Shirikishi - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live

more » « less
Video Language:
English
Team:
God's Heart TV
Duration:
43:05

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions