JINSI YA KUEPUKA MSONGO wa KIROHO! | Maneno ya kutia moyo pamoja na Kaka Chris
-
0:00 - 0:06Moyo wa maombi ni moyo wa amani
-
0:06 - 0:11lakini moyo usio na maombi ni moyo usiotulia.
-
0:13 - 0:22Neema na amani iwe kwenu nyote katika
jina la ajabu la Yesu Kristo. -
0:22 - 0:26Watu wa Mungu, ni baraka ya ajabu iliyoje
-
0:26 - 0:31kukuona umeunganishwa sasa hivi
kutoka kote ulimwenguni -
0:31 - 0:35kusikia Neno Hai la Mungu.
-
0:35 - 0:40Ndio maana tumekusanyika,
tumeunganishwa, tunatazama sasa hivi - -
0:40 - 0:42kupokea Neno la Mungu.
-
0:42 - 0:49Kwa sababu tunajua kwamba - bila kujali maswali ambayo maisha yanatupa,
-
0:49 - 0:56majibu yapo katika Neno la Mungu siku zote.
-
0:56 - 1:05Haijalishi uwongo ambao ulimwengu unachora karibu nawe, ukweli daima uko katika Neno la Mungu.
-
1:05 - 1:09Kwa hiyo leo tutazingatia Neno lake, tukizingatia Maandiko.
-
1:09 - 1:14Lakini bila shaka, tunaanza
na muda wa maombi. -
1:14 - 1:23Kwa hiyo watu wa Mungu, tuombe sasa hivi katika jina hilo kuu la Yesu Kristo.
-
1:23 - 1:36Bwana Yesu Kristo, tunakushukuru kwa neema hii ya ajabu kuwa katika uwepo wako.
-
1:36 - 1:48Acha nguvu ya Neno lako izungumze utulivu kwa kila moyo wenye shida.
-
1:48 - 1:59Acha nguvu za Neno Lako zivunje kila kizuizi kilichowekwa na mwanadamu.
-
1:59 - 2:16Utupe neema ya kuelewa Neno lako takatifu na kulitumia katika maisha yetu ya kila siku.
-
2:16 - 2:25Fungua mioyo yetu kwa ufunuo Wako
mtakatifu sasa hivi. -
2:25 - 2:31Katika jina kuu la Yesu Kristo tunaomba.
-
2:31 - 2:39Na watu wa Mungu wakasema, Amina!
-
2:39 - 2:42Asante, Yesu Kristo.
-
2:42 - 2:44Karibu tena, kila mtu.
-
2:44 - 2:48Karibuni watu wa Mungu katika Ibada ya Leo ya Kutia Moyo
-
2:48 - 2:53kutoka kwenye Studio ya God's Heart TV
hapa North Wales. -
2:53 - 3:01Na kama nilivyotaja katika utangulizi mdogo - maswali yoyote ambayo maisha yanatupa,
-
3:01 - 3:04majibu daima yako katika Neno la Mungu.
-
3:04 - 3:07Na hii ndio tunataka kufanya hivi sasa -
-
3:07 - 3:11tunataka kuchukua muda wa thamani kulipitia Neno la Mungu
-
3:11 - 3:16na usikie kile ambacho Mungu anatuambia leo kupitia Neno Lake, kwa Roho Wake.
-
3:16 - 3:22Kwa sababu kumbuka - nataka ujichunguze, maisha yako kwa muda.
-
3:22 - 3:25Hebu fikiria hili.
-
3:25 - 3:32Kiwango ambacho
hali za maisha zinakuelemea -
3:32 - 3:38inaonyesha kiwango ambacho
Neno la Mungu linakutawala. -
3:38 - 3:43Sisemi maswala, changamoto, hali za maisha sio sehemu ya safari yetu
-
3:43 - 3:47ikiwa tuko karibu na Mungu,
ikiwa Neno lake linatutawala. -
3:47 - 3:54Lakini majibu yako kwa hali hizo, masuala, changamoto
-
3:54 - 3:59ni taswira ya mahali ulipo kiroho.
-
3:59 - 4:10Ikiwa hali zinatuletea hofu, mashaka, kuomboleza, kunung'unika, kulalamika,
-
4:10 - 4:17wasiwasi au mashaka - angalia moyo wako.
-
4:17 - 4:22Hiyo ni taswira kwamba Neno la Mungu
haliutawala moyo wako. -
4:22 - 4:29Kwa hiyo tafadhali, watu wa Mungu, geuka pamoja nami kwenye kifungu cha uthibitisho cha ujumbe wa leo,
-
4:29 - 4:34ambayo imechukuliwa kutoka Wafilipi 4.
-
4:34 - 4:44Haya ni Maandiko ya ajabu!
Nitasoma kutoka Wafilipi 4:6-9. -
4:44 - 4:51Na nilipokuwa mahali pa maombi nikijiandaa kwa ajili ya ujumbe huu leo,
-
4:51 - 4:57Nilikumbuka ujumbe wa kutia moyo sana kutoka kwa Nabii TB Joshua, mshauri wangu.
-
4:57 - 5:01Alisema jambo ambalo nataka
ulizingatie kwa sababu litatusaidia -
5:01 - 5:02kupitia ujumbe wa leo.
-
5:02 - 5:15Alisema, “Unaweza kuwa na msongo wa mawazo. Unaweza kuwa na mkazo wa kihisia.
-
5:15 - 5:25Lakini tafadhali, usiwe na msongo wa kiroho.
-
5:25 - 5:37Kwa sababu ikiwa ndivyo, utapoteza mwelekeo kwa Mungu na kuanza kutafuta njia mbadala.”
-
5:37 - 5:40Ninataka kusema tena, watu wa Mungu.
-
5:40 - 5:43Unaweza kuwa na msongo wa kimwili.
-
5:43 - 5:49Iwe imeunganishwa na afya,
tumejifanyia kazi kupita kiasi, tumechoka -
5:49 - 5:53na miili yetu inaathirika -
tunaweza kuwa na msongo wa kimwili. -
5:53 - 5:55Tunaweza kuwa na msongo wa kihisia.
-
5:55 - 5:59Labda kuna mvutano au msongo katika mahusiano, mahali pa kazi - taja tu.
-
5:59 - 6:10Tunaweza kuwa na mfadhaiko wa kihisia,
lakini tafadhali usiwe na msongo wa kiroho -
6:10 - 6:18kwa sababu ukiwa hivyo, utapoteza mwelekeo kwa Mungu na kuanza kutafuta
-
6:18 - 6:24njia mbadala za binadamu, njia za mkato.
-
6:24 - 6:30Na nadhani ungekubaliana nami
kutokana na uzoefu wa maisha kwamba -
6:30 - 6:37jaribio lolote la kuchukua njia ya mkato
ili kuepuka mchakato wa Mungu -
6:37 - 6:41kwa kweli huishia kama 'njia ndefu'.
-
6:41 - 6:43Haifanyi kuwa fupi zaidi.
-
6:43 - 6:49Kwa kweli, bado unaishia kurudi pale ulipoanza
-
6:49 - 6:54kwa sababu mchakato wa Mungu ni muhimu.
-
6:54 - 6:57Hata ukipokea kitu
bila mchakato na Mungu, -
6:57 - 6:59haitaambatana na bidhaa za Mungu.
-
6:59 - 7:08Namaanisha nini? Unaweza kuwa na pesa bila mchakato wa Mungu lakini usiwe na amani.
-
7:08 - 7:11Mungu pekee ndiye anayeweza kutoa amani.
-
7:11 - 7:14Sasa, ninaposema 'msongo wa kiroho'...
tunakuja kwenye Maandiko haya. -
7:14 - 7:17Ninaposema 'msongo wa kiroho',
ninamaanisha nini? -
7:17 - 7:24Ninamaanisha nini ninaposema
'usiwe na msongo wa kiroho'? -
7:24 - 7:35Hali yako inapokukosesha raha, pumziko la ndani,
-
7:35 - 7:44ni ishara kwamba una msongo wa kiroho.
-
7:44 - 7:49Wakati changamoto yako, jaribio, shida, chochote kinaweza kuwa,
-
7:49 - 8:01vinapokuibia pumziko la ndani, amani ya moyo -
moyo wako unapusumbuka, kufadhaika - -
8:01 - 8:06ni ishara ya msongo wa kiroho.
-
8:06 - 8:13Wakati vita hiyo au mzigo huo
utakapoondoa macho yako kwa Yesu, -
8:13 - 8:16unapotenganisha moyo wako
na Yesu, kuwa mwangalifu. -
8:16 - 8:23Hiki ndicho kichwa cha ujumbe wa leo - 'Jihadhari na m=Msongo wa Kiroho'.
-
8:23 - 8:27Ikiwa una mtu karibu na wewe nyumbani anayetazama hii, mwambie tu,
-
8:27 - 8:31“Jihadhari na mkazo wa kiroho.”
-
8:31 - 8:39Moyo uliofadhaika ni mahali pa kuzaliwa
kwa maamuzi mabaya. -
8:39 - 8:44Sasa, twende kwenye Neno - Wafilipi 4.
-
8:44 - 8:49Naamini wengi wetu tunafahamu kifungu hiki;
ni kifungu maarufu sana. -
8:49 - 8:52Lakini ninataka kusisitiza ukweli fulani muhimu kutoka kwa kifungu hiki.
-
8:52 - 9:01Wafilipi 4:6 - "Msijisumbue kwa lolote..."
-
9:01 - 9:05Natumaini mnasikia Neno hili,
watu wa Mungu. -
9:05 - 9:13“Msijisumbue kwa neno lo lote, bali katika kila neno kwa kusali na kuomba,
-
9:13 - 9:24pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu;
-
9:24 - 9:35na amani ya Mungu...” - amani isiyo ya kawaida kutoka kwa Mungu asiye wa kawaida -
-
9:35 - 9:41“...na amani ya Mungu, ipitayo akili zote;
-
9:41 - 9:52itahifadhi mioyo yenu na nia zenu
kwa Kristo Yesu. -
9:52 - 9:57Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha;
-
9:57 - 10:02yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza;
-
10:02 - 10:05yo yote yenye sifa njema, kama kuna wema wo wote
-
10:05 - 10:12na ikiwa kuna sifa nzuri - yatafakarini hayo.
-
10:12 - 10:21Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea na kuyasikia na kuyaona kwangu, yafanyeni…”
-
10:21 - 10:25Sio tu 'Yasemeni haya' lakini "yafanyeni haya" -
iweke katika vitendo. -
10:25 - 10:32"...na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi."
-
10:32 - 10:35Asante, Yesu, kwa
Neno Hai la Mungu. -
10:35 - 10:42Ninataka tu kupitia Maandiko haya hatua kwa hatua na kutumia Maandiko haya
-
10:42 - 10:48kama msingi wa kuhimiza kila mmoja wenu aliyeungana nasi hivi sasa
-
10:48 - 10:50kutoka kwenye Neno la Mungu.
-
10:50 - 11:03Kuanza, mstari wa sita unasema hivi:
“Msijisumbue kwa lolote.” -
11:03 - 11:08Ninapenda jinsi taarifa hiyo ilivyo moja kwa moja.
-
11:08 - 11:13Maandiko hapa hayaweki daraja
kiwango cha hali yako. -
11:13 - 11:17'Sawa, ikiwa kuna jambo hapa, unaweza kuwa na wasiwasi kidogo kuhusu hilo.
-
11:17 - 11:21Au ikiwa kuna jambo katika kazi yako,
ambayo inatoa nafasi kwa wasiwasi kidogo.' -
11:21 - 11:24Hapana - hakuna kilichoachwa hapa.
-
11:24 - 11:30Inasema, "Msijisumbue kwa kitu chochote."
-
11:30 - 11:35Maandiko haya si pendekezo tu;
ni maagizo. Ni wazi sana. -
11:35 - 11:41Kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyosema kwa usawa katika Mathayo 6:25-mwisho,
-
11:41 - 11:46'Usijali kuhusu maisha yako.
Msiwe na wasiwasi juu ya kesho.' -
11:46 - 11:50Ni maagizo ya wazi.
-
11:50 - 11:56"Msiwe na wasiwasi juu ya kitu chochote."
-
11:56 - 12:12Hakuna suala maishani ambapo wasiwasi ni jibu linalofaa au jibu sahihi. Hakuna.
-
12:12 - 12:18Nimezungumza na watu wengine hapo awali na hili ni jambo ambalo wengi wetu hufanya -
-
12:18 - 12:25tunaangalia hali zetu wenyewe na kuhitimisha kwamba zinapaswa kufikia kiwango tofauti.
-
12:25 - 12:28Watu walikuwa wakiniambia kwenye
simu ninapozungumza nao, -
12:28 - 12:32'Angalia, kaka Chris, ninaelewa unachosema lakini hujui hali yangu.
-
12:32 - 12:34Hujui jinsi hali yangu ilivyo mbaya.
-
12:34 - 12:38Hujui uzito
wa changamoto yangu.' -
12:38 - 12:39Nakubaliana nawe!
-
12:39 - 12:44Labda sijui, lakini haibadilishi ukweli wa kile Mungu anachokuambia leo
-
12:44 - 12:49kupitia Neno Lake -
'Msijisumbue kwa neno lolote.' -
12:49 - 12:53“Msijisumbue kwa lolote.”
-
12:53 - 13:00Hakuna eneo la kijivu huko;
ni wazi sana. -
13:00 - 13:09Ikiwa hali yako inakufanya uwe na wasiwasi,
-
13:09 - 13:15inapendekeza uko kwenye
njia mbaya kiroho. -
13:15 - 13:21Weka hilo moyoni mwako tunaposogea
kwenye hatua inayofuata katika mstari huu. -
13:21 - 13:27"Msijisumbue kwa lolote ila katika kila jambo..."
-
13:27 - 13:31Natumai utazingatia
hilo tena - kila kitu. -
13:31 - 13:36Hakuna kiwango kwa hali tofauti.
-
13:36 - 13:41Hakuna mabadiliko katika Neno la Mungu kulingana na kiwango cha jinsi tunavyohisi
-
13:41 - 13:45hali yetu ni mbaya - hapana!
Neno la Mungu liko wazi. -
13:45 - 13:51“...bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru;
-
13:51 - 13:57haja zenu na zijulikane kwa Mungu…”
-
13:57 - 14:10Dawa ya wasiwasi iko wazi sana -
peleka hali yako kwa Mungu katika maombi. -
14:10 - 14:13Hili ndilo jibu, watu wa Mungu.
-
14:13 - 14:19Kuwa na afya nzuri kiroho hakuondoi ukweli wa jambo.
-
14:19 - 14:24Unaweza kuhudhuria ibada nzuri za kanisa,
-
14:24 - 14:28kuwa sehemu ya kanisa hai ambapo unapokea Neno la Mungu kila juma
-
14:28 - 14:30nakupokea maombi katika
nguvu za Roho Mtakatifu. -
14:30 - 14:34Labda umekuwa ukihudhuria Huduma za Maombi Shirikishi kwenye TV ya Moyo wa Mungu.
-
14:34 - 14:36Utukufu ni kwa Mungu!
-
14:36 - 14:40Asante Mungu kwa kuweka moyoni mwako kuwa sehemu ya jumuiya hii ya ajabu ya waumini.
-
14:40 - 14:46Lakini hiyo haibadilishi
uhalisi wa hali za maisha. -
14:46 - 14:54Hali zitakuja, changamoto zitakuja, masuala ya maisha yatakuja kwa kila mtu.
-
14:54 - 14:57Lakini jibu liko wazi katika Neno la Mungu.
-
14:57 - 15:09Usijisumbue kwa lolote ila katika kila jambo - mpe Mungu, peleka kwenye maombi
-
15:09 - 15:11Ni wazi sana!
-
15:11 - 15:24Shida ikigonga kwenye moyo wako,
acha ikuongoze kuomba. -
15:24 - 15:28Ikiwa hali yako inakusukuma kuomba,
-
15:28 - 15:32shetani hawezi kuitumia kuutenganisha moyo wako na Mungu
-
15:32 - 15:36na kukupeleka mahali penye msongo wa kiroho.
-
15:36 - 15:39Hii ndiyo nia yake. Hili ndilo lengo lake.
-
15:39 - 15:44Anataka kutenganisha mioyo yetu na Mungu,
-
15:44 - 15:50ili mioyo yetu ifadhaike, ihangaishwe, ielemewe.
-
15:50 - 15:55Na katika hali kama hiyo ya moyo,
tunaweza kufanya kosa kwa urahisi, -
15:55 - 16:00kutenda kwa urahisi kutokana na mihemko,
kuitikia uchokozi, -
16:00 - 16:06kutedenda kupitia lenzi ya kosa au kutenda kwa macho ya chuki - na mengine iyajuayo.
-
16:06 - 16:09Anataka moyo wako usumbuke.
Angalia mstari unaofuata. -
16:09 - 16:12Hebu nirukie mstari unaofuata katika hatua hii.
-
16:12 - 16:15"...na amani ya Mungu..."
-
16:15 - 16:18Unapopeleka hali yako kwa Mungu katika maombi, matokeo yake ni nini?
-
16:18 - 16:24“...na amani ya Mungu, ipitayo akili zote;
-
16:24 - 16:36itailinda mioyo yenu na nia zenu [kupitia] Kristo Yesu.”
-
16:36 - 16:39Uwanja wa kweli wa vita si kwa nje.
-
16:39 - 16:45Uwanja wa kweli wa vita ni moyo.
-
16:45 - 16:52Ibilisi anataka kuhamisha usikivu wetu,
mwelekeo wetu, nguvu zetu, maslahi yetu -
16:52 - 16:54kuje nje, kwennye mwili -
-
16:54 - 17:07kwa hivyo tunaishia kumaliza muda, umakini na rasilimali katika kutafuta vita vibaya.
-
17:07 - 17:16Uwanja wa kweli wa vita ni moyo -
kutunza mioyo yetu, kulinda mioyo yetu. -
17:16 - 17:19Na Maandiko yako wazi kabisa.
-
17:19 - 17:27Hali yako inapokusukuma kuomba, amani ya Mungu itaulinda moyo wako.
-
17:27 - 17:32Sio lazima kusema amani ya Mungu itabadilisha hali yako
-
17:32 - 17:33au kuondoa changamoto hiyo.
-
17:33 - 17:36Baadhi ya hali, lazima tuzipitie.
-
17:36 - 17:44Lakini kwa amani ya Mungu tutapita kati yake bila kutulemea.
-
17:44 - 17:51kutupotosha au kutupeleka
mahali nje ya imani yetu. -
17:51 - 17:55"... amani ya Mungu, ipitayo akili zote..."
-
17:55 - 17:59Ninasema nini hapa watu wa Mungu?
-
17:59 - 18:06Moyo wa maombi ni moyo wa amani
-
18:06 - 18:15lakini moyo usio na maombi ni moyo usiotulia.
-
18:15 - 18:17Nitasema tena - moyo wa maombi
ni moyo wenye amani -
18:17 - 18:23Nitasema tena - moyo wa maombi
ni moyo wenye amani -
18:23 - 18:29lakini moyo usio na maombi ni moyo usiotulia.
-
18:29 - 18:30lakini moyo usio na maombi ni moyo usiotulia.
-
18:30 - 18:36Shida ya kweli ni shida iliyo ndani,
sio ile inayokuzunguka, -
18:36 - 18:39sio hali ya nje.
-
18:39 - 18:46Shida ya kweli iko ndani - moyoni.
-
18:46 - 18:56Ndiyo maana ni lazima tuone chochote
tunachokabiliana nacho kama sababu ya kuomba. -
18:56 - 19:04Ikiwa hali yako inakusukuma kuomba, wewe ni zaidi ya mshindi kupitia Kristo.
-
19:04 - 19:08Lakini ikiwa hali yako inakufanya uogope,
-
19:08 - 19:14au hali yako inakufanya uwe na wasiwasi, ujilinganishe na wengine,
-
19:14 - 19:22uanze kujihurumia, ujipime kwa viwango vyako vya kibinadamu,
-
19:22 - 19:28au hali yako inakusukuma kukata tamaa,
-
19:28 - 19:36kutafuta njia mbadala, kutafuta njia ya suluhu kwa njia zote zinazowezekana katika asili -
-
19:36 - 19:45inaonyesha mioyo yetu haiko
mahali pazuri pamoja na Mungu. -
19:45 - 19:52Ambapo shida yako inakusukuma ni onyesho la mahali ulipo kiroho.
-
19:52 - 19:55Mwelekeo ambao shida yako inakuchukua -
-
19:55 - 19:58Je, inakurudisha kwa Mungu,
unakupelekea upige magoti? -
19:58 - 20:05Au inakupeleka kwenye chaguzi nyingine
nje ya Mungu? -
20:05 - 20:10Sijui ikiwa umegundua kuwa mara nyingi shida inapotokea katika maisha yetu,
-
20:10 - 20:14tunajaribu kwanza kulitatua sisi wenyewe
kabla hatujaja kwa Mungu. -
20:14 - 20:17Ni baada ya kumaliza
juhudi zetu wenyewe za kibinadamu - -
20:17 - 20:20'Haya! Hili ni zaidi yangu!
Acha niende kwa Mungu.' -
20:20 - 20:23Hiyo sio njia ambayo
Maandiko yanatuambia hapa. -
20:23 - 20:27Katika kila hali - ipeleke kwa Mungu kwa maombi.
-
20:27 - 20:29Sasa, nataka mzingatie jambo hili.
-
20:29 - 20:38Wengi wetu huenda moja kwa moja kwenye maombi
na kuruka shukrani. Hapana! -
20:38 - 20:43Maandiko yanasema nini?
-
20:43 - 20:49"Msijisumbue kwa neno lo lote, bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru..."
-
20:49 - 20:52Kwa nini ninasisitiza hilo, watu wa Mungu?
-
20:52 - 20:55Kwa sababu hii ni silaha
aliyotupa Yesu Kristo, -
20:55 - 20:59silaha ambayo Mungu ametupa ambayo
wengi wetu hatuitumii. -
20:59 - 21:03Wakati mwingine changamoto huja
na tunalemewa sana -
21:03 - 21:06kwa sababu tunaangazia
ukubwa wa changamoto hiyo. -
21:06 - 21:09Haijalishi changamoto yako ni kubwa kiasi gani,
si kubwa kuliko Mungu. -
21:09 - 21:16Wakati mwingine unahitaji kuchukua hatua nyuma na fikiria tu hii.
-
21:16 - 21:21Fikiria kile ambacho Mungu amekufanyia.
-
21:21 - 21:24Fikiria kile Mungu amefanya ndani yako.
-
21:24 - 21:27Fikiria kile Mungu amefanya kupitia wewe.
-
21:27 - 21:31Na mashaka yako yataondoka.
-
21:31 - 21:35Tafakari wema wa Mungu katika maisha yako.
-
21:35 - 21:41Kila mtu hapa, kila mtu aliyeunganishwa
na huduma hii sasa hivi, -
21:41 - 21:44hata kwa wakati huu ninapozungumza,
chukua tu muda kufikiria nyuma -
21:44 - 21:47juu ya wema wa Mungu katika maisha yako.
-
21:47 - 21:53Sisi sote tuna ushuhuda wa jinsi Mungu alivyotukomboa, jinsi alivyotuokoa,
-
21:53 - 21:59jinsi alivyoingilia kati kimiujiza katika hali hiyo, jinsi alivyotuhifadhi.
-
21:59 - 22:04Sisi sote tunatembea, tunaishi,
ni shuhuda zinazopumua. -
22:04 - 22:15Na kukumbuka rekodi ya Mungu ni silaha ya kushinda uwongo wa mashaka.
-
22:15 - 22:22Kwa sababu mashaka huzingatia tu kile kinachoonekana - ukubwa wa hali hiyo,
-
22:22 - 22:28watu wanasema nini kuhusu hali hiyo, maoni ya wengine kuhusu hali hiyo.
-
22:28 - 22:31Haya ndiyo mambo yanayojenga wasiwasi.
-
22:31 - 22:34Chukua hatua nyuma.
-
22:34 - 22:37Fikiri juu ya wema wa Mungu.
-
22:37 - 22:40Thamini wema wa Mungu.
-
22:40 - 22:42Tambua wema wa Mungu.
-
22:42 - 22:53Hii ni dawa bora ya udanganyifu wa wasiwasi na upoozaji wa hofu.
-
22:53 - 23:04Shukrani, shukrani - ni silaha ya ajabu namna gani, ambayo wengi wetu hatutumii.
-
23:04 - 23:08Kwa sababu katika joto la sasa,
hali inapojitokeza, -
23:08 - 23:12tatizo linapokuja,
tunazidiwa kwa urahisi. -
23:12 - 23:14Kwanini ni hivyo?
-
23:14 - 23:17Hapa ndipo ninapoenda katika
aya inayofuata, watu wa Mungu. -
23:17 - 23:22Ninataka kuunganisha sehemu hizi mbili
kwa uwazi sana. -
23:22 - 23:28Maandiko hayo katika Wafilipi 4:8 - ikiwa umelelewa katika nyumba ya Kikristo,
-
23:28 - 23:32unafundishwa mstari huo kutoka
shule ya Jumapili; tunaijua vizuri sana. -
23:32 - 23:38"Mambo yo yote yaliyo ya haki, safi, ya heshima, bora, yenye kupendeza, yenye kusifiwa -
-
23:38 - 23:39fikiri juu ya mambo haya.'
-
23:39 - 23:50Lakini angalia mistari inayotangulia maneno hayo yenye nguvu ambayo tumetoka kusoma.
-
23:50 - 24:04Ikiwa sisi ni waaminifu, kile tunacholisha roho zetu ndicho chanzo cha msongo wetu wa kiroho.
-
24:04 - 24:07Nitasema tena.
-
24:07 - 24:15Ikiwa sisi ni watu wa Mungu wanyoofu,
tunalisha roho zetu; -
24:15 - 24:26kile tunachozingatia
ndicho kitu hasa kinachotunyima pumziko. -
24:26 - 24:39Acha kulalamikia madhara ya sumu unayojilisha nayo.
-
24:39 - 24:45“Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha;
-
24:45 - 24:52yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza;
-
24:52 - 24:54mambo yoyote yenye sifa njema,
ukiwapo wema wo wote na -
24:54 - 24:59ikiwa kuna jambo lo lote la kusifiwa -
yatafakarini hayo.” -
24:59 - 25:06Wengi wetu leo tunazingatia,
-
25:06 - 25:14tunalisha roho zetu vitu vichafu, visivyo haki,
-
25:14 - 25:19mambo yasiyopendeza,
mambo yenye sifa mbaya; -
25:19 - 25:23mambo ambayo hakuna fadhila.
-
25:23 - 25:31Na tunashangaa kwa nini tunaanguka katika msongo wa kiroho mbele ya majitu yetu.
-
25:31 - 25:36Kwa sababu tunatoa uangalifu wetu, tunalisha mioyo yetu na mambo yasiyofaa.
-
25:36 - 25:40Kama Wakristo, tunapaswa kuwa waangalifu.
-
25:40 - 25:44Kumbuka kichwa cha ujumbe huu: 'Jihadhari na Msongo wa Kiroho'.
-
25:44 - 25:51Ikiwa hali yako inakufanya uwe na wasiwasi, angalia ni nini unaIlisha roho yako.
-
25:51 - 26:00Ikiwa changamoto yako inakufanya uwe na wasiwasi, angalia kile unachokizingatia.
-
26:00 - 26:03Ikiwa shida yako, inaweza kuwa chochote kile -
-
26:03 - 26:08kuwa Mkristo hakuondoi ukweli wa changamoto hizi -
-
26:08 - 26:16vyovyote iwavyo, ikiwa hali hiyo inakufanya ukate tamaa au uvunjike moyo,
-
26:16 - 26:22angalia kile unachoupatia moyo wako.
-
26:22 - 26:26Uko vile kulingana na unachokizingatia.
-
26:26 - 26:29Wakristo, tunapaswa kuwa waangalifu.
-
26:29 - 26:32Kuwa makini na kile unachotazama.
-
26:32 - 26:36Kuwa mwangalifu kwa kile unachosikia, sikiliza.
-
26:36 - 26:39Kuwa makini na unachosoma.
-
26:39 - 26:45Kwa sababu haya huathiri mawazo yako.
-
26:45 - 26:51Na vile mtu aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. ( Mithali 23:7 )
-
26:51 - 27:01Ikiwa tunalisha mioyo yetu mambo yasiyopatana na Neno la Mungu,
-
27:01 - 27:10usishangae kwamba mwitikio wako kwa majaribu ya maisha haupatani na Neno la Mungu.
-
27:10 - 27:20Nakumbuka wimbo wa zamani sana ambao tulifundishwa tukiwa watoto katika shule ya Jumapili.
-
27:20 - 27:23Sitakuimbia, usijali! Nitakupa tu maandishi.
-
27:23 - 27:26Mstari mmoja wa wimbo huu unasema,
-
27:26 - 27:35'Pale ukitoacho kinapozidi unachokiingiza, basi uhifadhi wako ndio utakuwa anguko lako.'
-
27:35 - 27:40Sasa, huu ni wimbo wa watoto
lakini ni ujumbe mzito sana. -
27:40 - 27:46'Wakati ukitoacho kinapozidi unachokiingiza, basi uhifadhi wako ndio utakuwa anguko lako.'
-
27:46 - 27:52Ikiwa unalisha mwili wako kuliko unavyolisha roho yako,
-
27:52 - 27:56usishangae
msongo wa kiroho unapotokea. -
27:56 - 28:03Ikiwa unalisha akili zako zaidi ya moyo wako,
-
28:03 - 28:14usishangae msongo wa kiroho unaposhambulia - moyo wenye shida, fadhaa, uliofadhaika.
-
28:14 - 28:22Na kama nilivyowaambia, watu wa Mungu - maisha yetu wenyewe ni kioo, mfano wa hii.
-
28:22 - 28:29Sisi sote tunaotazama sasa hivi, ikiwa hali itatokea na unaitikia kwa hisia
-
28:29 - 28:34katika wakati huo, jiangalie -
95% ya wakati unajutia majibu hayo. -
28:34 - 28:37Baadaye unasema, 'Lo, kwa nini nilisema hivyo?
-
28:37 - 28:41Kwa nini nilienda mbali sana?
Kwa nini niliitikia hivi?' -
28:41 - 28:48Unapaswa kuanza kuvipanga pamoja vipande ambavyo maafa yamesababishwa
-
28:48 - 28:54kwa mwitikio wako uliopitiliza kwa sababu
ya mhemuko, hisia. -
28:54 - 29:00Hiyo ni onyesho la kile
unalisha nacho moyo wako. -
29:00 - 29:05Ikiwa mnailisha mioyo yenu mambo yasiyopatana na Neno la Mungu,
-
29:05 - 29:12kuna madhara yake - inaweza kusababisha kwa urahisi msongo wa kiroho, kubadilisha malengo yako.
-
29:12 - 29:17Vita yako, mzigo wako unakuondoa
kutoka kwa Yesu. -
29:17 - 29:21Hii ndiyo sababu nilisema, watu wa Mungu,
jihadharini na msongo wa kiroho. -
29:21 - 29:27Nilikuwa nikizungumza na wanandoa kwa simu hivi majuzi, nikiwapa neno la ushauri.
-
29:27 - 29:31Ninakupa tu mfano huu mdogo kuelezea kile ninachokizungumza.
-
29:31 - 29:37Nilikuwa nikizungumza na wanandoa na mume alikuwa akilalamika kuhusu mke wake.
-
29:37 - 29:43Alisema, 'Yeye ni wa kushangaza sana! Kitu chochote kidogo kinachotokea nyumbani -
-
29:43 - 29:46inakuwa tatizo kubwa kama nini.'
-
29:46 - 29:48Na wanaanza kusimulia
maswala yote ya zamani. -
29:48 - 29:51Kila kitu kinaonekana kuwa kama mchezo wa kuigiza.
-
29:51 - 29:55Nami nikawasikiliza na kusema,
'Naweza kumwuliza mkeo? -
29:55 - 30:01Niambie, madam - ni mambo gani unayopenda au tabia, ni aina gani ya mambo unayozingatia?'
-
30:01 - 30:10Na alisema ana uraibu wa kutazama michezo ya kuigiza , tamthilia kwenye runinga.
-
30:10 - 30:18Ndipo nikasema, Vema, bwana, usishangae kama mkeo amegeuza shida yake kuwa mchezo wa kuigiza
-
30:18 - 30:23wakati anaulisha moyo wake kwa mchezo wa kuigiza.'
-
30:23 - 30:29Unaweza kuangalia na kusema ni hoja ndogo lakini ninatoa mfano wa vitendo.
-
30:29 - 30:32Unatilia maanani
kwa mambo ambayo ni njozi. -
30:32 - 30:35Drama si halisi; sio ukweli.
-
30:35 - 30:38Na kwa sababu unazingatia sana mchezo wa kuigiza,
-
30:38 - 30:40changamoto zinapotokea katika maisha yako,
-
30:40 - 30:44unaona ni fursa ya kutengeneza drama hiyo nyumbani kwako.
-
30:44 - 30:53Na hii ni hatari kwa sababu msingi wetu ni Neno la Mungu.
-
30:53 - 30:59Ni lazima tuwe waangalifu kwa kile tunachoipatia mioyo yetu, kile tunachozingatia,
-
30:59 - 31:04kile tunacholisha roho zetu.
-
31:04 - 31:05Huo ulikuwa ni mfano mdogo tu.
-
31:05 - 31:12Najua baadhi yetu wanaweza au wasihusiane kwa njia tofauti - lakini nyote mnaweza kujiangalia.
-
31:12 - 31:14Hakuna anayejua moyo wako kuliko wewe.
-
31:14 - 31:19Ikiwa unazingatia mambo yasiyofaa, niambie hali ya moyo wako.
-
31:19 - 31:22Moyo wako unaweza kufadhaika kwa urahisi.
-
31:22 - 31:26Unatazama kitu ambacho unajua kama Mkristo hutakiwi kutazama.
-
31:26 - 31:31Hakuna mtu anayeweza kukuona ukiitazama lakini moyo wako unajua kuwa umeitazama. Kwa nini?
-
31:31 - 31:39Moyo wako unataabishwa,
unahamakishwa, unafadhaishwa. -
31:39 - 31:45Na hakuna dawa kwa moyo uliofadhashwa nje ya Kristo.
-
31:45 - 31:50Moyo wako ukifadhaika, ungana tena na Muumba wako. Hiyo ndiyo njia pekee.
-
31:50 - 31:53Hakuna kiasi cha pesa kinaweza
kununua amani ya moyo. -
31:53 - 31:57Hakuna kiasi cha sifa kinachoweza
kupata amani ya moyo. -
31:57 - 32:00Kuna baadhi ya vitu Mungu pekee anaweza kutoa.
-
32:00 - 32:13Waebrania 4:3 inasema kwamba moyo wako ukiamini kweli, unaingia katika raha.
-
32:13 - 32:16Hiyo ndiyo ahadi ya Mwenyezi Mungu kwetu sisi waaminio.
-
32:16 - 32:22kuwa na amani ndani bila kujali
dhoruba nje. -
32:22 - 32:30Ukiweka shida zako mikononi mwa Mungu,
-
32:30 - 32:34Ataweka amani yake mioyoni mwenu.
-
32:34 - 32:44Katika Marko 4, tunaijua hii hadithi wakati Yesu alipokuwa kwenye dhoruba ndani ya mashua.
-
32:44 - 32:50Yesu alikuwa mtulivu katika dhoruba
kabla hajatuliza dhoruba. -
32:50 - 32:53Hiyo ndiyo ahadi ya Mungu
kwenye maisha yetu kama Wakristo - -
32:53 - 32:59si kuondolewa kwa dhoruba au kutokuwepo kwa dhoruba, lakini utulivu ndani ya dhoruba.
-
32:59 - 33:08Ni utulivu ndani, moyoni. Hivi ndivyo Mungu ametuahidi.
-
33:08 - 33:11Narudia tena watu wa Mungu.
-
33:11 - 33:19Ikiwa hali yako inakufanya uwe na wasiwasi, angalia ni nini unalisha roho yako.
-
33:19 - 33:22Angalia kile unachokizingatia.
-
33:22 - 33:33Angalia ni nini kinachoathiri mawazo yako kwa sababu hakuna mtu aliye juu ya ushawishi.
-
33:33 - 33:33Angalia ni nini kinachoathiri mawazo yako kwa sababu hakuna mtu aliye juu ya ushawishi.
-
33:33 - 33:40Neno la ushauri - usiyumbishwe
-
33:40 - 33:47na maoni ya watu
wasioshikilia maisha yako ya baadaye. -
33:47 - 33:53Usikengeushwe na maoni ya watu ambao hawaainishi hatima yako.
-
33:53 - 34:00Kila mtu ana maoni.
Si kila mtu ana hekima. -
34:00 - 34:04Acha nikusomee Wafilipi 4:9.
-
34:04 - 34:14“Mambo mliyojifunza na kuyapokea na kuyasikia na kuyaona kwangu;
-
34:14 - 34:24yafanyeni haya...” - Nimeipenda hii, watu wa Mungu!
Ninapenda kauli hii! -
34:24 - 34:29Sisi ni kile tunachofanya,
si tu kile tunachosema. -
34:29 - 34:39Matunda yetu ni utangulizi bora wa imani yetu na maelezo bora ya imani yetu.
-
34:39 - 34:53Matunda yako - upendo, furaha, amani, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi,
-
34:53 - 34:59"Kwa matunda yao tutawatambua." ( Mathayo 7:20 )
-
34:59 - 35:04Kwa nini ninasisitiza hili?
Kwa sababu Mtume Paulo anasema hapa, -
35:04 - 35:08'Angalia, mambo uliyoyasikia,
yale ambayo umesoma hapo sasa -yatendeni.' -
35:08 - 35:14Kitendo huongea zaidi kuliko maneno.
-
35:14 - 35:17Ukienda kanisani,
unahudhuria kanisani, -
35:17 - 35:20na kisha baada ya kanisa
unarudi kusengenya, -
35:20 - 35:24usitegemee amani itawale moyoni mwako.
-
35:24 - 35:27Kutoka kanisani hadi kwenye uchoyo - usitarajie amani.
-
35:27 - 35:31Kutoka kanisani hadi kwenye tamaa - usitarajie amani.
-
35:31 - 35:37Kwenda kanisani
hakutufanyi sisi kuwa Wakristo - -
35:37 - 35:43si zaidi ya kuvaa shati la mpira wa miguu
wa Manchester United, -
35:43 - 35:48haimaanishi kuwa nachezea
Manchester United. -
35:48 - 35:59Ni tendo letu, tabia yetu inayoshuhudia ukweli wa maungamo yetu.
-
35:59 - 36:05'Yafanyeni haya, na
Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.' -
36:05 - 36:10Hii ndiyo ahadi ya Mungu.
Aliahidi kuwa pamoja nasi. -
36:10 - 36:15Aliahidi kamwe
hatatuacha au kututelekeza. -
36:15 - 36:23Aliahidi kuwa nasi kupitia yeyote yaletwayo na maisha na kutupa amani yake.
-
36:23 - 36:34Ukikosa amani, suala si
Mungu kuwa mbali na wewe. -
36:34 - 36:38Labda ni wewe kutokuwa karibu Naye.
-
36:38 - 36:42Yuko pamoja nawe. Je, tuko pamoja Naye?
-
36:42 - 36:53Je, tumeunganishwa Naye, tumejitoa Kwake, daima katika uhusiano wetu Naye?
-
36:53 - 36:58"...Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi."
-
36:58 - 37:01Aliahidi kuwa pamoja nasi.
-
37:01 - 37:05Yeye yu pamoja nasi kupitia Neno Lake, kwa Roho Wake.
-
37:05 - 37:13Lakini ikiwa hali yako inakunyima kupumzika,
ni ishara kwamba una msongo wa kiroho. -
37:13 - 37:17Na sababu ya msongo wetu wa kiroho,
napendekeza kwenu watu wa Mungu, -
37:17 - 37:23haiko mbali sana na yale tunayoruhusu mioyoni mwetu,
-
37:23 - 37:25kile tunacholisha roho zetu.
-
37:25 - 37:31Huu ni utiaji moyo wangu kwenu nyote leo - jihadharini na msongo wa kiroho
-
37:31 - 37:39Ikiwa kitu kinakusumbua,
acha kikushawishi kuomba. -
37:39 - 37:44Suala lolote - lipeleke kwa Mungu.
Suala lolote - kipeleke kwenye maombi. -
37:44 - 37:48Hilo ndilo jibu. Hiyo ndiyo
dawa ya wasiwasi, ya mashaka, -
37:48 - 37:52kwa zana za shetani zilikusudia kutenganisha mioyo yetu na Mungu.
-
37:52 - 37:54Jibu - zirudishe Kwake.
-
37:54 - 37:59Nenda kwenye maombi - utapata amani ipitayo akili zote
-
37:59 - 38:03ambayo itakutegemeza katika hali hiyo.
-
38:03 - 38:09Sio lazima uiondoe,
bali ikutegemeze kupitia kwayo. -
38:09 - 38:17Nataka kuhitimisha ujumbe huu kwa kusisitiza tena na kuwakumbusha
-
38:17 - 38:25kuhusu ushauri nilioutoa
kutuingiza katika Mwaka Mpya wa 2024. -
38:25 - 38:29Mwishoni mwa ujumbe huo,
nilitoa ushauri wa vitendo. -
38:29 - 38:34Kwa sababu tunasikia Neno na
Neno hugusa mioyo yetu. -
38:34 - 38:35Kwa wengi wetu, tunaposikia ujumbe huu sasa,
-
38:35 - 38:40dhamiri zetu zinathibitisha ukweli wa ujumbe huu.
-
38:40 - 38:43'Ni kweli! Ninahitaji kuwa na maombi zaidi.
-
38:43 - 38:45Ninahitaji kuwa makini zaidi katika uhusiano wangu na Mungu.
-
38:45 - 38:48Ninahitaji kuwa mwangalifu kwa kile
ninachozingatia.' -
38:48 - 38:58Nzuri. Sasa, hisia za ujumbe huu kwa wakati huu zitafifia hivi karibuni
-
38:58 - 39:01na masuala ya maisha yanarudi haraka.
-
39:01 - 39:06Kilicho muhimu sasa ni kujenga tabia za kimungu ambazo zitakusaidia
-
39:06 - 39:11kwa sababu roho i radhi
lakini mwili ni dhaifu. -
39:11 - 39:13Kwa hivyo, hapa kuna ushauri ambao
ninataka kusisitiza tena. -
39:13 - 39:26Ninashauri kila mtu - nyumbani kwako,
tenga mahali pa maombi. -
39:26 - 39:30Ninataka kusisitiza tena -
maombi yanaweza kuwa popote. -
39:30 - 39:33Sisemi hapo ndipo
mahali pekee unapoweza kusali -
39:33 - 39:36na hupaswi kuomba popote pengine. Hapana! Moyo wetu ni chumba cha maombi.
-
39:36 - 39:40Hata ninapotoa ujumbe huu sasa hivi,
tunapaswa kuomba, kuwa katika hali ya maombi. -
39:40 - 39:48Maombi hayatokani na eneo la asili, bali kuwa na mahali palipotengwa nyumbani kwako
-
39:48 - 39:56kwa ajili ya maombi kunaweza kuwa chanzo kikuu cha kutia moyo
-
39:56 - 40:04ili kutukumbusha kanuni hizi -
kwa sababu mwili ni dhaifu. -
40:04 - 40:07Wakati mwingine suala limetokea.
-
40:07 - 40:09Labda watoto wetu wamekosa adabu.
-
40:09 - 40:12Tunachokozwa au hamakishwa.
-
40:12 - 40:17Labda kumekuwa na changamoto kazini au habari mbaya imekuja.
-
40:17 - 40:21Unaweza kujua pale moyo wako unapofadhaika.
-
40:21 - 40:25Wakati mwingine unahitaji mahali fulani
kwa nje ambapo unaweza kwenda -
40:25 - 40:29kuungana tena na Mungu,
kuungana tena na Muumba wako, -
40:29 - 40:31rudisha moyo wako kwenye mambo ya Roho.
-
40:31 - 40:34Na kisha unaenda na kukabiliana na chochote unachohitaji kukabiliana nacho.
-
40:34 - 40:36Huiahirishi au kuichelewesha; unakabiliana nayo.
-
40:36 - 40:39Lakini unakabiliana nayo kwa hali thabiti ya moyo.
-
40:39 - 40:42Changamoto kuu ambayo
wengi wetu tunakabiliana nayo leo -
40:42 - 40:47ni kwa sababu tunashughulikia masuala
kutoka mahali pa fujo. -
40:47 - 40:51Moyo uliofadhaika ni mahali pa kuzaliwa
kwa maamuzi mabaya. -
40:51 - 40:55Moyo wako ukifadhaika, moyo wako hauna amani;
-
40:55 - 40:58unaweza kwa urahisi sana kuchukua hatua mbaya
-
40:58 - 41:05kwa sababu umezidiwa na hisia, hali, uchochezi - yote uyajuayo.
-
41:05 - 41:06Na tunachukua hatua mbaya.
-
41:06 - 41:10Wakati mwingine, unahitaji kupiga hatua nyuma na kwenda mahali pako pa maombi.
-
41:10 - 41:12Kuwa na nafasi katika nyumba yako
iliyotengwa kwa ajili ya maombi. -
41:12 - 41:14Nenda ukaombe huko.
Nendeni mkamwabudu Mungu. -
41:14 - 41:18Vaeni muziki wa kuabudu na kuabudu.
Nendeni mkamshukuru Mungu! -
41:18 - 41:25Kumbuka nilichosema kuhusu shukrani.
Usiruke tu moja kwa moja kwenye ombi. -
41:25 - 41:29Wakati fulani baada ya kutoa shukrani, hutahitaji hata kuombea suala hilo tena
-
41:29 - 41:32kwa sababu shukrani imeweka upya mtazamo wako, imeweka upya moyo wako.
-
41:32 - 41:39Na unajua - Mungu ambaye amefanya hivyo kabla atafanya tena. Yeye ni mwaminifu!
-
41:39 - 41:44Huu ni ushauri wangu kwenu, watu wa Mungu,
kuwaimarisha kiroho. -
41:44 - 41:47Adui hataacha kamwe
kushambulia mioyo yetu. -
41:47 - 41:52Uwanja wa kweli wa vita uko ndani.
-
41:52 - 41:56Basi linda moyo wako.
Linda moyo wako. -
41:56 - 42:02Suala lolote, changamoto, shida -
ipeleke kwa Mungu, ipeleke kwa maombi. -
42:02 - 42:11Huu ni utumainishaji wangu kwenu nyote siku ya leo, na tunamshukuru Mungu kwa Neno lake.
-
42:11 - 42:15Tunamshukuru Mungu kwa nafasi hii ya kupokea Neno lake.
-
42:15 - 42:26Na ninaamini Neno
limeingia kwenye mioyo iliyo wazi, -
42:26 - 42:35mioyo ambayo iko tayari kutenda Neno na kulifanya litende kazi kama Mungu anavyolifanya kuwa zuri.
- Title:
- JINSI YA KUEPUKA MSONGO wa KIROHO! | Maneno ya kutia moyo pamoja na Kaka Chris
- Description:
-
Ikiwa unatamani kukua katika uhusiano wako na Mungu, ujumbe huu ni kwa ajili yako! Jifunze kutoruhusu mfadhaiko wa kihisia au kimwili kuwa msongo wa kiroho unapotazama neno hili la kutia moyo kutoka kwa Kaka Chris lenye jina la ‘Jihadhari na Msongo wa Kiroho’.
➡️ Pata kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Saidia TV ya Moyo wa Mungu kifedha - https://godsheart.tv/financial/
➡️ Habari kuhusu Maombi Shirikishi - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live - Video Language:
- English
- Team:
God's Heart TV
- Duration:
- 43:05
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for HOW TO AVOID SPIRITUAL STRESS! | Encouraging Words with Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for HOW TO AVOID SPIRITUAL STRESS! | Encouraging Words with Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for HOW TO AVOID SPIRITUAL STRESS! | Encouraging Words with Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for HOW TO AVOID SPIRITUAL STRESS! | Encouraging Words with Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for HOW TO AVOID SPIRITUAL STRESS! | Encouraging Words with Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for HOW TO AVOID SPIRITUAL STRESS! | Encouraging Words with Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for HOW TO AVOID SPIRITUAL STRESS! | Encouraging Words with Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for HOW TO AVOID SPIRITUAL STRESS! | Encouraging Words with Brother Chris |