< Return to Video

Ushuhuda wa Maombi ya MTANDAONI! | UPONYWAJI kutoka kwenye MIAKA 17 ya BAWASIRI (HAEMORRHOIDS)

  • 0:00 - 0:10
    Tangu 2007 - hadi sasa, ni kama miaka 17 -
    nilikuwa nikiishi katika maumivu haya na mateso,
  • 0:10 - 0:14
    kwa kiwango ambacho nilianza
    kuwa na mashaka kama kweli Mungu yupo.
  • 0:14 - 0:16
    Je, anaponya kama alivyosema katika Neno Lake?
  • 0:16 - 0:20
    Lakini sikupoteza tumaini kamwe.
    Nilijua siku yangu itafika!
  • 0:22 - 0:31
    Sasa hivi, watu wa Mungu,
    chochote kinachowaibia furaha yenu,
  • 0:31 - 0:43
    kunyang'anya amani yako, kuumiza afya yako - ugonjwa huo, maradhi, udhaifu -
  • 0:43 - 0:49
    kwa mamlaka katika jina la Yesu Kristo, natangaza uponyaji sasa hivi!
  • 0:49 - 0:57
    Upone kwa jina la Yesu! Urejeshwe!
  • 0:59 - 1:02
    Jina langu ni Lastone kutoka Zambia.
  • 1:02 - 1:10
    Sababu iliyonifanya nijiunganishe na God's Heart TV ilikuwa changamoto ya bawasiri (haemorrhoids),
  • 1:10 - 1:14
    ambayo nimekuwa nayo tangu 2007.
  • 1:14 - 1:18
    Kwa hiyo tatizo hili lilianza
    nikiwa mdogo sana.
  • 1:18 - 1:24
    Iliendelea kutoka
    na kurudi tena.
  • 1:24 - 1:30
    Nilipogundua hili linahitaji uangalizi,
    nilitembelea zahanati na hospitali.
  • 1:30 - 1:36
    Niliambiwa nilihitaji kufanyiwa upasuaji au kuchukua dawa.
  • 1:36 - 1:43
    Nilianza kutumia baadhi ya dawa lakini bawasiri(haemorrhoids) haikuisha.
  • 1:43 - 1:46
    Ingetoka na kurudi - vivyo hivyo.
  • 1:46 - 1:50
    Tatizo hili lilinipa nyakati ngumu sana.
  • 1:50 - 1:52
    Nilianza kutokwa na damu.
  • 1:52 - 1:57
    Kila nilipotembelea choo,
    niliona damu ikitoka.
  • 1:57 - 2:04
    Ile sehemu ya haja kubwa ilitoka
    na nilikuwa naishi kwa maumivu.
  • 2:04 - 2:11
    Kama mwanaume, kulikuwa na
    mambo fulani ambayo nililazimika kupunguza.
  • 2:11 - 2:18
    Sikuweza kuchangamana na watu au kushirikiana na watu wengi kwa sababu ya maumivu.
  • 2:18 - 2:20
    Wangekuuliza,
    'Kwa nini umeketi hivyo?'
  • 2:20 - 2:26
    Kwa hivyo ningependelea kuwa mpweke, nibaki tu ndani au niwe na familia yangu.
  • 2:26 - 2:32
    Sikuweza kukaa juu ya kitu ambacho
    kilikuwa yabisi au kigumu. Ilikuwa ngumu sana!
  • 2:32 - 2:36
    Kwa hivyo kutoka wakati huo, nilijaribu mimea.
  • 2:36 - 2:41
    Nilijaribu kupokea msaada kutoka kwa watu
    ambao walisema wanaweza kuikata.
  • 2:41 - 2:49
    Walijaribu kufanya hivyo lakini tatizo
    halikuisha - hadi mwaka huu, 2024.
  • 2:49 - 2:57
    Nilikutana na Ndugu Chris,
    na ilinipa furaha kumuona tena.
  • 2:57 - 3:01
    Nilijiambia, 'Acha
    nitume ombi la maombi.'
  • 3:01 - 3:11
    Tarehe 6 Julai, mwezi uliopita, nilijiunga na Huduma Ya Maombi Ya Pamoja kupitia TV ya Moyo wa Mungu.
  • 3:11 - 3:18
    Kwa mshangao wangu, nilipojaribu kuingiza barua pepe yangu, nenosiri langu halikupita.
  • 3:18 - 3:22
    Ilikuwa ikiniambia, 'Ni nenosiri lisilo sahihi'.
  • 3:22 - 3:27
    Nilichanganyikiwa na kufadhaika lakini
    'nilijipoza' na kusema,
  • 3:27 - 3:31
    'Kuna sababu kwa nini haya
    yanatokea - ni siku yangu!'
  • 3:31 - 3:33
    Kwa sababu, watu wa Mungu, nilikuwa na maumivu.
  • 3:33 - 3:39
    Hebu fikiria - huwezi kukaa vizuri
    kwa sababu ya maumivu katika mkundu wako.
  • 3:39 - 3:46
    Kwa hivyo nikasema, 'Leo ni siku yangu. Ni siku yangu ya ukombozi, siku yangu ya mafanikio!'
  • 3:46 - 3:47
    Niliendelea kujiambia.
  • 3:47 - 3:53
    Kwa hivyo nilienda kwenye Facebook badala ya kupitia mwaliko wa Huduma Ya Maombi Ya Pamoja kupitia Zoom.
  • 3:53 - 3:57
    Nilienda Facebook na kujiambia,
    'Leo ni siku yangu.'
  • 3:57 - 4:02
    Nilisikiliza shuhuda.
    Niliendelea kujenga imani yangu na kuomba.
  • 4:02 - 4:05
    Na Ndugu Chris alihubiri
    na kutuombea.
  • 4:05 - 4:08
    Nilijiungana na kujidhihirisha!
  • 4:08 - 4:13
    Nilihisi kitu kilikuwa kinatembea
    tumboni mwangu.
  • 4:13 - 4:17
    Sehemu hii ya tumbo langu ilikuwa ikitetemeka.
  • 4:17 - 4:20
    Kuanzia hapo, nilijikuta tu
    chini sakafuni.
  • 4:20 - 4:28
    Sala ilipokwisha jioni, nilienda chumbani kwangu kujiangalia.
  • 4:28 - 4:32
    Niligundua kuwa bawasiri (hemorrhoids)
    ilikuwa imeanza kupungua.
  • 4:32 - 4:34
    Ilikuwa ndogo sana.
  • 4:34 - 4:38
    Basi nikampigia simu mke wangu aje kuona.
  • 4:38 - 4:43
    Kwa hivyo akaja na nikasema,
    'Jambo hili linapungua'.
  • 4:43 - 4:48
    Kwa hivyo alijaribu kuangalia na tochi na akasema, 'Ndiyo, inapungua kweli.'
  • 4:48 - 4:53
    Kwa utukufu wa Mungu, wana wa Mungu,
    niliponywa mara moja.
  • 4:53 - 4:56
    Bawasiri (hemorrhoid) hiyo ilikauka papo hapo.
  • 4:56 - 5:03
    Wiki hiyo ilipokwisha,
    nilikuwa mzima kabisa!
  • 5:03 - 5:10
    Ninapozungumza nanyi wana wa Mungu,
    mimi nipo huru. Nimepona kwa utukufu wa Mungu.
  • 5:10 - 5:15
    Sasa naweza kuketi kwa utukufu wa Mungu.
  • 5:15 - 5:18
    Kama unavyoona, sasa naweza kuketi.
  • 5:18 - 5:27
    Hiki ni kiti kigumu cha plastiki lakini sasa naweza kukikalia na hata kuruka hivi.
  • 5:27 - 5:32
    Hakuna maumivu. Niko huru!
  • 5:32 - 5:35
    Ninachoweza kusema ni, 'Asante, Yesu!'
  • 5:35 - 5:44
    Watoto wa Mungu, kama mlivyosikia, tangu 2007 - hadi sasa, ni kama miaka 17 -
  • 5:44 - 5:49
    Nilikuwa nikiishi katika maumivu haya na mateso,
  • 5:49 - 5:53
    kwa kiwango ambacho nilianza
    kuwa na mashaka kama kweli Mungu yupo.
  • 5:53 - 5:56
    Je, anaponya kama alivyosema katika Neno Lake?
  • 5:56 - 6:00
    Lakini sikupoteza tumaini kamwe.
    Nilijua siku yangu itafika!
  • 6:00 - 6:05
    Na Ndugu Chris 'akaingia' na
    nimepona kwa utukufu wa Yesu!
  • 6:05 - 6:08
    Maumivu yote niliyokuwa nayasikia yamekwisha!
  • 6:08 - 6:13
    Ule moto niliouhisi kutokana na bawasiri (haemorrhoids) ile umetoweka!
  • 6:13 - 6:18
    Wana wa Mungu, kamwe usipoteze matumaini.
    Endelea kuamini.
  • 6:18 - 6:23
    Kama unavyoona, sikujiunga na Maombi ya Pamoja kupitia Zoom
  • 6:23 - 6:27
    lakini niliomba kupitia Facebook;
    NIlijiunga kupitia Facebook.
  • 6:27 - 6:32
    Nilijiambia, 'Leo ni siku yangu!'
    Ni vivyo hivyo kwako.
  • 6:32 - 6:36
    Haijalishi changamoto unayokutana nayo au maumivu unayopitia,
  • 6:36 - 6:44
    ili mradi unaamini na umeunganishwa na Huduma hii ya Maombi ya Pamoja,
  • 6:44 - 6:48
    Mungu anakwenda kukugusa,
    kukuponya na kukukomboa.
  • 6:48 - 6:50
    Unachohitaji ni kuamini.
  • 6:50 - 6:54
    Mwamini Bwana na Mungu
    atakugusa na kukuponya. Amina!
Title:
Ushuhuda wa Maombi ya MTANDAONI! | UPONYWAJI kutoka kwenye MIAKA 17 ya BAWASIRI (HAEMORRHOIDS)
Description:

Lastone kutoka Zambia alikuwa ameishi 'katika maumivu na mateso' kwa miaka kumi na saba kutokana na bawasiri (haemorrhoids). Lakini shida yake ilifikia tamati kwa njia ya kimuujiza baada ya kujiunga na mkondo wa moja kwa moja wa Ibada ya Pamoja ya Maombi na Ndugu Chris kupitia Facebook. Alipojiunga na maombi hayo kwa imani, nguvu za Mungu zilimpata na kujikuta yuko chini. Usiku huo huo, bawasiri (hemorrhoids) ilianza kupungua na kisha kukauka kwa namna ya kushangaza.

Je, ungependa kupokea maombi mtandaoni bila malipo kutoka kwa Ndugu Chris kupitia Zoom? Tafadhali wasilisha ombi lako la maombi hapa - https://www.godsheart.tv/zoom

➡️ Pata Kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Saidia TV ya Moyo wa Mungu kifedha - https://godsheart.tv/financial/
➡️ Habari kuhusu Maombi ya Mwingiliano - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live

more » « less
Video Language:
English
Team:
God's Heart TV
Duration:
07:25

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions