< Return to Video

Ushuhuda wa Maombi ya MTANDAONI! | UPONYWAJI kutoka kwenye MIAKA 17 ya BAWASIRI (HAEMORRHOIDS)

  • 0:00 - 0:10
    Tangu 2007 - hadi sasa, ni kama miaka 17 -
    nilikuwa nikiishi katika maumivu haya na mateso,
  • 0:10 - 0:14
    kwa kiwango ambacho nilianza
    kuwa na mashaka kama kweli Mungu yupo.
  • 0:14 - 0:16
    Je, anaponya kama alivyosema katika Neno Lake?
  • 0:16 - 0:20
    Lakini sikupoteza tumaini kamwe.
    Nilijua siku yangu itafika!
  • 0:22 - 0:31
    Sasa hivi, watu wa Mungu,
    chochote kinachowaibia furaha yenu,
  • 0:31 - 0:43
    kunyang'anya amani yako, kuumiza afya yako - ugonjwa huo, maradhi, udhaifu -
  • 0:43 - 0:49
    kwa mamlaka katika jina la Yesu Kristo, natangaza uponyaji sasa hivi!
  • 0:49 - 0:57
    Upone kwa jina la Yesu! Urejeshwe!
  • 0:59 - 1:02
    Jina langu ni Lastone kutoka Zambia.
  • 1:02 - 1:10
    Sababu iliyonifanya nijiunganishe na God's Heart TV ilikuwa changamoto ya bawasiri (haemorrhoids),
  • 1:10 - 1:14
    ambayo nimekuwa nayo tangu 2007.
  • 1:14 - 1:18
    Kwa hiyo tatizo hili lilianza
    nikiwa mdogo sana.
  • 1:18 - 1:24
    Iliendelea kutoka
    na kurudi tena.
  • 1:24 - 1:30
    Nilipogundua hili linahitaji uangalizi,
    nilitembelea zahanati na hospitali.
  • 1:30 - 1:36
    Niliambiwa nilihitaji kufanyiwa upasuaji au kuchukua dawa.
  • 1:36 - 1:43
    Nilianza kutumia baadhi ya dawa lakini bawasiri(haemorrhoids) haikuisha.
  • 1:43 - 1:46
    Ingetoka na kurudi - vivyo hivyo.
  • 1:46 - 1:50
    Tatizo hili lilinipa nyakati ngumu sana.
  • 1:50 - 1:52
    Nilianza kutokwa na damu.
  • 1:52 - 1:57
    Kila nilipotembelea choo,
    niliona damu ikitoka.
  • 1:57 - 2:04
    Ile sehemu ya haja kubwa ilitoka
    na nilikuwa naishi kwa maumivu.
  • 2:04 - 2:11
    Kama mwanaume, kulikuwa na
    mambo fulani ambayo nililazimika kupunguza.
  • 2:11 - 2:18
    Sikuweza kuchangamana na watu au kushirikiana na watu wengi kwa sababu ya maumivu.
  • 2:18 - 2:20
    Wangekuuliza,
    'Kwa nini umeketi hivyo?'
  • 2:20 - 2:26
    Kwa hivyo ningependelea kuwa mpweke, nibaki tu ndani au niwe na familia yangu.
  • 2:26 - 2:32
    Sikuweza kukaa juu ya kitu ambacho
    kilikuwa yabisi au kigumu. Ilikuwa ngumu sana!
  • 2:32 - 2:36
    Kwa hivyo kutoka wakati huo, nilijaribu mimea.
  • 2:36 - 2:41
    Nilijaribu kupokea msaada kutoka kwa watu
    ambao walisema wanaweza kuikata.
  • 2:41 - 2:49
    Walijaribu kufanya hivyo lakini tatizo
    halikuisha - hadi mwaka huu, 2024.
  • 2:49 - 2:57
    Nilikutana na Ndugu Chris,
    na ilinipa furaha kumuona tena.
  • 2:57 - 3:01
    Nilijiambia, 'Acha
    nitume ombi la maombi.'
  • 3:01 - 3:11
    Tarehe 6 Julai, mwezi uliopita, nilijiunga na Huduma Ya Maombi Ya Pamoja kupitia TV ya Moyo wa Mungu.
  • 3:11 - 3:18
    Kwa mshangao wangu, nilipojaribu kuingiza barua pepe yangu, nenosiri langu halikupita.
  • 3:18 - 3:22
    Ilikuwa ikiniambia, 'Ni nenosiri lisilo sahihi'.
  • 3:22 - 3:27
    Nilichanganyikiwa na kufadhaika lakini
    'nilijipoza' na kusema,
  • 3:27 - 3:31
    'Kuna sababu kwa nini haya
    yanatokea - ni siku yangu!'
  • 3:31 - 3:33
    Kwa sababu, watu wa Mungu, nilikuwa na maumivu.
  • 3:33 - 3:39
    Hebu fikiria - huwezi kukaa vizuri
    kwa sababu ya maumivu katika mkundu wako.
  • 3:39 - 3:46
    Kwa hivyo nikasema, 'Leo ni siku yangu. Ni siku yangu ya ukombozi, siku yangu ya mafanikio!'
  • 3:46 - 3:47
    Niliendelea kujiambia.
  • 3:47 - 3:53
    Kwa hivyo nilienda kwenye Facebook badala ya kupitia mwaliko wa Huduma Ya Maombi Ya Pamoja kupitia Zoom.
  • 3:53 - 3:57
    Nilienda Facebook na kujiambia,
    'Leo ni siku yangu.'
  • 3:57 - 4:02
    Nilisikiliza shuhuda.
    Niliendelea kujenga imani yangu na kuomba.
  • 4:02 - 4:05
    Na Ndugu Chris alihubiri
    na kutuombea.
  • 4:05 - 4:08
    Nilijiungana na kujidhihirisha!
  • 4:08 - 4:13
    Nilihisi kitu kilikuwa kinatembea
    tumboni mwangu.
  • 4:13 - 4:17
    Sehemu hii ya tumbo langu ilikuwa ikitetemeka.
  • 4:17 - 4:20
    Kuanzia hapo, nilijikuta tu
    chini sakafuni.
  • 4:20 - 4:28
    Sala ilipokwisha jioni, nilienda chumbani kwangu kujiangalia.
  • 4:28 - 4:32
    Niligundua kuwa bawasiri (hemorrhoids)
    ilikuwa imeanza kupungua.
  • 4:32 - 4:34
    Ilikuwa ndogo sana.
  • 4:34 - 4:38
    Basi nikampigia simu mke wangu aje kuona.
  • 4:38 - 4:43
    Kwa hivyo akaja na nikasema,
    'Jambo hili linapungua'.
  • 4:43 - 4:48
    Kwa hivyo alijaribu kuangalia na tochi na akasema, 'Ndiyo, inapungua kweli.'
  • 4:48 - 4:53
    Kwa utukufu wa Mungu, wana wa Mungu,
    niliponywa mara moja.
  • 4:53 - 4:56
    Bawasiri (hemorrhoid) hiyo ilikauka papo hapo.
  • 4:56 - 5:03
    Wiki hiyo ilipokwisha,
    nilikuwa mzima kabisa!
  • 5:03 - 5:10
    Ninapozungumza nanyi wana wa Mungu,
    mimi nipo huru. Nimepona kwa utukufu wa Mungu.
  • 5:10 - 5:15
    Sasa naweza kuketi kwa utukufu wa Mungu.
  • 5:15 - 5:18
    Kama unavyoona, sasa naweza kuketi.
  • 5:18 - 5:27
    Hiki ni kiti kigumu cha plastiki lakini sasa naweza kukikalia na hata kuruka hivi.
  • 5:27 - 5:32
    Hakuna maumivu. Niko huru!
  • 5:32 - 5:35
    Ninachoweza kusema ni, 'Asante, Yesu!'
  • 5:35 - 5:44
    Watoto wa Mungu, kama mlivyosikia, tangu 2007 - hadi sasa, ni kama miaka 17 -
  • 5:44 - 5:49
    Nilikuwa nikiishi katika maumivu haya na mateso,
  • 5:49 - 5:53
    kwa kiwango ambacho nilianza
    kuwa na mashaka kama kweli Mungu yupo.
  • 5:53 - 5:56
    Je, anaponya kama alivyosema katika Neno Lake?
  • 5:56 - 6:00
    Lakini sikupoteza tumaini kamwe.
    Nilijua siku yangu itafika!
  • 6:00 - 6:05
    Na Ndugu Chris 'akaingia' na
    nimepona kwa utukufu wa Yesu!
  • 6:05 - 6:08
    Maumivu yote niliyokuwa nayasikia yamekwisha!
  • 6:08 - 6:13
    Ule moto niliouhisi kutokana na bawasiri (haemorrhoids) ile umetoweka!
  • 6:13 - 6:18
    Wana wa Mungu, kamwe usipoteze matumaini.
    Endelea kuamini.
  • 6:18 - 6:23
    Kama unavyoona, sikujiunga na Maombi ya Pamoja kupitia Zoom
  • 6:23 - 6:27
    lakini niliomba kupitia Facebook;
    NIlijiunga kupitia Facebook.
  • 6:27 - 6:32
    Nilijiambia, 'Leo ni siku yangu!'
    Ni vivyo hivyo kwako.
  • 6:32 - 6:36
    Haijalishi changamoto unayokutana nayo au maumivu unayopitia,
  • 6:36 - 6:44
    ili mradi unaamini na umeunganishwa na Huduma hii ya Maombi ya Pamoja,
  • 6:44 - 6:48
    Mungu anakwenda kukugusa,
    kukuponya na kukukomboa.
  • 6:48 - 6:50
    Unachohitaji ni kuamini.
  • 6:50 - 6:54
    Mwamini Bwana na Mungu
    atakugusa na kukuponya. Amina!
Title:
Ushuhuda wa Maombi ya MTANDAONI! | UPONYWAJI kutoka kwenye MIAKA 17 ya BAWASIRI (HAEMORRHOIDS)
Description:

more » « less
Video Language:
English
Team:
God's Heart TV
Duration:
07:25

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions