< Return to Video

Mtoto Wetu Ni UTHIBITISHO kuwa Mungu Anajibu MAOMBI!!!

  • 0:00 - 0:06
    Siku moja ilipowadia mnamo Agosti 2022,
    nilikuja tu nyumbani na mke wangu akaniambia,
  • 0:06 - 0:08
    'Hongera - unakwenda kuwa baba!'
  • 0:08 - 0:11
    Nikasema, 'Unamaanisha nini?'
  • 0:12 - 0:20
    Jina langu ni Kenneth. Ameketi kando
    yangu ni mke wangu kipenzi Evetha.
  • 0:20 - 0:26
    Na huyu ndiye
    binti yetu mrembo Krista.
  • 0:26 - 0:32
    Kwa asili tunatokea Tanzania lakini kwa sasa tunaishi USA.
  • 0:32 - 0:39
    Kwa hiyo, ushuhuda wetu ni kuhusu jinsi Mungu alivyotupa tunda la tumbo la uzazi
  • 0:39 - 0:45
    ambalo, kama wanandoa, tulilitafuta
    kwa zaidi ya miaka mitatu.
  • 0:45 - 0:52
    Yote yalianza tulipofunga ndoa mnamo Desemba 2019.
  • 0:52 - 0:58
    Tulipofunga ndoa, tulitamani sana kupata mtoto haraka iwezekanavyo.
  • 0:58 - 1:08
    Lakini kadiri siku na miezi ilivyokuwa inasonga mbele,
    niliona kwamba mke wangu alikuwa hapati mimba.
  • 1:08 - 1:15
    Tulianza kugundua vitu ambavyo havikuwepo hapo awali au mke wangu hajawahi kukumbana navyo
  • 1:15 - 1:19
    alipokuwa hajaolewa na pia sikuwahi kukumbana navyo pindi sijaoa.
  • 1:19 - 1:25
    Mke wangu alianza kupata mizunguko ya hedhi isiyo ya kawaida.
  • 1:25 - 1:32
    Ilifikia hatua ambapo, kwa muda wa miezi 2 hadi 3, hangeweza kuona mzunguko wake wa hedhi.
  • 1:32 - 1:38
    Tulianza kuchanganyikiwa kwa kweli.
    Tulidhani ni suala la matibabu
  • 1:38 - 1:41
    na kwa hivyo tuliamua kutafuta ushauri toka kwa madaktari.
  • 1:41 - 1:49
    Pamoja na mzunguko wake wa hedhi usio wa kawaida, pia alikuwa na maambukizi ya chachu
  • 1:49 - 1:53
    ambayo hajawahi kukumbana nayo hapo awali,
    kwa hiyo tulifadhaika sana.
  • 1:53 - 1:58
    Tulianza kuomba, lakini wakati huo tukakata kauli kwamba ni tatizo la kiafya,
  • 1:58 - 2:00
    sio shida ya kiroho.
  • 2:00 - 2:02
    Kwa hivyo, tuliwasiliana na madaktari hapa USA.
  • 2:02 - 2:07
    Walifanya vipimo vyote kisha wakasema hakuna wanachoweza kufanya.
  • 2:07 - 2:13
    Walitupatia dawa tu na aliendelea kutumia dawa hizo,
  • 2:13 - 2:18
    tukiamini kwamba ingesuluhisha suala hilo na labda hivi karibuni tutapata mtoto wetu.
  • 2:18 - 2:26
    Lakini haikuwa hivyo, hivyo tulizidi kuchanganyikiwa kwa sababu
  • 2:26 - 2:32
    hilo suala la kutafuta mtoto lilichukua nafasi kubwa sana katika maisha yetu.
  • 2:32 - 2:39
    Hatukuzingatia sana maombi;
    umakini wetu ulikuwa juu yake.
  • 2:39 - 2:43
    Hata mimi - nakumbuka kuna
    nyakati hatukuweza kulala.
  • 2:43 - 2:47
    Mke wangu aliendelea kulia
    kwa uchungu usiku mzima.
  • 2:47 - 2:52
    Nilifadhaika sana na mwishowe,
    nilipata udhaifu huu wa mwili,
  • 2:52 - 2:58
    hiyo ilikuja wakati tulipofikiria, ikiwa tutakutana kama mume na mke,
  • 2:58 - 3:00
    mke wangu angepata mimba.
  • 3:00 - 3:07
    Nilidhoofika sana
    wakati huo.
  • 3:07 - 3:09
    Kwa kuongezea, na kile ambacho mke wangu alikuwa akipitia,
  • 3:09 - 3:12
    nyakati fulani, hatukuweza hata kukutana kama mume na mke.
  • 3:12 - 3:19
    Mara tu baada ya hapo, ningekuwa na nguvu sana
    kana kwamba hakuna kilichotokea.
  • 3:19 - 3:26
    Kwa aina hizo za dalili, tuligundua kuwa ilikuwa shida zaidi ya kiroho,
  • 3:26 - 3:30
    badala ya tatizo la kiafya.
    Kwa hiyo tulianza kusali kuhusu hilo.
  • 3:30 - 3:34
    Hatujawahi kufunga kama mume
    na mke, lakini hali hii
  • 3:34 - 3:40
    ilitusukuma tufunge pamoja
    na kuomba pamoja zaidi.
  • 3:40 - 3:46
    Baada ya kufunga mnamo Agosti 2021, mnamo Septemba, mke wangu alipata mimba.
  • 3:46 - 3:53
    Tulifurahi sana na tuliendelea kumsifu Mungu, lakini furaha yetu ilipunguzwa,
  • 3:53 - 4:05
    kwa sababu baada ya wiki 4 au 5 tu,
    mke wangu alipoteza mimba.
  • 4:05 - 4:08
    Ilikuwa ni wakati usiovumilika.
  • 4:08 - 4:11
    Kwa sababu lilikuwa jambo ambalo tulikuwa tukiomba kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu.
  • 4:11 - 4:14
    Hatukuwa na
    nguvu za kutosha tena za kuomba.
  • 4:14 - 4:16
    Tulijiambia - nini kinatokea?
  • 4:16 - 4:20
    Tulihisi kama Mungu amejibu
    maombi yetu lakini sasa haya yalikuwa yametukia.
  • 4:20 - 4:24
    Baada ya mimba kuharibika
    alilazwa kisha tukasema,
  • 4:24 - 4:32
    'Tuhakikishe madaktari wanachukua vipimo vyote ili kufahamu chanzo cha mimba kuharibika.'
  • 4:32 - 4:37
    Lakini kwa mshangao, daktari alitoka
    nje na kusema,
  • 4:37 - 4:42
    "Hakuna dalili ya nini kinaweza kusababisha kuharibika kwa mimba.
  • 4:42 - 4:45
    Kiafya, mkeo anaonekana yuko sawa;
    viwango vyake vya homoni viko sawa.'
  • 4:45 - 4:51
    Baada ya kuchukua vipimo vya damu, walisema kila kitu kiko sawa.
  • 4:51 - 4:59
    Kwa hiyo, tulirudi nyumbani kwa huzuni sana,
    tukitafakari hatua zetu zinazofuata.
  • 4:59 - 5:04
    Lakini baada ya muda tuliendelea kujipa moyo kwani tulisema maisha lazima yasonge mbele.
  • 5:04 - 5:12
    Tulianza polepole kuboresha maisha yetu ya maombi, tukimwomba Mungu rehema na msamaha,
  • 5:12 - 5:16
    na kumwomba atukomboe kutokana na
    chochote tulichokuwa tukipitia.
  • 5:16 - 5:23
    Kwa sababu wakati huo, tulikuwa na uhakika wa asilimia 100 kwamba hiiki kilikuwa kisa cha kiroho na sio matibabu.
  • 5:23 - 5:26
    Mungu pekee ndiye angeweza kutatua tatizo.
  • 5:26 - 5:33
    Mnamo Januari 2022, katika kuanzishwa
    kwa Televisheni ya Moyo wa Mungu -
  • 5:33 - 5:38
    tulijifunza kuhusu TV ya Moyo wa Mungu
    kupitia kutazama YouTube,
  • 5:38 - 5:45
    na tukasema hii inaweza kuwa fursa kwetu kuomba maombi.
  • 5:45 - 5:50
    Kwa hivyo tulituma ombi la maombi
    kwa TV ya Moyo wa Mungu.
  • 5:50 - 5:58
    Mnamo Februari 2022, TV ya Moyo wa Mungu
    ilitujibu ikisema hivyo
  • 5:58 - 6:03
    tulialikwa kwa mawasiliano kupitia simu ya WhatsApp
    na Ndugu Chris.
  • 6:03 - 6:11
    Wakati huo, hakukuwa na Huduma ya Maombi ya Pamoja ya moja kwa moja kwa sababu ilikuwa mwanzo tu
  • 6:11 - 6:13
    wa TV ya Moyo wa Mungu.
  • 6:13 - 6:25
    Tulikuwa na bahati katika siku hiyo mbaya mnamo Februari 2022 kupokea maombi kutoka kwa Ndugu Chris.
  • 6:25 - 6:34
    Ndugu Chris alipokuwa akiomba, tulihisi uwepo mkuu wa Mungu wakati wa maombi hayo.
  • 6:34 - 6:43
    Ghafla mke wangu alianza kujisikia tofauti
    na alianza kutapika.
  • 6:43 - 6:49
    Tulimweleza Ndugu Chris na
    akatuambia hivi
  • 6:49 - 6:52
    ilikuwa dhihirisho kwamba Mungu alikuwa
    akifanyia kazi kisa chetu.
  • 6:52 - 6:57
    Kwa kweli iliinua imani yetu
    - kwamba Mungu anatujali.
  • 6:57 - 7:01
    Yeye yuko katikati ya hali yetu kwa hivyo hatupaswi kukata tamaa.
  • 7:01 - 7:07
    Muda mfupi baada ya Ndugu Chris kukata simu,
    mke wangu aliendelea kutapika.
  • 7:07 - 7:11
    Harufu ilikuwa mbaya sana na sio kama
    alikula chochote kabla ya sala hiyo.
  • 7:11 - 7:14
    Baada ya yote, tulikuwa tukifunga kabla ya maombi hayo.
  • 7:14 - 7:18
    Kwa hiyo, tulishangaa sana mambo haya yote yalikuwa yanatoka wapi katika mwili wake.
  • 7:18 - 7:22
    Lakini mwisho, tulimpa Mungu utukufu kwa sababu tulijua haya yalitokana
  • 7:22 - 7:27
    na pepo wachafu wakitenda kazi ndani yake
    na walikuwa wanatoka.
  • 7:27 - 7:31
    Baada ya maombi, tulitazamia
    muujiza wa Mungu kwelikweli.
  • 7:31 - 7:38
    Tulijua baraka ilikuwa njiani lakini kwa sababu mioyo yetu ilikuwa imekata tamaa,
  • 7:38 - 7:41
    tulifikiri ni jambo
    ambalo lingekuja hivi karibuni.
  • 7:41 - 7:45
    Tulifikiri kwamba baada ya mwezi mmoja au miwili baada ya maombi kutoka kwa Ndugu Chris, tungeona matokeo
  • 7:45 - 7:47
    lakini haikuwa hivyo.
  • 7:47 - 7:52
    Kwa hiyo, ilianza kusumbua sana mioyo yetu
    na polepole tukajikuta wenyewe
  • 7:52 - 7:58
    kurudi mahali ambapo tuliruhusu
    hali hiyo itulemee.
  • 7:58 - 8:04
    Kwa hiyo, nilianza kupata udhaifu kwa sababu tuliruhusu hali hiyo itulemee
  • 8:04 - 8:11
    na kusahau ahadi za Mungu zilizokuja
    kwa kinywa cha Ndugu Chris.
  • 8:11 - 8:19
    Wakati fulani nilimpigia simu mke wangu na kusema, 'Hali hii inachukua nafasi kuu katika maisha yetu.
  • 8:19 - 8:25
    Mungu tayari ametuahidi kwamba
    atatupa mtoto.
  • 8:25 - 8:31
    Kwa hiyo, hebu tusahau kuhusu hilo. Tusijaribu kudhibiti hali hiyo.
  • 8:31 - 8:34
    Hebu tu tuikabidhi kabisa
    hali hii kwa Mungu.
  • 8:34 - 8:39
    Tuishi maisha yetu kana kwamba tatizo hili halipo kwa sababu Mungu analifahamu.'
  • 8:39 - 8:45
    'Tulikosa' maisha mengi kwa sababu hicho ndicho
    kitu pekee tulichotaka.
  • 8:45 - 8:50
    Dakika tulipoamua hivyo,
    Mungu alitupa neema ya kuliachilia.
  • 8:50 - 8:53
    Mke wangu akawa na furaha zaidi;
    Nilifurahi zaidi.
  • 8:53 - 8:58
    Tungeweza kuzungumza na kufanya mambo mengine.
  • 8:58 - 9:02
    Siku moja mahsusi mnamo Agosti 2022, nilirudi nyumbani
  • 9:02 - 9:05
    na mke wangu akaniambia, 'Hongera -
    utakuwa baba!'
  • 9:05 - 9:09
    Nikasema, 'Unamaanisha nini?'
  • 9:09 - 9:14
    Mke wangu alikuwa mjamzito tena na
    tulifurahi sana kuhusu hilo.
  • 9:14 - 9:20
    Wakati huu, haikutoka katika
    msomgo tuliokuwa nao.
  • 9:20 - 9:23
    Ilitoka katika furaha tuliyokuwa nayo
  • 9:23 - 9:26
    kwa sababu tuliamua
    kumwachia Mungu kila kitu.
  • 9:26 - 9:30
    Katika safari hiyo yote ya ujauzito,
    hakukuwa na dalili ya kuharibika kwa mimba.
  • 9:30 - 9:34
    Hakukuwa na chochote isipokuwa
    maradhi ya kawaida tu.
  • 9:34 - 9:39
    Ilienda vizuri sana hadi miezi tisa.
  • 9:39 - 9:44
    Kulikuwa na matatizo fulani kwani mtoto hakugeuka katika nafasi nzuri ya kutoka.
  • 9:44 - 9:47
    Lakini mwisho wa siku akageuka.
  • 9:47 - 9:54
    Mke wangu alikuwa na uzoefu wa uchungu wa muda mrefu, ambao ni kawaida kwa wanawake wengi.
  • 9:54 - 10:02
    Na kisha mnamo Aprili 2023,
    mtoto huyu mrembo Krista alikuja maishani mwetu.
  • 10:02 - 10:11
    Kwa hiyo, tunajawa na furaha na
    tunampa Mungu utukufu na heshima yote.
  • 10:11 - 10:17
    Hadi sasa, ana umri wa miezi kumi na moja,
    anaenda kwenye siku yake ya kuzaliwa ya kwanza
  • 10:17 - 10:22
    na ana nguvu, furaha na afya.
  • 10:22 - 10:28
    Hajatupa shida yoyote -
    hakuna magonjwa makubwa.
  • 10:28 - 10:33
    Tunaendelea kumfurahia na kumshukuru Mungu
    kwa baraka zake maishani mwetu.
  • 10:33 - 10:38
    Kwa upande wa umbile lako, ulisema unasumbuliwa na udhaifu katika mwili wako.
  • 10:38 - 10:41
    Unajisikiaje sasa hivi?
  • 10:41 - 10:43
    Sasa, ninajisikia vizuri!
  • 10:43 - 10:50
    Sala hiyo tuliyopokea kutoka kwa Ndugu Chris ilionekana kimwili.
  • 10:50 - 10:55
    Mara tu baada ya hapo,
    udhaifu wa jumla wa mwili uliniacha.
  • 10:55 - 11:02
    Na tangu wakati huo, sijawahi kupata
    aina yoyote ya udhaifu katika maisha yangu.
  • 11:02 - 11:10
    Mke wangu pia anaweza kuthibitisha kwamba
    maambukizo yote ya mara kwa mara aliyokuwa nayo -
  • 11:10 - 11:13
    hakumbani nayo tena.
  • 11:13 - 11:18
    Kwa mtazamo wa kimatibabu, tulifanya
    kila aina ya vipimo na ilikuwa sawa.
  • 11:18 - 11:21
    Kwa hivyo unafikiri uko sawa lakini
    mambo yalikuwa hayatokei.
  • 11:21 - 11:26
    Ilikuwa kiyu kibaya sana na chenye msongo na
    wakati huo huo haiaminiki kwa sababu
  • 11:26 - 11:34
    kabla ya kuolewa, nilifikiri ningepata mimba mara tu baada ya ndoa.
  • 11:34 - 11:39
    Lakini haikutokea jinsi tulivyotarajia.
    Kwa hivyo, ilikuwa chungu sana na mfadhaiko kwangu.
  • 11:39 - 11:43
    Tunajisikia furaha na vizuri sana.
  • 11:43 - 11:46
    Tangu nilipogundua kuwa nina mimba,
  • 11:46 - 11:50
    ilikuwa kama mlango unafunguliwa.
    Tunajisikia furaha sana!
  • 11:50 - 11:54
    Tunaona ulimwengu kwa mtazamo tofauti.
  • 11:54 - 11:59
    Kwa hivyo, imekuwa baraka ya kubadilisha maisha
  • 11:59 - 12:03
    na mpaka sasa tunamshukuru Mungu sana kwa hilo.
  • 12:03 - 12:09
    Ushauri mkuu nilionao kwa wengine
    kutokana na uzoefu huu ni kwamba
  • 12:09 - 12:15
    kadiri tunavyothamini baraka za Mungu -
    kama vile baraka za mtoto -
  • 12:15 - 12:20
    tunapaswa pia kuthamini mchakato wa Mungu.
  • 12:20 - 12:26
    Baada ya kupata mtoto, baadaye nilitafakari
    juu ya yale tuliyopitia
  • 12:26 - 12:30
    na safari ya kiroho tuliyopitia
    kupata mtoto.
  • 12:30 - 12:36
    Kwa hivyo, mwisho wa siku, haikuwa baraka ya Krista tu bali sisi kama wanandoa.
  • 12:36 - 12:41
    tuliimarishwa pia na hali hiyo.
  • 12:41 - 12:46
    Hapo awali, hatukuomba mara nyingi
    kama mume na mke.
  • 12:46 - 12:51
    Ilikuwa ngumu kwetu kukubaliana pamoja -
    kwa mfano, kufunga juu ya jambo fulani.
  • 12:51 - 12:58
    Kwa hiyo, tabia yetu katika Mungu kweli ilikua
    na tukaja kuthamini maisha.
  • 12:58 - 13:03
    Mungu alitumia hali hii
    kuimarisha maisha yetu ya kiroho,
  • 13:03 - 13:06
    mmoja mmoja na kama wanandoa pamoja.
  • 13:06 - 13:12
    Kwa hivyo, kwa yeyote anayesikiliza,
    kwa kadiri unavyohitaji baraka za Mungu -
  • 13:12 - 13:18
    Labda leo una shida
    ambayo unatamani Mungu atatue -
  • 13:18 - 13:20
    unapaswa pia kuthamini usindikaji wa Mungu.
  • 13:20 - 13:23
    Kwa sababu mara tu unapothamini mchakato wa Mungu,
  • 13:23 - 13:28
    utapata neema ya kusubiri wakati wa Mungu bila kufadhaika sana.
  • 13:28 - 13:32
    Na ninakumbuka Ndugu Chris alisema
    kwamba baraka tunazopokea
  • 13:32 - 13:37
    sio mwisho wenyewe bali ni njia ya kufikia mwisho, ambayo ni wokovu wa nafsi zetu.
Title:
Mtoto Wetu Ni UTHIBITISHO kuwa Mungu Anajibu MAOMBI!!!
Description:

Utiwe moyo na ushuhuda huu mzito kutoka kwa Mr & Mrs Keneth, Watanzania waishio Marekani, ambao Mungu aliwabariki kwa tunda la tumbo la uzazi baada ya kupokea maombi kutoka kwa Ndugu Chris - muda mfupi baada ya uzinduzi wa TV ya Moyo wa Mungu kabla hata Huduma za Maombi ya Pamoja hazijaanza - na kuchagua kukabidhi hali zao kabisa kwa Mungu!

Je, ungependa kujiunga na Huduma ya Maombi ya Pamoja na Ndugu Chris ili kupokea maombi bila malipo kupitia Zoom? Tuma ombi lako la maombi hapa - https://www.godsheart.tv/zoom

#Ushuhuda

➡️ Pata Kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Saidia TV ya Moyo wa Mungu kifedha - https://godsheart.tv/financial/
➡️ Habari kuhusu Maombi ya Pamoja - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live

more » « less
Video Language:
English
Team:
God's Heart TV
Duration:
14:08

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions