Mtoto Wetu Ni UTHIBITISHO kuwa Mungu Anajibu MAOMBI!!!
-
0:00 - 0:06Siku moja ilipowadia mnamo Agosti 2022,
nilikuja tu nyumbani na mke wangu akaniambia, -
0:06 - 0:08'Hongera - unakwenda kuwa baba!'
-
0:08 - 0:11Nikasema, 'Unamaanisha nini?'
-
0:12 - 0:20Jina langu ni Kenneth. Ameketi kando
yangu ni mke wangu kipenzi Evetha. -
0:20 - 0:26Na huyu ndiye
binti yetu mrembo Krista. -
0:26 - 0:32Kwa asili tunatokea Tanzania lakini kwa sasa tunaishi USA.
-
0:32 - 0:39Kwa hiyo, ushuhuda wetu ni kuhusu jinsi Mungu alivyotupa tunda la tumbo la uzazi
-
0:39 - 0:45ambalo, kama wanandoa, tulilitafuta
kwa zaidi ya miaka mitatu. -
0:45 - 0:52Yote yalianza tulipofunga ndoa mnamo Desemba 2019.
-
0:52 - 0:58Tulipofunga ndoa, tulitamani sana kupata mtoto haraka iwezekanavyo.
-
0:58 - 1:08Lakini kadiri siku na miezi ilivyokuwa inasonga mbele,
niliona kwamba mke wangu alikuwa hapati mimba. -
1:08 - 1:15Tulianza kugundua vitu ambavyo havikuwepo hapo awali au mke wangu hajawahi kukumbana navyo
-
1:15 - 1:19alipokuwa hajaolewa na pia sikuwahi kukumbana navyo pindi sijaoa.
-
1:19 - 1:25Mke wangu alianza kupata mizunguko ya hedhi isiyo ya kawaida.
-
1:25 - 1:32Ilifikia hatua ambapo, kwa muda wa miezi 2 hadi 3, hangeweza kuona mzunguko wake wa hedhi.
-
1:32 - 1:38Tulianza kuchanganyikiwa kwa kweli.
Tulidhani ni suala la matibabu -
1:38 - 1:41na kwa hivyo tuliamua kutafuta ushauri toka kwa madaktari.
-
1:41 - 1:49Pamoja na mzunguko wake wa hedhi usio wa kawaida, pia alikuwa na maambukizi ya chachu
-
1:49 - 1:53ambayo hajawahi kukumbana nayo hapo awali,
kwa hiyo tulifadhaika sana. -
1:53 - 1:58Tulianza kuomba, lakini wakati huo tukakata kauli kwamba ni tatizo la kiafya,
-
1:58 - 2:00sio shida ya kiroho.
-
2:00 - 2:02Kwa hivyo, tuliwasiliana na madaktari hapa USA.
-
2:02 - 2:07Walifanya vipimo vyote kisha wakasema hakuna wanachoweza kufanya.
-
2:07 - 2:13Walitupatia dawa tu na aliendelea kutumia dawa hizo,
-
2:13 - 2:18tukiamini kwamba ingesuluhisha suala hilo na labda hivi karibuni tutapata mtoto wetu.
-
2:18 - 2:26Lakini haikuwa hivyo, hivyo tulizidi kuchanganyikiwa kwa sababu
-
2:26 - 2:32hilo suala la kutafuta mtoto lilichukua nafasi kubwa sana katika maisha yetu.
-
2:32 - 2:39Hatukuzingatia sana maombi;
umakini wetu ulikuwa juu yake. -
2:39 - 2:43Hata mimi - nakumbuka kuna
nyakati hatukuweza kulala. -
2:43 - 2:47Mke wangu aliendelea kulia
kwa uchungu usiku mzima. -
2:47 - 2:52Nilifadhaika sana na mwishowe,
nilipata udhaifu huu wa mwili, -
2:52 - 2:58hiyo ilikuja wakati tulipofikiria, ikiwa tutakutana kama mume na mke,
-
2:58 - 3:00mke wangu angepata mimba.
-
3:00 - 3:07Nilidhoofika sana
wakati huo. -
3:07 - 3:09Kwa kuongezea, na kile ambacho mke wangu alikuwa akipitia,
-
3:09 - 3:12nyakati fulani, hatukuweza hata kukutana kama mume na mke.
-
3:12 - 3:19Mara tu baada ya hapo, ningekuwa na nguvu sana
kana kwamba hakuna kilichotokea. -
3:19 - 3:26Kwa aina hizo za dalili, tuligundua kuwa ilikuwa shida zaidi ya kiroho,
-
3:26 - 3:30badala ya tatizo la kiafya.
Kwa hiyo tulianza kusali kuhusu hilo. -
3:30 - 3:34Hatujawahi kufunga kama mume
na mke, lakini hali hii -
3:34 - 3:40ilitusukuma tufunge pamoja
na kuomba pamoja zaidi. -
3:40 - 3:46Baada ya kufunga mnamo Agosti 2021, mnamo Septemba, mke wangu alipata mimba.
-
3:46 - 3:53Tulifurahi sana na tuliendelea kumsifu Mungu, lakini furaha yetu ilipunguzwa,
-
3:53 - 4:05kwa sababu baada ya wiki 4 au 5 tu,
mke wangu alipoteza mimba. -
4:05 - 4:08Ilikuwa ni wakati usiovumilika.
-
4:08 - 4:11Kwa sababu lilikuwa jambo ambalo tulikuwa tukiomba kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu.
-
4:11 - 4:14Hatukuwa na
nguvu za kutosha tena za kuomba. -
4:14 - 4:16Tulijiambia - nini kinatokea?
-
4:16 - 4:20Tulihisi kama Mungu amejibu
maombi yetu lakini sasa haya yalikuwa yametukia. -
4:20 - 4:24Baada ya mimba kuharibika
alilazwa kisha tukasema, -
4:24 - 4:32'Tuhakikishe madaktari wanachukua vipimo vyote ili kufahamu chanzo cha mimba kuharibika.'
-
4:32 - 4:37Lakini kwa mshangao, daktari alitoka
nje na kusema, -
4:37 - 4:42"Hakuna dalili ya nini kinaweza kusababisha kuharibika kwa mimba.
-
4:42 - 4:45Kiafya, mkeo anaonekana yuko sawa;
viwango vyake vya homoni viko sawa.' -
4:45 - 4:51Baada ya kuchukua vipimo vya damu, walisema kila kitu kiko sawa.
-
4:51 - 4:59Kwa hiyo, tulirudi nyumbani kwa huzuni sana,
tukitafakari hatua zetu zinazofuata. -
4:59 - 5:04Lakini baada ya muda tuliendelea kujipa moyo kwani tulisema maisha lazima yasonge mbele.
-
5:04 - 5:12Tulianza polepole kuboresha maisha yetu ya maombi, tukimwomba Mungu rehema na msamaha,
-
5:12 - 5:16na kumwomba atukomboe kutokana na
chochote tulichokuwa tukipitia. -
5:16 - 5:23Kwa sababu wakati huo, tulikuwa na uhakika wa asilimia 100 kwamba hiiki kilikuwa kisa cha kiroho na sio matibabu.
-
5:23 - 5:26Mungu pekee ndiye angeweza kutatua tatizo.
-
5:26 - 5:33Mnamo Januari 2022, katika kuanzishwa
kwa Televisheni ya Moyo wa Mungu - -
5:33 - 5:38tulijifunza kuhusu TV ya Moyo wa Mungu
kupitia kutazama YouTube, -
5:38 - 5:45na tukasema hii inaweza kuwa fursa kwetu kuomba maombi.
-
5:45 - 5:50Kwa hivyo tulituma ombi la maombi
kwa TV ya Moyo wa Mungu. -
5:50 - 5:58Mnamo Februari 2022, TV ya Moyo wa Mungu
ilitujibu ikisema hivyo -
5:58 - 6:03tulialikwa kwa mawasiliano kupitia simu ya WhatsApp
na Ndugu Chris. -
6:03 - 6:11Wakati huo, hakukuwa na Huduma ya Maombi ya Pamoja ya moja kwa moja kwa sababu ilikuwa mwanzo tu
-
6:11 - 6:13wa TV ya Moyo wa Mungu.
-
6:13 - 6:25Tulikuwa na bahati katika siku hiyo mbaya mnamo Februari 2022 kupokea maombi kutoka kwa Ndugu Chris.
-
6:25 - 6:34Ndugu Chris alipokuwa akiomba, tulihisi uwepo mkuu wa Mungu wakati wa maombi hayo.
-
6:34 - 6:43Ghafla mke wangu alianza kujisikia tofauti
na alianza kutapika. -
6:43 - 6:49Tulimweleza Ndugu Chris na
akatuambia hivi -
6:49 - 6:52ilikuwa dhihirisho kwamba Mungu alikuwa
akifanyia kazi kisa chetu. -
6:52 - 6:57Kwa kweli iliinua imani yetu
- kwamba Mungu anatujali. -
6:57 - 7:01Yeye yuko katikati ya hali yetu kwa hivyo hatupaswi kukata tamaa.
-
7:01 - 7:07Muda mfupi baada ya Ndugu Chris kukata simu,
mke wangu aliendelea kutapika. -
7:07 - 7:11Harufu ilikuwa mbaya sana na sio kama
alikula chochote kabla ya sala hiyo. -
7:11 - 7:14Baada ya yote, tulikuwa tukifunga kabla ya maombi hayo.
-
7:14 - 7:18Kwa hiyo, tulishangaa sana mambo haya yote yalikuwa yanatoka wapi katika mwili wake.
-
7:18 - 7:22Lakini mwisho, tulimpa Mungu utukufu kwa sababu tulijua haya yalitokana
-
7:22 - 7:27na pepo wachafu wakitenda kazi ndani yake
na walikuwa wanatoka. -
7:27 - 7:31Baada ya maombi, tulitazamia
muujiza wa Mungu kwelikweli. -
7:31 - 7:38Tulijua baraka ilikuwa njiani lakini kwa sababu mioyo yetu ilikuwa imekata tamaa,
-
7:38 - 7:41tulifikiri ni jambo
ambalo lingekuja hivi karibuni. -
7:41 - 7:45Tulifikiri kwamba baada ya mwezi mmoja au miwili baada ya maombi kutoka kwa Ndugu Chris, tungeona matokeo
-
7:45 - 7:47lakini haikuwa hivyo.
-
7:47 - 7:52Kwa hiyo, ilianza kusumbua sana mioyo yetu
na polepole tukajikuta wenyewe -
7:52 - 7:58kurudi mahali ambapo tuliruhusu
hali hiyo itulemee. -
7:58 - 8:04Kwa hiyo, nilianza kupata udhaifu kwa sababu tuliruhusu hali hiyo itulemee
-
8:04 - 8:11na kusahau ahadi za Mungu zilizokuja
kwa kinywa cha Ndugu Chris. -
8:11 - 8:19Wakati fulani nilimpigia simu mke wangu na kusema, 'Hali hii inachukua nafasi kuu katika maisha yetu.
-
8:19 - 8:25Mungu tayari ametuahidi kwamba
atatupa mtoto. -
8:25 - 8:31Kwa hiyo, hebu tusahau kuhusu hilo. Tusijaribu kudhibiti hali hiyo.
-
8:31 - 8:34Hebu tu tuikabidhi kabisa
hali hii kwa Mungu. -
8:34 - 8:39Tuishi maisha yetu kana kwamba tatizo hili halipo kwa sababu Mungu analifahamu.'
-
8:39 - 8:45'Tulikosa' maisha mengi kwa sababu hicho ndicho
kitu pekee tulichotaka. -
8:45 - 8:50Dakika tulipoamua hivyo,
Mungu alitupa neema ya kuliachilia. -
8:50 - 8:53Mke wangu akawa na furaha zaidi;
Nilifurahi zaidi. -
8:53 - 8:58Tungeweza kuzungumza na kufanya mambo mengine.
-
8:58 - 9:02Siku moja mahsusi mnamo Agosti 2022, nilirudi nyumbani
-
9:02 - 9:05na mke wangu akaniambia, 'Hongera -
utakuwa baba!' -
9:05 - 9:09Nikasema, 'Unamaanisha nini?'
-
9:09 - 9:14Mke wangu alikuwa mjamzito tena na
tulifurahi sana kuhusu hilo. -
9:14 - 9:20Wakati huu, haikutoka katika
msomgo tuliokuwa nao. -
9:20 - 9:23Ilitoka katika furaha tuliyokuwa nayo
-
9:23 - 9:26kwa sababu tuliamua
kumwachia Mungu kila kitu. -
9:26 - 9:30Katika safari hiyo yote ya ujauzito,
hakukuwa na dalili ya kuharibika kwa mimba. -
9:30 - 9:34Hakukuwa na chochote isipokuwa
maradhi ya kawaida tu. -
9:34 - 9:39Ilienda vizuri sana hadi miezi tisa.
-
9:39 - 9:44Kulikuwa na matatizo fulani kwani mtoto hakugeuka katika nafasi nzuri ya kutoka.
-
9:44 - 9:47Lakini mwisho wa siku akageuka.
-
9:47 - 9:54Mke wangu alikuwa na uzoefu wa uchungu wa muda mrefu, ambao ni kawaida kwa wanawake wengi.
-
9:54 - 10:02Na kisha mnamo Aprili 2023,
mtoto huyu mrembo Krista alikuja maishani mwetu. -
10:02 - 10:11Kwa hiyo, tunajawa na furaha na
tunampa Mungu utukufu na heshima yote. -
10:11 - 10:17Hadi sasa, ana umri wa miezi kumi na moja,
anaenda kwenye siku yake ya kuzaliwa ya kwanza -
10:17 - 10:22na ana nguvu, furaha na afya.
-
10:22 - 10:28Hajatupa shida yoyote -
hakuna magonjwa makubwa. -
10:28 - 10:33Tunaendelea kumfurahia na kumshukuru Mungu
kwa baraka zake maishani mwetu. -
10:33 - 10:38Kwa upande wa umbile lako, ulisema unasumbuliwa na udhaifu katika mwili wako.
-
10:38 - 10:41Unajisikiaje sasa hivi?
-
10:41 - 10:43Sasa, ninajisikia vizuri!
-
10:43 - 10:50Sala hiyo tuliyopokea kutoka kwa Ndugu Chris ilionekana kimwili.
-
10:50 - 10:55Mara tu baada ya hapo,
udhaifu wa jumla wa mwili uliniacha. -
10:55 - 11:02Na tangu wakati huo, sijawahi kupata
aina yoyote ya udhaifu katika maisha yangu. -
11:02 - 11:10Mke wangu pia anaweza kuthibitisha kwamba
maambukizo yote ya mara kwa mara aliyokuwa nayo - -
11:10 - 11:13hakumbani nayo tena.
-
11:13 - 11:18Kwa mtazamo wa kimatibabu, tulifanya
kila aina ya vipimo na ilikuwa sawa. -
11:18 - 11:21Kwa hivyo unafikiri uko sawa lakini
mambo yalikuwa hayatokei. -
11:21 - 11:26Ilikuwa kiyu kibaya sana na chenye msongo na
wakati huo huo haiaminiki kwa sababu -
11:26 - 11:34kabla ya kuolewa, nilifikiri ningepata mimba mara tu baada ya ndoa.
-
11:34 - 11:39Lakini haikutokea jinsi tulivyotarajia.
Kwa hivyo, ilikuwa chungu sana na mfadhaiko kwangu. -
11:39 - 11:43Tunajisikia furaha na vizuri sana.
-
11:43 - 11:46Tangu nilipogundua kuwa nina mimba,
-
11:46 - 11:50ilikuwa kama mlango unafunguliwa.
Tunajisikia furaha sana! -
11:50 - 11:54Tunaona ulimwengu kwa mtazamo tofauti.
-
11:54 - 11:59Kwa hivyo, imekuwa baraka ya kubadilisha maisha
-
11:59 - 12:03na mpaka sasa tunamshukuru Mungu sana kwa hilo.
-
12:03 - 12:09Ushauri mkuu nilionao kwa wengine
kutokana na uzoefu huu ni kwamba -
12:09 - 12:15kadiri tunavyothamini baraka za Mungu -
kama vile baraka za mtoto - -
12:15 - 12:20tunapaswa pia kuthamini mchakato wa Mungu.
-
12:20 - 12:26Baada ya kupata mtoto, baadaye nilitafakari
juu ya yale tuliyopitia -
12:26 - 12:30na safari ya kiroho tuliyopitia
kupata mtoto. -
12:30 - 12:36Kwa hivyo, mwisho wa siku, haikuwa baraka ya Krista tu bali sisi kama wanandoa.
-
12:36 - 12:41tuliimarishwa pia na hali hiyo.
-
12:41 - 12:46Hapo awali, hatukuomba mara nyingi
kama mume na mke. -
12:46 - 12:51Ilikuwa ngumu kwetu kukubaliana pamoja -
kwa mfano, kufunga juu ya jambo fulani. -
12:51 - 12:58Kwa hiyo, tabia yetu katika Mungu kweli ilikua
na tukaja kuthamini maisha. -
12:58 - 13:03Mungu alitumia hali hii
kuimarisha maisha yetu ya kiroho, -
13:03 - 13:06mmoja mmoja na kama wanandoa pamoja.
-
13:06 - 13:12Kwa hivyo, kwa yeyote anayesikiliza,
kwa kadiri unavyohitaji baraka za Mungu - -
13:12 - 13:18Labda leo una shida
ambayo unatamani Mungu atatue - -
13:18 - 13:20unapaswa pia kuthamini usindikaji wa Mungu.
-
13:20 - 13:23Kwa sababu mara tu unapothamini mchakato wa Mungu,
-
13:23 - 13:28utapata neema ya kusubiri wakati wa Mungu bila kufadhaika sana.
-
13:28 - 13:32Na ninakumbuka Ndugu Chris alisema
kwamba baraka tunazopokea -
13:32 - 13:37sio mwisho wenyewe bali ni njia ya kufikia mwisho, ambayo ni wokovu wa nafsi zetu.
- Title:
- Mtoto Wetu Ni UTHIBITISHO kuwa Mungu Anajibu MAOMBI!!!
- Description:
-
Utiwe moyo na ushuhuda huu mzito kutoka kwa Mr & Mrs Keneth, Watanzania waishio Marekani, ambao Mungu aliwabariki kwa tunda la tumbo la uzazi baada ya kupokea maombi kutoka kwa Ndugu Chris - muda mfupi baada ya uzinduzi wa TV ya Moyo wa Mungu kabla hata Huduma za Maombi ya Pamoja hazijaanza - na kuchagua kukabidhi hali zao kabisa kwa Mungu!
Je, ungependa kujiunga na Huduma ya Maombi ya Pamoja na Ndugu Chris ili kupokea maombi bila malipo kupitia Zoom? Tuma ombi lako la maombi hapa - https://www.godsheart.tv/zoom
#Ushuhuda
➡️ Pata Kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Saidia TV ya Moyo wa Mungu kifedha - https://godsheart.tv/financial/
➡️ Habari kuhusu Maombi ya Pamoja - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live - Video Language:
- English
- Team:
God's Heart TV
- Duration:
- 14:08
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Our Baby Is PROOF God Answers PRAYERS!!! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Our Baby Is PROOF God Answers PRAYERS!!! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Our Baby Is PROOF God Answers PRAYERS!!! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Our Baby Is PROOF God Answers PRAYERS!!! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Our Baby Is PROOF God Answers PRAYERS!!! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Our Baby Is PROOF God Answers PRAYERS!!! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Our Baby Is PROOF God Answers PRAYERS!!! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Our Baby Is PROOF God Answers PRAYERS!!! |