Mgongano na Ujinga| Shafique Virani | TEDxUTSC
-
0:14 - 0:16Kwa hiyo nimetua tu kwa ajili ya mkutano wa TED,
-
0:16 - 0:18na wakati nilipokuwa nasubiria ndege uwanjani
-
0:18 - 0:21Nilitokea kukutana na rafiki wa familia
ambaye hatujaonana kwa muda mrefu. -
0:21 - 0:23Tunamwita mjomba Anwar
-
0:23 - 0:27na anafanana sana Babar wa komedia maarufu ya Kikanada
-
0:27 - 0:28Msikiti mdogo kwenye Praire.
-
0:28 - 0:29(Vicheko)
-
0:29 - 0:32Anapenda kuvaa nguo zake za kiasili za
pajama za kurta, -
0:32 - 0:37anajitambia ndevu na lafudhi ya kupendeza ya Kipakistani.
-
0:37 - 0:39Kwa hiyo alinikimbilia na kunikumbatia,
-
0:39 - 0:43na kusema, "Unaendeleaje?
Unafanya nini siku hizi? " -
0:43 - 0:46Kwa hiyo nikamwambia kuwa nimekuwa Profesa wa Mafunzo ya Kiislamu,
-
0:46 - 0:50na najiweka bize nikisafiri na kutoa mafunzo
-
0:50 - 0:52kusaidia watu kuuelewa Uislamu
kidogo zaidi, -
0:52 - 0:55hasa baada ya 9/11.
-
0:56 - 0:58Alinitazama machoni na kusema,
-
0:58 - 1:01"Usizungumze na mimi kuhusu 9/11!
-
1:01 - 1:06Kila ninapoenda, kila mtu ananiangalia
kama ninawajibika kwa 9/11! -
1:06 - 1:10Mimi, nawajibika kwa 9/11?
-
1:10 - 1:13Maduka ya 7-Eleven labda, lakini sio 9/11! "
-
1:13 - 1:16(Vicheko) (Makofi)
-
1:16 - 1:18Kama nilivyomwambia Uncle Anwar,
-
1:18 - 1:21Nimekuwa nikisafiri sana
na kutoa mazungumzo mengi, -
1:21 - 1:23na moja yao ilikuwa katika Kilabu ya Taifa ya Waandishi wa Habari.
-
1:23 - 1:28Kipindi hicho, kemikali ya DHM ilikuwa ikizungumziwa sana.
-
1:28 - 1:32Kiuhalisia, katika Idaho, asilimia 86 ya waliofanyiwa uchunguzi
-
1:32 - 1:35walitaka kuipiga marufuku kemikali hii.
-
1:35 - 1:39Ningependa kuwaambia mambo kadhaa muhimu kuhusu kemikali hii,
-
1:39 - 1:41na kisha kuwauliza maoni yenu.
-
1:41 - 1:43Mambo yote nitayowaambia
-
1:43 - 1:47yamechapishwa katika fasihi zilizopitiwa na wanataaluma
-
1:47 - 1:50na zimethibitishwa na wanasayansi mahiri
-
1:50 - 1:53huko Harvard, MIT, Chuo Kikuu
cha Toronto, na Oxford. -
1:54 - 1:59DHM haina rangi, harufu wala ladha.
-
1:59 - 2:05Kuihema DHM kwa muda mrefu hudhuru sana mwili wa binadamu
-
2:06 - 2:11Dalili za kumeza DHM
ni pamoja na jasho jingi, kukojoa, -
2:11 - 2:17na kuhisi kujaa gesi, kizunguzungu, kichefuchefu, kutapika na kukosa usawa wa elektrolaiti ya mwili.
-
2:18 - 2:24DHM imekutwa katika wagonjwa wa kansa.
-
2:25 - 2:27Kuivuta DHM kwa bahati mbaya
-
2:27 - 2:31ni chanzo kikuu cha tatu duniani cha kifo cha bila kunuia,
-
2:31 - 2:34na kusababisha vifo karibu 400,000 kila mwaka,
-
2:34 - 2:38kulingana na takwimu za Shirika la Afya Duniani.
-
2:39 - 2:41Kwa wale ambao watakuwa wategemezi,
-
2:41 - 2:45Uondoaji wa DHM humaanisha namna fulani ya kifo.
-
2:46 - 2:53Kutokana na habari hii, wangapi kati yenu mtaruhusu DHM kupatikana bure?
-
2:55 - 2:57Karibia hamna yoyote.
-
2:57 - 2:59Mmekubaliana kikamilifu na watu
-
2:59 - 3:02niliyoongea nao katika Kilabu ya Taifa ya Waandishi wa Habari.
-
3:02 - 3:04Napenda kuwaambia zaidi kidogo kuhusu hilo.
-
3:04 - 3:07DHM ni Dioksidi ya Hidrojeni Monoksidi.
-
3:07 - 3:11Pia inajulikana kama Hidrojeni Hydroksidi.
-
3:11 - 3:14Lakini wengi wetu labda tunajua
kwa jina lake la kawaida, -
3:14 - 3:16ambayo ni maji.
-
3:18 - 3:22Kila nilichowaambia ni ukweli
-
3:22 - 3:27uliothibitishwa na wanasayansi bora duniani kote.
-
3:27 - 3:31Na bado, karibu kila mtu katika hadhira hapa
-
3:31 - 3:35yuko tayari kupunguza upatikanaji wetu wa maji.
-
3:36 - 3:40Tunapowasilishiwa kipengele fulani cha habari tu,
-
3:40 - 3:45hujikuta tukifanya makosa katika ukadirifu wetu na maamuzi mabaya.
-
3:46 - 3:49Hadithi ya DHM inadhihirisha mengi kuhusu
-
3:49 - 3:52mada ambayo nataka
kuzungumza nanyi, -
3:52 - 3:57aina nyingine ya DHM
ambayo ni mbaya zaidi kuliko hii. -
3:57 - 4:01DHM ya kwanza ni
Dioksidi ya Hidrojeni Monoksidi, -
4:01 - 4:05lakini ya pili ni kubagua utu wa Waislamu.
-
4:06 - 4:07Media Tenor,
-
4:07 - 4:11moja ya mashirika ya ulimwengu yanayoongoza katika maarifa na ufanisi wa vyombo vya habari,
-
4:11 - 4:14ilipitia karibia nukuu milioni moja
kuhusu Waislamu -
4:14 - 4:18katika vyombo vya habari vya Marekani na Ulaya.
-
4:18 - 4:24asilimia 98 ya simulizi zilikuwa kuhusu ya wanamgambo wa Kiislam.
-
4:24 - 4:31asilimia 2 tu zilikuwa kuhusu Waislamu wa kawaida bilioni 1.5,
-
4:31 - 4:35robo ya wakazi wa dunia,
-
4:35 - 4:37ambao tunaishi wote kwenye hii dunia.
-
4:38 - 4:43Hii hali ni sawa na taarifa kuhusu niliyowapa kuhusu DHM.
-
4:43 - 4:50Wakati habari zote tulizonazo ni kuhusu kipengele kimoja kisicho cha kawaida
-
4:50 - 4:54sio tu tunashindwa kukielezea kipengele hicho,
-
4:54 - 4:58lakini tunapata maana isiyo sahihi kabisa kuhusu suala hilo.
-
4:58 - 5:03Tumechanganya vitendo
-
5:03 - 5:08vya sehemu ndogo sana ya Waislamu duniani
-
5:08 - 5:12na vya watu bilioni 1.5 duniani kote.
-
5:12 - 5:16Ni sawa kama tukichukulia matendo ya Ku Klux Klan,
-
5:16 - 5:18kuchoma msalaba, na kusema,
-
5:18 - 5:22"Hii ni uwakilishi
wa Ukristo wote. " -
5:22 - 5:26Kwa bahati mbaya, aina hii ya mchanganyiko unazidi kuongezeka na kuwa wa kawaida,
-
5:26 - 5:31kama tunavyoona katika ujumbe nyuma ya lori hilo, ambao unasema,
-
5:31 - 5:36"Kila kitu nilicho wahi kuhitaji kujifunza kuhusu Uislamu nilijifunza 9/11. "
-
5:38 - 5:41Naikumbuka 9/11 vizuri sana.
-
5:41 - 5:44Nilikuwa nimeteuliwa katika kitivo cha Chuo Kikuu cha Harvard,
-
5:44 - 5:48na nilipokuwa nikijiandaa na darasa langu la kwanza.
-
5:48 - 5:50Nakumbuka darasa hilo.
-
5:50 - 5:54Wanafunzi na mimi tulijitahidi kuelewa
-
5:54 - 5:57uovu tuliokuwa tumeshuhudia.
-
5:58 - 6:00Nilichokuta kinatia moyo
-
6:00 - 6:07ilikuwa kwamba wote walikuwa wazi na wenye nia ya kujifunza na kuelewa.
-
6:07 - 6:11Waligundua kuwa katika miaka yao yote ya kujifunza shuleni
-
6:11 - 6:16hawakuwa na ukaribu na ulimwengu wa Kiislamu
-
6:16 - 6:19na kwa hiyo, walitaka kuelewa.
-
6:19 - 6:24Walitaka kuiona
dunia hii katika uhalisia wake. -
6:24 - 6:29Tofauti kati ya ujumbe nyuma ya lori hii na hawa wanafunzi
-
6:29 - 6:33inanikumbusha kifungu katika kitabu ambacho ninatafsiri
-
6:33 - 6:38kilichotungwa na mwandishi maarufu
kwa jina la Nasiruddin Tusi, -
6:38 - 6:40mmoja ya wanasayansi maarufu wa Kiislamu
-
6:40 - 6:43na wanafalsafa kutoka zama za Kati.
-
6:43 - 6:45Kifungu hiki kinasema,
-
6:45 - 6:52"Yeye asiyejua na hajui
kwamba hajui ni mpumbavu. -
6:52 - 6:54Muepuke.
-
6:54 - 6:59Yeye asiyejua na anajua
kwamba hajui ni mtafutaji. -
6:59 - 7:01Mfundishe.
-
7:02 - 7:07Yeye anayejua na hajui
kwamba anajua amelala. -
7:07 - 7:08Muamshe.
-
7:09 - 7:15Na yeye anayejua na anajua kwamba anajua ni mwenye hekima.
-
7:15 - 7:17Mfuate. "
-
7:19 - 7:23Moja ya sababu 9/11 imewekwa kwenye kumbukumbu yangu,
-
7:23 - 7:26labda kuliko watu wengine wengi
-
7:28 - 7:30inaweza kusimuliwa na picha hii.
-
7:31 - 7:35Huyu ni mjomba wangu, Salman Dhanani.
-
7:35 - 7:39Alikuwa anajitolea katika jamii yake New York;
-
7:39 - 7:45mpiganaji wa kweli wa haki za binadamu aliyekuwa daima akisaidia katika nchi zinazoendelea.
-
7:47 - 7:51Alikuwa Makamu wa Rais
wa kampuni ya bima inayoitwa Aon, -
7:51 - 7:54ambayo ilikuwa na ofisi zake kwenye sakafu ya 99
-
7:54 - 7:58ya Mnara wa Kusini
ya Kituo cha Biashara cha Dunia -
7:59 - 8:02Katika siku hiyo ya huzuni,
-
8:02 - 8:05wakati ndege hizo
ziliangukia ndani ya majengo hayo, -
8:05 - 8:09alikuwa na jukumu
kwa kuwaokoa wafanyakazi wenzake. -
8:09 - 8:15Aliokoa maisha ya wenzake 80, na wakakimbia.
-
8:16 - 8:20Lakini hadi walipotoka,
alikuwa kachelewa. -
8:20 - 8:23Alikuwa amenaswa.
-
8:23 - 8:28Na leo amezikwa chini ya saruji
-
8:28 - 8:31ya lililowahi kuwa Kituo cha Biashara cha Dunia.
-
8:31 - 8:33Alikuwa na miaka 63.
-
8:35 - 8:39Picha hii imechukuliwa siku chache kabla ya kifo chake,
-
8:39 - 8:41wakati baadhi ya watu katika familia yangu,
-
8:41 - 8:47mjomba wangu Nizar, shangazi yangu Mumtaz
na binamu yangu Fatima walimtembelea -
8:47 - 8:50na walipiga picha hii
nje ya Umoja wa Mataifa. -
8:51 - 8:56Hawa ni Waislamu wa kawaida ambao hatusikii hadithi zao.
-
8:58 - 9:01Utupu wa ufahamu ambao tunao
-
9:01 - 9:04kuhusu ni robo ya binadamu
katika ulimwengu wa Kiislamu. -
9:04 - 9:09Nadhani imedhihirishwa vyema na kura iliyotolewa mwezi uliopita,
-
9:09 - 9:12na kati ya makampuni yanayoheshimika kwa upigaji kura dodoso nchini Marekani,
-
9:12 - 9:14Upigaji kura kwa ajili ya Sera ya Umma.
-
9:14 - 9:19Walihoji Wamarekani elfu moja, wa chama cha Democratic na cha Republican,
-
9:19 - 9:22na matokeo yake, ninakuahidi
-
9:22 - 9:26nisingeweza kufoji hata nikijaribu.
-
9:26 - 9:30Robo moja ya Wamarekani
wanafurahia kulipua Agrabah. -
9:30 - 9:32(Vicheko)
-
9:32 - 9:36Sasa, kwa wale ambao hamjui,
Agrabah ni ufalme wa kufikirika -
9:36 - 9:38kutoka hadithi maarufu ya Disney ya Aladdin.
-
9:38 - 9:41(Vicheko) (Makofi)
-
9:41 - 9:44Inashtua kwamba robo ya watu
-
9:44 - 9:47walitaka kulipua ufalme wa kufikirika
-
9:47 - 9:52labda kwa sababu itakuwa mahali fulani katika Mashariki ya Kati.
-
9:52 - 9:57Lakini nadhani hilo, inaelezea tu kidogo, sivyo?
-
9:57 - 10:04Kwa sababu picha tuliyo nayo
ya watu wa kawaida -
10:04 - 10:09wanaoishi katika sehemu hiyo ya ulimwengu ni kama ya kufikirika, sivyo?
-
10:10 - 10:15Na ni kitu ambacho nadhani
kimekua kutokea vizazi kadhaa. -
10:15 - 10:18Hata hivyo, labda ni kama unabii
-
10:18 - 10:21kwamba hii ilikuwa kuhusu ya kufikiria
ufalme katika Aladdin, -
10:21 - 10:24kwa sababu hiyo ilikuwa kati ya filamu nilizopenda nikiwa mdogo.
-
10:24 - 10:29Na ninakumbuka wimbo wa kwanza
wa msimulizi. -
10:29 - 10:33Waliimba, "Oh, nimetokea katika nchi,
Kutoka mahali pa mbali, -
10:33 - 10:36Ambapo ngamia za wasafiri huzunguka,
-
10:36 - 10:39Ambapo hukata sikio lako
Ikiwa hawapendi uso wako, -
10:39 - 10:43haijastaarabika, lakini ati, ni nyumbani! "
-
10:43 - 10:48Kutokea umri mdogo, watoto wanajifunza
-
10:48 - 10:55kwamba watu wa ulimwengu huu wa Kiislam sio wastaarabu, wakatili.
-
10:56 - 11:01Hakuna aliyefanya utafiti zaidi
kuhusu hili kuliko Profesa Jack Shaheen. -
11:01 - 11:03Alipitia filamu karibu na elfu moja
-
11:03 - 11:07zilizozalishwa zaidi ya kozi
ya zaidi ya miaka mia kupitia Hollywood -
11:07 - 11:11na kupatikana kumi na mbili tu
-
11:11 - 11:16ambayo ilionyesha Waislam au Waarabu
kwa nuru nzuri. -
11:16 - 11:18Kwa kweli, alifikia hitimisho
-
11:18 - 11:23kwamba kama kulikuwa na muigizaji wa kiume wa Kiislamu au wa Kiarabu katika filamu,
-
11:23 - 11:26kutakuwa na nafasi ya 95%
kwamba angeonyeshwa -
11:26 - 11:30kama mgomvi, mwenye tamaa au asiye muaminifu -
-
11:30 - 11:3395%!
-
11:36 - 11:40Watu kama Samuel Huntington
wameelezea hali yetu ya sasa ya ulimwengu -
11:40 - 11:43kama "Mgongano wa Ustaarabu."
-
11:44 - 11:45Zaidi kuwa wafikiriaji,
-
11:45 - 11:50ambao tunatambua na kuelewa
sehemu nyingine za dunia bora zaidi, -
11:50 - 11:55kutambua kwamba tunakabiliwa na "Mgongano wa Ujinga."
-
11:56 - 11:59Tunawezaje kukabiliana na Mgongano wa Ujinga?
-
11:59 - 12:02Naam, hili ni wazo
ambalo nadhani ni muhimu kueneza. -
12:03 - 12:05Mimi kukaa kwenye bodi ya uongozi
-
12:05 - 12:09ya Mpango wa Madrasa ya Watoto Afrika Mashariki,
-
12:09 - 12:16ambayo hufikia zaidi
maeneo duni ya mahali hapa, -
12:16 - 12:19kwa watoto ambao hawana uwezo wa kwenda shule.
-
12:20 - 12:22Miaka thelathini iliyopita,
-
12:22 - 12:25viongozi wa Kiislam kando ya pwani ya eneo hili
-
12:25 - 12:27walionana na mtukufu Aga Khan,
-
12:27 - 12:32ambaye babu yake alianzisha
shule za kwanza za jamii ya mchanganyiko wa taifa -
12:32 - 12:33katika mkoa mzima,
-
12:33 - 12:38kuuliza kama angeweza kuwasaidia kuwaelimisha watoto wadogo
-
12:38 - 12:41katika jamii hizi zisizohitajika.
-
12:42 - 12:46Kwa wakati huo, walianzisha mtaala wa ubunifu
-
12:46 - 12:49ambao umesisitizwa
kwenye CNN na BBC, -
12:49 - 12:53ambao unafundisha masomo yote
kama inavyotegemewa kawaida, -
12:53 - 12:54lakini kwa kuongeza,
-
12:54 - 12:57sehemu ya msingi ya mtaala
-
12:57 - 13:00kwamba watoto wangu, unaowaona katika picha hii,
-
13:00 - 13:03hujifunza kutoka katika umri mdogo
-
13:04 - 13:09ni kwamba lazima wautambue wingi wa ulimwengu.
-
13:09 - 13:11Wanapaswa kujifunza
kuhusu vikundi vya lugha, -
13:11 - 13:15makabila,
aina ya kabila na dini -
13:15 - 13:20wanaoshirikiana nao vijiji vyao, miji yao,
nchi yao na dunia yetu. -
13:20 - 13:26Kwa maneno mengine, watoto hawa wadogo
kukua na "maadili ya tamaduni nyingi." -
13:27 - 13:31Sasa, wengi wenu mnaweza kukumbuka,
mwanzoni mwa mwaka 2008, -
13:31 - 13:35Kenya ilikuwa inakabiliwa na vurugu kali.
-
13:35 - 13:38Vurugu za baada ya uchaguzi
zilipotokea kote nchini, -
13:38 - 13:41kulikuwa na mauaji mabaya
-
13:41 - 13:44pale wafuasi
wa rais Mwai Kibaki -
13:44 - 13:47walipigana dhidi ya wafuasi
wa mpinzani wake. -
13:48 - 13:52Kabila la Kikuyu, kabila la Luo, kabila la Kalenjin
walikuwa wanauana. -
13:52 - 13:57Maelfu ya watu waliuawa;
mamia ya maelfu walihamishwa. -
13:57 - 14:01Shule zetu zote sabini na tano
Kenya zilifungwa. -
14:01 - 14:03Tulikuwa na wasiwasi.
-
14:03 - 14:07Shule zetu zilipatikana
katika maeneo maskini zaidi ya nchi, -
14:07 - 14:12maeneo ambayo yanawezekana zaidi
kuathirika na vurugu hii. -
14:13 - 14:17Wakati bodi yetu ilipokuwa na mkutano wake,
-
14:17 - 14:23Niliomba mara moja ripoti iwe tayari kutuambia,
-
14:23 - 14:25"Ni nini kilichotokea kwa watoto wetu?"
-
14:25 - 14:28"Ni nini kilichotokea kwa walimu wetu?"
-
14:28 - 14:31"Je! Wazazi wanaojitolea
katika shule zetu wapo salama? " -
14:31 - 14:34"Je, jamii zetu zipo salama?"
-
14:34 - 14:36"Ni wangapi wamefariki?"
-
14:37 - 14:41Ripoti hiyo iliporudi,
tulishangazwa kwa kile tulichosoma. -
14:42 - 14:47Hakuna shule hata moja katika jumuiya zetu
-
14:47 - 14:51ilikuwa imeathiriwa na vurugu.
-
14:52 - 14:53Hata moja.
-
14:54 - 15:00Na nina uhakika kwamba ni kwa sababu,
kwa miaka thelathini iliyopita, -
15:00 - 15:04watoto hawa wamekua
kujifunza kuhusu majirani zao, -
15:04 - 15:08kujifunza kuhusu makabila,
na lugha, na nyimbo, -
15:08 - 15:13na dansi ya kila mtu
katika mazingira yao, -
15:13 - 15:15na katika ulimwengu unaowazunguka.
-
15:15 - 15:21Wamepewa chanjo ya kuepuka
virusi vya chuki na uharibifu -
15:21 - 15:24kwamba mara nyingi watu wanavyojaribu kueneza.
-
15:25 - 15:31Je! Unaweza kufikiri kama watoto
kote ulimwenguni wangepaswa kufundishwa -
15:31 - 15:33kama watoto hawa walivyofundishwa?
-
15:34 - 15:39Je! Tungeweza kuona unyanyasaji wa dini
katika nchi za Iraq na Syria kama tunavyoona sasa? -
15:39 - 15:43Je! Matatizo ya ubaguzi wa rangi
nchini Marekani yangekuwa kama yalivyo sasa? -
15:43 - 15:48Je! Unyanyapaa wa Uislamu ungekuwepo katika ulimwengu wa magharibi kama tunaoshuhudia sasa?
-
15:49 - 15:53Unajua, ufafanuzi wetu
ya mtu mwenye elimu nchi za Magharibi -
15:54 - 15:58ina maana kwamba wanapaswa kutuambia
kitu kuhusu Sir Isaac Newton, -
15:58 - 16:01kuhusu Mozart, kuhusu Napoleon.
-
16:02 - 16:05Lakini tungekuwa na wakati mgumu sana
-
16:05 - 16:08kugundua hata wengi ya watu walioelimika katika ulimwengu wa Magharibi
-
16:08 - 16:13ambao wanajua sawa na wale
katika ulimwengu wa Kiislamu. -
16:14 - 16:15Hii ni ukweli pamoja na kwamba
-
16:15 - 16:19kwamba maneno kama "algebra" na "algorithm" yametoka katika lugha ya Kiarabu;
-
16:19 - 16:24kwamba baadhi ya majengo mahiri ya kisanifu duniani,
-
16:24 - 16:29kama Taj Mahal,
yametokea katika tamaduni za Kiislamu; -
16:29 - 16:33na kwamba "Kanuni ya Utabibu", na Ibn Sina,
-
16:33 - 16:38ilikuwa ni kitabu kikuu cha utabibu Ulaya kwa miaka mingi.
-
16:40 - 16:45Tunahitaji kutekeleza maono ya kimataifa katika mtaala wetu wa elimu
-
16:45 - 16:48kutokea umri mdogo kabisa,
-
16:48 - 16:53ili watoto wakue na ufahamu wa
ulimwengu ambao tunaishi, -
16:53 - 16:55watu ambao ni sehemu ya jamii yetu.
-
16:56 - 17:01Katika mlango wa Umoja wa Mataifa
kumeandikwa shairi la Kiajemi -
17:01 - 17:06la Sa'di-yi Shirazi, mshairi wa Kiislamu wa karne ya 13, ambaye ameandika,
-
17:07 - 17:10(Kiajemi) Watoto wa Adamu
ni kama viungo vinavyotegemeana. -
17:10 - 17:15"Watoto wa Adamu
ni kama viungo vya mmoja na mwingine -
17:15 - 17:18Kwa maana wote walikuwa wameumbwa kutoka kwa nafsi moja.
-
17:19 - 17:23Pale misukosuko ya wakati
huumiza mguu mmoja, -
17:23 - 17:28inawezekana vipi viungo vingine kuwa na amani?
-
17:28 - 17:32Wewe usiyehisi maumivu ya wengine
-
17:32 - 17:37Unawezaje kujiiita mwana wa Adamu?
-
17:37 - 17:41Unawezaje kujiita binadamu? "
-
17:41 - 17:43Ile hisia kwamba sisi ni familia moja ya binadamu
-
17:43 - 17:50imepelekea baadhi ya hadithi za kusisimua zinazotia moyo katika siku za hivi karibuni.
-
17:50 - 17:54Katika miezi michache iliyopita,
kama matokeo ya mashambulizi ya kigaidi, -
17:54 - 17:57baadhi ya misimamo ya kikatili katika Magharibi
-
17:57 - 17:59imegeuka dhidi ya Waislamu kati yao,
-
17:59 - 18:03ambao hawakuwa na la kufanya
na mashambulizi haya ya kigaidi. -
18:03 - 18:07Tumeona wanawake wakisukumizwa
mbele ya mabasi yanayotembea, -
18:07 - 18:09misikiti ikichomwa moto,
-
18:09 - 18:14na kichwa cha nguruwe
kutupwa katika shule ya watoto. -
18:14 - 18:16Wakati matukio haya yalianza kutokea
-
18:16 - 18:20na Waislamu waliogopa
kwenda nje katika jamii zao, -
18:20 - 18:24ndani ya masaa manne
jumbe za Twitter 150,000 nchini Australia, -
18:24 - 18:28zenye lebo
"Nitaendesha na wewe", ziliwekwa mtandaoni. -
18:28 - 18:30"Nitaendesha na wewe."
-
18:30 - 18:33Tuko pamoja nawe.
Wewe ni sehemu ya jumuiya yetu. -
18:33 - 18:36Huna chochote cha kuhofia.
-
18:36 - 18:37Wiki chache zilizopita,
-
18:37 - 18:42al-Shabab walishambulia basi
njiani kwenda Mandera -
18:42 - 18:45kwenye mpaka wa Somalia na Kenya.
-
18:45 - 18:47Walijaribu kuchukua Wakristo tu kutoka kwenye basi
-
18:47 - 18:50kuwaua kinyama,
-
18:50 - 18:52lakini Waislamu wailo kwenye basi hilo
-
18:52 - 18:57walikataa kuruhusu ndugu zao wakristo wauawe.
-
18:57 - 19:02Waliwaambia magaidi,
"Huwezi kuchukua Wakristo hawa." -
19:02 - 19:06"Ikiwa unataka kuwaua,
utatuua sisi sote. " -
19:06 - 19:11Wale magaidi waliogopa sana
kwamba wakimbia. -
19:14 - 19:19Ikiwa tuna ufahamu kuhusu majirani zetu,
-
19:19 - 19:22watu wanaounda ulimwengu wetu,
-
19:22 - 19:26tutakuwa na silaha ya
kusimama dhidi ya mtu yeyote -
19:26 - 19:31ambaye anatarajia kutoa utu wa wengine,
ambaye anatarajia kutugawanya, -
19:32 - 19:38kwa sababu katika maneno ya Sa'di wa Shiraz,
sisi wote ni watoto wa Adamu, -
19:38 - 19:42sisi ni familia moja ya binadamu.
-
19:42 - 19:44Asante.
-
19:44 - 19:46(Kushangilia)(Makofi)
- Title:
- Mgongano na Ujinga| Shafique Virani | TEDxUTSC
- Description:
-
Akitoa ushahidi wa kustaajabisha, simulizi binafsi za kuvunja moyo, na ufahamu maridadi katika matukio ya ulimwengu, Dk. Shafique Virani anatuhimiza kukabiliana na mgongano na Ujinga kati ya Ulimwengu wa Magharibi na Uislamu, kuiondoa kuta za habari zisizo sahihi na kuweka madaraja ya ufahamu. Akitoa wito kwa uanadamu wetu, Dk. Virani anatoa njia ya maono, na huhamasisha matumaini kwa ajilli ya siku za mbeleni.
Profesa maarufu wa Mafunzo ya Kiislamu katika Chuo Kikuu cha Toronto, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha utamaduni wa Kusini mwa Asia, na Mwenyekiti wa awali wa Idara ya Mafunzo ya Historia, Dr Shafique Virani (PhD, Chuo Kikuu cha Harvard) ni mwandishi mwenye tuzo na kutambulika kimataifa kama msemaji wa umma aliyehutubia watu kutoka zaidi ya nchi 50 na wasikilizaji zaidi ya 15,000. Kitabu chake, Kina Ismaili katika zama za Kati: Historia ya uhimidi, Utafutaji wa Wokovu, inaaminika kuwa kitabu cha kwanza cha kitaaluma kutoka kwenye chuo kikuu kuu kuwa trailer yake cheyewe. Akitambulika kama”muonaji," Umoja wa Mataifa ulimtukuza kwa juhudi zake "katika kupanua mipaka ya ujuzi na ustawi wa wanadamu."
Majadiliano haya yalitolewa kwenye tukio la TEDx kwa kutumia muundo wa mkutano wa TED lakini kwa uhuru uliopangwa na jumuiya ya eneo. Jifunze zaidi katika http://ted.com/tedx
- Video Language:
- English
- Team:
closed TED
- Project:
- TEDxTalks
- Duration:
- 19:54
![]() |
Aviva Nassimi edited Swahili subtitles for Confronting the clash of ignorance | Shafique Virani | TEDxUTSC | |
![]() |
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for Confronting the clash of ignorance | Shafique Virani | TEDxUTSC | |
![]() |
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for Confronting the clash of ignorance | Shafique Virani | TEDxUTSC | |
![]() |
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for Confronting the clash of ignorance | Shafique Virani | TEDxUTSC | |
![]() |
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for Confronting the clash of ignorance | Shafique Virani | TEDxUTSC | |
![]() |
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for Confronting the clash of ignorance | Shafique Virani | TEDxUTSC | |
![]() |
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for Confronting the clash of ignorance | Shafique Virani | TEDxUTSC | |
![]() |
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for Confronting the clash of ignorance | Shafique Virani | TEDxUTSC |