< Return to Video

President Obama Speaks on the Death of Nelson Mandela - captioned

  • 0:02 - 0:09
    Akishtakiwa mahakamani mnamo mwaka wa1964, Nelson Mandela alifunga kauli yake akisema
  • 0:10 - 0:17
    "Nimepigana dhidi ya utawala usio na haki wa watu weupi pia dhidi ya utawala usio na haki ya watu weusi."
  • 0:18 - 0:23
    Nimetunza maadili ya jamii huria na ya kidemokrasia
  • 0:23 - 0:29
    ambapo watu wote wanaishi pamoja wakisikilizana katika amani wakiwa na fursa iliyo na haki kujiendeleza.
  • 0:29 - 0:36
    Ni maadili yenye matumaini ya kuendesha maisha yangu ili yatekelezwe. Lakini vinginevyo ni maadili ambayo
  • 0:36 - 0:40
    mimi niko tayari kufa kwa ajili yake.
  • 0:40 - 0:47
    Naye Marehemu Mheshimiwa Nelson Mandela akaishi katika harakati zenye kutekeleza maadili hayo akayafanya kuwa wa ukweli.
  • 0:47 - 0:51
    Alitimiza zaidi ya yanayo tarajiwa na mtu yeyote yule.
  • 0:51 - 0:53
    Leo ameenda nyumbani kwa Mola Wetu.
  • 0:53 - 0:58
    Mtu mheshimiwa shujaa, mashuhuri, ametuacha
  • 0:58 - 1:00
    naye mtu mzuri kwa dhati mfano kwa watu wote
  • 1:00 - 1:04
    ambaye tutapaswa kushirikiana naye duniani humu.
  • 1:04 - 1:10
    ametuacha si mmojawetu tena yupo na wahenga.
  • 1:10 - 1:12
    Kwa heshima zake za kishujaa ikiwa na nia yake imara
  • 1:12 - 1:17
    kujitolea mhanga kwa ajili ya uhuru wa wengine pasi na uhuru wake mwenyewe,
  • 1:17 - 1:22
    Madiba alibadilisha Afrika Kusini akitusukuma sisi sote tuendelee kutafuta haki.
  • 1:22 - 1:27
    Safari yake ya kwenda katika uraisi ilipoanza akiwa mfungwa ilijumuisha ahadi ya kuwa
  • 1:27 - 1:33
    binadamu wote pamoja na nchi zote zinaweza kubadilika ziwe bora zaidi.
  • 1:33 - 1:36
    Ahadi yake kuhamisha utawala kutoka kwa wabeberu kwa watu wote wa Afrika Kusini
  • 1:36 - 1:37
    akipatana na wale walimofunga jela
  • 1:37 - 1:43
    ikawa mfano kwa watu wote kuutamani
  • 1:43 - 1:46
    ama ukiwa katika maisha ya mataifa au maisha kibinafsi.
  • 1:46 - 1:51
    Tusisahu hulka zake za adabu, uungwana na uchangamfu
  • 1:51 - 1:54
    akijikosoa
  • 1:54 - 1:58
    ndio awe mtu wa kusifika.
  • 1:58 - 1:58
    Kama alivyosema mara,
  • 1:58 - 2:05
    "Mimi si mtakatifu isipokuwa umembunia mtakatifu kama mwenye dhambi ambaye daima anajaribu awe mtii.
  • 2:08 - 2:09
    Mimi ni mmojawapo wa wale wasiohesabika
  • 2:09 - 2:13
    aliyetiliwa moyo na maisha ya Marehemu Nelson Mandela.
  • 2:13 - 2:16
    Kitendo changu cha kwanza cha kisiasa
  • 2:16 - 2:23
    cha kwanza kilichohusika na masuala ya sera ama siasa
  • 2:24 - 2:26
    kilikuwa kupinga sera za kugawanya watu kutokana na rangi ya ngozi inayoitwa apartheid.
  • 2:26 - 2:32
    Nilisoma kwa makini maneno na maandishi yake.
  • 2:32 - 2:35
    Siku alipoachiliwa huru
  • 2:35 - 2:37
    ilinipa mimi uelewano wa uwezo wa binadamu
  • 2:37 - 2:41
    wanapoongozwa na matumaini yao si uwoga wao.
  • 2:41 - 2:44
    Na kama wengine wengi duniani kote, siwezi kujifikiria katika maisha yangu
  • 2:44 - 2:49
    pasi na mfano uliowekwa na Marehemu Mheshimiwa Nelson Mandela.
  • 2:49 - 2:55
    Katika maisha yangu yote nitafanya kadiri niwezavyo kujifunza kutoka kwake.
  • 2:55 - 2:59
    Kwa Graca Machel na jamaa zake
  • 2:59 - 3:04
    mimi pamoja na mke wangu Michelle tunatoa pole pole sana ikiwa na shukrani mno
  • 3:04 - 3:08
    kwa kumshirikisha mtu asiye na kifani na sisi.
  • 3:08 - 3:13
    Kazi yake ya maisha ilimtenga siku nyingi ndefu na wapendwa wake wa moyo.
  • 3:13 - 3:16
    Tumaini la pekee langu ni muda huu mfupi mliokuwa naye
  • 3:16 - 3:20
    ulileta amani na utulivu kwa jamaa zake wote.
  • 3:20 - 3:22
    Kwa raia wa Afrika Kusini,
  • 3:22 - 3:28
    sisi tunanufaika kutoka kwa mfano wa ufanyaji upya ukiwa na usuluhisho na unyumbukaji
  • 3:28 - 3:30
    mliofanya kuwa ukweli.
  • 3:30 - 3:37
    Afrika Kusini huria ikiwa na usalama wa wenyewe kwa wenyewe ndiyo mfano kwa dunia nzima.
  • 3:37 - 3:44
    Ndio urithi wa Madiba kwa talifa alilolipenda.
  • 3:44 - 3:49
    Huenda hatutawahi kumpata mfano wake Marehemu Mheshimiwa Nelson Mandela kwa mara nyingine.
  • 3:49 - 3:56
    Ndio sisi tuliovalishwa njuga kadiri tuwezavyo kusogeza mbele mfano uliowekwa naye:
  • 3:56 - 3:59
    Kukata shauri zikiongozwa na upendo si chuki;
  • 3:59 - 4:03
    kutompunguzia umuhimu wa mchango wa mtu mmoja;
  • 4:03 - 4:09
    kujitashidi kutengeneza mambo ya usoni yanayostahiki kujitolea mhanga kwake.
  • 4:09 - 4:16
    Sasa hivi, tusite tukishukuru ukweli wa maisha yake Mheshimiwa Marehemu Nelson Mandela
  • 4:16 - 4:23
    mtu ambaye alishika mambo ya kale mikononi mwake akipinda tao la ulimwengu wa maadili iielekee kwa haki ya binadamu
  • 4:24 - 4:27
    Mungu ibariki kumbukumbu yake Amwekee mahali pema upeponi.
Title:
President Obama Speaks on the Death of Nelson Mandela - captioned
Description:

Original video: http://youtu.be/eIbwXCbiklY
Transcript: http://www.whitehouse.gov/the-press-office/2013/12/05/statement-president-death-nelson-mandela

more » « less
Video Language:
English
Team:
Captions Requested
Duration:
04:38

Swahili subtitles

Revisions