< Return to Video

Solving two-step equations | Linear equations | Algebra I | Khan Academy

  • 0:01 - 0:04
    Sasa tumechanganya vitu kidogo:
  • 0:04 - 0:07
    upande wa kushoto wa mizani, sio tu tuna
  • 0:07 - 0:11
    hivi vitu vitatu vya bluu vinavyofanana vyenye uzito usiofamika kila kimoja kikiwa na uzito x,
  • 0:11 - 0:14
    pia tuna vitu vya uzito wa kg 1 hapa,
  • 0:14 - 0:16
    tunavyo viwili.
  • 0:16 - 0:19
    Sasa, tunaenda kutafuta X ni ngapi.
  • 0:19 - 0:23
    Lakini kabla hata hatujafanya hivyo, nataka ufikirie mlinganyo wa kihesabu
  • 0:23 - 0:28
    utakaowakilisha kinachoendelea, tulichonacho upande wa kushoto kikilinganishwa na
  • 0:28 - 0:32
    tulichonacho upande wa kulia katika mizani.
  • 0:32 - 0:33
    Nitakupa sekunde chache ufukirie...
  • 0:35 - 0:38
    Hebu tufikirie tulichonacho upande wa kushoto:
  • 0:38 - 0:46
    tuna vitu vitatu vyenye uzito X, kwa hiyo unaweza sema tuna 3x
  • 0:46 - 0:52
    na halafu tuna vitu viwili vya uzito wa kilogramu 1, kwa ujumla tuna kg 2. Kwa hiyo + 2.
  • 0:52 - 0:57
    Kwa hiyo njia moja ya kufikiria kuhusu uzito wa upande wa kushoto ni 3x + 2.
  • 0:57 - 1:01
    Vitu vitatu vyenye uzito X jumlisha kilogram mbili.
  • 1:01 - 1:03
    Hicho ndicho tulichonacho upande wa kushoto.
  • 1:03 - 1:06
    Sasa, hebu tufukirie kuhusu tulichonacho upande wa kulia.
  • 1:06 - 1:07
    Tunaweza kuvihesabu.
  • 1:07 - 1:12
    Viko 14.
  • 1:12 - 1:19
    Vipande 14, kila kimoja kina uziti wa kg 1, kwa hiyo jumla ya uzito ni kg 14.
  • 1:19 - 1:24
    Na tunaona kwamba mizani iko sawa, haijapinda chini au juu.
  • 1:24 - 1:29
    Kwa huu uzito wa hapa lazima uwe sawa na huu uzito wa jumla.
  • 1:29 - 1:34
    Mizani iko sawa, kwa hiyo tunaweza kuandika alama ya sawa sawa.
  • 1:34 - 1:37
    ngoja niandike kwa rangi ya kijivu.
  • 1:37 - 1:41
    Sasa, ninachotaka ufikiri,
  • 1:41 - 1:45
    na unaweza kufikiria ama kwa kutumia alama au mizani, ni:
  • 1:45 - 1:48
    utafanyaje -- hebu tufikirie vitu vichache:
  • 1:48 - 1:54
    utafanyaje kwanza ili uondoe hivi vipande vidogo vya kg 1?
  • 1:54 - 1:57
    Nakupa muda ufilirie kuhusu hilo..
  • 1:59 - 2:01
    Kitu kirahisi ni:
  • 2:01 - 2:04
    unaweza kuondoa hivi vipande vya kg 1 upande wa kushoto,
  • 2:04 - 2:07
    lakini kumbuka, ukiviondoa hivi vipande upande wa kushoto,
  • 2:07 - 2:10
    na mizani ilikuwa sawa, sasa upande wa kushoto utakuwa mwepesi
  • 2:10 - 2:14
    na utapanda juu. Lakini tunataka kuuweka sawa ili tuendelee kusema
  • 2:14 - 2:16
    Uzito huu ni sawa na uzito huo.
  • 2:16 - 2:21
    Kwa hiyo tukiondoa vipande viwili upande wa kushoto, tunatakiwa pia tuondoe vipande viwili upande wa kulia.
  • 2:21 - 2:26
    Kwa hiyo, tutaondoa viwili pale, na halafu tutaondoa viwili pale.
  • 2:26 - 2:31
    Kihesabu, tunachokifanya, tunatoa kilogramu 2 kila upande.
  • 2:31 - 2:34
    Tunatoa 2 upande huu,
  • 2:34 - 2:39
    Kwa hiyo upande wa kushoto sasa tuna 3x + 2, kutoa 2
  • 2:39 - 2:43
    tunatakiwa na 3x,
  • 2:43 - 2:48
    na upande wa kulia tuna 14 na tumetoa 2
  • 2:48 - 2:53
    kwa hiyo tutaenda kubakiwa na vipande 12.
  • 2:53 - 2:56
    Na unaweza kuona nilizozikata, nimebakiwa na 12,
  • 2:56 - 2:59
    na hapa bloku 3 za X.
  • 2:59 - 3:02
    Kwa vile tumeondoa kiwango kile kile pande zote,
  • 3:02 - 3:08
    mizani yetu bado iko sawa. Na mlinganyo wetu: 3x ni sawa na 12.
  • 3:08 - 3:13
    Sasa , hii imekuwa sawa na hesabu tulioiona katika video ya mwisho.
  • 3:13 - 3:17
    sasa ninakuukiza: tufanye nini tuitenge x moja,
  • 3:17 - 3:21
    kuwa na X moja tu upande wa kushoto wa mizani,
  • 3:21 - 3:25
    wakati tunaendelea kuifanya mizani sawa?
  • 3:28 - 3:31
    Njia rahisi ya kufikiria hii ni:
  • 3:31 - 3:35
    Kama nikitaka X moja upande wa kushoto, hiyo ni theluthi ya jumla ya X hapa.
  • 3:35 - 3:39
    Kwa hiyo vipi kama nikizidisha upande wa kushoto na theluthi --
  • 3:39 - 3:44
    -- lakini kama nataka kuufanya mzani sawa, natakiwa kuzidisha upande wa kulia na theluthi.
  • 3:44 - 3:46
    Kama tunaweza kufanya hilo kihesabu,
  • 3:46 - 3:50
    Hapa naweza kuzidisha upande wa kushoto kwa 1/3,
  • 3:50 - 3:55
    na kama nikitaka mzani wangu kuwa sawa pia natakiwa kuzidisha upande wa kulia kwa 1/3.
  • 3:55 - 4:01
    Kuzidisha kwa uhalisia inamaanisha; baki na 1/3 ya kiasi ulichokuwa nacho mwanzo
  • 4:01 - 4:04
    Tutaondoa hizi mbili.
  • 4:04 - 4:06
    Kama tukitaka kunakuwa na theluthi ya kiasi tulichokuwa nacho mwanzo,
  • 4:06 - 4:09
    -- kuna vipande 12 vimebaki baada ya kuondoa viwili vya mwanzo --
  • 4:09 - 4:15
    kwa hiyo, 1/3 ya 12: tutaenda kubakiwa na vipande vinne vya kg 1.
  • 4:15 - 4:21
    Hebu niondoe vyote nibakishe vinne
  • 4:21 - 4:25
    Na nimebakiwa na 4 hapa.
  • 4:25 - 4:28
    Na kwa hiyo ukichobakiwa nacho,
  • 4:28 - 4:33
    ni hii 'X'. - Nitaiwekea kivuli kuonyesha hii moja ndiyo tuliyobakiwa nayo -
  • 4:33 - 4:37
    na halafu tuna hivi vipande vya kg 1.
  • 4:37 - 4:41
    Unaweza kuona kihesabu hapa: 1/3 * 3x
  • 4:41 - 4:46
    -- au unaweza kusema 3x gawanya kwa 3 -- kwa njia yoyote hii inatupa
  • 4:46 - 4:50
    -- hizi tatu zinakwisha, kwa hiyo hiyo inakupa X
  • 4:50 - 4:57
    na upande wa kulia 12 * 1/3 - ambayo ni sawa na 12/3, ni sawa na 4.
  • 4:57 - 5:03
    Na kwa vile tumefanya kitu kile kile kwa pande zote, mizani yetu bado iko sawa.
  • 5:03 - 5:08
    Kwa hiyo unaona uzito wa kitu hiki unatakiwa uwe sawa na uzito wa vioande hivi 4.
  • 5:08 - 5:11
    x ni sawa na kilogramu 4.
Title:
Solving two-step equations | Linear equations | Algebra I | Khan Academy
Description:

more » « less
Video Language:
English
Team:
Khan Academy
Duration:
05:12

Swahili subtitles

Revisions