< Return to Video

Je, unahangaika na MSONGO WA MAWAZO? USHUHUDA huu utakutia moyo!

  • 0:00 - 0:02
    Sina msononeko tena.
  • 0:02 - 0:09
    Kwa kweli, msononeko uliniacha siku hiyo baada ya kumaliza Maombi ya Pamoja.
  • 0:09 - 0:12
    Nilihisi amani sana.
  • 0:15 - 0:23
    Je, ni eneo gani la maisha yako unapitia, unakumbana na utumwa?
  • 0:23 - 0:28
    Leo ni siku yako ya uhuru.
    Pokea uhuru sasa hivi!
  • 0:28 - 0:40
    Uhuru katika familia yako, afya, kazi, fedha, biashara - pokea uhuru!
  • 0:42 - 0:46
    Naitwa Tumpale,
    nikishuhudia kutoka Tanzania.
  • 0:46 - 0:53
    Mwaka jana tarehe 2 Machi 2024,
    nilijiunga na Maombi ya Pamoja.
  • 0:53 - 0:57
    Nilikuwa na matatizo matatu makubwa maishani mwangu.
  • 0:57 - 1:05
    Niligunduliwa na ugonjwa wa uvimbe anuai kwenye ovari (Polycystic Ovarian Syndrome) , ambao nilikuwa nao kwa zaidi ya miaka kumi.
  • 1:05 - 1:12
    Kwa muda wote huo, nilikuwa nikipambana na hedhi isiyo ya kawaida.
  • 1:12 - 1:17
    Kulikuwa na nyakati ambapo
    mwaka mzima ungepita bila ya mimi
  • 1:17 - 1:22
    kupata hedhi yangu,
    na hilo liliniathiri sana.
  • 1:22 - 1:31
    Nchini Tanzania, mimi na mama yangu tulijaribu kutafuta matibabu kutoka kwa madaktari tofauti.
  • 1:31 - 1:36
    Nilitumia dawa nyingi tofauti
    bila mafanikio
  • 1:36 - 1:44
    na utambuzi niliopewa hapa ni kwamba nilikuwa na ukosefu wa usawa wa homoni.
  • 1:44 - 1:52
    Shida iliendelea hadi nikalazimika kusafiri kwenda India kwa ajili ya Shahada yangu ya Kwanza.
  • 1:52 - 1:58
    Nikiwa India, nilijiambia, 'Acha nitafute matibabu hapa.
  • 1:58 - 2:02
    Ngoja nione kama naweza kupata msaada
    wa kuliondoa tatizo hili'-
  • 2:02 - 2:07
    kwa sababu ilikuwa ikiniathiri kiakili
    na nilikuwa na wasiwasi.
  • 2:07 - 2:12
    Wanawake wengi walio na ugonjwa wa uvimbe anuai kwenye ovari (Polycystic Ovarian Syndrome) wana shida
  • 2:12 - 2:15
    katika kupata watoto katika ndoa zao.
  • 2:15 - 2:24
    Kwa hiyo nikiwa India, nilienda hospitalini
    na nilipewa vipimo tofauti.
  • 2:24 - 2:28
    Hao ndio walionigundua
    na ugonjwa wa uvimbe anuai kwenye ovari (Polycystic Ovarian Syndrome) .
  • 2:28 - 2:31
    Lakini kwa Tanzania, niliambiwa kwamba
    nilikuwa na ukosefu wa usawa wa homoni.
  • 2:31 - 2:38
    Baada ya utambuzi huo, nilipewa
    dawa ambazo nilitumia,
  • 2:38 - 2:41
    lakini bado shida yangu haikutatuliwa.
  • 2:41 - 2:49
    Niliizoea lakini iliniathiri -
    ningejiona sijakamilika.
  • 2:49 - 2:52
    Ukiwa msichana, unatarajia kuwa 'wa kawaida'
    kama wenzako.
  • 2:52 - 2:55
    Niliiona kama sehemu ya maisha yangu.
  • 2:55 - 3:02
    Wakati huo mnamo Machi 2024,
    pia nilikuwa na maambukizi ya njia ya mkojo.
  • 3:02 - 3:08
    Matatizo hayo mawili hayakuwa matatizo yaliyonileta kwenye
  • 3:08 - 3:10
    Huduma ya Maombi ya Pamoja.
  • 3:10 - 3:14
    Tatizo kubwa lililoniletea
    ni msononeko.
  • 3:14 - 3:18
    Niliporudi Tanzania
    kwa ajili ya mafunzo yangu ya vitendo,
  • 3:18 - 3:23
    Niligundua kuwa mfumo hapa ni tofauti.
  • 3:23 - 3:31
    Sifa zinazohitajika ili mtu ajiandikishe kwa Shahada ya Kwanza
  • 3:31 - 3:35
    katika unusukaputi(anesthesia) hapa katika nchi yangu ni tofauti
  • 3:35 - 3:41
    na zile ambazo mtu anatakiwa kuwa nazo
    ili ajiandikishe nchini India.
  • 3:41 - 3:46
    Kwa hivyo katika nchi yangu sifa zinakuwa tofauti, ili uweze kwenda kwa digrii ya Shahada ya utaalamu wa unusukaputi(anesthesia).
  • 3:46 - 3:53
    inabidi uwe muuguzi mwenye uzoefu wa kufanya kazi usiopungua miaka miwili.
  • 3:53 - 3:56
    Hiyo ilikuwa changamoto kwangu
    kwa sababu niliporudi,
  • 3:56 - 4:03
    Ilinibidi nianze kufanya kazi kama
    muuguzi na mtaalamu wa unusukaputi.
  • 4:03 - 4:10
    Kwa hiyo ilikuwa vigumu kwa sababu sikuwahi kuwa muuguzi; kila kitu kilikuwa kipya kwangu.
  • 4:10 - 4:16
    Tofauti na wenzangu, hata mimi sikuwa na uzoefu. Nilikuwa sina uzoefu kabisa.
  • 4:16 - 4:21
    Ilikuwa mbaya sana kiasi
    kwamba nilikuwa nikidhihakiwa.
  • 4:21 - 4:28
    Nilichukuliwa kuwa mtu asiye na uzoefu zaidi. Nilikuwa najiona sina maana.
  • 4:28 - 4:35
    Ilikuwa mbaya sana - hadi nilikuwa
    na msongo huu.
  • 4:35 - 4:43
    Kwa hivyo nilikuwa nikipitia Facebook na YouTube, kisha nikakutana na TV ya Moyo wa Mungu.
  • 4:43 - 4:51
    Kisha nikatuma ombi la maombi. Hivyo ndivyo nilivyojiunga na Maombi ya Pamoja tarehe 2 Machi 2024.
  • 4:51 - 4:56
    Maombi yalipokuwa yakiendelea,
    nilihisi nguvu za Roho Mtakatifu
  • 4:56 - 4:58
    kwa sababu miguu yangu ilianza kutetemeka.
  • 4:58 - 5:06
    Nilianza kutetemeka na nilihisi maumivu makali ya kichwa na maumivu katika eneo la nyonga.
  • 5:06 - 5:11
    Mwishoni mwa maombi,
    nilihisi amani sana.
  • 5:11 - 5:17
    Kabla ya maombi, moyo wangu ulikuwa
    mzito sana. Nilikuwa nimepoteza matumaini.
  • 5:17 - 5:22
    Nilitaka hata kuacha. Sikutaka
    kwenda kazini tena.
  • 5:22 - 5:29
    Sikutaka kuendelea na kitu chochote kinachohusu unusukaputi (anesthesia) au mafunzo yangu ya kazi.
  • 5:29 - 5:34
    Lakini mwisho wa maombi, nilihisi amani.
  • 5:34 - 5:40
    Siwezi hata kuielezea lakini ilikuwa ni amani hii ambayo sijawahi kuhisi hapo awali.
  • 5:40 - 5:46
    Na mwisho wa Machi, nilipata hedhi.
  • 5:46 - 5:56
    Na kisha tangu wakati huo hadi sasa, sijawahi kukosa hedhi na ni kawaida.
  • 5:56 - 6:02
    Nilifurahi sana lakini nilijiambia,
    'Labda ni kama miaka hiyo
  • 6:02 - 6:06
    ambapo ningeiona mara tatu
    au labda mara mbili kwa mwaka.
  • 6:06 - 6:10
    Acha nione kama nitapata kila mwezi.'
  • 6:10 - 6:13
    Na ilikuwa kama Mungu akisema,
    'Hii ni ya kudumu!'
  • 6:13 - 6:20
    Kwa hiyo mwaka mzima hadi leo,
    sijawahi kukosa kipindi changu.
  • 6:20 - 6:26
    Kwa maambukizi ya njia ya mkojo,
    nilipona kwa sababu tangu wakati huo,
  • 6:26 - 6:30
    Sijapata maambukizi hayo mpaka leo.
  • 6:30 - 6:36
    Na kwa upande wa masomo yangu...
  • 6:36 - 6:41
    Kama nilivyosema, nilipoteza tumaini langu
    na hata nilitaka kuacha.
  • 6:41 - 6:47
    Kulikuwa na siku ambapo, asubuhi, sikutaka kuamka na kwenda kazini
  • 6:47 - 6:51
    kwa sababu ilikuwa mbaya sana.
  • 6:51 - 6:55
    Sikutarajia kupata alama nzuri
  • 6:55 - 6:59
    kwa sababu mwisho wa mafunzo,
    wanakutahini .
  • 6:59 - 7:07
    Na ukifaulu, utastahiki kufanya mtihani wa leseni kwa leseni yako ya kufanya kazi.
  • 7:07 - 7:11
    Na kulikuwa na idara
    ambazo zilinitisha sana,
  • 7:11 - 7:15
    kama vile ICU (Kitengo cha Wagonjwa Mahututi)
    na Idara ya Dharura.
  • 7:15 - 7:17
    Haya ni maeneo muhimu sana.
  • 7:17 - 7:23
    Kwa utukufu wa Mungu, nilimaliza
    mafunzo yangu ya kazi kwa alama nzuri.
  • 7:23 - 7:31
    Nilipata A katika idara hizo ambazo
    nilikuwa na matumaini kidogo ya kufuzu.
  • 7:31 - 7:38
    Nilijiambia, 'Nikipata C katika idara hii, nitakushukuru, Mungu.'
  • 7:38 - 7:39
    Lakini Mungu alinipa A.
  • 7:39 - 7:43
    Kwa hivyo nilipata A na B.
  • 7:43 - 7:47
    Haya ni matokeo yangu.
  • 7:47 - 8:03
    Alama ya jumla ya mafunzo yangu - nilipata 92.9%.
  • 8:03 - 8:05
    Sina msononeko tena.
  • 8:05 - 8:12
    Kwa kweli, msononeko uliniacha siku hiyo baada ya kumaliza Maombi ya Pamoja.
  • 8:12 - 8:15
    Nilihisi amani sana.
  • 8:15 - 8:24
    Ushauri wangu ungekuwa - hakuna kitu ambacho Mungu hawezi kukufanyia ukimkimbilia.
  • 8:24 - 8:31
    Kwa kila suluhu, kila jibu, kimbilia Kwake, na hatakuangusha kamwe.
  • 8:31 - 8:35
    Watu wanaweza kukukatisha tamaa, lakini Mungu
    hawezi kamwe kukukatisha tamaa.
  • 8:35 - 8:39
    Na kwa wanafunzi - usikate tamaa.
  • 8:39 - 8:48
    Kama mimi, watu waliniambia, 'Huna akili. Hutakiwi kuwa hapa.
  • 8:48 - 8:50
    Ulichagua njia mbaya ya kazi.'
  • 8:50 - 8:54
    Usiruhusu mawazo hasi kichwani mwako.
  • 8:54 - 8:58
    Kuna kitu kizuri ambacho
    Mungu anasema juu yako.
  • 8:58 - 9:01
    Ukimkimbilia Yeye, atakuonyesha
    wewe ni nani hasa.
Title:
Je, unahangaika na MSONGO WA MAWAZO? USHUHUDA huu utakutia moyo!
Description:

Je, unapigana vita kichwani mwako na mawazo hasi yanayoendelea? Ushuhuda wa Tumpale kutoka Tanzania hakika UTAKUTIA MOYO! Baada ya kupokea maombi mtandaoni, hakupata tu uhuru kutoka kwenye mfadhaiko bali kuponywa kutokana na ugonjwa wa ovari ya poly-cystic na ukosefu wa usawa wa homoni, pamoja na mafanikio ya kitaaluma. Utukufu wote uwe kwa Mungu!

Ili kupokea maombi bila malipo kutoka kwa Ndugu Chris kupitia Zoom, wasilisha ombi lako la maombi hapa - https://www.godsheart.tv/zoom

➡️ Pata Kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Kuwa Mshirika wa TV wa Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/partnership
➡️ Habari kuhusu Maombi ya Pamoja - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live

more » « less
Video Language:
English
Team:
God's Heart TV
Duration:
09:32

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions