-
Karibu katika Chuo Kikuu cha Mungu.
-
Tunataka kuwashukuru ninyi nyote mliotuma maswali yenu kwetu.
-
Kama mshauri wetu Nabii TB Joshua alivyotuambia:
-
Ikiwa una nia ya somo na una hamu ya kujifunza,
-
utajitahidi kukaa mbele kila wakati,
-
uliza maswali na ushirikiane na mwalimu.
-
Kumbuka katika Chuo Kikuu cha Mungu,
-
moyo, roho ya mtu ni warsha,
-
na Roho Mtakatifu, Mwalimu wa Kimungu.
-
Ndiyo, na hiyo ndiyo ahadi ya Mungu
-
ambayo Yesu alitupa katika Kitabu cha Mathayo 7:7
-
kwamba ukimtafuta, utampata.
-
Ukimtafuta kwa moyo wako wote.
-
Kumbuka, kuutafuta Ufalme wa Mungu
-
ni kuwa na Ufalme wa Mungu.
-
Ndiyo, Mungu hajali, shaka au maswali,
-
mradi maswali hayo yanatufanya tumtafute,
-
kumkaribia Yeye zaidi, kutafuta Neno Lake,
-
Neno la Mungu ndilo mamlaka ya mwisho suluhu
-
ya maswali na matatizo yote.
-
Leo, chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu,
-
tutachunguza baadhi ya maswali yako
-
katika nuru ya Neno la Mungu.
-
Ndiyo, kabisa, na miongoni mwa maswali yaliyotumwa kwetu
-
ni kutoka kwa Anthony anayetokea Kanada
-
Anauliza swali hili la kuvutia, anasema,
-
"Ikiwa hisia zetu ni pazia linatotutenganisha sisi na Munga, je, kazi ya hizi hisia ni zipi sasa?
-
Kwa nini Mungu alitupatia hizi hisia?
-
Je, hisia hizi zinaweza tumika kumtafuta Mungu?"
-
Ahsante Anthony kwa kututumia maswali haya.
-
Anthony, ahsante kwa maswali yako.
-
Acha nikupeleke kwenye Biblia.
-
Kitabu cha Zaburi 115:4-7 katika kuonyesha sanamu,
-
kinatupatia picha ya mchoro wa hizi hisia tano.
-
"4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu.
-
5 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,
-
6 Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,
-
7 Zina mikono lakini hazishiki...
-
Mungu alitupa fahamu kuu tano
-
ambazo hutuwezesha kuingiliana na ulimwengu wa mwili
-
ambamo tunaishi kama wanadamu.
-
Kazi ya msingi ya hisi hizi tano ni kutusaidia kuwasiliana
-
vya kutosha na watu wanaotuzunguka.
-
Pia hutusaidia kupata, kutambua
-
na kukamata vitu vinavyotuzunguka na kutembea kwa usalama
-
katika mazingira yetu.
-
Hisia hizi zote zimeunganishwa.
-
Namaanisha, zinafanya kazi pamoja
-
na kutuma kwenye ubongo ishara pokezi
-
au habari kutoka kwenye mazingira,
-
ubongo wetu, ambao ni maabara ya maarifa ya hisia
-
huchakata taarifa hizi zote,
-
hutambua ishara hizo kupitia hifadhidata ya kumbukumbu zetu
-
na hutoa majibu sahihi.
-
Haya yote hutokea katika wakati halisi.
-
Basi hebu tuaiangalie milango hiyo mitano ya fahamu.
-
Kwa mlango wa fahamu wa kuona, tunaweza kuona na kutambua vitu
-
ambavyo Mungu aliviumba, vitu na watu wanaotuzunguka.
-
Kuona ndio hisia kuu katika
-
kusafiri kwa usalama katika mazingira yetu,
-
kuendesha, kutembea, kusoma.
-
Kwa mlango wa fahamu wa kusikia,
-
hata bila mawasiliano ya kuona, tunaweza kuwa na maarifa wazi
-
ya mazingira yetu ya sasa
-
kwa kutofautisha sauti maalum ambazo hutoa.
-
Kwa mfano, sauti ya ndege au kutambua sauti ya rafiki.
-
Kwa hisia ya harufu
-
tunaweza kujua harufu, manukato,
-
na kuangalia ikiwa kitu ni kizuri au labda chakula kimeharibika.
-
Kwa hisia ya ladha,
-
tunaweza kutathmini utamu au uchungu wa chakula
-
kabla ya kukitumia.
-
Kwa hisia ya kuhisi au kugusa,
-
tunaweza kuhisi halijoto iliyoko
-
kujua mavazi sahihi ya kuvaa ili kulinda miili yetu ipasavyo.
-
Tunaweza kuhisi uzito au ugumu wa kitu.
-
Kwa mfano, chakula hiki kina harufu nzuri.
-
Je, ni chakula gani unachopenda zaidi, Racine?
-
Mchele wa Jollof.
-
Chakula hiki kina harufu nzuri - ndio, nataka kuionja.
-
Au nguo hizi ni nzuri -
-
Nataka kuzinunua.
-
Au ni baridi sana na kuna upepo leo -
-
Sitaki kwenda ufukweni tena.
-
Unaweza kuona jinsi hisia zetu zaweza
-
kuwa na ushawishi kwenye chaguzi na matendo yetu.
-
Zingatia matumizi ya hisi zetu.
-
Kwa mfano, unaendesha gari.
-
Ghafla, mtembea kwa miguu anavuka barabara.
-
Kama dereva, unajikuta mara moja
-
na uamuzi, jibu la kuchukua. Unaweza kuvuta breki,
-
au kama kasi yako ni kubwa sana,
-
inabidi uende mbali na mtu huyo.
-
Unaweza kuona hisia zote zikifanya kazi pamoja;
-
naona, navuta breki; Ninageuza gurudumu.
-
Kwa hivyo vitendo hivi vyote hufanyika wakati huo huo kwa wakati halisi.
-
Vyote wameunganishwa.
-
Vinafanya kazi pamoja.
-
Unaweza kuona ni ushawishi kiasi gani
-
hisia zetu zinaweza kuwa kwenye chaguzi na matendo yetu.
-
Tunachoona, kusikia, kunusa, kuonja, kuhisi kinaweza kuathiri mawazo yetu.
-
Ninamaanisha nini kwa kushawishi mawazo yetu?
-
Ninamaanisha, vina ushawishi juu ya tamaa na mapenzi yetu.
-
Mawazo yetu yanaweza kuathiri matendo yetu au kutotenda.
-
Kwa nini?
-
Kwa sababu mwanadamu hufanya mapenzi yake kupitia akili yake.
-
Hiyo ndiyo maana ya busara au kufikiri.
-
Binadamu ni tofauti na wanyama.
-
Binadamu sio roboti.
-
Yeye ni wakala huru wa maamuzi.
-
Kwa sababu ya ushawishi kutokana na mwingiliano na mazingira
-
ambayo yanahitaji majibu au mtazamo sahihi,
-
Mungu anamtaka mtu kuwa na akili huru -
-
akili inayofikiri yenyewe.
-
Mungu amempa mwanadamu
-
uwezo wa kufikiria na kuchagua kati ya kile kinachofaa au la -
-
hiyo ni akili ya kawaida,
-
kuchagua kati ya mema au mabaya,
-
hiyo ni hisia ya hukumu,
-
kuchagua kati ya mema na mabaya - hiyo ni hisia ya maadili.
-
Hayo ni matokeo ya hisia za kufikiri na uwajibikaji -
-
ambazo ni muhimu kwa maisha katika jamii au kikundi.
-
Mwanadamu kulingana na urefu wa maisha yake, hukua kimwili
-
kutoka kwa kiinitete hadi kwa mtoto mchanga
-
kupitia utoto, ujana, utu uzima na uzee.
-
Tunaweza kuona kwamba kukua kimwili ni kazi ya wakati.
-
Tunapokua katika umri,
-
tunapitia hatua za maisha ya mwanadamu.
-
Mwanadamu si mtu wa kimwili tu
-
bali mtu mwenye akili na maadili.
-
Hasa! Na ni muhimu kukumbuka kwamba
-
kwa sababu maisha na majukumu yake yako katika hatua,
-
mwanadamu pia lazima akue katika ukomavu wa kiakili.
-
Kivipi?
-
Ukuaji wa kiakili ni kazi ya kujifunza -
-
kujifunza kutokana na kile tunachofanya.
-
Kujifunza kutoka kwa kile tunachojifunza, kile kinachotokea karibu nasi
-
na kujifunza kile kinachotokea kwetu.
-
Umewahi kujiuliza kila mtu anapokutana na mtu mpya
-
katika uhusiano mpya?
-
Maswali ya kwanza watakayojiuliza wenyewe
-
yatahusu historia yao, elimu, kazi katika maisha.
-
Wachache sana watashughulikia maisha yao ya kiroho.
-
Na hilo ndilo linaloleta tofauti kati ya mtazamo wa mwanadamu
-
na mtazamo wa Mungu.
-
Ndiyo, katika Wagalatia 5,
-
Mungu asingetuamuru tuenende katika Roho
-
kama hakututengeneza sisi kufanya kazi katika Roho.
-
Biblia ilisema kwamba Mungu alimuumba mwanadamu,
-
wanadamu, kwa sura na mfano wake.
-
Kitabu cha Ayubu 33:4 kinasema
-
mwanadamu ni zao kuu la Roho Mtakatifu;
-
mwanadamu ni kazi ya kiungu ya sanaa.
-
Kwa nini?
-
Kwa sababu wanadamu wamekusudiwa kufikiri, kuzungumza,
-
kutenda na kupanga na Mungu.
-
Kwa hiyo mwanadamu amekusudiwa kuishi katika kupatana na Mungu.
-
Je, tunaishi sambamba na Mungu?
-
Siku zote kumbuka Mungu ni Roho.
-
Kwa hiyo swali ambalo tunapaswa kujiuliza ni:
-
Mwanadamu ni nani?
-
Hilo ndilo swali.
-
Biblia ni hifadhidata ya mwamini kwa maoni yake binafsi.
-
Je, Biblia inasema nini kuhusu mwanadamu, kuhusu wewe na mimi?
-
Biblia inasema katika kitabu cha 1Wathesalonike 5:23
-
kwamba, mtu ni kiumbe wa kiroho
-
ambaye ana roho na mwili.
-
Kwa maneno mengine, mwanadamu ana asili ya kimwili na ya kiroho.
-
Mwanadamu sio tu mtu wa kimwili, kiakili;
-
yeye pia ni mtu wa maadili na mtu wa kiroho,
-
kwa sababu tumeumbwa kuwa kama Mungu
-
ndani ya mioyo yetu na Mungu ni Roho.
-
Kwa hivyo zingatia.
-
Kila mara Biblia inaporejelea moyo wa mwanadamu,
-
inazungumzia roho ya mtu - roho ya mwanadamu.
-
Ndio maana katika Kitabu cha 1 Samweli 16:7, Mathayo 15:8,
-
Biblia inakazia kwamba
-
inapokuja kwa hukumu ya haki, mtazamo wa Mungu,
-
kuhusu mwanadamu daima huelekea kwenye moyo wa mwanadamu, roho ya mwanadamu.
-
Hii ina maana kwamba Mungu humwona mwanadamu kama kiumbe cha roho,
-
anayeishi katika mwili wa kawaida.
-
Roho ya mwanadamu ni sehemu ya mwanadamu ambayo ina ufahamu wa kiroho.
-
Namaanisha, uelewa wa kiroho.
-
Roho ya mwanadamu ni sehemu ya mwanadamu
-
ambayo imeunganishwa na ulimwengu wa kiroho
-
na hupokea miongozo na ufunuo kutoka kwa Mungu, ambaye ni Roho.
-
Hebu tumfikirie sasa mtu kutoka kwenye kibiblia
-
ambaye alikuwa hasa katika maelewano na Mungu katika roho.
-
Tunapaswa kumkumbuka Musa.
-
Fikiria mtazamo wa Musa
-
pale yeye na watu wake walipokuwa wamenaswa
-
katikati ya Bahari Nyekundu na majeshi ya Misri yanayowafuatia.
-
Hakika watu wa Israeli walikuwa na kila sababu
-
kufikiri kwamba mwisho ulikuwa umefika
-
ukizingatia ukubwa na nguvu za kijeshi za majeshi ya Misri.
-
Tunaweza kusoma kuhusu hili katika Kitabu cha Kutoka 14:10.
-
Basi Waisraeli wakalia si kwa hofu tu,
-
bali pia katika uasi na hasira iliyoelekezwa dhidi ya Musa na Mungu wake.
-
Waliruhusu hisia zao kuamuru mwelekeo wa imani yao
-
na kuingiwa na hofu
-
na kusahau kabisa miujiza yote ambayo Mungu alikuwa amewafanyia
-
na kufanya kwa niaba yao.
-
Badala ya kukasirishwa na mwitikio wa watu wake - ukosefu wa imani,
-
Musa alikuwa mtulivu, makini na dhabiti.
-
Hata katikati ya uchochezi mkali,
-
Biblia inasema alikuwa mtulivu sana, mwenye kujiamini na mwenye amani.
-
Kwa nini?
-
Kwa sababu mtazamo wake ulikuwa kwa Mungu.
-
Namaanisha, roho yake ilikuwa imeunganishwa na Mungu.
-
Na ndio maana aliweza kushinda kile ambacho akili zake zilikuwa zikimwambia.
-
Kweli - mtu wa kiroho na mtu wa imani - Musa.
-
Mafunzo mengi ya kujifunza kutoka kwake.
-
Swali ni kwa nini mwanadamu hawezi kutumia hisia zake kumtafuta Mungu?
-
Hilo ndilo swali.
-
Jibu la swali hili ni la moja kwa moja.
-
Mungu ni Roho.
-
Kwa hiyo, hatuwezi kumjua Mungu kwa hisia na
-
na ufahamu au uwezo wa nje wa binadamu
-
kwa sababu Mungu haonekani, ni wa kiroho, si wa kimwili.
-
Yeye ni kiumbe mkuu anayeishi katika ulimwengu juu ya hisia.
-
Anaishi katika roho.
-
Kwa hiyo, ili kumtafuta Mungu, ni lazima uwe katika roho.
-
Na unaweza tu kumuona na kuhusiana Naye
-
katika ulimwengu wa roho kupitia ufunuo.
-
Je, tunamaanisha nini kwa ufunuo?
-
Ufunuo huleta katika hisia zetu za kiroho
-
ukweli wa mambo ya kiroho ambayo hayawezi kutambulika
-
kwa hisi zetu za asili za kibinadamu.
-
Kama vile tulivyo na viungo vya asili vilivyowekwa katika miili yetu ya kimwili
-
ambazo hulisha hisi zetu za kibinadamu kwa habari
-
kutoka kwenye mazingira
-
kama macho yetu, masikio yetu, mikono yetu, nk
-
Mungu pia ametujalia hisia za kiroho
-
vile vile, zilizounganishwa katika roho zetu.
-
Hisia kuu ya kiroho ambayo Mungu ameiweka ndani ya roho zetu
-
ni dhamiri zetu.
-
Dhamiri ni kiungo cha roho cha kutambua mambo ya kiroho.
-
Hiyo ndiyo maana Nabii TB Joshua anaiita hali ya haki.
-
Hebu tumsikilize Mtume Paulo alivyosema katika kitabu cha Warumi 8:16.
-
Paulo alisema,
-
16 Ni Roho mwenyewe anayeshuhudia pamoja na roho zetu kwamba sisi ni wana wa Mungu.
-
Hii ina maana gani?
-
Hii ina maana kwamba hisia ya haki
-
huleta mwamko wa kujijua.
-
Namaanisha, ufahamu wa wewe ni nani katika Kristo Yesu.
-
Swali ni: Je, ufahamu huu unakujaje?
-
Ufahamu huo unakuja kwa njia ya ufunuo
-
wakati Roho Mtakatifu anaposhuhudia rohoni mwetu.
-
Roho Mtakatifu anashuhudiaje rohoni mwetu?
-
Kupitia dhamiri zetu.
-
Paulo alielezea zaidi katika Warumi 9:1.
-
Anasema,
-
9 Ninasema kweli katika Kristo na dhamiri yangu inanishuhudia kwa njia ya Roho Mtakatifu kuwa sisemi uongo
-
Kwa hiyo, 1 Wakorintho 2:9-15 inafundisha kwamba hisi zetu za asili
-
haziwezi kufahamu wala kujua mambo ya Mungu au mambo ya Roho
-
kwa sababu yanaweza tu kutambulika kiroho.
-
Na ikiwa haya yote yanaonekana kuwa mengi kwako, usijali.
-
Katika safu ya msingi tunapoendelea, haya yote yatanyambulishwa.
-
ili kwamba uweze kuelewa kweli
-
jinsi tunavyoweza kuhusiana na Mungu kupitia roho zetu
-
na mtu ni nini hasa - roho yake, mwili wake, nafsi yake.
-
Kwa hivyo subiri unapopata zaidi juu ya haya kwenye safu ya msingi
-
inayokuja hivi karibuni.
-
Kwa hivyo inapokuja kwenye maarifa ya mwanadamu,
-
hisia zetu haziwezi kuona moyo au roho ya mwanadamu.
-
Vinaweza tu kuona mwili wa mwanadamu kwa sababu ndiyo
-
sehemu ya mwanadamu ambayo imeunganishwa na ulimwengu huu unaoonekana.
-
Eneo la hisia.
-
Mwili na hisi za mwanadamu haziwezi kuunganishwa na ulimwengu wa kiroho.
-
Ni roho ya mwanadamu pekee ambayo ni sehemu ya kiroho ya mwanadamu
-
ambayo inaweza kuunganishwa na makao ya roho, ambayo ni mahala pa Mungu.
-
Kweli, ndivyo hivyo.
-
Swali ni: Je, tunaangaliaje katika mwelekeo huo?
-
Ili kuingia kwenye ulimwengu huo wa roho,
-
mwanadamu lazima awe katika roho akiongozwa na Roho Mtakatifu.
-
Roho zetu, mioyo yetu ndio sehemu ya mawasiliano,
-
mahali pa kuwasiliana na Roho Mtakatifu.
-
Roho Mtakatifu anatumia mioyo yetu
-
kuwasiliana nasi.
-
Na Mungu anazungumza na mioyo yetu, na roho zetu, sio masikio yetu.
-
Ninakushauri usome Kitabu cha Matendo 17 -
-
wakati watu wa Athene walipokuwa wakimtafuta Mungu
-
kwa akili zao na maarifa ya hisia
-
ili kumtafuta na kumwabudu Mungu.
-
Acha nisome
-
Matendo ya Mitume 17:23
-
23 Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini niliona sehemu nyingi za kuabudia. Niliona pia madhabahu moja iliyoan dikwa, ‘Kwa Mungu asiyejulikana.’ Huyo Mungu mnayemwabudu bila kumfahamu, ndiye ninayemtangaza kwenu.
-
24 Mungu aliyeumba dunia na vitu vyote vilivyomo, ambaye pia ni Bwana wa mbingu na nchi, haishi katika mahekalu yaliyojengwa na wanadamu.
-
25 Wala hahu dumiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji cho chote; kwa sababu yeye ndiye anayewapa watu wote uhai na pumzi na kila kitu.
-
26 Yeye aliumba mataifa yote ya wanadamu waishi juu ya nchi kutokana na mtu mmoja. Pia amepanga muda wa maisha ya watu wote, akaweka na mipaka ya mahali watakapoishi
-
27 ili wamtafute Mungu na wamfahamu. Lakini Yeye hayuko mbali nasi kwa maana
-
28 ‘Tunaishi na kuenenda na kuwa na uhai ndani yake,’ na kama mtunga mashairi wenu alivyosema, ‘Sisi ni uzao wa Mungu.’
-
29 Kwa kuwa sisi ni wa uzao wa Mungu hatupaswi kudhani kuwa yeye ni kama sanamu ya dhahabu au fedha au jiwe iliyotengenezwa kwa akili na ufundi wa mwanadamu.
-
Kwa kuwa watu wote wana roho, tunapaswa kujiuliza swali
-
Kwa nini inaonekana kwamba wanadamu wengi hawana uhusiano wowote na Mungu?
-
Ukweli ni kwamba Mungu amewaumba wanadamu
-
kufanya kazi katika ulimwengu wa asili na wa kiroho.
-
Lakini wengi wetu tunaishi katika hisia, namaanisha katika asili.
-
Na sisi tuko butu inapokuja kwa mambo ya Roho.
-
Kwa sababu kama Maandiko yanavyosema katika Kitabu cha 1 Wakorintho 2:9
-
mambo ya Rohoni si dhahiri.
-
Hatuwezi kuyaona.
-
Na Biblia inasema zaidi katika 1 Wakorintho 15:46-47,
-
Ngoja nisome.
-
1 Wakorintho 15:46.
-
46 Lakini si yule wa kiroho aliyekuja kwanza; bali ni yule wa mwili, na kisha yule wa kiroho.
-
47 Mtu wa kwanza alitoka katika nchi, alifanywa kwa mavumbi; mtu wa pili ni Bwana kutoka mbinguni.
-
48 Na kama alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na alivyo mtu wa mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
-
Maandiko haya tuliyosoma hivi punde yanabainisha aina mbili za wanaume.
-
Mtu wa asili na mtu wa kiroho.
-
Mwanadamu wa asili ni kipofu wa kiroho na ni butu katika ufahamu
-
katika ulimwengu usioonekana.
-
Ulimwengu wa roho umefungwa kabisa nje ya maono yake ya kiroho.
-
Ni wakati tu Roho Mtakatifu anaangaza macho yake ya kiroho
-
ili aweze kuona na kuelewa mambo ya Rohoni.
-
Waefeso 1:7-18 inasema kwamba Bwana Mungu wetu Yesu Kristo,
-
Baba wa Utukufu, anaweza kutupa Roho wa Ufunuo
-
na hekima katika kumjua Yeye
-
ili macho ya ufahamu wetu yafumbuliwe
-
Ili tuweze kujua tumaini la mwito wake ni nini
-
na utajiri wa utukufu wake ukoje
-
katika urithi wake wa watakatifu.
-
Na tumai mna Biblia zenu hapo, twende sasa kwenye 1 Wakorintho 2:9 na tusome pamoja kuanzia mstari wa 9 mpaka ule wa 12.
-
9 Lakini, kama Maandiko yasemavyo, “Hakuna aliyeona, hakuna aliyesikia, hakuna aliyewaza, kile ambacho Mungu amekiandaa kwa ajili ya watu wampendao.”
-
10 Lakini Mungu amekidhihirisha kwetu kwa njia ya Roho wake. Roho huchunguza kila kitu, hata mambo ya ndani ya Mungu.
-
11 Kwa maana ni nani anajua mawazo ya mtu isipo kuwa roho aliye ndani ya huyo mtu? Vivyo hivyo hakuna mtu anayeelewa mawazo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.
-
12 Sisi hatukupokea roho ya dunia hii bali Roho aliyetoka kwa Mungu ili tuweze kuelewa yale ambayo Mungu ametupatia bure
-
Kwa hivyo swali ni: Je, tunaunganishwaje na Roho?
-
Je, unaunganaje na Roho?
-
Kwa imani.
-
Kumwamini Kristo Yesu - huo ndio muunganiko wetu pekee.
-
Kwa hiyo tunaishije kwa imani?
-
Kumbuka, tunaishi kwa imani
-
tunapotambua muungano wetu na Yesu Kristo katika roho.
-
Kuishi kwa imani,
-
roho zetu lazima zitawale hisia zetu,
-
na ili roho zetu zitawale hisia zetu,
-
mawazo yetu lazima yafanywe upya kwa kulijua Neno
-
na kulifanyia kazi.
-
Kwa hiyo tunajuaje kwamba akili zetu zimefanywa upya?
-
Swali zuri.
-
Akili zetu zinafanywa upya
-
tunapoanza kufikiria sio juu ya udhaifu wetu
-
na mapungufu, bali haki yetu katika Kristo Yesu.
-
2 Wakorintho 12:7-10
-
Yote ni kuhusu uzoefu wa Mtume Paulo na mwiba.
-
7 Na ili nisijione bora kuliko nilivyo, kutokana na mafunuo haya makuu, nilipewa mwiba katika mwili wangu, mtumishi wa shetani, ili anitese.
-
8 Nimemsihi Bwana mara tatu aniondolee mwiba huu.
-
9 Lakini aliniambia, “Neema yangu inakutosha, kwa kuwa uwezo wangu unakamilika katika udhaifu.” Kwa hiyo nitajisifu kwa furaha zaidi kuhusu udhaifu wangu ili uwezo wa Kristo ukae juu yangu.
-
Unaona, wakati Paulo alipoteswa na mwiba katika mwili wake.
-
alimwomba Mungu mara nyingi ili Mungu aondoe mwiba huo.
-
Lakini Mungu akamwambia: “Neema yangu yakutosha.”
-
Kwa nini?
-
Maana nguvu zangu hukamilishwa katika udhaifu.
-
Mara, ufunuo wa mapenzi ya Mungu ulippomjia,
-
Paulo hakulalamika tena.
-
Akasema badala yake, ninapokuwa dhaifu, nina nguvu.
-
Akili yake ilifanywa upya na akaacha kuwa na wasiwasi
-
kuhusu mwiba katika mwili wake.
-
Kwa hivyo, hebu tufanye muhtasari wa majibu ya maswali haya yote.
-
Mtu wa asili - mtu wa hisia anaufahamu kuhusu mwili wake tu.
-
na hana ufahamu wa ulimwengu wa roho.
-
Kwa nini iko hivyo?
-
Biblia inasema tangu kuanguka kwa mwanadamu,
-
mwanadamu amepoteza fahamu zake za roho
-
kwa sababu ya dhambi na hufanya kazi katika asili tu.
-
Tunaweza kusoma kuhusu hili katika Mwanzo 6:3.
-
Roho ya mwanadamu wa asili imekufa kwa Mungu kwa sababu ya dhambi
-
tangu Adamu,
-
mwili wa mwanadamu, ambao Biblia inauita utu wa nje,
-
mtu wa nje au mzee ni sehemu ya mwili ya mwanadamu
-
iliyoundwa na Mungu kuingiliana na ulimwengu unaoonekana au wa mwili.
-
Hiyo ni kweli.
-
Wakati roho ya mwanadamu
-
ni sehemu ya kiroho ya mwanadamu iliyoundwa na Mungu
-
kuingiliana au kuwasiliana na yasiyoonekana
-
au ulimwengu wa kiroho ambapo Mungu anakaa.
-
Kwa hiyo mtu wa kiroho ni,
-
yule ambaye roho yake imeumbwa upya au kufanywa upya
-
kwa nguvu za Mungu katika hatua ya kuzaliwa upya kiroho kwa imani
-
katika Kristo Yesu.
-
Hivyo ndivyo Yesu alimaanisha alipomwambia Nikodemo
-
katika kitabu cha Yohana 3:3.
-
Unahitaji kuzaliwa mara ya pili.
-
Yesu akajibu, akamwambia, Hakika,
-
Nawaambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili,
-
hawezi kuuona ufalme wa Mungu” (Yohana 3:3).
-
Tuko hapa leo kuutafuta Ufalme wa Mungu
-
Unamaanisha nini unaposema kwa nje?
-
Kwa hivyo unamaanisha nini unaposema kwa "nje"?
-
Kwa "nje", tunamaanisha kile kinachoonekana, nyenzo, kimwili -
-
vitu unavyoweza kuona kwa macho yako ya asili,
-
kusikia kwa masikio yako,
-
mambo ambayo unaweza kuhisi au kuyajua kiakili.
-
Kinyume chake, 'ndani' inarejelea
-
kwa mambo ambayo hatuwezi kuyaona, kama moyo wa mwanadamu, roho ya mwanadamu,
-
ambayo ni hali ya kiroho ya mwanadamu ambayo ni Mungu pekee anaweza kuona.
-
Ndiyo maana, kuhusu wanadamu,
-
mtu anahitaji kuongozwa na ufunuo wa kiungu
-
ili kupata kiini cha jambo linapokuja suala la hukumu.
-
Tunapolijuajua hili.
-
Tunajua kwamba hatupaswi kumhukumu mtu yeyote kwa sura
-
kwa sababu Mungu pekee ndiye anayejua hali halisi
-
ya moyo wa mwanadamu.
-
Inapokuja kwa mambo ya Mungu asiyeonekana,
-
tunahitaji kuwa katika roho
-
kwa sababu imani pekee ndiyo impendezayo Mungu.
-
Waebrania 11:6
-
Pasipo imani haiwezekani kumpendeza;
-
kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba Mungu yuko
-
na kwamba Yeye ndiye Mlipaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii.
-
Tunamtafuta kwa bidii, kama tulivyosema leo, kwa imani.
-
Kumbuka, imani inamlenga Mungu asiyeonekana,
-
wakati maono ya asili yanalenga nje, kinachoonekana,
-
kile kinachoonekana, ambacho ni halisi.
-
Kwa hiyo mtu wa kiroho, namaanisha, mtu wa imani
-
haridhiki na ujuzi wa akili bali hutazama zaidi ya hayo,
-
kwa sababu Biblia inasema katika 2 Wakorintho 5:7,
-
tunaenenda kwa imani, si kwa kuona.
-
Ndiyo, imani ni kutoka katika roho ya mwanadamu.
-
Ninamaanisha ulimwengu usioonekana au ulimwengu wa kiroho.
-
Na kuona ni kutoka katika mwili wa mwanadamu,
-
ulimwengu unaoonekana au ulimwengu wa asili.
-
Na sasa, hebu tutazame tena katika kitabu cha 2 Wakorintho 4 kuanzia mstari wa 19.
-
Hebu tusome pamoja.
-
2 Wakorintho 4:18
-
18 Kwa maana hatuweki mawazo yetu kwenye vitu vinavyoonekana bali kwenye vitu visivyoonekana. Maana vile vinavyoonekana ni vya muda mfupi, lakini vile visivyoonekana vinadumu milele.
-
Na Biblia inasema zaidi katika 1 Samweli 16:6-13, unaweza kusoma zaidi kwa undani katika wakati wako.
-
yote ni kuhusu Samweli na Daudi, mfalme wa kwanza wa Israeli.
-
Samweli, nabii alitumwa kwenye nyumba ya Yese huko Bethlehemu
-
kumtia mafuta Mfalme mpya aliyewekwa rasmi wa Israeli.
-
Alipofika, alimtazama mwana wa Yese mwenye sura nzuri zaidi
-
kama mfalme mteule lakini Mungu alimkataa
-
na akamchagua aliyepuuzwa.
-
mvulana wa kawaida mdogo na mchungaji, Daudi
-
Muulize Nabii Samweli katika Kitabu cha 1 Samweli 16:7
-
na angekufundisha kwamba
-
tunapaswa kujifunza kuzingatia sio nje
-
Ninamaanisha, sio juu ya sifa za nje za mwanadamu zinazoonekana.
-
Lakini tunapaswa kuzingatia ndani kwa kuangalia ndani
-
moyoni kwa msaada wa Roho Mtakatifu.
-
Ikiwa tunataka kuona mambo jinsi Mungu anavyoyaona juu ya mwanadamu.
-
Kwa hiyo asante sana.
-
Ndiyo, huo ulikuwa mtazamo mfupi wa maana yake - 'nje' na 'ndani'.
-
Na ndio, sote tunahitaji kuukuza utu wetu wa ndani, mtu wetu wa kiroho.
-
Na kwa msaada wa Roho Mtakatifu kila siku, kila wakati tunaweza.
-
Mtu anawezaje kukuza imani kwa Mungu, kwa dhati?
-
Kwanza, kuna haja ya kujua imani ni nini.
-
Tatizo la imani linafanywa kuwa rahisi kueleweka pale tu
-
tunapojua kwamba imani ni kutenda tu
-
juu ya kile ambacho Mungu amesema.
-
Suala kuu la imani yetu ni ukweli wa imani hiyo.
-
Ili imani iwe ya kweli, lazima itegemee Neno la Mungu,
-
ambayo ni Roho na uzima. ( Yohana 6:63 )
-
Mwanadamu huongea maneno ya kawaida
-
bali Mungu hunena Maneno ambayo ni Roho na uzima.
-
Lakini ili neno la mwanadamu liwe Neno la Mungu,
-
lazima liathiriwe na Roho Mtakatifu kwa uzima.
-
Swali ni: Je, mwanadamu anaweza kusema Maneno ya uzima?
-
Mwanadamu huongea maneno ya kawaida
-
lakini mwanadamu anaweza kunena Maneno ya uzima ambayo ni roho na uzima
-
yanapoathiriwa na Roho Mtakatifu.
-
Maneno hayo lazima yaathiriwe na Roho Mtakatifu kwa uzima.
-
Ninamaanisha nini naposema kwa uzima katika Neno?
-
Neno la Mungu ni Roho na uzima
-
kwa sababu lina uwezo wa kuzalisha nguvu ya kiroho
-
ambayo hukua na kustawi ndani ya mioyo yetu iitwayo imani.
-
Imani hiyo ndiyo inayosukuma maneno yetu kufanya maajabu.
-
Hiyo ni imani ya Biblia.
-
Imani ya Biblia inaitwa Imani ya Kiroho, katika kitabu cha 2 Wakorintho 4:13
-
13 Lakini kwa kuwa tuna roho ile ile ya imani; kama ilivyoandikwa, Niliamini, na kwa sababu hiyo nilinena; sisi nasi twaamini, na kwa sababu hiyo twanena
-
Kwa hivyo imani hufanyika katika sehemu mbili:
-
Kwa mioyo yetu tunaamini;
-
Kwa vinywa vyetu tunakiri, na imani ni yote mawili.
-
Unajua, mfano wa wana saba wa Skeva unaonyesha hivyo
-
imani ya kweli si kuiga.
-
Imani lazima itokee katika moyo wa kila mtu
-
au katika usadikisho, ambao unaongoza kwenye harakati halisi
-
au maungamo halisi ya imani.
-
Ili imani iwe ya kweli, moyo na kinywa havipaswi kupingana kamwe.
-
Kwa maneno mengine, tunapaswa kumaanisha kile tunachosema.
-
Hii ina maana kwamba tunapaswa kuamini kile tunachokiri.
-
Je, unaamini unachokiri?
-
Unamaanisha unachosema?
-
Kwa sababu imani ya kimaandiko au imani ya kibiblia imeonyeshwa
-
kwa kuamini kwenye moyo na kukiri kwa kinywa.
-
Kinywa lazima kiwe na makubaliano kamili ya moyo
-
kabla ya kuwa na maungamo ya imani yanayokubalika au ya kweli.
-
Kweli kabisa.
-
Huo ndio ufunguo, makubaliano.
-
Swali ni: Imani inaweza kusitawije?
-
Ukuaji wa Neno la Mungu moyoni mwako,
-
huzaa imani ndani ya moyo wako.
-
Warumi 10:17
-
Imani hukua tunaposikia na kutii Neno la Mungu.
-
Je, mtu anahamaje kutoka kwenye ujuzi wa hisia hadi ujuzi wa ufunuo?
-
Je, mtu anahamaje kutoka kwenye ujuzi wa hisia hadi ujuzi wa ufunuo?
-
Ndiyo, hilo ndilo jambo ambalo sisi sote waamini tunapaswa kujiuliza.
-
Hebu tukumbuke kilichompata mtumishi wa Elisha.
-
Kwa macho yake ya kimwili,
-
mtumishi wa Elisha aliona hatari ya papo hapo na hofu ikamshika.
-
Bwana wake alipomwomba Mungu amfungue macho ya rohoni.
-
Macho yake yakafunguliwa na katika roho,
-
aliona malaika wakimzunguka.
-
Na nini kilitokea?
-
Hofu yake ikatoweka.
-
Ndiyo.
-
Kwa hivyo kuhama kutoka maarifa ya hisi hadi maarifa ya ufunuo
-
ni suala la kuukabidhi moyo wako kwa Roho Mtakatifu.
-
Roho Mtakatifu ndiye anayefungua macho ya imani yetu
-
kuona ukweli uliofichwa katika Neno la Mungu.
-
Kutafakari katika Neno la Mungu huleta ufunuo.
-
Huo ndio ufunguo.
-
Tunatafakari hadi Mungu atupe nuru iliyo wazi, ufahamu wazi.
-
Kwa hiyo unapotafakari Neno la Mungu,
-
kumruhusu Roho Mtakatifu kuchukua uongozi, ufunuo utakuja
-
na utakapokuja wahyi, utakubeba
-
zaidi ya ulimwengu wa hisi ndani ya uwepo wa Mungu
-
katika roho na huko utaona waziwazi;
-
hapo ndipo ufahamu wa kiroho unakuja.
-
Jiweke katika Maandiko
-
na kumsikia Mungu akikuambia,
-
Walio pamoja nawe ni wengi kuliko wale walio kinyume chako.
-
Wengi leo katika nyumba zao wanalemewa na hali zao
-
kwa sababu tunaitazama kwa asili
-
na unazidiwa na hofu inakuja na shaka inakuja.
-
Kwa hivyo kuna haja ya sisi kubadili mtazamo wetu
-
kutoka asili hadi kiroho.
-
Kwa hivyo kuhama kutoka maarifa ya hisi kwenda kwenye ufunuo
-
ni kwa neema.
-
Unachohitaji kufanya ni kunyenyekea
-
chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu - Roho wa Ufunuo.
-
Mabadiliko hayo, hatua hiyo ni kidogo kidogo,
-
kila siku, kidogo kidogo, kila dakika, kidogo kidogo.
-
Ni safari na safari ya maili elfu moja huanza na hatua moja.
-
Kwa hivyo tuna furaha sana leo
-
kwamba ulijiunga nasi kuchukua hatua hiyo, hatua hiyo kuelekea kiroho
-
kwa kuungana nasi kwenye programu leo.
-
Kwa hivyo safari hiyo leo imeanza na hatua hii ambayo umechukua.
-
Na kumbuka mfululizo wa FOUNDATION SERIES,
-
MIHADHARA YA KIMUNGU
-
ambayo umekuwa ukiona kwenye Chuo Kikuu cha Mungu -
-
Huhitaji tu kuzitazama mara moja
-
unajua, Neno la Mungu halifungwi na wakati.
-
Kila Neno la Mungu ni Roho na Uzima.
-
Chukua muda kutazama tena na tena,
-
pitia vifungu vya Biblia, tafakari ukweli uliofichwa hapo
-
na ukitaka kutafuta mahali mafundisho hayo yalipo,
-
unaweza kuangalia katika maelezo hapa chini.
-
Kuna kiunga na ikiwa una maswali zaidi, kumbuka,
-
unapotafakari mafundisho haya, maswali yatatokea moyoni mwako
-
na unaweza kutuma maswali yako kwetu kwa kwenda
-
kwa tovuti yetu - theuog.org - kwenda kwa sehemu ya mawasiliano
-
na kututumia ujumbe.
-
Na tutapitia maswali yako yote na kwa neema ya Mungu,
-
wajibu chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu.
-
Hakuna njia ya mkato ya ukomavu wa kiroho.
-
Ufahamu wetu wa kidunia lazima utoe nafasi kwa ufahamu wa kiroho au ufunuo, kufikia ukomavu. ” – Nabii TB Joshua
-
au ufunuo kufikia ukomavu.
-
Mafundisho yote tunayokupa hayana muda.
-
Tafadhali pitia, tafakari juu yake,
-
na umwombe Roho Mtakatifu akusaidie
-
kuwa na uelewa mzuri juu yake.
-
Hiyo ndiyo njia pekee ya imani inaweza kukua katika maisha yetu.
-
Kwamba tuna ufunuo haimaanishi
-
tunaweza kukulazimisha kuamini;
-
lazima uwe na ufunuo na usadikisho wako mwenyewe.
-
Inakujaje?
-
Isome, itafakari.
-
Ruhusu Roho wa Mungu akuongezee ufahamu wako.
-
Tunahitaji kuwa wakristo wakomavu
-
kwa sababu tuko katika mazingira yenye changamoto nyingi
-
na Mungu anataka uishi kwa imani, uwe hodari katika imani.
-
Unaweza kufanya hivyo jinsi gani?
-
Unaweza kufikia hilo tu kwa kuendeleza uhusiano wako
-
pamoja na Mgeni wa ajabu asiyeonekana - Roho Mtakatifu.
-
Vipi? Kuvutia umakini wake.
-
Na unaweza kufanya hivyo tu unapotafakari Neno na kuomba
-
na atakuja na kuziboresha pwani za kiroho.
-
katika jina la Yesu.
-
Kama vile Nikodemo alivyomwendea Yesu usiku ili kuuliza maswali,
-
kujua na kukuza imani katika Yesu,
-
wewe pia unaweza kutazama hili na kuuliza maswali moyoni mwako kwa Mungu
-
na Roho Mtakatifu,
-
Msaidizi, Mshauri atakuja na kujibu maswali yako
-
kupitia Neno la Mungu.
-
Ndiyo, ndiyo maana kila kitu kiko katika nuru ya Neno la Mungu.
-
Amina. Watakatifu, ndugu, dada, waumini duniani kote,
-
tunaenda kukuombea.
-
Tumeona barua pepe nyingi sana.
-
Tulipitia maswali na majibu yote.
-
Tumeona watu wengi wakipitia uchungu,
-
maumivu na matatizo.
-
Kwa hiyo tunaenda kuomba pamoja, mwamini Mungu
-
kwamba Mungu Mwenyezi atakutana nawe katika hatua ya hitaji lako muhimu,
-
kwa maana Yesu hafanyi neno lolote pasipo Neno lake.
-
Usisahau, Neno la Mungu lina kipaumbele kuliko jina.
-
Ndio maana tunakupa mafundisho haya.
-
Lakini tunasimama mbele za Mungu tukiwaombea,
-
na Mungu atakuweka katika rehema zake, katika jina la Yesu.
-
Kwa hivyo, endelea kuungana nasi hapa kwenye Chuo Kikuu cha Mungu.
-
Ujuzi wa hisia hukoma wakati ufunuo unakuja.