< Return to Video

MAJIBU YA BIBLIA YALIYOFICHIKA | INGIA KATIKA ROHO - SEHEMU YA 2

  • 0:17 - 0:20
    Karibu katika Chuo Kikuu cha Mungu.
  • 0:20 - 0:25
    Tunataka kuwashukuru ninyi nyote mliotuma maswali yenu kwetu.
  • 0:25 - 0:28
    Kama mshauri wetu Nabii TB Joshua alivyotuambia:
  • 0:28 - 0:33
    Ikiwa una nia ya somo na una hamu ya kujifunza,
  • 0:33 - 0:35
    utajitahidi kukaa mbele kila wakati,
  • 0:35 - 0:39
    uliza maswali na ushirikiane na mwalimu.
  • 0:39 - 0:42
    Kumbuka katika Chuo Kikuu cha Mungu,
  • 0:42 - 0:45
    moyo, roho ya mtu ni warsha,
  • 0:45 - 0:47
    na Roho Mtakatifu, Mwalimu wa Kimungu.
  • 0:47 - 0:49
    Ndiyo, na hiyo ndiyo ahadi ya Mungu
  • 0:49 - 0:52
    ambayo Yesu alitupa katika Kitabu cha Mathayo 7:7
  • 0:52 - 0:55
    kwamba ukimtafuta, utampata.
  • 0:55 - 0:58
    Ukimtafuta kwa moyo wako wote.
  • 0:58 - 1:00
    Kumbuka, kuutafuta Ufalme wa Mungu
  • 1:00 - 1:02
    ni kuwa na Ufalme wa Mungu.
  • 1:02 - 1:05
    Ndiyo, Mungu hajali, shaka au maswali,
  • 1:05 - 1:08
    mradi maswali hayo yanatufanya tumtafute,
  • 1:08 - 1:12
    kumkaribia Yeye zaidi, kutafuta Neno Lake,
  • 1:12 - 1:14
    Neno la Mungu ndilo mamlaka ya mwisho suluhu
  • 1:14 - 1:18
    ya maswali na matatizo yote.
  • 1:18 - 1:21
    Leo, chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu,
  • 1:21 - 1:24
    tutachunguza baadhi ya maswali yako
  • 1:24 - 1:27
    katika nuru ya Neno la Mungu.
  • 1:27 - 1:31
    Ndiyo, kabisa, na miongoni mwa maswali yaliyotumwa kwetu
  • 1:31 - 1:33
    ni kutoka kwa Anthony anayetokea Kanada
  • 1:33 - 1:35
    Anauliza swali hili la kuvutia, anasema,
  • 1:35 - 1:42
    "Ikiwa hisia zetu ni pazia linatotutenganisha sisi na Munga, je, kazi ya hizi hisia ni zipi sasa?
  • 1:42 - 1:44
    Kwa nini Mungu alitupatia hizi hisia?
  • 1:44 - 1:48
    Je, hisia hizi zinaweza tumika kumtafuta Mungu?"
  • 1:48 - 1:52
    Ahsante Anthony kwa kututumia maswali haya.
  • 1:54 - 1:57
    Anthony, ahsante kwa maswali yako.
  • 1:58 - 2:00
    Acha nikupeleke kwenye Biblia.
  • 2:00 - 2:06
    Kitabu cha Zaburi 115:4-7 katika kuonyesha sanamu,
  • 2:06 - 2:10
    kinatupatia picha ya mchoro wa hizi hisia tano.
  • 2:11 - 2:16
    "4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu.
  • 2:17 - 2:24
    5 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,
  • 2:24 - 2:30
    6 Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,
  • 2:30 - 2:38
    7 Zina mikono lakini hazishiki...
  • 2:38 - 2:42
    Mungu alitupa fahamu kuu tano
  • 2:42 - 2:45
    ambazo hutuwezesha kuingiliana na ulimwengu wa mwili
  • 2:45 - 2:50
    ambamo tunaishi kama wanadamu.
  • 2:50 - 2:55
    Kazi ya msingi ya hisi hizi tano ni kutusaidia kuwasiliana
  • 2:55 - 2:59
    vya kutosha na watu wanaotuzunguka.
  • 2:59 - 3:03
    Pia hutusaidia kupata, kutambua
  • 3:03 - 3:08
    na kukamata vitu vinavyotuzunguka na kutembea kwa usalama
  • 3:08 - 3:12
    katika mazingira yetu.
  • 3:12 - 3:14
    Hisia hizi zote zimeunganishwa.
  • 3:14 - 3:17
    Namaanisha, zinafanya kazi pamoja
  • 3:17 - 3:21
    na kutuma kwenye ubongo ishara pokezi
  • 3:21 - 3:25
    au habari kutoka kwenye mazingira,
  • 3:25 - 3:28
    ubongo wetu, ambao ni maabara ya maarifa ya hisia
  • 3:28 - 3:30
    huchakata taarifa hizi zote,
  • 3:30 - 3:35
    hutambua ishara hizo kupitia hifadhidata ya kumbukumbu zetu
  • 3:35 - 3:38
    na hutoa majibu sahihi.
  • 3:38 - 3:42
    Haya yote hutokea katika wakati halisi.
  • 3:42 - 3:44
    Basi hebu tuaiangalie milango hiyo mitano ya fahamu.
  • 3:44 - 3:49
    Kwa mlango wa fahamu wa kuona, tunaweza kuona na kutambua vitu
  • 3:49 - 3:52
    ambavyo Mungu aliviumba, vitu na watu wanaotuzunguka.
  • 3:52 - 3:54
    Kuona ndio hisia kuu katika
  • 3:54 - 3:56
    kusafiri kwa usalama katika mazingira yetu,
  • 3:56 - 3:59
    kuendesha, kutembea, kusoma.
  • 3:59 - 4:00
    Kwa mlango wa fahamu wa kusikia,
  • 4:00 - 4:03
    hata bila mawasiliano ya kuona, tunaweza kuwa na maarifa wazi
  • 4:03 - 4:05
    ya mazingira yetu ya sasa
  • 4:05 - 4:09
    kwa kutofautisha sauti maalum ambazo hutoa.
  • 4:09 - 4:14
    Kwa mfano, sauti ya ndege au kutambua sauti ya rafiki.
  • 4:14 - 4:15
    Kwa hisia ya harufu
  • 4:15 - 4:18
    tunaweza kujua harufu, manukato,
  • 4:18 - 4:22
    na kuangalia ikiwa kitu ni kizuri au labda chakula kimeharibika.
  • 4:22 - 4:24
    Kwa hisia ya ladha,
  • 4:24 - 4:27
    tunaweza kutathmini utamu au uchungu wa chakula
  • 4:27 - 4:29
    kabla ya kukitumia.
  • 4:29 - 4:32
    Kwa hisia ya kuhisi au kugusa,
  • 4:32 - 4:35
    tunaweza kuhisi halijoto iliyoko
  • 4:35 - 4:39
    kujua mavazi sahihi ya kuvaa ili kulinda miili yetu ipasavyo.
  • 4:39 - 4:43
    Tunaweza kuhisi uzito au ugumu wa kitu.
  • 4:43 - 4:46
    Kwa mfano, chakula hiki kina harufu nzuri.
  • 4:46 - 4:48
    Je, ni chakula gani unachopenda zaidi, Racine?
  • 4:48 - 4:50
    Mchele wa Jollof.
  • 4:50 - 4:54
    Chakula hiki kina harufu nzuri - ndio, nataka kuionja.
  • 4:54 - 4:56
    Au nguo hizi ni nzuri -
  • 4:56 - 4:57
    Nataka kuzinunua.
  • 4:57 - 5:00
    Au ni baridi sana na kuna upepo leo -
  • 5:00 - 5:03
    Sitaki kwenda ufukweni tena.
  • 5:03 - 5:06
    Unaweza kuona jinsi hisia zetu zaweza
  • 5:06 - 5:11
    kuwa na ushawishi kwenye chaguzi na matendo yetu.
  • 5:11 - 5:12
    Zingatia matumizi ya hisi zetu.
  • 5:12 - 5:15
    Kwa mfano, unaendesha gari.
  • 5:15 - 5:18
    Ghafla, mtembea kwa miguu anavuka barabara.
  • 5:18 - 5:21
    Kama dereva, unajikuta mara moja
  • 5:21 - 5:24
    na uamuzi, jibu la kuchukua. Unaweza kuvuta breki,
  • 5:24 - 5:27
    au kama kasi yako ni kubwa sana,
  • 5:27 - 5:30
    inabidi uende mbali na mtu huyo.
  • 5:30 - 5:33
    Unaweza kuona hisia zote zikifanya kazi pamoja;
  • 5:33 - 5:37
    naona, navuta breki; Ninageuza gurudumu.
  • 5:37 - 5:41
    Kwa hivyo vitendo hivi vyote hufanyika wakati huo huo kwa wakati halisi.
  • 5:41 - 5:43
    Vyote wameunganishwa.
  • 5:43 - 5:46
    Vinafanya kazi pamoja.
  • 5:46 - 5:49
    Unaweza kuona ni ushawishi kiasi gani
  • 5:49 - 5:54
    hisia zetu zinaweza kuwa kwenye chaguzi na matendo yetu.
  • 5:54 - 6:02
    Tunachoona, kusikia, kunusa, kuonja, kuhisi kinaweza kuathiri mawazo yetu.
  • 6:02 - 6:04
    Ninamaanisha nini kwa kushawishi mawazo yetu?
  • 6:04 - 6:10
    Ninamaanisha, vina ushawishi juu ya tamaa na mapenzi yetu.
  • 6:10 - 6:14
    Mawazo yetu yanaweza kuathiri matendo yetu au kutotenda.
  • 6:14 - 6:15
    Kwa nini?
  • 6:15 - 6:19
    Kwa sababu mwanadamu hufanya mapenzi yake kupitia akili yake.
  • 6:19 - 6:23
    Hiyo ndiyo maana ya busara au kufikiri.
  • 6:23 - 6:26
    Binadamu ni tofauti na wanyama.
  • 6:26 - 6:28
    Binadamu sio roboti.
  • 6:28 - 6:32
    Yeye ni wakala huru wa maamuzi.
  • 6:32 - 6:36
    Kwa sababu ya ushawishi kutokana na mwingiliano na mazingira
  • 6:36 - 6:40
    ambayo yanahitaji majibu au mtazamo sahihi,
  • 6:40 - 6:45
    Mungu anamtaka mtu kuwa na akili huru -
  • 6:45 - 6:49
    akili inayofikiri yenyewe.
  • 6:49 - 6:51
    Mungu amempa mwanadamu
  • 6:51 - 6:55
    uwezo wa kufikiria na kuchagua kati ya kile kinachofaa au la -
  • 6:55 - 6:57
    hiyo ni akili ya kawaida,
  • 6:57 - 7:00
    kuchagua kati ya mema au mabaya,
  • 7:00 - 7:02
    hiyo ni hisia ya hukumu,
  • 7:02 - 7:06
    kuchagua kati ya mema na mabaya - hiyo ni hisia ya maadili.
  • 7:06 - 7:10
    Hayo ni matokeo ya hisia za kufikiri na uwajibikaji -
  • 7:10 - 7:15
    ambazo ni muhimu kwa maisha katika jamii au kikundi.
  • 7:15 - 7:20
    Mwanadamu kulingana na urefu wa maisha yake, hukua kimwili
  • 7:20 - 7:24
    kutoka kwa kiinitete hadi kwa mtoto mchanga
  • 7:24 - 7:30
    kupitia utoto, ujana, utu uzima na uzee.
  • 7:30 - 7:35
    Tunaweza kuona kwamba kukua kimwili ni kazi ya wakati.
  • 7:35 - 7:37
    Tunapokua katika umri,
  • 7:37 - 7:42
    tunapitia hatua za maisha ya mwanadamu.
  • 7:42 - 7:45
    Mwanadamu si mtu wa kimwili tu
  • 7:45 - 7:49
    bali mtu mwenye akili na maadili.
  • 7:49 - 7:52
    Hasa! Na ni muhimu kukumbuka kwamba
  • 7:52 - 7:56
    kwa sababu maisha na majukumu yake yako katika hatua,
  • 7:56 - 8:00
    mwanadamu pia lazima akue katika ukomavu wa kiakili.
  • 8:00 - 8:02
    Kivipi?
  • 8:02 - 8:05
    Ukuaji wa kiakili ni kazi ya kujifunza -
  • 8:05 - 8:07
    kujifunza kutokana na kile tunachofanya.
  • 8:07 - 8:10
    Kujifunza kutoka kwa kile tunachojifunza, kile kinachotokea karibu nasi
  • 8:10 - 8:14
    na kujifunza kile kinachotokea kwetu.
  • 8:14 - 8:17
    Umewahi kujiuliza kila mtu anapokutana na mtu mpya
  • 8:17 - 8:19
    katika uhusiano mpya?
  • 8:19 - 8:22
    Maswali ya kwanza watakayojiuliza wenyewe
  • 8:22 - 8:28
    yatahusu historia yao, elimu, kazi katika maisha.
  • 8:28 - 8:32
    Wachache sana watashughulikia maisha yao ya kiroho.
  • 8:32 - 8:36
    Na hilo ndilo linaloleta tofauti kati ya mtazamo wa mwanadamu
  • 8:36 - 8:40
    na mtazamo wa Mungu.
  • 8:40 - 8:44
    Ndiyo, katika Wagalatia 5,
  • 8:44 - 8:49
    Mungu asingetuamuru tuenende katika Roho
  • 8:49 - 8:54
    kama hakututengeneza sisi kufanya kazi katika Roho.
  • 8:54 - 8:57
    Biblia ilisema kwamba Mungu alimuumba mwanadamu,
  • 8:57 - 9:02
    wanadamu, kwa sura na mfano wake.
  • 9:02 - 9:04
    Kitabu cha Ayubu 33:4 kinasema
  • 9:04 - 9:08
    mwanadamu ni zao kuu la Roho Mtakatifu;
  • 9:08 - 9:12
    mwanadamu ni kazi ya kiungu ya sanaa.
  • 9:12 - 9:13
    Kwa nini?
  • 9:13 - 9:17
    Kwa sababu wanadamu wamekusudiwa kufikiri, kuzungumza,
  • 9:17 - 9:22
    kutenda na kupanga na Mungu.
  • 9:22 - 9:26
    Kwa hiyo mwanadamu amekusudiwa kuishi katika kupatana na Mungu.
  • 9:26 - 9:28
    Je, tunaishi sambamba na Mungu?
  • 9:28 - 9:32
    Siku zote kumbuka Mungu ni Roho.
  • 9:32 - 9:36
    Kwa hiyo swali ambalo tunapaswa kujiuliza ni:
  • 9:36 - 9:39
    Mwanadamu ni nani?
  • 9:39 - 9:41
    Hilo ndilo swali.
  • 9:41 - 9:48
    Biblia ni hifadhidata ya mwamini kwa maoni yake binafsi.
  • 9:48 - 9:54
    Je, Biblia inasema nini kuhusu mwanadamu, kuhusu wewe na mimi?
  • 9:55 - 10:00
    Biblia inasema katika kitabu cha 1Wathesalonike 5:23
  • 10:00 - 10:04
    kwamba, mtu ni kiumbe wa kiroho
  • 10:04 - 10:08
    ambaye ana roho na mwili.
  • 10:08 - 10:15
    Kwa maneno mengine, mwanadamu ana asili ya kimwili na ya kiroho.
  • 10:15 - 10:19
    Mwanadamu sio tu mtu wa kimwili, kiakili;
  • 10:19 - 10:25
    yeye pia ni mtu wa maadili na mtu wa kiroho,
  • 10:25 - 10:28
    kwa sababu tumeumbwa kuwa kama Mungu
  • 10:28 - 10:33
    ndani ya mioyo yetu na Mungu ni Roho.
  • 10:33 - 10:34
    Kwa hivyo zingatia.
  • 10:34 - 10:38
    Kila mara Biblia inaporejelea moyo wa mwanadamu,
  • 10:38 - 10:43
    inazungumzia roho ya mtu - roho ya mwanadamu.
  • 10:43 - 10:50
    Ndio maana katika Kitabu cha 1 Samweli 16:7, Mathayo 15:8,
  • 10:50 - 10:53
    Biblia inakazia kwamba
  • 10:53 - 10:57
    inapokuja kwa hukumu ya haki, mtazamo wa Mungu,
  • 10:57 - 11:02
    kuhusu mwanadamu daima huelekea kwenye moyo wa mwanadamu, roho ya mwanadamu.
  • 11:02 - 11:06
    Hii ina maana kwamba Mungu humwona mwanadamu kama kiumbe cha roho,
  • 11:06 - 11:10
    anayeishi katika mwili wa kawaida.
  • 11:10 - 11:15
    Roho ya mwanadamu ni sehemu ya mwanadamu ambayo ina ufahamu wa kiroho.
  • 11:15 - 11:18
    Namaanisha, uelewa wa kiroho.
  • 11:18 - 11:21
    Roho ya mwanadamu ni sehemu ya mwanadamu
  • 11:21 - 11:24
    ambayo imeunganishwa na ulimwengu wa kiroho
  • 11:24 - 11:30
    na hupokea miongozo na ufunuo kutoka kwa Mungu, ambaye ni Roho.
  • 11:30 - 11:33
    Hebu tumfikirie sasa mtu kutoka kwenye kibiblia
  • 11:33 - 11:37
    ambaye alikuwa hasa katika maelewano na Mungu katika roho.
  • 11:37 - 11:38
    Tunapaswa kumkumbuka Musa.
  • 11:38 - 11:40
    Fikiria mtazamo wa Musa
  • 11:40 - 11:43
    pale yeye na watu wake walipokuwa wamenaswa
  • 11:43 - 11:48
    katikati ya Bahari Nyekundu na majeshi ya Misri yanayowafuatia.
  • 11:48 - 11:52
    Hakika watu wa Israeli walikuwa na kila sababu
  • 11:52 - 11:56
    kufikiri kwamba mwisho ulikuwa umefika
  • 11:56 - 12:00
    ukizingatia ukubwa na nguvu za kijeshi za majeshi ya Misri.
  • 12:00 - 12:03
    Tunaweza kusoma kuhusu hili katika Kitabu cha Kutoka 14:10.
  • 12:03 - 12:07
    Basi Waisraeli wakalia si kwa hofu tu,
  • 12:07 - 12:12
    bali pia katika uasi na hasira iliyoelekezwa dhidi ya Musa na Mungu wake.
  • 12:12 - 12:17
    Waliruhusu hisia zao kuamuru mwelekeo wa imani yao
  • 12:17 - 12:20
    na kuingiwa na hofu
  • 12:20 - 12:25
    na kusahau kabisa miujiza yote ambayo Mungu alikuwa amewafanyia
  • 12:25 - 12:28
    na kufanya kwa niaba yao.
  • 12:28 - 12:33
    Badala ya kukasirishwa na mwitikio wa watu wake - ukosefu wa imani,
  • 12:33 - 12:37
    Musa alikuwa mtulivu, makini na dhabiti.
  • 12:37 - 12:41
    Hata katikati ya uchochezi mkali,
  • 12:41 - 12:45
    Biblia inasema alikuwa mtulivu sana, mwenye kujiamini na mwenye amani.
  • 12:45 - 12:46
    Kwa nini?
  • 12:46 - 12:49
    Kwa sababu mtazamo wake ulikuwa kwa Mungu.
  • 12:49 - 12:53
    Namaanisha, roho yake ilikuwa imeunganishwa na Mungu.
  • 12:53 - 12:57
    Na ndio maana aliweza kushinda kile ambacho akili zake zilikuwa zikimwambia.
  • 12:57 - 13:01
    Kweli - mtu wa kiroho na mtu wa imani - Musa.
  • 13:01 - 13:04
    Mafunzo mengi ya kujifunza kutoka kwake.
  • 13:04 - 13:10
    Swali ni kwa nini mwanadamu hawezi kutumia hisia zake kumtafuta Mungu?
  • 13:10 - 13:12
    Hilo ndilo swali.
  • 13:12 - 13:15
    Jibu la swali hili ni la moja kwa moja.
  • 13:15 - 13:18
    Mungu ni Roho.
  • 13:18 - 13:22
    Kwa hiyo, hatuwezi kumjua Mungu kwa hisia na
  • 13:22 - 13:25
    na ufahamu au uwezo wa nje wa binadamu
  • 13:25 - 13:31
    kwa sababu Mungu haonekani, ni wa kiroho, si wa kimwili.
  • 13:31 - 13:35
    Yeye ni kiumbe mkuu anayeishi katika ulimwengu juu ya hisia.
  • 13:35 - 13:38
    Anaishi katika roho.
  • 13:38 - 13:45
    Kwa hiyo, ili kumtafuta Mungu, ni lazima uwe katika roho.
  • 13:45 - 13:48
    Na unaweza tu kumuona na kuhusiana Naye
  • 13:48 - 13:52
    katika ulimwengu wa roho kupitia ufunuo.
  • 13:52 - 13:54
    Je, tunamaanisha nini kwa ufunuo?
  • 13:54 - 13:58
    Ufunuo huleta katika hisia zetu za kiroho
  • 13:58 - 14:03
    ukweli wa mambo ya kiroho ambayo hayawezi kutambulika
  • 14:03 - 14:08
    kwa hisi zetu za asili za kibinadamu.
  • 14:08 - 14:14
    Kama vile tulivyo na viungo vya asili vilivyowekwa katika miili yetu ya kimwili
  • 14:14 - 14:18
    ambazo hulisha hisi zetu za kibinadamu kwa habari
  • 14:18 - 14:20
    kutoka kwenye mazingira
  • 14:20 - 14:26
    kama macho yetu, masikio yetu, mikono yetu, nk
  • 14:26 - 14:31
    Mungu pia ametujalia hisia za kiroho
  • 14:31 - 14:36
    vile vile, zilizounganishwa katika roho zetu.
  • 14:36 - 14:40
    Hisia kuu ya kiroho ambayo Mungu ameiweka ndani ya roho zetu
  • 14:40 - 14:43
    ni dhamiri zetu.
  • 14:43 - 14:50
    Dhamiri ni kiungo cha roho cha kutambua mambo ya kiroho.
  • 14:50 - 14:55
    Hiyo ndiyo maana Nabii TB Joshua anaiita hali ya haki.
  • 14:55 - 15:11
    Hebu tumsikilize Mtume Paulo alivyosema katika kitabu cha Warumi 8:16.
  • 15:12 - 15:14
    Paulo alisema,
  • 15:17 - 15:25
    16 Ni Roho mwenyewe anayeshuhudia pamoja na roho zetu kwamba sisi ni wana wa Mungu.
  • 15:25 - 15:28
    Hii ina maana gani?
  • 15:28 - 15:31
    Hii ina maana kwamba hisia ya haki
  • 15:31 - 15:34
    huleta mwamko wa kujijua.
  • 15:34 - 15:40
    Namaanisha, ufahamu wa wewe ni nani katika Kristo Yesu.
  • 15:40 - 15:44
    Swali ni: Je, ufahamu huu unakujaje?
  • 15:44 - 15:47
    Ufahamu huo unakuja kwa njia ya ufunuo
  • 15:47 - 15:52
    wakati Roho Mtakatifu anaposhuhudia rohoni mwetu.
  • 15:52 - 15:56
    Roho Mtakatifu anashuhudiaje rohoni mwetu?
  • 15:56 - 15:59
    Kupitia dhamiri zetu.
  • 15:59 - 16:05
    Paulo alielezea zaidi katika Warumi 9:1.
  • 16:05 - 16:07
    Anasema,
  • 16:07 - 16:24
    9 Ninasema kweli katika Kristo na dhamiri yangu inanishuhudia kwa njia ya Roho Mtakatifu kuwa sisemi uongo
  • 16:26 - 16:34
    Kwa hiyo, 1 Wakorintho 2:9-15 inafundisha kwamba hisi zetu za asili
  • 16:34 - 16:39
    haziwezi kufahamu wala kujua mambo ya Mungu au mambo ya Roho
  • 16:39 - 16:43
    kwa sababu yanaweza tu kutambulika kiroho.
  • 16:43 - 16:46
    Na ikiwa haya yote yanaonekana kuwa mengi kwako, usijali.
  • 16:46 - 16:50
    Katika safu ya msingi tunapoendelea, haya yote yatanyambulishwa.
  • 16:50 - 16:52
    ili kwamba uweze kuelewa kweli
  • 16:52 - 16:56
    jinsi tunavyoweza kuhusiana na Mungu kupitia roho zetu
  • 16:56 - 17:00
    na mtu ni nini hasa - roho yake, mwili wake, nafsi yake.
  • 17:00 - 17:04
    Kwa hivyo subiri unapopata zaidi juu ya haya kwenye safu ya msingi
  • 17:04 - 17:05
    inayokuja hivi karibuni.
  • 17:05 - 17:07
    Kwa hivyo inapokuja kwenye maarifa ya mwanadamu,
  • 17:07 - 17:10
    hisia zetu haziwezi kuona moyo au roho ya mwanadamu.
  • 17:10 - 17:13
    Vinaweza tu kuona mwili wa mwanadamu kwa sababu ndiyo
  • 17:13 - 17:18
    sehemu ya mwanadamu ambayo imeunganishwa na ulimwengu huu unaoonekana.
  • 17:18 - 17:20
    Eneo la hisia.
  • 17:20 - 17:25
    Mwili na hisi za mwanadamu haziwezi kuunganishwa na ulimwengu wa kiroho.
  • 17:25 - 17:30
    Ni roho ya mwanadamu pekee ambayo ni sehemu ya kiroho ya mwanadamu
  • 17:30 - 17:35
    ambayo inaweza kuunganishwa na makao ya roho, ambayo ni mahala pa Mungu.
  • 17:35 - 17:37
    Kweli, ndivyo hivyo.
  • 17:37 - 17:41
    Swali ni: Je, tunaangaliaje katika mwelekeo huo?
  • 17:41 - 17:45
    Ili kuingia kwenye ulimwengu huo wa roho,
  • 17:45 - 17:50
    mwanadamu lazima awe katika roho akiongozwa na Roho Mtakatifu.
  • 17:50 - 17:53
    Roho zetu, mioyo yetu ndio sehemu ya mawasiliano,
  • 17:53 - 17:56
    mahali pa kuwasiliana na Roho Mtakatifu.
  • 17:56 - 17:58
    Roho Mtakatifu anatumia mioyo yetu
  • 17:58 - 18:01
    kuwasiliana nasi.
  • 18:01 - 18:08
    Na Mungu anazungumza na mioyo yetu, na roho zetu, sio masikio yetu.
  • 18:08 - 18:13
    Ninakushauri usome Kitabu cha Matendo 17 -
  • 18:13 - 18:17
    wakati watu wa Athene walipokuwa wakimtafuta Mungu
  • 18:17 - 18:20
    kwa akili zao na maarifa ya hisia
  • 18:20 - 18:25
    ili kumtafuta na kumwabudu Mungu.
  • 18:25 - 18:26
    Acha nisome
  • 18:33 - 18:39
    Matendo ya Mitume 17:23
  • 18:39 - 18:58
    23 Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini niliona sehemu nyingi za kuabudia. Niliona pia madhabahu moja iliyoan dikwa, ‘Kwa Mungu asiyejulikana.’ Huyo Mungu mnayemwabudu bila kumfahamu, ndiye ninayemtangaza kwenu.
  • 18:58 - 19:09
    24 Mungu aliyeumba dunia na vitu vyote vilivyomo, ambaye pia ni Bwana wa mbingu na nchi, haishi katika mahekalu yaliyojengwa na wanadamu.
  • 19:09 - 19:20
    25 Wala hahu dumiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji cho chote; kwa sababu yeye ndiye anayewapa watu wote uhai na pumzi na kila kitu.
  • 19:21 - 19:35
    26 Yeye aliumba mataifa yote ya wanadamu waishi juu ya nchi kutokana na mtu mmoja. Pia amepanga muda wa maisha ya watu wote, akaweka na mipaka ya mahali watakapoishi
  • 19:35 - 19:47
    27 ili wamtafute Mungu na wamfahamu. Lakini Yeye hayuko mbali nasi kwa maana
  • 19:47 - 20:00
    28 ‘Tunaishi na kuenenda na kuwa na uhai ndani yake,’ na kama mtunga mashairi wenu alivyosema, ‘Sisi ni uzao wa Mungu.’
  • 20:00 - 20:21
    29 Kwa kuwa sisi ni wa uzao wa Mungu hatupaswi kudhani kuwa yeye ni kama sanamu ya dhahabu au fedha au jiwe iliyotengenezwa kwa akili na ufundi wa mwanadamu.
  • 20:23 - 20:27
    Kwa kuwa watu wote wana roho, tunapaswa kujiuliza swali
  • 20:27 - 20:36
    Kwa nini inaonekana kwamba wanadamu wengi hawana uhusiano wowote na Mungu?
  • 20:36 - 20:40
    Ukweli ni kwamba Mungu amewaumba wanadamu
  • 20:40 - 20:45
    kufanya kazi katika ulimwengu wa asili na wa kiroho.
  • 20:45 - 20:51
    Lakini wengi wetu tunaishi katika hisia, namaanisha katika asili.
  • 20:51 - 20:56
    Na sisi tuko butu inapokuja kwa mambo ya Roho.
  • 20:56 - 21:00
    Kwa sababu kama Maandiko yanavyosema katika Kitabu cha 1 Wakorintho 2:9
  • 21:00 - 21:03
    mambo ya Rohoni si dhahiri.
  • 21:03 - 21:05
    Hatuwezi kuyaona.
  • 21:05 - 21:12
    Na Biblia inasema zaidi katika 1 Wakorintho 15:46-47,
  • 21:12 - 21:15
    Ngoja nisome.
  • 21:16 - 21:38
    1 Wakorintho 15:46.
  • 21:38 - 21:46
    46 Lakini si yule wa kiroho aliyekuja kwanza; bali ni yule wa mwili, na kisha yule wa kiroho.
  • 21:47 - 22:01
    47 Mtu wa kwanza alitoka katika nchi, alifanywa kwa mavumbi; mtu wa pili ni Bwana kutoka mbinguni.
  • 22:01 - 22:14
    48 Na kama alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na alivyo mtu wa mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
  • 22:15 - 22:21
    Maandiko haya tuliyosoma hivi punde yanabainisha aina mbili za wanaume.
  • 22:21 - 22:25
    Mtu wa asili na mtu wa kiroho.
  • 22:25 - 22:31
    Mwanadamu wa asili ni kipofu wa kiroho na ni butu katika ufahamu
  • 22:31 - 22:34
    katika ulimwengu usioonekana.
  • 22:34 - 22:40
    Ulimwengu wa roho umefungwa kabisa nje ya maono yake ya kiroho.
  • 22:40 - 22:44
    Ni wakati tu Roho Mtakatifu anaangaza macho yake ya kiroho
  • 22:44 - 22:50
    ili aweze kuona na kuelewa mambo ya Rohoni.
  • 22:50 - 22:55
    Waefeso 1:7-18 inasema kwamba Bwana Mungu wetu Yesu Kristo,
  • 22:55 - 22:58
    Baba wa Utukufu, anaweza kutupa Roho wa Ufunuo
  • 22:58 - 23:02
    na hekima katika kumjua Yeye
  • 23:02 - 23:06
    ili macho ya ufahamu wetu yafumbuliwe
  • 23:06 - 23:10
    Ili tuweze kujua tumaini la mwito wake ni nini
  • 23:10 - 23:13
    na utajiri wa utukufu wake ukoje
  • 23:13 - 23:17
    katika urithi wake wa watakatifu.
  • 23:17 - 23:32
    Na tumai mna Biblia zenu hapo, twende sasa kwenye 1 Wakorintho 2:9 na tusome pamoja kuanzia mstari wa 9 mpaka ule wa 12.
  • 23:32 - 23:43
    9 Lakini, kama Maandiko yasemavyo, “Hakuna aliyeona, hakuna aliyesikia, hakuna aliyewaza, kile ambacho Mungu amekiandaa kwa ajili ya watu wampendao.”
  • 23:43 - 23:53
    10 Lakini Mungu amekidhihirisha kwetu kwa njia ya Roho wake. Roho huchunguza kila kitu, hata mambo ya ndani ya Mungu.
  • 23:53 - 24:06
    11 Kwa maana ni nani anajua mawazo ya mtu isipo kuwa roho aliye ndani ya huyo mtu? Vivyo hivyo hakuna mtu anayeelewa mawazo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.
  • 24:06 - 24:15
    12 Sisi hatukupokea roho ya dunia hii bali Roho aliyetoka kwa Mungu ili tuweze kuelewa yale ambayo Mungu ametupatia bure
  • 24:15 - 24:20
    Kwa hivyo swali ni: Je, tunaunganishwaje na Roho?
  • 24:20 - 24:22
    Je, unaunganaje na Roho?
  • 24:22 - 24:25
    Kwa imani.
  • 24:25 - 24:31
    Kumwamini Kristo Yesu - huo ndio muunganiko wetu pekee.
  • 24:31 - 24:34
    Kwa hiyo tunaishije kwa imani?
  • 24:34 - 24:37
    Kumbuka, tunaishi kwa imani
  • 24:37 - 24:45
    tunapotambua muungano wetu na Yesu Kristo katika roho.
  • 24:45 - 24:46
    Kuishi kwa imani,
  • 24:46 - 24:51
    roho zetu lazima zitawale hisia zetu,
  • 24:51 - 24:53
    na ili roho zetu zitawale hisia zetu,
  • 24:53 - 24:57
    mawazo yetu lazima yafanywe upya kwa kulijua Neno
  • 24:57 - 25:00
    na kulifanyia kazi.
  • 25:00 - 25:05
    Kwa hiyo tunajuaje kwamba akili zetu zimefanywa upya?
  • 25:05 - 25:07
    Swali zuri.
  • 25:07 - 25:10
    Akili zetu zinafanywa upya
  • 25:10 - 25:14
    tunapoanza kufikiria sio juu ya udhaifu wetu
  • 25:14 - 25:21
    na mapungufu, bali haki yetu katika Kristo Yesu.
  • 25:21 - 25:26
    2 Wakorintho 12:7-10
  • 25:26 - 25:32
    Yote ni kuhusu uzoefu wa Mtume Paulo na mwiba.
  • 25:35 - 25:54
    7 Na ili nisijione bora kuliko nilivyo, kutokana na mafunuo haya makuu, nilipewa mwiba katika mwili wangu, mtumishi wa shetani, ili anitese.
  • 25:54 - 26:00
    8 Nimemsihi Bwana mara tatu aniondolee mwiba huu.
  • 26:01 - 26:21
    9 Lakini aliniambia, “Neema yangu inakutosha, kwa kuwa uwezo wangu unakamilika katika udhaifu.” Kwa hiyo nitajisifu kwa furaha zaidi kuhusu udhaifu wangu ili uwezo wa Kristo ukae juu yangu.
  • 26:22 - 26:27
    Unaona, wakati Paulo alipoteswa na mwiba katika mwili wake.
  • 26:27 - 26:31
    alimwomba Mungu mara nyingi ili Mungu aondoe mwiba huo.
  • 26:31 - 26:35
    Lakini Mungu akamwambia: “Neema yangu yakutosha.”
  • 26:35 - 26:36
    Kwa nini?
  • 26:36 - 26:42
    Maana nguvu zangu hukamilishwa katika udhaifu.
  • 26:42 - 26:46
    Mara, ufunuo wa mapenzi ya Mungu ulippomjia,
  • 26:46 - 26:49
    Paulo hakulalamika tena.
  • 26:49 - 26:53
    Akasema badala yake, ninapokuwa dhaifu, nina nguvu.
  • 26:53 - 26:57
    Akili yake ilifanywa upya na akaacha kuwa na wasiwasi
  • 26:57 - 27:00
    kuhusu mwiba katika mwili wake.
  • 27:00 - 27:05
    Kwa hivyo, hebu tufanye muhtasari wa majibu ya maswali haya yote.
  • 27:05 - 27:11
    Mtu wa asili - mtu wa hisia anaufahamu kuhusu mwili wake tu.
  • 27:11 - 27:13
    na hana ufahamu wa ulimwengu wa roho.
  • 27:13 - 27:16
    Kwa nini iko hivyo?
  • 27:16 - 27:18
    Biblia inasema tangu kuanguka kwa mwanadamu,
  • 27:18 - 27:22
    mwanadamu amepoteza fahamu zake za roho
  • 27:22 - 27:26
    kwa sababu ya dhambi na hufanya kazi katika asili tu.
  • 27:26 - 27:29
    Tunaweza kusoma kuhusu hili katika Mwanzo 6:3.
  • 27:29 - 27:33
    Roho ya mwanadamu wa asili imekufa kwa Mungu kwa sababu ya dhambi
  • 27:33 - 27:35
    tangu Adamu,
  • 27:35 - 27:39
    mwili wa mwanadamu, ambao Biblia inauita utu wa nje,
  • 27:39 - 27:44
    mtu wa nje au mzee ni sehemu ya mwili ya mwanadamu
  • 27:44 - 27:48
    iliyoundwa na Mungu kuingiliana na ulimwengu unaoonekana au wa mwili.
  • 27:48 - 27:50
    Hiyo ni kweli.
  • 27:50 - 27:52
    Wakati roho ya mwanadamu
  • 27:52 - 27:56
    ni sehemu ya kiroho ya mwanadamu iliyoundwa na Mungu
  • 27:56 - 28:00
    kuingiliana au kuwasiliana na yasiyoonekana
  • 28:00 - 28:05
    au ulimwengu wa kiroho ambapo Mungu anakaa.
  • 28:05 - 28:07
    Kwa hiyo mtu wa kiroho ni,
  • 28:07 - 28:11
    yule ambaye roho yake imeumbwa upya au kufanywa upya
  • 28:11 - 28:16
    kwa nguvu za Mungu katika hatua ya kuzaliwa upya kiroho kwa imani
  • 28:16 - 28:18
    katika Kristo Yesu.
  • 28:18 - 28:21
    Hivyo ndivyo Yesu alimaanisha alipomwambia Nikodemo
  • 28:21 - 28:23
    katika kitabu cha Yohana 3:3.
  • 28:23 - 28:25
    Unahitaji kuzaliwa mara ya pili.
  • 28:25 - 28:28
    Yesu akajibu, akamwambia, Hakika,
  • 28:28 - 28:32
    Nawaambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili,
  • 28:32 - 28:36
    hawezi kuuona ufalme wa Mungu” (Yohana 3:3).
  • 28:37 - 28:40
    Tuko hapa leo kuutafuta Ufalme wa Mungu
  • 28:57 - 29:05
    Unamaanisha nini unaposema kwa nje?
  • 29:07 - 29:12
    Kwa hivyo unamaanisha nini unaposema kwa "nje"?
  • 29:12 - 29:18
    Kwa "nje", tunamaanisha kile kinachoonekana, nyenzo, kimwili -
  • 29:18 - 29:22
    vitu unavyoweza kuona kwa macho yako ya asili,
  • 29:22 - 29:24
    kusikia kwa masikio yako,
  • 29:24 - 29:29
    mambo ambayo unaweza kuhisi au kuyajua kiakili.
  • 29:29 - 29:31
    Kinyume chake, 'ndani' inarejelea
  • 29:31 - 29:36
    kwa mambo ambayo hatuwezi kuyaona, kama moyo wa mwanadamu, roho ya mwanadamu,
  • 29:36 - 29:41
    ambayo ni hali ya kiroho ya mwanadamu ambayo ni Mungu pekee anaweza kuona.
  • 29:41 - 29:44
    Ndiyo maana, kuhusu wanadamu,
  • 29:44 - 29:46
    mtu anahitaji kuongozwa na ufunuo wa kiungu
  • 29:46 - 29:51
    ili kupata kiini cha jambo linapokuja suala la hukumu.
  • 29:51 - 29:53
    Tunapolijuajua hili.
  • 29:53 - 29:56
    Tunajua kwamba hatupaswi kumhukumu mtu yeyote kwa sura
  • 29:56 - 29:59
    kwa sababu Mungu pekee ndiye anayejua hali halisi
  • 29:59 - 30:03
    ya moyo wa mwanadamu.
  • 30:03 - 30:08
    Inapokuja kwa mambo ya Mungu asiyeonekana,
  • 30:08 - 30:10
    tunahitaji kuwa katika roho
  • 30:10 - 30:13
    kwa sababu imani pekee ndiyo impendezayo Mungu.
  • 30:13 - 30:17
    Waebrania 11:6
  • 30:17 - 30:22
    Pasipo imani haiwezekani kumpendeza;
  • 30:22 - 30:27
    kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba Mungu yuko
  • 30:27 - 30:32
    na kwamba Yeye ndiye Mlipaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii.
  • 30:32 - 30:37
    Tunamtafuta kwa bidii, kama tulivyosema leo, kwa imani.
  • 30:37 - 30:41
    Kumbuka, imani inamlenga Mungu asiyeonekana,
  • 30:41 - 30:45
    wakati maono ya asili yanalenga nje, kinachoonekana,
  • 30:45 - 30:49
    kile kinachoonekana, ambacho ni halisi.
  • 30:49 - 30:52
    Kwa hiyo mtu wa kiroho, namaanisha, mtu wa imani
  • 30:52 - 30:56
    haridhiki na ujuzi wa akili bali hutazama zaidi ya hayo,
  • 30:56 - 31:00
    kwa sababu Biblia inasema katika 2 Wakorintho 5:7,
  • 31:00 - 31:02
    tunaenenda kwa imani, si kwa kuona.
  • 31:02 - 31:05
    Ndiyo, imani ni kutoka katika roho ya mwanadamu.
  • 31:05 - 31:08
    Ninamaanisha ulimwengu usioonekana au ulimwengu wa kiroho.
  • 31:08 - 31:11
    Na kuona ni kutoka katika mwili wa mwanadamu,
  • 31:11 - 31:15
    ulimwengu unaoonekana au ulimwengu wa asili.
  • 31:16 - 31:22
    Na sasa, hebu tutazame tena katika kitabu cha 2 Wakorintho 4 kuanzia mstari wa 19.
  • 31:22 - 31:23
    Hebu tusome pamoja.
  • 31:23 - 31:27
    2 Wakorintho 4:18
  • 31:28 - 31:42
    18 Kwa maana hatuweki mawazo yetu kwenye vitu vinavyoonekana bali kwenye vitu visivyoonekana. Maana vile vinavyoonekana ni vya muda mfupi, lakini vile visivyoonekana vinadumu milele.
  • 31:42 - 31:50
    Na Biblia inasema zaidi katika 1 Samweli 16:6-13, unaweza kusoma zaidi kwa undani katika wakati wako.
  • 31:50 - 31:55
    yote ni kuhusu Samweli na Daudi, mfalme wa kwanza wa Israeli.
  • 31:55 - 32:00
    Samweli, nabii alitumwa kwenye nyumba ya Yese huko Bethlehemu
  • 32:00 - 32:05
    kumtia mafuta Mfalme mpya aliyewekwa rasmi wa Israeli.
  • 32:05 - 32:10
    Alipofika, alimtazama mwana wa Yese mwenye sura nzuri zaidi
  • 32:10 - 32:15
    kama mfalme mteule lakini Mungu alimkataa
  • 32:15 - 32:17
    na akamchagua aliyepuuzwa.
  • 32:17 - 32:23
    mvulana wa kawaida mdogo na mchungaji, Daudi
  • 32:23 - 32:27
    Muulize Nabii Samweli katika Kitabu cha 1 Samweli 16:7
  • 32:27 - 32:30
    na angekufundisha kwamba
  • 32:30 - 32:33
    tunapaswa kujifunza kuzingatia sio nje
  • 32:33 - 32:39
    Ninamaanisha, sio juu ya sifa za nje za mwanadamu zinazoonekana.
  • 32:39 - 32:42
    Lakini tunapaswa kuzingatia ndani kwa kuangalia ndani
  • 32:42 - 32:45
    moyoni kwa msaada wa Roho Mtakatifu.
  • 32:45 - 32:51
    Ikiwa tunataka kuona mambo jinsi Mungu anavyoyaona juu ya mwanadamu.
  • 32:51 - 32:53
    Kwa hiyo asante sana.
  • 32:53 - 32:57
    Ndiyo, huo ulikuwa mtazamo mfupi wa maana yake - 'nje' na 'ndani'.
  • 32:57 - 33:02
    Na ndio, sote tunahitaji kuukuza utu wetu wa ndani, mtu wetu wa kiroho.
  • 33:02 - 33:06
    Na kwa msaada wa Roho Mtakatifu kila siku, kila wakati tunaweza.
  • 33:11 - 33:18
    Mtu anawezaje kukuza imani kwa Mungu, kwa dhati?
  • 33:18 - 33:24
    Kwanza, kuna haja ya kujua imani ni nini.
  • 33:24 - 33:28
    Tatizo la imani linafanywa kuwa rahisi kueleweka pale tu
  • 33:28 - 33:31
    tunapojua kwamba imani ni kutenda tu
  • 33:31 - 33:34
    juu ya kile ambacho Mungu amesema.
  • 33:34 - 33:40
    Suala kuu la imani yetu ni ukweli wa imani hiyo.
  • 33:40 - 33:44
    Ili imani iwe ya kweli, lazima itegemee Neno la Mungu,
  • 33:44 - 33:52
    ambayo ni Roho na uzima. ( Yohana 6:63 )
  • 33:52 - 33:55
    Mwanadamu huongea maneno ya kawaida
  • 33:55 - 34:02
    bali Mungu hunena Maneno ambayo ni Roho na uzima.
  • 34:02 - 34:05
    Lakini ili neno la mwanadamu liwe Neno la Mungu,
  • 34:05 - 34:09
    lazima liathiriwe na Roho Mtakatifu kwa uzima.
  • 34:09 - 34:14
    Swali ni: Je, mwanadamu anaweza kusema Maneno ya uzima?
  • 34:14 - 34:16
    Mwanadamu huongea maneno ya kawaida
  • 34:16 - 34:21
    lakini mwanadamu anaweza kunena Maneno ya uzima ambayo ni roho na uzima
  • 34:21 - 34:25
    yanapoathiriwa na Roho Mtakatifu.
  • 34:25 - 34:31
    Maneno hayo lazima yaathiriwe na Roho Mtakatifu kwa uzima.
  • 34:31 - 34:34
    Ninamaanisha nini naposema kwa uzima katika Neno?
  • 34:34 - 34:36
    Neno la Mungu ni Roho na uzima
  • 34:36 - 34:41
    kwa sababu lina uwezo wa kuzalisha nguvu ya kiroho
  • 34:41 - 34:47
    ambayo hukua na kustawi ndani ya mioyo yetu iitwayo imani.
  • 34:47 - 34:52
    Imani hiyo ndiyo inayosukuma maneno yetu kufanya maajabu.
  • 34:52 - 34:55
    Hiyo ni imani ya Biblia.
  • 34:55 - 35:14
    Imani ya Biblia inaitwa Imani ya Kiroho, katika kitabu cha 2 Wakorintho 4:13
  • 35:14 - 35:37
    13 Lakini kwa kuwa tuna roho ile ile ya imani; kama ilivyoandikwa, Niliamini, na kwa sababu hiyo nilinena; sisi nasi twaamini, na kwa sababu hiyo twanena
  • 35:37 - 35:43
    Kwa hivyo imani hufanyika katika sehemu mbili:
  • 35:43 - 35:45
    Kwa mioyo yetu tunaamini;
  • 35:45 - 35:52
    Kwa vinywa vyetu tunakiri, na imani ni yote mawili.
  • 35:52 - 35:56
    Unajua, mfano wa wana saba wa Skeva unaonyesha hivyo
  • 35:56 - 35:59
    imani ya kweli si kuiga.
  • 35:59 - 36:03
    Imani lazima itokee katika moyo wa kila mtu
  • 36:03 - 36:07
    au katika usadikisho, ambao unaongoza kwenye harakati halisi
  • 36:07 - 36:10
    au maungamo halisi ya imani.
  • 36:10 - 36:15
    Ili imani iwe ya kweli, moyo na kinywa havipaswi kupingana kamwe.
  • 36:15 - 36:19
    Kwa maneno mengine, tunapaswa kumaanisha kile tunachosema.
  • 36:19 - 36:22
    Hii ina maana kwamba tunapaswa kuamini kile tunachokiri.
  • 36:22 - 36:24
    Je, unaamini unachokiri?
  • 36:24 - 36:26
    Unamaanisha unachosema?
  • 36:26 - 36:29
    Kwa sababu imani ya kimaandiko au imani ya kibiblia imeonyeshwa
  • 36:29 - 36:35
    kwa kuamini kwenye moyo na kukiri kwa kinywa.
  • 36:35 - 36:39
    Kinywa lazima kiwe na makubaliano kamili ya moyo
  • 36:39 - 36:42
    kabla ya kuwa na maungamo ya imani yanayokubalika au ya kweli.
  • 36:42 - 36:45
    Kweli kabisa.
  • 36:45 - 36:47
    Huo ndio ufunguo, makubaliano.
  • 36:47 - 36:52
    Swali ni: Imani inaweza kusitawije?
  • 36:52 - 36:56
    Ukuaji wa Neno la Mungu moyoni mwako,
  • 36:56 - 37:01
    huzaa imani ndani ya moyo wako.
  • 37:01 - 37:02
    Warumi 10:17
  • 37:02 - 37:08
    Imani hukua tunaposikia na kutii Neno la Mungu.
  • 37:16 - 37:30
    Je, mtu anahamaje kutoka kwenye ujuzi wa hisia hadi ujuzi wa ufunuo?
  • 37:37 - 37:42
    Je, mtu anahamaje kutoka kwenye ujuzi wa hisia hadi ujuzi wa ufunuo?
  • 37:42 - 37:47
    Ndiyo, hilo ndilo jambo ambalo sisi sote waamini tunapaswa kujiuliza.
  • 37:47 - 37:51
    Hebu tukumbuke kilichompata mtumishi wa Elisha.
  • 37:51 - 37:53
    Kwa macho yake ya kimwili,
  • 37:53 - 37:58
    mtumishi wa Elisha aliona hatari ya papo hapo na hofu ikamshika.
  • 37:58 - 38:03
    Bwana wake alipomwomba Mungu amfungue macho ya rohoni.
  • 38:03 - 38:08
    Macho yake yakafunguliwa na katika roho,
  • 38:08 - 38:11
    aliona malaika wakimzunguka.
  • 38:11 - 38:12
    Na nini kilitokea?
  • 38:12 - 38:14
    Hofu yake ikatoweka.
  • 38:14 - 38:15
    Ndiyo.
  • 38:15 - 38:20
    Kwa hivyo kuhama kutoka maarifa ya hisi hadi maarifa ya ufunuo
  • 38:20 - 38:26
    ni suala la kuukabidhi moyo wako kwa Roho Mtakatifu.
  • 38:26 - 38:30
    Roho Mtakatifu ndiye anayefungua macho ya imani yetu
  • 38:30 - 38:34
    kuona ukweli uliofichwa katika Neno la Mungu.
  • 38:34 - 38:38
    Kutafakari katika Neno la Mungu huleta ufunuo.
  • 38:46 - 38:48
    Huo ndio ufunguo.
  • 38:48 - 38:55
    Tunatafakari hadi Mungu atupe nuru iliyo wazi, ufahamu wazi.
  • 38:55 - 38:57
    Kwa hiyo unapotafakari Neno la Mungu,
  • 38:57 - 39:03
    kumruhusu Roho Mtakatifu kuchukua uongozi, ufunuo utakuja
  • 39:03 - 39:06
    na utakapokuja wahyi, utakubeba
  • 39:06 - 39:10
    zaidi ya ulimwengu wa hisi ndani ya uwepo wa Mungu
  • 39:10 - 39:14
    katika roho na huko utaona waziwazi;
  • 39:14 - 39:17
    hapo ndipo ufahamu wa kiroho unakuja.
  • 39:55 - 39:56
    Jiweke katika Maandiko
  • 39:56 - 39:58
    na kumsikia Mungu akikuambia,
  • 39:58 - 40:02
    Walio pamoja nawe ni wengi kuliko wale walio kinyume chako.
  • 40:33 - 40:37
    Wengi leo katika nyumba zao wanalemewa na hali zao
  • 40:37 - 40:39
    kwa sababu tunaitazama kwa asili
  • 40:39 - 40:43
    na unazidiwa na hofu inakuja na shaka inakuja.
  • 40:43 - 40:45
    Kwa hivyo kuna haja ya sisi kubadili mtazamo wetu
  • 40:45 - 40:49
    kutoka asili hadi kiroho.
  • 40:49 - 40:52
    Kwa hivyo kuhama kutoka maarifa ya hisi kwenda kwenye ufunuo
  • 40:52 - 40:55
    ni kwa neema.
  • 40:55 - 40:58
    Unachohitaji kufanya ni kunyenyekea
  • 40:58 - 41:05
    chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu - Roho wa Ufunuo.
  • 41:05 - 41:08
    Mabadiliko hayo, hatua hiyo ni kidogo kidogo,
  • 41:08 - 41:12
    kila siku, kidogo kidogo, kila dakika, kidogo kidogo.
  • 41:12 - 41:17
    Ni safari na safari ya maili elfu moja huanza na hatua moja.
  • 41:17 - 41:18
    Kwa hivyo tuna furaha sana leo
  • 41:18 - 41:22
    kwamba ulijiunga nasi kuchukua hatua hiyo, hatua hiyo kuelekea kiroho
  • 41:22 - 41:26
    kwa kuungana nasi kwenye programu leo.
  • 41:29 - 41:34
    Kwa hivyo safari hiyo leo imeanza na hatua hii ambayo umechukua.
  • 41:34 - 41:35
    Na kumbuka mfululizo wa FOUNDATION SERIES,
  • 41:35 - 41:36
    MIHADHARA YA KIMUNGU
  • 41:36 - 41:39
    ambayo umekuwa ukiona kwenye Chuo Kikuu cha Mungu -
  • 41:39 - 41:41
    Huhitaji tu kuzitazama mara moja
  • 41:41 - 41:43
    unajua, Neno la Mungu halifungwi na wakati.
  • 41:43 - 41:45
    Kila Neno la Mungu ni Roho na Uzima.
  • 41:45 - 41:48
    Chukua muda kutazama tena na tena,
  • 41:48 - 41:52
    pitia vifungu vya Biblia, tafakari ukweli uliofichwa hapo
  • 41:52 - 41:55
    na ukitaka kutafuta mahali mafundisho hayo yalipo,
  • 41:55 - 41:57
    unaweza kuangalia katika maelezo hapa chini.
  • 41:57 - 42:01
    Kuna kiunga na ikiwa una maswali zaidi, kumbuka,
  • 42:01 - 42:06
    unapotafakari mafundisho haya, maswali yatatokea moyoni mwako
  • 42:06 - 42:09
    na unaweza kutuma maswali yako kwetu kwa kwenda
  • 42:09 - 42:12
    kwa tovuti yetu - theuog.org - kwenda kwa sehemu ya mawasiliano
  • 42:12 - 42:14
    na kututumia ujumbe.
  • 42:14 - 42:19
    Na tutapitia maswali yako yote na kwa neema ya Mungu,
  • 42:19 - 42:22
    wajibu chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu.
  • 42:22 - 42:26
    Hakuna njia ya mkato ya ukomavu wa kiroho.
  • 42:26 - 42:31
    Ufahamu wetu wa kidunia lazima utoe nafasi kwa ufahamu wa kiroho au ufunuo, kufikia ukomavu. ” – Nabii TB Joshua
  • 42:31 - 42:33
    au ufunuo kufikia ukomavu.
  • 42:33 - 42:36
    Mafundisho yote tunayokupa hayana muda.
  • 42:36 - 42:40
    Tafadhali pitia, tafakari juu yake,
  • 42:40 - 42:41
    na umwombe Roho Mtakatifu akusaidie
  • 42:41 - 42:43
    kuwa na uelewa mzuri juu yake.
  • 42:43 - 42:47
    Hiyo ndiyo njia pekee ya imani inaweza kukua katika maisha yetu.
  • 42:47 - 42:49
    Kwamba tuna ufunuo haimaanishi
  • 42:49 - 42:51
    tunaweza kukulazimisha kuamini;
  • 42:51 - 42:54
    lazima uwe na ufunuo na usadikisho wako mwenyewe.
  • 42:54 - 42:55
    Inakujaje?
  • 42:55 - 42:57
    Isome, itafakari.
  • 42:57 - 43:01
    Ruhusu Roho wa Mungu akuongezee ufahamu wako.
  • 43:01 - 43:03
    Tunahitaji kuwa wakristo wakomavu
  • 43:03 - 43:06
    kwa sababu tuko katika mazingira yenye changamoto nyingi
  • 43:06 - 43:09
    na Mungu anataka uishi kwa imani, uwe hodari katika imani.
  • 43:09 - 43:11
    Unaweza kufanya hivyo jinsi gani?
  • 43:11 - 43:14
    Unaweza kufikia hilo tu kwa kuendeleza uhusiano wako
  • 43:14 - 43:18
    pamoja na Mgeni wa ajabu asiyeonekana - Roho Mtakatifu.
  • 43:18 - 43:20
    Vipi? Kuvutia umakini wake.
  • 43:20 - 43:24
    Na unaweza kufanya hivyo tu unapotafakari Neno na kuomba
  • 43:24 - 43:28
    na atakuja na kuziboresha pwani za kiroho.
  • 43:28 - 43:30
    katika jina la Yesu.
  • 43:35 - 43:40
    Kama vile Nikodemo alivyomwendea Yesu usiku ili kuuliza maswali,
  • 43:40 - 43:44
    kujua na kukuza imani katika Yesu,
  • 43:44 - 43:48
    wewe pia unaweza kutazama hili na kuuliza maswali moyoni mwako kwa Mungu
  • 43:48 - 43:49
    na Roho Mtakatifu,
  • 43:49 - 43:53
    Msaidizi, Mshauri atakuja na kujibu maswali yako
  • 43:53 - 43:55
    kupitia Neno la Mungu.
  • 43:55 - 43:59
    Ndiyo, ndiyo maana kila kitu kiko katika nuru ya Neno la Mungu.
  • 43:59 - 44:03
    Amina. Watakatifu, ndugu, dada, waumini duniani kote,
  • 44:03 - 44:07
    tunaenda kukuombea.
  • 44:07 - 44:09
    Tumeona barua pepe nyingi sana.
  • 44:09 - 44:11
    Tulipitia maswali na majibu yote.
  • 44:11 - 44:14
    Tumeona watu wengi wakipitia uchungu,
  • 44:14 - 44:16
    maumivu na matatizo.
  • 44:16 - 44:20
    Kwa hiyo tunaenda kuomba pamoja, mwamini Mungu
  • 44:20 - 44:24
    kwamba Mungu Mwenyezi atakutana nawe katika hatua ya hitaji lako muhimu,
  • 44:24 - 44:26
    kwa maana Yesu hafanyi neno lolote pasipo Neno lake.
  • 44:26 - 44:30
    Usisahau, Neno la Mungu lina kipaumbele kuliko jina.
  • 44:30 - 44:32
    Ndio maana tunakupa mafundisho haya.
  • 44:32 - 44:36
    Lakini tunasimama mbele za Mungu tukiwaombea,
  • 44:36 - 44:40
    na Mungu atakuweka katika rehema zake, katika jina la Yesu.
  • 44:40 - 44:44
    Kwa hivyo, endelea kuungana nasi hapa kwenye Chuo Kikuu cha Mungu.
  • 44:44 - 44:47
    Ujuzi wa hisia hukoma wakati ufunuo unakuja.
Title:
MAJIBU YA BIBLIA YALIYOFICHIKA | INGIA KATIKA ROHO - SEHEMU YA 2
Description:

more » « less
Video Language:
English
Team:
The University of God
Duration:
44:49

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions