Makosa Yako Hayakutafsiri!!! | Kaka Chris
-
0:09 - 0:12Neema na amani iwe kwenu nyote katika jina kuu la Yesu
-
0:12 - 0:20na karibu katika toleo jingine la 'Imani Ni Asili' hapa kwenye TV ya Moyo wa Mungu.
-
0:20 - 0:26Leo, nataka kuzungumzia suala ambalo limejitokeza mara nyingi sana
-
0:26 - 0:33katika mazungumzo na watu - katika nyakati za maombi, ushauri na kutia moyo.
-
0:33 - 0:40Nimeona tu kwamba watu wengi sana leo
-
0:40 - 0:47wanaishi maisha yao kupitia lenzi hii ya jana,
-
0:47 - 0:49kupitia lenzi ya walivyokuwa -
-
0:49 - 0:56mabaya yao ya zamani, makosa, maumivu na uchungu.
-
0:56 - 1:02Na kama matokeo ya hii, wengi hujikuta wamenaswa
-
1:02 - 1:12katika mzunguko huu mbaya wa hatia na hukumu kwa makosa waliyofanya
-
1:12 - 1:18au vilevile mzunguko mbaya wa uchungu na chuki
-
1:18 - 1:23juu ya mabaya waliyofanyiwa huko nyuma.
-
1:23 - 1:27Na ni hatari sana.
-
1:27 - 1:35Watu wa Mungu, hii si chochote ila ni njama ya hila, hila ya kawaida ya shetani
-
1:35 - 1:40ili kukutenganisha na Mungu.
-
1:40 - 1:45Shetani anafurahia kujadili mambo yako ya nyuma na wewe.
-
1:45 - 1:52Anafurahi kukukumbusha juu ya kutofaulu kwako zamani, makosa ya zamani, maumivu ya zamani.
-
1:52 - 1:57Kwa sababu hicho ndicho kitu pekee kinachokuunganisha naye.
-
1:57 - 2:04Hiyo ndiyo habari pekee ambayo anayo kuhusu wewe - siku zako za nyuma.
-
2:04 - 2:11Na shetani atachukua kila njia inayopatikana
-
2:11 - 2:19kujaribu na kukuzuia usitende Neno la Mungu sasa.
-
2:19 - 2:24Angalia, hajali ikiwa utalichambua tu Neno.
-
2:24 - 2:30Haijalishi kama unastaajabia Neno au hata kukubali ukweli wa Neno
-
2:30 - 2:35mradi hutendi Neno hilo.
-
2:35 - 2:39Hataki utende neno la Mungu!
-
2:39 - 2:48Anataka uishi maisha yako kupitia lenzi ya maisha yako ya zamani yasiyofaa,
-
2:48 - 2:53kwa wewe kuchuja kila kitu kupitia hiyo,
-
2:53 - 3:00ili kulemaza uwezo wako wa kutenda imani muda huu
-
3:00 - 3:07na hivyo kuharibu maisha yako ya baadaye.
-
3:07 - 3:20Watu wa Mungu, ni hatari kuchukua safari zisizo za lazima hadi jana.
-
3:20 - 3:23Ni hatari sana.
-
3:23 - 3:30Angalia, siku zako za nyuma haziamui sasa yako
-
3:30 - 3:36na haiamui mustakabali wako.
-
3:36 - 3:41Unaweza kujifunza kutoka kwa maisha yako ya zamani bila kuishi katika maisha yako ya zamani.
-
3:41 - 3:45Usiishi ndani yake; jifunze kutoka kwake.
-
3:45 - 3:54Usiheshimu udanganyifu wa shetani kwa umakini wako - umakini wako wa thamani.
-
3:54 - 4:00Kwa sababu makosa yako hayakufafanui wewe.
-
4:00 - 4:03Zaburi 37:24
-
4:03 - 4:08Narudia - makosa yako hayakufafanui.
-
4:08 - 4:13Kwa kweli, yanaweza hata kukuboresha.
-
4:13 - 4:21Namaanisha, Mungu anaweza hata kutumia makosa yako kukupeleka mahali
-
4:21 - 4:32anapotaka uwe - kulingana na mwitikio wako.
-
4:32 - 4:35Jambo kuu liko kwenye mwitikio wako.
-
4:35 - 4:37Je, uaikiaje kwenye kosa hilo?
-
4:37 - 4:41Sasa, ngoja nikupe mfano mzuri sana.
-
4:41 - 4:44Hebu wazia uko safarini mahali fulani.
-
4:44 - 4:46Unaenda mahali fulani; unajua unakokwenda.
-
4:46 - 4:51Na katika safari hii, ghafla unatambua kuwa uko mahali pasipofaa.
-
4:51 - 4:54Umechukua hatua mbaya; umekosa mwelekeo.
-
4:54 - 4:56Unafanya nini?
-
4:56 - 5:03Unahitaji kurejea hatua zako na kurudi kwenye mstari.
-
5:03 - 5:06Ikiwa unatambua kuwa umeenda katika mwelekeo mbaya, je, unasema tu,
-
5:06 - 5:11'Oh sawa, nimechelewa mno! Acha niendelee tu katika njia hii mbaya.'
-
5:11 - 5:23Hapana! Unarudi haraka kwenye njia sahihi, rudi kwenye mstari na uendelee na safari yako.
-
5:23 - 5:32Watu wa Mungu, katika safari hii ya maisha,
-
5:32 - 5:39ukichukua hatua mbaya, unajibuje?
-
5:39 - 5:42Je, unaitikiaje?
-
5:42 - 5:52Je, unatambua kosa lako, rudia hatua zako na kumkimbilia Mungu kwa toba?
-
5:52 - 5:59Au unakataa kujichunguza,
-
5:59 - 6:03galagala kwa kujihurumia
-
6:03 - 6:16na kuanguka ndani zaidi katika mtandao huo tatanishi wa hatia, lawama na uduni?
-
6:16 - 6:24Je, unarudi kwenye mstari au unaenda nje zaidi?
-
6:24 - 6:28Chaguo ni lako.
-
6:28 - 6:39Kuchagua kuishi katika maisha yako ya zamani ni kuchagua kwenda zaidi nje ya njia.
-
6:39 - 6:45Kuanguka katika hatia na hukumu hiyo - unaenda nje zaidi.
-
6:45 - 6:47Vivyo hivyo, ikiwa unahalalisha kosa lako
-
6:47 - 6:50au unanyosha vidole kushoto, kulia na katikati
-
6:50 - 6:57au kutoa visingizio, natoka nje ya njia.
-
6:57 - 7:01Na jambo la hatari hapa ni kwamba
-
7:01 - 7:09kadiri unavyoongeza kukaa kwako katika makosa,
-
7:09 - 7:18ndivyo uharibifu zaidi shetani anavyoweza kuuletea moyoni mwako.
-
7:18 - 7:27Na shetani anapokuwa na nafasi ndani ya moyo wako.
-
7:27 - 7:32uharibifu huo unaweza kuenea kwa urahisi kwenye nyumba yako,
-
7:32 - 7:38ndoa, familia, mahusiano na kazi yako.
-
7:38 - 7:44Tunasuka mtandao uliochanganyikiwa
-
7:44 - 7:52wakati makosa yetu, tunakataa kuondoka.
-
7:52 - 7:54Sisemi kwamba hutafanya makosa.
-
7:54 - 7:58Kila mtu hufanya makosa katika safari hii.
-
7:58 - 8:00Kila mtu hukosa alama.
-
8:00 - 8:05Ninamaanisha, angalia tu Biblia, mwongozo wetu, Neno la Mungu -
-
8:05 - 8:10wahusika wengi wakuu wa Biblia tunaowasoma.
-
8:10 - 8:14Nuhu alipambana na pombe.
-
8:14 - 8:16Yakobo alitumia udanganyifu.
-
8:16 - 8:19Lutu alipambana na uchu.
-
8:19 - 8:25Vipi kuhusu Musa ambaye alipambana na hasira.
-
8:25 - 8:31Petro mara nyingi aliingiwa na woga, Tomaso na mashaka.
-
8:31 - 8:36Vipi kuhusu Mfalme Daudi, Sulemani, Samsoni - wote walishindwa na tamaa.
-
8:36 - 8:44Hakuna mkamilifu katika ulimwengu huu (Warumi 3:10, 23)
-
8:44 - 8:51Sisi sote hujikwaa kwa njia nyingi (Yakobo 3:2)
-
8:51 - 8:58Katika ulimwengu huu mwovu, kutakuwa na mzozo huo daima,
-
8:58 - 9:04ile vita ndani ya moyo wa mwanadamu kati ya mwili na roho.
-
9:04 - 9:11Wazo lililo moyoni mwako ni vita utakayokabiliana nayo hadi siku ya mwisho,
-
9:11 - 9:15mpaka Yesu atakapokuja - ndivyo vita utakavyokabiliana nayo.
-
9:15 - 9:22Kwa hiyo, faraja yangu kwenu leo, watu wa Mungu, ni hii:
-
9:22 - 9:30Mara tu unapogundua kuwa umechukua hatua mbaya,
-
9:30 - 9:36hrudi haraka kwenye mstari.
-
9:36 - 9:45Usiongeze muda wa kukaa kwako katika makosa kwa kujitetea kwenye hilo.
-
9:45 - 9:54Angalia, kama mtoto wa Mungu, unaweza kujua unapochukua hatua mbaya.
-
9:54 - 10:02Vipi? Roho wa Mungu atachochea dhamiri yako kutubu.
-
10:02 - 10:07Warumi 9:1, 2 Wakorintho 7:10
-
10:07 - 10:14Roho Mtakatifu ataisukuma dhamiri yako kutubu.
-
10:14 - 10:25Swali ni - roho yako ni sikivu kiasi gani?
-
10:25 - 10:32una haraka kiasi gani kujitetea?
-
10:32 - 10:42Kasi ambayo unatambua kosa lako ni sawia
-
10:42 - 10:52na kiwango ambacho Neno la Mungu linatawala moyo wako.
-
10:52 - 11:03Na kuwa mwangalifu zaidi kwa msukumo wa Roho wa Mungu katika roho yako,
-
11:03 - 11:09inakupasa kutumia muda mwingi zaidi miguuni pake,
-
11:09 - 11:13muda mwingi mbele zake,
-
11:13 - 11:16muda zaidi katika Neno Lake.
-
11:16 - 11:22Lazima aongezeke; lazima upungue (Yohana 3:30).
-
11:22 - 11:26Kwa sababu yote yanamhusu Yesu; haikuhusu wewe.
-
11:26 - 11:31Sio juu ya kustahili kwako kwa sababu hakuna mtu anayestahili.
-
11:31 - 11:39Sio juu ya udhaifu wako kwa sababu kila mtu ana udhaifu.
-
11:39 - 11:45Yote ni juu ya utayari wako -
-
11:45 - 11:49utayari wako wa kukiri kosa lako,
-
11:49 - 11:53kuweka kiburi chako kando,
-
11:53 - 11:59rudia hatua zako, rudi kwenye mstari na Mungu
-
11:59 - 12:03na endelea na safari yako ya imani.
-
12:03 - 12:10Kwa sababu si lazima uwe mkamilifu ili uwe mtoto wa Mungu;
-
12:10 - 12:14unatakiwa tu upatikane.
-
12:14 - 12:18Watu wa Mungu, nitawaacha leo na neno la Maandiko
-
12:18 - 12:22kutoka kwa Mtume Paulo katika Warumi 8:1.
-
12:22 - 12:35Akasema, Sasa basi, hakuna hukumu ya adhabu
-
12:35 - 12:39kwa wale walio katika Kristo Yesu."
-
12:39 - 12:44Sasa, Maandiko haya hayatupi msingi wa kuhurumia dhambi,
-
12:44 - 12:50kuhalalisha makosa au kuchukua neema kirahisi. Hapana!
-
12:50 - 13:00Lakini inasisitiza tu kwamba hatupaswi kuruhusu hatia ya makosa yetu
-
13:00 - 13:10kutunyang'anya amani ya pekee inayopatikana katika msamaha wa Kristo.
-
13:10 - 13:15Badala ya kosa lako kukutoa mbele za Mungu,
-
13:15 - 13:23inapaswa kuwa sababu ya wewe kumkaribia Yeye zaidi.
-
13:23 - 13:27Kwa sababu katika maneno ya Nabii TB Joshua:
-
13:27 - 13:38"Unaweza kujua wewe ni mtoto wa Mungu wakati makosa yako yanapochochea maisha yako ya kiroho."
-
13:38 - 13:40Asante, Yesu Kristo.
-
13:40 - 13:44Sasa hivi, watu wa Mungu, ni wakati wa maombi.
-
13:51 - 13:59Hivi sasa, kwa kila moyo uliochafuliwa na hatia -
-
13:59 - 14:05takaswa, katika jina kuu la Yesu Kristo!
-
14:05 - 14:10kwa kila roho inayosumbuliwa na hukumu,
-
14:10 - 14:18takaswa kwa Damu ya thamani ya Yesu Kristo!
-
14:18 - 14:26Damu ya Yesu Kristo inapokusafisha, umetakaswa kwelikweli!
-
14:26 - 14:29Jitakase sasa hivi!
-
14:29 - 14:38Katika roho yako, katika nafsi yako, katika mwili wako - takaswa!
-
14:38 - 14:48Kila roho ya dhiki, utumwa, udhaifu, ndoto mbaya -
-
14:48 - 14:53uoshwe kwa Damu ya Yesu Kristo!
-
14:53 - 15:03Uoshwe sasa hivi, katika jina kuu la Yesu Kristo!
-
15:03 - 15:07Pokea ujasiri!
-
15:07 - 15:10Pokea nguvu!
-
15:10 - 15:20Pokea usadikisho wa kushikilia msimamo wako katika Kristo!
-
15:20 - 15:27Ee Bwana, rekebisha kila moyo mkaidi na utashi.
-
15:27 - 15:30Ongoza hatua zinazoenda kombo.
-
15:30 - 15:35Osha madoa ya hatia.
-
15:35 - 15:41Tusaidie kuona kupitia macho yako.
-
15:41 - 15:48Tuvute kwa uhusiano wa karibu na Wewe
-
15:48 - 15:56na utujalie ufahamu mkubwa zaidi wa moyo Wako.
-
15:56 - 16:06Katika jina kuu la Yesu Kristo! Amina!
-
16:06 - 16:08Asante, Yesu Kristo.
- Title:
- Makosa Yako Hayakutafsiri!!! | Kaka Chris
- Description:
-
Unaweza kujifunza kutoka kwenye maisha yako ya zamani bila kuishi katika maisha yako ya zamani! Jikomboe kutoka kwenye mtego wa hatia na kulaaniwa na utiwe moyo katika safari yako ya imani na ujumbe huu wenye uhalisia kutoka kwa Ndugu Chris unaoitwa, 'Rudi Kwenye Njia'.
‘Imani Ni Asili’ ni kipindi kwenye God’s Heart TV chenye maneno mafupi ya kuhamasisha na kutia moyo kwa ajili ya maisha yako ya kila siku kutoka kwa Neno Hai la Mungu – katika uzuri wa uumbaji Wake. Ubarikiwe unapojiunga nasi, katika jina la Yesu!
SURA:
00:00 - Utangulizi wa 'Imani ni Asili'
00:36 - Wengi leo wanaishi maisha kupitia lenzi ya zamani
01:41 - Shetani anajadili mambo yako ya nyuma na wewe
03:09 - Ni hatari kuchukua safari zisizo za lazima hadi jana
04:06 - Makosa yako hayakutafsiri; yanaweza hata kukusafisha
05:25 - Unajibuje unapochukua hatua mbaya?
07:01 - Usiongeze muda wa kukaa kwako katika makosa
08:10 - Hakuna mtu mkamilifu katika ulimwengu huu
09:55 - Roho Mtakatifu atachochea dhamiri yako kutubu
12:22 Hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu
13:50 - Maombi kwa ajili ya watazamaji pamoja na Ndugu Chris#ImaniNiAsili
➡️ Pata kutiwa moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Saidia TV ya Moyo wa Mungu kifedha - https://godsheart.tv/financial/
➡️ Habari kuhusu Maombi Shirikishi- https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/ - Video Language:
- English
- Team:
God's Heart TV
- Duration:
- 16:33
![]() |
Translation_Admin edited Swahili subtitles for Your Mistakes Do Not DEFINE You!!! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Your Mistakes Do Not DEFINE You!!! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Your Mistakes Do Not DEFINE You!!! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Your Mistakes Do Not DEFINE You!!! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Your Mistakes Do Not DEFINE You!!! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Your Mistakes Do Not DEFINE You!!! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Your Mistakes Do Not DEFINE You!!! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for Your Mistakes Do Not DEFINE You!!! | Brother Chris |