< Return to Video

Dini na watoto

  • 0:00 - 0:04
    Nitaenda kuongelea kuhusu dini.
  • 0:05 - 0:09
    Lakini ni mada pana na nyeti sana,
  • 0:09 - 0:11
    hivyo itabidi nijiwekee mpaka.
  • 0:12 - 0:14
    Na kwahiyo nitajiwekea mpaka
  • 0:14 - 0:18
    kuongelea tu kuhusu uhusiano kati ya dini
    na kujamiiana.
  • 0:18 - 0:20
    (Kicheko)
  • 0:20 - 0:22
    Haya ni majadiliano yenye uzito sana.
  • 0:23 - 0:26
    Hivyo, nitaongelea juu ya ninachokumbuka
    kua cha ajabu sana.
  • 0:26 - 0:29
    Ni pale wanandoa vijana walinong'oneza,
  • 0:29 - 0:32
    "Usiku tutaenda kutengeneza mtoto."
  • 0:32 - 0:37
    Maongezi yangu yatahusu athari ya dini
  • 0:37 - 0:41
    kwa idadi ya watoto kwa mwanamke.
  • 0:41 - 0:43
    Hii ni muhimu kweli,
  • 0:43 - 0:44
    kwa sababu kila mtu anaelewa
  • 0:44 - 0:47
    kua kuna aina fulani ya mpaka
  • 0:47 - 0:50
    kwa jinsi watu wengi wanaweza kua kwenye
    hii sayari.
  • 0:50 - 0:52
    Na kuna baadhi ya watu
  • 0:52 - 0:55
    wanaosema kua idadi ya watu duniani imekua
    kama hivi --
  • 0:55 - 0:57
    bilioni tatu mwaka 1960,
  • 0:57 - 1:00
    bilioni saba mwaka jana tu --
  • 1:00 - 1:01
    na itaendelea kukua
  • 1:01 - 1:05
    kwa sababu kuna dini zinazozuia wanawake
    kuwa na watoto wachache,
  • 1:05 - 1:08
    na inaweza kuendelea hivi.
  • 1:08 - 1:11
    Ni kwa kiasi gani hawa watu wako sahihi?
  • 1:11 - 1:16
    Nilivyozaliwa kulikua na watoto chini ya
    bilioni moja duniani,
  • 1:16 - 1:20
    na leo, 2000, kuna karibia bilioni mbili.
  • 1:20 - 1:22
    Nini kimetokea tangu hapo,
  • 1:22 - 1:25
    na nini wataalam wanatabiri kitatokea
  • 1:25 - 1:27
    na idadi ya watoto karne hii?
  • 1:27 - 1:30
    Hili ni jaribio. Unafikiri nini?
  • 1:30 - 1:34
    Unafikiri itapungua mpaka bilioni moja?
  • 1:34 - 1:38
    Itabaki sawa na kua bilioni mbili ifikapo
    mwisho wa karne?
  • 1:38 - 1:41
    Idadi ya watoto itaongezeka kila mwaka
    hadi miaka 15,
  • 1:41 - 1:44
    au itaendelea na kiwango cha haraka
    kile kile
  • 1:44 - 1:46
    na kua watoto bilioni nne huko juu?
  • 1:46 - 1:50
    Nitawaambia ifikapo mwisho wa hotuba
    yangu.
  • 1:50 - 1:55
    Lakini sasa, dini inahusika vipi?
  • 1:55 - 1:57
    Unapotaka kuainisha dini,
  • 1:57 - 1:59
    ni ngumu kuliko unavyofikiri.
  • 1:59 - 2:02
    Unaenda Wikipedia na ramani ya kwanza
    unayopata ni hii.
  • 2:02 - 2:07
    Inagawanyisha dunia kwenye dini za
    Ibrahimu na dini za Mashariki,
  • 2:07 - 2:09
    lakini hio haina undani wa kutosha.
  • 2:09 - 2:13
    Hivyo tukaenda zaidi na kuangalia kwenye
    Wikipedia, tukapata hii ramani.
  • 2:13 - 2:18
    Lakni hio inaianisha Ukristo, Uislamu na
    Ubuddha
  • 2:18 - 2:19
    kwenye makundi mengi madogo,
  • 2:19 - 2:21
    ambayo yalikua ya kina sana.
  • 2:21 - 2:24
    Kwa hiyo pale Gapminder tulitengeneza
    ramani yetu,
  • 2:24 - 2:27
    Na inaonekana hivi.
  • 2:27 - 2:30
    Kila nchi ni puto.
  • 2:30 - 2:33
    Ukubwa ni idadi ya watu -- China kubwa,
    India kubwa hapa.
  • 2:33 - 2:38
    Na rangi sasa ni dini yenye wengi.
  • 2:38 - 2:41
    Ni dini ambayo watu zaidi ya asilimia 50
  • 2:41 - 2:42
    wanasema wanahusika.
  • 2:42 - 2:47
    Ni dini ya Mashariki huko India na
    China na nchi jirani za Asia.
  • 2:47 - 2:49
    Uislamu ni dini ya wingi
  • 2:49 - 2:52
    njia yote kutoka Bahari ya Atlantiki
    kupitia Mashariki ya Kati,
  • 2:52 - 2:55
    Ulaya ya Kusini na kupitia Asia
  • 2:55 - 2:57
    njia yote mpaka Indonesia.
  • 2:57 - 3:00
    Hapo ndipo tunapata Waislamu wengi.
  • 3:00 - 3:05
    Na dini nyingi za Kikristo, tunaona kwenye
    hizi nchi. Ni za bluu.
  • 3:05 - 3:09
    Na hizo ni nchi nyingi za Marekani na
    Ulaya,
  • 3:09 - 3:12
    nchi nyingi za Afrika na chache za Asia.
  • 3:12 - 3:15
    Nyeupe hapa ni nchi ambazo haziwezi kuwa
    kuainishwa,
  • 3:15 - 3:18
    kwa sababu dini moja haifiki asilimia 50
  • 3:18 - 3:21
    au kuna shaka kuhusu takwimu au sababu
    yoyote nyingine.
  • 3:21 - 3:23
    Hivyo tulikua makini na hilo.
  • 3:23 - 3:27
    Hivyo vumilia urahisi wetu sasa
    nikiwapeleka kwenye hii picha.
  • 3:27 - 3:29
    Hii ni 1960.
  • 3:29 - 3:32
    Na sasa naonyesha idadi ya watoto kwa
    mwanamke hapa:
  • 3:32 - 3:35
    mbili, nne au sita --
  • 3:35 - 3:38
    watoto wengi, watoto wachache.
  • 3:38 - 3:41
    Na hapa mapato kwa mtu ikilinganishwa
    dola.
  • 3:41 - 3:44
    Sababu ya hio ni kua watu wengi wanasema
    unapaswa kua tajiri kwanza
  • 3:44 - 3:46
    kabla hujapata watoto wachache.
  • 3:46 - 3:50
    Hivyo mapato ya chini hapa, mapato ya juu
    pale.
  • 3:50 - 3:51
    Na kweli mwaka 1960,
  • 3:51 - 3:54
    ulitakiwa uwe Mkristo tajiri kuwa na
    watoto wachache.
  • 3:54 - 3:56
    Ilikua isipokua Japan.
  • 3:56 - 3:59
    Japan hapa ilionekana ya kipekee.
  • 3:59 - 4:02
    Vinginevyo ni nchi za Kikristo tu.
  • 4:02 - 4:04
    Lakini pia kulikua na nchi nyingi za
    Kikristo
  • 4:04 - 4:06
    zilizokua na watoto sita mpaka saba kwa
    mwanamke.
  • 4:06 - 4:12
    Lakini zilikua Amerika ya Kusini au
    zilikua Afrika.
  • 4:12 - 4:16
    Na nchi zenye Kiislamu kama dini kuu,
  • 4:16 - 4:21
    zote zilikua na karibia watoto sita mpaka
    saba kwa mwanamke,
  • 4:21 - 4:23
    bila kujali kiwango cha mapato.
  • 4:23 - 4:27
    Na dini zote za mashariki isipokua Japan
    zilikua na kiwango sawa.
  • 4:27 - 4:29
    Sasa tuone kilichotokea kwenye dunia.
  • 4:29 - 4:31
    Ninaanzisha dunia, na tunaenda hivi.
  • 4:31 - 4:34
    Sasa 1962 -- unaweza kuona wanakua
    tajiri zaidi,
  • 4:34 - 4:37
    lakini idadi ya watoto kwa mwanamke
    inashuka?
  • 4:37 - 4:39
    Angalia China. Wanashuka kwa haraka sana.
  • 4:39 - 4:44
    Na nchi zote zenye Wasilamu wengi katika
    mapato zinakuja chini,
  • 4:44 - 4:49
    kama nchi zenye Wakristo wengi kwenye eneo
    lenye mapato ya kati.
  • 4:49 - 4:51
    Na tunapoingia kwenye karne hii,
  • 4:51 - 4:55
    utakuta zaidi ya nusu ya watu huku chini.
  • 4:55 - 5:00
    Na ifikapo 2010, tuko kwa kweli asilimia
    80 ya watu
  • 5:00 - 5:04
    wanaoishi kwenye nchi zenye kama watoto
    wawili kwa mwanamke.
  • 5:04 - 5:08
    (Makofi)
  • 5:08 - 5:11
    Ni maendeleo ya kushangaza kabisa ambayo
    yametokea.
  • 5:11 - 5:13
    (Makofi)
  • 5:13 - 5:16
    Na hizi ni nchi za Marekani hapa,
  • 5:16 - 5:18
    zenye $40,000 kwa kila mtu,
  • 5:18 - 5:21
    Ufaransa, Urusi, Uajemi,
  • 5:21 - 5:25
    Mexico, Uturuki, Algeria,
  • 5:25 - 5:27
    Indonesia, India
  • 5:27 - 5:30
    na moja kwa moja mpaka Bangladesh na
    Vietnam,
  • 5:30 - 5:34
    ambazo zinazo chini ya asilimia tano ya
    mapato kwa mtu wa Marekani
  • 5:34 - 5:37
    na kiasi sawa cha watoto kwa mwanamke.
  • 5:37 - 5:40
    Naweza kukuambia kua takwimu ya idadi ya
    watoto kwa mwanamke
  • 5:40 - 5:42
    ina uzuri wa kushangaza nchi zote.
  • 5:42 - 5:44
    Tunapata hizo kutoka takwimu za sensa.
  • 5:44 - 5:48
    Sio moja ya hizi takwimu zilizo na
    mashaka sana.
  • 5:48 - 5:49
    Hivyo tunachohitimisha
  • 5:49 - 5:52
    ni hauhitaji kua tajiri kuwa na watoto
    wachache.
  • 5:52 - 5:54
    Imetokea katika dunia.
  • 5:54 - 5:57
    Na kisha tunapoangalia dini.
  • 5:57 - 5:59
    tunaona kua dini za mashariki,
  • 5:59 - 6:02
    kwa kweli hakuna nchi hata moja yenye
    wingi wa hio dini
  • 6:02 - 6:04
    ambayo ina zaidi ya watoto watatu.
  • 6:04 - 6:08
    Ambapo na Uislamu kama dini ya wingi na
    Ukristo,
  • 6:08 - 6:10
    unaona nchi njia yote.
  • 6:10 - 6:12
    Lakini hakuna tofauti kubwa.
  • 6:12 - 6:15
    Hakuna tofauti kubwa kati ya hizi dini.
  • 6:15 - 6:18
    Kuna tofauti kwenye mapato.
  • 6:18 - 6:22
    Nchi ambazo zina watoto wengi kwa mwanamke
    hapa,
  • 6:22 - 6:24
    zina mapato ya chini kweli.
  • 6:24 - 6:27
    Nyingi zao ziko Afrika kusini mwa Sahara.
  • 6:27 - 6:30
    Lakini pia kuna nchi huku
  • 6:30 - 6:34
    kama Guatemala, kama Papua New Guinea,
  • 6:34 - 6:37
    kama Yemen na Afghanistan.
  • 6:37 - 6:40
    Wengi hufikiri kua Afghanistan hapa
    na Kongo,
  • 6:40 - 6:44
    ambazo zimeteseka na migogoro mikali,
  • 6:44 - 6:47
    kua hazina ukuaji wa idadi ya watu wa
    haraka.
  • 6:47 - 6:48
    Ni kinyume chake.
  • 6:48 - 6:52
    Kwenye dunia leo, ni nchi zenye
    kiwango cha juu cha vifo
  • 6:52 - 6:55
    ambazo zina ukuaji wa haraka wa idadi ya
    watu.
  • 6:55 - 6:59
    Kwa sababu kifo cha mtoto kimefidiwa
    na mtoto mmoja zaidi.
  • 6:59 - 7:01
    Hizi nchi zina watoto sita kwa mwanake.
  • 7:01 - 7:06
    Zina kiwango cha vifo cha kusikitisha cha
    mtoto mmoja mpaka wawili kwa mwanamke.
  • 7:06 - 7:09
    Lakini miaka 30 kutoka sasa, Afghanistan
    inatoka milioni 30 mpaka milioni 60.
  • 7:09 - 7:13
    Kongo inaenda kutoka 60 mpaka 120.
  • 7:13 - 7:16
    Hapo ndipo tunapata ukuaji wa idadi ya
    watu.
  • 7:16 - 7:20
    Na wengi wanafikiri kua hizi nchi ziko
    palepale, lakini hazipo.
  • 7:20 - 7:24
    Ngoja nilinganishe Senegal, nchi
    iliotawaliwa na Waislamu,
  • 7:24 - 7:26
    na nchi iliotawaliwa na Wakristo, Ghana.
  • 7:26 - 7:30
    Nazipeleka nyuma hapa kwenye uhuru wao,
  • 7:30 - 7:33
    ambapo walikua huku juu mwanzoni mwa miaka
    ya 1960.
  • 7:33 - 7:35
    Angalia tu walichokifanya.
  • 7:35 - 7:37
    Ni maendeleo ya kushangaza,
  • 7:37 - 7:39
    kutoka watoto saba kwa mwanake,
  • 7:39 - 7:42
    wameenda moja kwa moja chini mpaka
    wanne na watano.
  • 7:42 - 7:44
    Ni maendeleo makubwa.
  • 7:44 - 7:45
    Hivyo inachukua nini?
  • 7:45 - 7:49
    Basi tunajua vizuri kabisa
    kinachohitajika kwenye hizi nchi.
  • 7:49 - 7:51
    Unahitaji kua na watoto kuishi.
  • 7:51 - 7:54
    Unahitaji kutoka nje ya umasikini
    uliokithiri
  • 7:54 - 7:58
    hivyo watoto sio wa muhimu kwa kazi kwenye
    familia.
  • 7:58 - 8:00
    Unahitaji kua na upatikanaji wa baadhi ya
    uzazi wa mpango.
  • 8:00 - 8:05
    Na unahitaji sababu ya nne, ambayo pengine
    ni sababu muhimu kuliko zote.
  • 8:05 - 8:08
    Lakini ngoja nionyeshe hio sababu ya nne
  • 8:08 - 8:10
    kwa kuangalia Qatar.
  • 8:10 - 8:14
    Hapa tuna Qatar leo, na pale tuna
    Bangladesh leo.
  • 8:14 - 8:17
    Kama nikizipeleka hizi nchi nyuma kwenye
    miaka ya uhuru wao,
  • 8:17 - 8:20
    ambazo ni karibia mwaka mmoja
    -- '71, '72 --
  • 8:20 - 8:24
    ni maendeleo ya kushangaza kabisa ambayo
    yalitokea.
  • 8:24 - 8:26
    Angalia Bangladesh na Qatar.
  • 8:26 - 8:29
    Zenye mapato yanayotofautiana kabisa, ni
    karibia muanguko sawa
  • 8:29 - 8:31
    kwenye idadi ya watoto kwa mwanamke.
  • 8:31 - 8:33
    Na nini sababu ya Qatar?
  • 8:33 - 8:35
    Basi kama kawaida yangu.
  • 8:35 - 8:39
    Nilienda kwenye mamlaka ya takwimu ya
    Qatar, kwenye tovuti yao --
  • 8:39 - 8:41
    Ni tovuti nzuri sana. Ninaipendekeza --
  • 8:41 - 8:47
    na nikaangalia juu -- ndio, ni burudani
    nyingi hapa --
  • 8:47 - 8:51
    na zinatolewa bure, nilikuta mwenendo
    wa kijamii wa Qatar.
  • 8:51 - 8:54
    Ya kuvutia sana. Vingi vya kusoma.
  • 8:54 - 8:58
    Nilikuta nguvu ya uzazi, na nikaangalia
    jumla ya kiwango cha uzazi kwa mwanamke.
  • 8:58 - 9:02
    Hawa ni wasomi na wataalamu kwenye wakala
    wa serikali wa Qatar,
  • 9:02 - 9:05
    na wakasema sababu za muhimu zaidi ni:
  • 9:05 - 9:06
    "Ongezeko la umri kwenye ndoa ya kwanza,
  • 9:06 - 9:10
    ongezeko la kiwango cha elimu cha mwanamke
    wa Qatar
  • 9:10 - 9:13
    na wanawake zaidi kujumuika kwenye
    nguvukazi."
  • 9:13 - 9:17
    Nisingekubali zaidi. Sayansi isingekubali
    zaidi.
  • 9:17 - 9:19
    Hii ni nchi ambayo kweli imepitia
  • 9:19 - 9:23
    utamaduni wa kushangaza sana sana.
  • 9:23 - 9:25
    Hivyo kilichopo, ni hizi nne:
  • 9:25 - 9:28
    Watoto wanatakiwa waishi, watoto
    hawatakiwi kuhitajika kwa kazi,
  • 9:28 - 9:31
    wanawake wanatakiwa kupata elimu na
    kujiunga na nguvukazi
  • 9:31 - 9:33
    na uzazi wa mpango unatakiwa kupatikana.
  • 9:33 - 9:37
    Sasa angalia tena hii.
  • 9:37 - 9:39
    Wastani ya idadi ya watoto duniani
  • 9:39 - 9:43
    ni kama ya Colombia -- ni 2.4 leo.
  • 9:43 - 9:46
    Kuna nchi huku juu amabazo ni maskini
    sana.
  • 9:46 - 9:50
    Na ndipo uzazi wa mpango, maisha bora ya
    watoto zinahitajika.
  • 9:50 - 9:53
    Nina pendekeza kwa nguvu mazungumzo ya
    TED ya mwisho ya Melinda Gates.
  • 9:53 - 9:59
    Na hapa, chini, kuna nchi nyingi ambazo
    zina chini ya watoto wawili kwa mwanamke.
  • 9:59 - 10:02
    Hivyo nikirudi sasa kuwapa jibu la
    jaribio,
  • 10:02 - 10:04
    ni mbili.
  • 10:04 - 10:07
    Tumefikia kilele mtoto.
  • 10:07 - 10:09
    Idadi ya watoto haikui tena zaidi duniani.
  • 10:09 - 10:11
    Bado tunajadili kilele mafuta,
  • 10:11 - 10:14
    lakini ni dhahiri tumefika kilele mtoto.
  • 10:14 - 10:17
    Idadi ya watu duniani itaacha kukua.
  • 10:17 - 10:19
    Umoja wa Mataifa kitengo cha Wakazi
    kilisema
  • 10:19 - 10:22
    kitaacha kukua kwenye bilioni 10.
  • 10:22 - 10:26
    Lakini kwanini tunaongezeka kama idadi ya
    watoto haiongezeki?
  • 10:26 - 10:28
    Basi nitawaonyesha hapa.
  • 10:28 - 10:32
    Nitatumia hizi sanduku za kadi ambazo
    madaftari yenu yalikuja.
  • 10:32 - 10:36
    Ni muhimu sana kwa madhumuni ya elimu.
  • 10:36 - 10:39
    Kila kisanduku ni watu bilioni moja.
  • 10:39 - 10:41
    Na kuna watoto bilioni mbili duniani.
  • 10:41 - 10:48
    Kuna vijana bilioni mbili kati ya 15
    na 30.
  • 10:48 - 10:50
    Hizi ni namba zilizokadiriwa.
  • 10:50 - 10:55
    Halafu kuna bilioni moja kati ya 30 na 45,
  • 10:55 - 10:58
    karibia moja kati ya 45 na 60.
  • 10:58 - 11:00
    na tena kuna sanduku langu.
  • 11:00 - 11:02
    Huyu ni mimi: 60-na zaidi.
  • 11:02 - 11:04
    Tupo hapa juu.
  • 11:04 - 11:10
    Hivyo kitakachotokea sasa hivi ni
    tunachoita "ujazo mkubwa."
  • 11:10 - 11:13
    Utaona kua kuna kama bilioni tatu
    inayokosekana hapa.
  • 11:13 - 11:17
    Haionekani kwa sababu wamekufa; hawakuwahi
    kuzaliwa.
  • 11:17 - 11:21
    Kwa sababu kabla ya 1980, kulikua na watu
    wachache zaidi waliozaliwa
  • 11:21 - 11:24
    kuliko waliopo wakati wa miaka 30
    iliopita.
  • 11:24 - 11:27
    Hivyo kitakachotokea sasa ni wazi sana.
  • 11:27 - 11:30
    Wazee, kwa sikitiko, tutakufa.
  • 11:30 - 11:34
    Nyie wengine, mtakua wakubwa na mtapata
    watoto bilioni mbili.
  • 11:34 - 11:37
    Kisha wazee watakufa.
  • 11:37 - 11:41
    Wengine watakua wakubwa na kupata watoto
    bilioni mbili.
  • 11:41 - 11:47
    Na tena wazee watakufa na mtapata watoto
    bilioni mbili.
  • 11:47 - 11:49
    (Makofi)
  • 11:49 - 11:53
    Hii ni ujazo mkubwa.
  • 11:53 - 11:55
    Haiepukiki.
  • 11:55 - 11:58
    Na unaona kua hili ongezeko lilitokea
  • 11:58 - 12:03
    bila maisha kua marefu na bila kuongeza
    watoto?
  • 12:03 - 12:08
    Dini inahusika kidogo sana kwenye idadi ya
    watoto kwa mwanamke.
  • 12:08 - 12:11
    Dini zote duniani zina uwezo wa kikamilifu
  • 12:11 - 12:16
    kudumisha thamani zao na kukabiliana
    na hii dunia mpya.
  • 12:16 - 12:21
    Na tutakua tu bilioni 10 kwenye dunia hii,
  • 12:21 - 12:25
    kama watu maskini watatoka kwenye
    umaskini,
  • 12:25 - 12:28
    watoto wao wataishi, watakua na
    upatikanaji wa uzazi wa mpango.
  • 12:28 - 12:30
    Hio inahitajika.
  • 12:30 - 12:36
    Lakini haiepukiki kua tutakua bilioni
    mbili mpaka tatu zaidi.
  • 12:36 - 12:39
    Hivyo unavyojadili na unavyopanga
  • 12:39 - 12:42
    kwa rasilimali na nishati zinazohitajika
    baadae,
  • 12:42 - 12:45
    kwa wanadamu kwenye hii sayari,
  • 12:45 - 12:47
    unatakiwa upange kwa bilioni 10
  • 12:47 - 12:49
    Asante sana.
  • 12:49 - 12:55
    (Makofi)
Title:
Dini na watoto
Speaker:
Hans Rosling
Description:

Hans Rosling alikua na swali: Kuna baadhi ya dini zenye kiwango cha juu cha uzazu zaidi ya nyingine -- na jinsi gani hii ina athiri ongezeko la idadi ya watu duniani? Akiongea kwenye TEDxSummit huko Doha, Qatar, alionyesha jedwali la takwimu kwa mda na katika dini. Akiwa na ishara yake ya ucheshi na ufahamu wa makini, Hans alifikia hatima ya kushangaza juu ya viwango vya uzazi duniani.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
13:20
Nelson Simfukwe approved Swahili subtitles for Religions and babies
Nelson Simfukwe accepted Swahili subtitles for Religions and babies
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for Religions and babies
Doris Mangalu edited Swahili subtitles for Religions and babies
Doris Mangalu edited Swahili subtitles for Religions and babies
Doris Mangalu edited Swahili subtitles for Religions and babies
Doris Mangalu edited Swahili subtitles for Religions and babies
Doris Mangalu edited Swahili subtitles for Religions and babies
Show all

Swahili subtitles

Revisions