< Return to Video

Mgogoro wa wakimbizi ni kipimo cha utu wetu

  • 0:00 - 0:04
    Ninaenda kuongea nanyi kuhusu janga la kidunia la wakimbizi
  • 0:04 - 0:08
    na lengo langu ni kuwaonyesha kwamba janga hili
  • 0:08 - 0:11
    Linaweza kusimamiwa, halishindikani kutatuliwa,
  • 0:12 - 0:17
    lakini pia kuwaonyesha kwamba hili jambo ni zaidi kuhusu sisi na vile tulivyo
  • 0:17 - 0:21
    kama lilivyo ni jaribu kwa wakimbizi waliopo mstari wa mbele.
  • 0:21 - 0:24
    Kwangu mimi, hili sio jukumu la kikazi tu,
  • 0:24 - 0:29
    kwa vile ninaendesha taasisi isiyo ya kiserikali inayoshughululika na wakimbuzi duniani kote.
  • 0:29 - 0:30
    nachukulia kama jukumu la kibinafsi.
  • 0:31 - 0:33
    Naipenda picha hii.
  • 0:34 - 0:36
    Yule kijana mtanashati sana upande wa kulia,
  • 0:36 - 0:37
    yule sio mimi.
  • 0:38 - 0:41
    Ni baba yangu, Ralph, akiwa London, mwaka 1940
  • 0:41 - 0:43
    akiwa na baba yake Samwel.
  • 0:44 - 0:46
    Walikuwa wakimbizi wa Kiyahudi tokea Ubelgiji.
  • 0:46 - 0:50
    Walikimbia siku ambazo Nazi wa Ujerumani walivamia.
  • 0:51 - 0:52
    Na naipenda picha hii, pia.
  • 0:53 - 0:55
    Ni kundi la watoto wakimbizi
  • 0:55 - 0:58
    walipowasili Uingereza mwaka 1946 kutokea Poland.
  • 0:59 - 1:02
    Na katikati ni mama yangu, Marion.
  • 1:03 - 1:06
    Alitumwa kwenda kuanza maisha mapya
  • 1:06 - 1:07
    katika nchi mpya
  • 1:07 - 1:08
    yeye mwenyewe
  • 1:08 - 1:10
    akiwa na miaka 12.
  • 1:11 - 1:13
    Najua hili;
  • 1:13 - 1:16
    Kama Waingereza wasingeruhusu wakimbizi
  • 1:16 - 1:17
    mwaka 1940,
  • 1:18 - 1:21
    Nina uhakika nisingekuwa hapa leo.
  • 1:22 - 1:26
    Bado katika miaka 70, gurudumu limezunguka kuwa kamili.
  • 1:27 - 1:30
    Sauti za kuta ambazo zimejengwa,
  • 1:30 - 1:32
    siasa za visasi,
  • 1:32 - 1:36
    thamani ya ubinadamu na misingi katika moto
  • 1:37 - 1:41
    katika nchi ambazo miaka 70 iliyopita zilisema hakuna tena kamwe
  • 1:41 - 1:45
    wataokuwa bila mataifa na matumaini ambao ni wahanga wa vita.
  • 1:47 - 1:49
    Mwaka uliopita, kila dakika,
  • 1:50 - 1:54
    zaidi ya watu 24 walikuwa wakiondolewa kutoka majumbani mwao
  • 1:54 - 1:56
    kwa mafarakano, machafuko na unyanyapaa wa kibaguzi:
  • 1:57 - 2:00
    shambulio lingine la silaha za kemikali nchini Syria,
  • 2:00 - 2:03
    Watalibani na machafuko nchini Afghanistan,
  • 2:03 - 2:09
    wasichana waliotekwa na Boko Haram wakiwa shule Kaskazini- Mashariki mwa Nigeria.
  • 2:10 - 2:13
    Hawa sio watu ambao wanahamia nchi nyingine
  • 2:13 - 2:15
    kupata maisha bora.
  • 2:15 - 2:17
    Wanahama kwa kuokoa maisha yao.
  • 2:19 - 2:20
    Ni jambo la kuhuzunisha mno
  • 2:22 - 2:27
    kwamba mkimbizi maarufu duniani hawezi kuja kuongea hapa leo hii.
  • 2:27 - 2:29
    Wengi wenu mtaitambua picha hii.
  • 2:30 - 2:32
    Inaonyesha mwili usio na maisha
  • 2:32 - 2:35
    mwa mvulana wa miaka mitano aitwaye Alan Kurdi,
  • 2:35 - 2:39
    mkimbizi wa Syria aliyefariki Mediterenian mwaka 2015.
  • 2:39 - 2:43
    Alifariki na wengine 3700 wakati wakijaribu kuingia Ulaya.
  • 2:44 - 2:46
    Mwaka uliofata, 2016,
  • 2:47 - 2:49
    Watu 5000 walifariki.
  • 2:51 - 2:52
    Walikuwa wamechelewa mno,
  • 2:53 - 2:56
    lakini ni mapema kwa wengine mamilioni.
  • 2:56 - 2:58
    Bado ni mapema kwa watu kama Frederick.
  • 2:59 - 3:02
    Nilikutana nae katika kambi ya wakimbizi inayofahamika kama Nyarugusu nchini Tanzania.
  • 3:02 - 3:03
    Anatokea Burundi.
  • 3:04 - 3:06
    Alitaka kujua ni wapi angeweza kumaliza masomo yake.
  • 3:06 - 3:09
    Amesoma madarasa 11, na alitaka malizia mwaka wa 12.
  • 3:09 - 3:14
    Aliniambia, "Ninaomba kwa Mungu siku zangu zisiiishie hapa
  • 3:14 - 3:15
    katika kambi hii ya wakimbizi."
  • 3:16 - 3:18
    Na bado ni mapema kwa Halud.
  • 3:19 - 3:22
    Wazazi wake walikuwa ni wakimbizi wa Kipalestina
  • 3:22 - 3:25
    wanaoishi katika kambi ya Yarmouk nje ya mji mkuu wa Damascus.
  • 3:25 - 3:27
    Alizaliwa wazazi wakimbizi,
  • 3:27 - 3:30
    na sasa ni mkimbizi akiwa peke yake nchini Lebanon.
  • 3:31 - 3:34
    Anafanya kazi katika kamati ya kimataifa ya kusaidia wakimbizi wengine,
  • 3:35 - 3:38
    lakini hana uhakika wowote
  • 3:38 - 3:40
    kuhusu maisha yake ya baadaye,
  • 3:40 - 3:42
    yapo wapi na yana ahadi gani.
  • 3:42 - 3:46
    Hotuba hii ni kuhusu Frederick, na kuhusu Halud
  • 3:46 - 3:48
    na kuhusu mamilioni ya wengine;
  • 3:48 - 3:50
    na walikuwa wameondolewa,
  • 3:50 - 3:55
    wanaishi vipi, msaada gani wanahitaji na majukumu yetu ni yapi.
  • 3:56 - 3:57
    Ninaamini katika hili,
  • 3:58 - 4:01
    kwamba swali kubwa katika karne ya 21
  • 4:02 - 4:05
    linahusu majukumu yetu kwa watu tusiowafahamu.
  • 4:05 - 4:09
    Kesho yako inahusu majukumu yako
  • 4:09 - 4:10
    kwa usiowafahamu.
  • 4:10 - 4:12
    Unajua vyema kuliko mwingine yoyote,
  • 4:12 - 4:16
    dunia imeunganishwa kirahisi sana kuliko miaka ya nyuma,
  • 4:17 - 4:18
    lakini hatari kubwa
  • 4:18 - 4:21
    ni kwamba tunatumia muda mwingi katika utengano wetu.
  • 4:22 - 4:24
    Na hakuna jaribio bora kwa hilo
  • 4:24 - 4:26
    kuliko jinsi tunavyowajali wakimbizi.
  • 4:27 - 4:30
    Huu ni ukweli: watu milioni 65
  • 4:30 - 4:33
    waliondolewa kutoka majumbani mwao kwa machafuko mwaka uliopita.
  • 4:33 - 4:35
    Kama ingekuwa ni nchi,
  • 4:35 - 4:38
    ingekuwa ni nchi kubwa kuliko zote duniani katika karne ya 21.
  • 4:39 - 4:44
    Wengi ya hawa watu, takribani milioni 40, wanaishi katika nchi zao,
  • 4:44 - 4:45
    lakini milioni 25 ni wakimbizi.
  • 4:45 - 4:48
    Hii inamaanisha wanavuka mpaka kwenda nchi jirani.
  • 4:49 - 4:53
    Wengi wao wanaishi katika nchi masikini,
  • 4:53 - 4:56
    nchi za umasikini wa ulinganifu au zilizo na kipato cha chini cha kati, kama Lebanon,
  • 4:56 - 4:57
    ambapo Halud anaishi.
  • 4:59 - 5:03
    Nchini Lebanon, mtu mmoja kati ya wanne ni mkimbizi,
  • 5:04 - 5:07
    robo ya watu wote.
  • 5:07 - 5:09
    Na wakimbizi hukaa kwa muda mrefu.
  • 5:09 - 5:11
    Muda wa wastani wa kukimbia
  • 5:11 - 5:12
    ni miaka kumi.
  • 5:13 - 5:18
    Nilikwenda katika kambi kubwa ya wakimbizi duniani, mashariki ya Kenya.
  • 5:18 - 5:19
    Inafahamika kama Dadaab.
  • 5:19 - 5:21
    Ilijengwa kati mwaka 1991 hadi 92
  • 5:21 - 5:25
    kama kambi ya muda kwa Wasomali waliokimbia kutokana na vita ya kisiasa.
  • 5:26 - 5:27
    Nilikutana na Silo.
  • 5:28 - 5:31
    Na nikajisemea kwa Silo,
  • 5:31 - 5:33
    "Unadhani utaweza kurudi nyumbani Somalia?"
  • 5:34 - 5:36
    Na alisema, "Unamaanisha nini, kurudi nyumbani?
  • 5:36 - 5:38
    Nimezaliwa hapa."
  • 5:39 - 5:41
    Na kisha nilipouliza utawala wa kambi ile
  • 5:41 - 5:45
    ni wangapi kati ya watu 330,000 walizaliwa palepale kambini,
  • 5:45 - 5:46
    Walinipa jibu;
  • 5:47 - 5:49
    100,000
  • 5:50 - 5:52
    Hii ndiyo maana ya ukimbizi wa muda mrefu.
  • 5:53 - 5:56
    Sasa, chanzo cha haya matatizo kina kina kirefu;
  • 5:56 - 5:58
    mataifa dhaifu ambayo hayawezi kujali watu wao,
  • 5:59 - 6:01
    mfumo wa kimataifa wa siasa
  • 6:01 - 6:04
    dhaifu kuliko muda wowote kuanzia 1945
  • 6:04 - 6:08
    na tofauti za imani za kidini, utawala, mahusiano na dunia ya nje
  • 6:08 - 6:11
    katika sehemu muhimu ya dunia ya Kiislamu
  • 6:13 - 6:16
    Sasa, hizi ni changamoto za vizazi ambazo ni za muda mrefu.
  • 6:16 - 6:19
    Ndiyo maana ninasema hili janga la wakimbizi ni jambo ambalo ni muendelezo na sio la kushtukiza.
  • 6:20 - 6:25
    Ni tata, na pale unapokuwa na matatizo ambayo ni makubwa, ya muda mrefu,
  • 6:25 - 6:27
    watu hufikiri hamna jambo linaloweza fanyika.
  • 6:28 - 6:30
    Wakati Papa Francis alipokwenda Lampedusa,
  • 6:31 - 6:33
    katika pwani za Italia, mwaka 2014,
  • 6:33 - 6:36
    alitushutumu sisi sote na dunia nzima
  • 6:36 - 6:40
    ambapo aliita ni dunia ya "utandawazi wa wasiojali."
  • 6:41 - 6:42
    Ni msemo ambao upo nasi mara zote.
  • 6:42 - 6:45
    Ina maana kwamba mioyo yetu imegeuka kuwa ya mawe.
  • 6:47 - 6:48
    Sasa, sifahamu, uniambie.
  • 6:48 - 6:52
    Unatakiwa kulumbana na Papa, hata katika mkutano wa TED?
  • 6:53 - 6:54
    Lakini nafikiri si sahihi.
  • 6:54 - 6:56
    Nadhani watu wanataka kufanya mabadiliko,
  • 6:56 - 7:00
    lakini hawajui kama kuna utatuzi wowote wa hili janga.
  • 7:00 - 7:02
    Na ninachotaka kuwaambia leo
  • 7:02 - 7:05
    Ni kwamba ingawa matatizo ni makubwa, na ufumbuzi wake ni mkubwa pia
  • 7:06 - 7:07
    Ufumbuzi wa kwanza:
  • 7:07 - 7:11
    wakimbizi hawa wanatakiwa wajishughulishe katika nchi wanazoishi.
  • 7:11 - 7:14
    na nchi ambazo wanaishi zinatakiwa kupewa msaada mkubwa wa kiuchumi.
  • 7:14 - 7:16
    Mwaka 2014 nchini Uganda, walifanya utafiti:
  • 7:17 - 7:20
    Asilimia 80 ya wakimbizi katika mji mkuu wa Kampala
  • 7:20 - 7:22
    hawakuhitaji msaada wa kibinadamu kwa sababu walikuwa wakifanya kazi.
  • 7:22 - 7:24
    Walikuwa wakisaidiwa katika kazi.
  • 7:24 - 7:26
    Ufumbuzi namba mbili:
  • 7:26 - 7:30
    elimu kwa watoto ni msingi wa maisha, sio starehe,
  • 7:30 - 7:32
    Unapokuwa umekimbia kwa muda mrefu.
  • 7:33 - 7:38
    Watoto wanaweza shindwa pale wanapopewa msaada sahihi wa kijamii na kihisia
  • 7:38 - 7:39
    pamoja na maarifa
  • 7:39 - 7:41
    Nimejionea mwenyewe.
  • 7:43 - 7:46
    Lakini nusu wa wakimbizi watoto duniani walio katika umri wa elimu ya msingi
  • 7:46 - 7:48
    hawapati elimu kabisa,
  • 7:48 - 7:51
    na robo tatu ya umri wa shule ya sekondari hawapati elimu kabisa.
  • 7:51 - 7:53
    Inachanganya akili sana!
  • 7:54 - 7:56
    Ufumbuzi namba tatu:
  • 7:56 - 8:00
    wakimbizi wengi wapo katika maeneo ya mijini, katika majiji, na sio katika makambi.
  • 8:00 - 8:02
    Ni kipi utachotaka au nitachotaka kama tungekuwa wakimbizi katika jiji?
  • 8:02 - 8:05
    Tungehitaji fedha kwa ajili ya kulipa kodi na kununua nguo.
  • 8:07 - 8:09
    Hiyo ni kesho ya mfumo wa kibinadamu,
  • 8:09 - 8:10
    au nyanja muhimu:
  • 8:10 - 8:13
    wape watu fedha ili uongeze nguvu ya wakimbizi
  • 8:13 - 8:15
    na utasaidia uchumi wa eneo husika.
  • 8:15 - 8:17
    Na kuna ufumbuzi wa nne, pia,
  • 8:17 - 8:20
    unatatiza lakini unatakiwa kuongelewa.
  • 8:20 - 8:23
    Wale wakimbizi ambao wapo katika mazingira hatarishi wanatakiwa kupewa mwanzo mpya
  • 8:23 - 8:25
    na maisha mapya katika nchi mpya,
  • 8:26 - 8:27
    ukijumuisha na nchi za Magharibi.
  • 8:28 - 8:32
    Takwimu ni ndogo sana ukilinganisha, mamia ya maelfu, na sio mamilioni,
  • 8:32 - 8:35
    lakini ubaguzi ni mkubwa.
  • 8:36 - 8:39
    Sasa sio muda wa kukataa wakimbizi,
  • 8:39 - 8:40
    kama vile utawala wa Trump unavyohimiza.
  • 8:40 - 8:44
    Ni muda wa kuwapa msaada wale ambao ni wahanga wa machafuko.
  • 8:44 - 8:45
    Na kumbuka --
  • 8:45 - 8:48
    (Makofi)
  • 8:52 - 8:56
    Kumbuka, kila anayekuuliza, "Wamechunguzwa vyema?"
  • 8:56 - 8:59
    hilo ni swali muhimu mno kuuliza.
  • 9:00 - 9:04
    Ukweli ni kwamba, wakimbizi wanaowasili kutokana na machafuko
  • 9:04 - 9:08
    huchunguzwa kuliko wakimbizi wengine wote wanaoingia katika nchi.
  • 9:08 - 9:10
    Kwa hiyo pale ambapo ina maana kuuliza swali,
  • 9:10 - 9:14
    si sahihi kusema kwamba mkimbizi ni neno lingine linalomaanisha gaidi.
  • 9:15 - 9:16
    Sasa, kipi kinatokea --
  • 9:16 - 9:20
    (Makofi)
  • 9:20 - 9:23
    Kipi kinatokea kama wakimbizi hawawezi kupata kazi,
  • 9:23 - 9:25
    hawawezi peleka watoto wao shuleni,
  • 9:25 - 9:28
    hawawezi kupata fedha, hawawezi kupata njia halali ya matumaini?
  • 9:28 - 9:30
    Kinachotokea ni kwamba wanaamua kufanya njia hatarishi.
  • 9:30 - 9:35
    Nilikwenda Lesbos, kisiwa kizuri kilichopo Ugiriki, miaka miwili iliyopita.
  • 9:35 - 9:37
    Kina wakazi 90,000.
  • 9:37 - 9:41
    Katika mwaka mmoja, wakimbizi 500,000 walikwenda katika kisiwa hiki.
  • 9:41 - 9:43
    Na ninataka kuwaonyesha nilichoshuhudia
  • 9:43 - 9:46
    Nilipokuwa nikiendesha kuelekea kaskazini ya kisiwa:
  • 9:46 - 9:50
    mrundikano wa makoti ya kuokoa maisha ya wale waliofankiwa kufika katika kile kisiwa.
  • 9:51 - 9:52
    Na nilipoangalia kwa ukaribu,
  • 9:52 - 9:55
    kulikuwa na makoti madogo ya kuokoa maisha ya watoto,
  • 9:55 - 9:56
    ya rangi ya njano.
  • 9:56 - 9:58
    Na nikachukua picha hii.
  • 9:58 - 10:02
    Huwezi kuona maandishi, lakini nataka nikusomee.
  • 10:02 - 10:05
    "Ilani: haitakukinga na dhidi za kuzama."
  • 10:06 - 10:07
    Katika katika karne ya 21,
  • 10:08 - 10:11
    watoto wanapewa makoti ya kuokoa maisha
  • 10:11 - 10:13
    ili kufika salama Ulaya
  • 10:13 - 10:16
    hata kama yale makoti hayawezi kuokoa maisha yao
  • 10:16 - 10:19
    kama wataanguka kutoka katika mtumbwi ambao unawavusha.
  • 10:21 - 10:24
    Hili sio janga, ni jaribio.
  • 10:26 - 10:29
    Ni jaribio kwamba ustaarabu unaangalia chini.
  • 10:30 - 10:31
    Ni jaribio la ubinadamu wetu.
  • 10:32 - 10:34
    Ni jaribio la sisi tuliopo dunia ya Magharibi
  • 10:34 - 10:37
    ya jinsi tulivyo na msimamo wetu.
  • 10:39 - 10:42
    Ni jaribio la tabia zetu, sio sera zetu.
  • 10:43 - 10:45
    Na wakimbizi ni kesi ngumu.
  • 10:45 - 10:47
    Wanatokea mbali katika pande za dunia.
  • 10:48 - 10:50
    Wamepitia magumu.
  • 10:50 - 10:52
    Wengi wao ni wa dini tofauti.
  • 10:52 - 10:55
    Hizi ni sababu sahihi ambazo zinatupasa kuwasaidia wakimbizi,
  • 10:55 - 10:57
    na sio sababu za kutowasaidia.
  • 10:57 - 11:01
    Na ni sababu ya kuwasaidia kwa sababu ya vile inavyosema kuhusu sisi.
  • 11:02 - 11:04
    Inaonyesha thamani yetu.
  • 11:05 - 11:10
    Uelewa na kujali ni misingi miwili ya ustaarabu.
  • 11:11 - 11:14
    Badili uelewa na kujali katika vitendo
  • 11:14 - 11:16
    na tutaishi katika mila ya kistaarabu.
  • 11:17 - 11:19
    Na katika dunia ya sasa, hatuwezi toa sababu.
  • 11:19 - 11:23
    Hatuwezi sema hatufahamu kinachotokea Juba, Sudani Kusini
  • 11:23 - 11:25
    au Aleppo, Syria.
  • 11:25 - 11:28
    Kipo hapa, katika simujanja zetu
  • 11:28 - 11:29
    zilizopo mikononi mwetu.
  • 11:29 - 11:32
    Ukosefu wa maarifa sio sababu kabisa.
  • 11:32 - 11:36
    Kushindwa kusaidia, tutaonyesha hatuna dira ya ustaarabu kabisa.
  • 11:37 - 11:40
    Na pia inaonyesha kuhusu pengine kama tunatambua historia yetu.
  • 11:41 - 11:43
    Sababu ya kwamba wakimbizi wana haki duniani kote.
  • 11:43 - 11:46
    ni kwa sababu ya uongozi usio wa kawaida ya Magharibi
  • 11:46 - 11:49
    wa viongozi wake kwa waume baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia
  • 11:49 - 11:51
    ikaja kuwa haki ya wote.
  • 11:52 - 11:55
    Ukitupa jalalani ulinzi wa wakimbizi, unatupa historia yetu pia.
  • 11:56 - 11:58
    Hii ni --
  • 11:58 - 11:59
    (Makofi)
  • 11:59 - 12:03
    Hii inadhihirisha nguvu ya demokrasia
  • 12:03 - 12:06
    kama kimbilio kutokana na udikteta.
  • 12:06 - 12:08
    Ni wanasiasa wangapi umewahi kuwasikia wakisema,
  • 12:09 - 12:13
    "Tunaamini katika nguvu ya mifano yetu, na sio mifano ya nguvu yetu."
  • 12:14 - 12:17
    Wanachomaanisha ndicho tunachoamini ni muhimu sana kuliko mabomu tunayodondosha.
  • 12:18 - 12:20
    Wakimbizi wanaotafuta utakatifu
  • 12:21 - 12:25
    wameona Magharibi ndiyo chanzo cha matumaini na bandari salama.
  • 12:27 - 12:29
    Warusi, Wairan,
  • 12:29 - 12:32
    Wachina, Waeritrea, Wakyuba,
  • 12:32 - 12:34
    wamekuja magharibi kwa ajili ya usalama.
  • 12:35 - 12:37
    Hatujali ili kuepuka maafa.
  • 12:38 - 12:40
    Na kuna kitu kimoja kingine kinachodhihirisha kuhusu sisi:
  • 12:40 - 12:43
    kama tuna unyenyekevu wowote kutokana na makosa yetu.
  • 12:43 - 12:45
    Mimi sio mmoja ya watu hawa
  • 12:45 - 12:49
    ambae naamini kwamba matatizo yote ya dunia yanasababishwa na nchi za Magharibi.
  • 12:49 - 12:50
    Hapana.
  • 12:50 - 12:52
    Lakini tunapofanya makosa, lazima tuyatambue.
  • 12:53 - 12:55
    Sio ajali kwamba nchi ambayo imechukua
  • 12:55 - 12:58
    wakimbizi wengi zaidi kuliko nchi nyingine, Marekani,
  • 12:58 - 13:01
    imechukua wakimbizi wengi zaidi kutoka Vietnam kuliko nchi yoyote ile.
  • 13:02 - 13:03
    Inaongea katika historia.
  • 13:04 - 13:07
    Lakini kuna historia ya hivi karibuni, nchini Iraq na Afghanistan.
  • 13:08 - 13:11
    Huwezi rekebisha makosa ya siasa za nje
  • 13:11 - 13:13
    kwa kutumia hatua za kibinadamu,
  • 13:13 - 13:17
    lakini unapovunja kitu fulani, una jukumu la kusaidia katika kujaribu kukiunga tena,
  • 13:17 - 13:19
    na ni jukumu letu sasa.
  • 13:22 - 13:24
    Unakumbuka mwanzo wa hii hotuba yangu,
  • 13:24 - 13:26
    Nilisema nataka kueleza kwamba janga la wakimbizi
  • 13:26 - 13:28
    linaweza kusimamiwa, na sio lisiloshindikana?
  • 13:29 - 13:32
    Ni ukweli, Nataka muwaze katika namna mpya,
  • 13:32 - 13:34
    lakini pia nataka mfanye vitu.
  • 13:36 - 13:38
    Kama wewe ni mwajiri,
  • 13:38 - 13:39
    ajiri mkimbizi.
  • 13:40 - 13:43
    Kama unapitishwa katika malumbano,
  • 13:43 - 13:45
    waza mambo ya nyuma
  • 13:45 - 13:47
    pale familia au marafiki au wafanyakazi wenzio wanaporudia.
  • 13:48 - 13:51
    Kama una hela, toa kama msaada
  • 13:51 - 13:53
    inaleta utofauti kwa wakimbizi wote duniani.
  • 13:54 - 13:55
    Kama wewe ni mwananchi,
  • 13:56 - 13:58
    mpigie kura mwanasiasa
  • 13:58 - 14:02
    ambaye atafanyia kazi utatuzi wa haya niliyoongelea.
  • 14:02 - 14:06
    (Makofi)
  • 14:06 - 14:08
    Jukumu la asiyejulikana
  • 14:08 - 14:10
    hujionyesha
  • 14:10 - 14:13
    katika njia ndogo na kubwa,
  • 14:13 - 14:15
    kawaida na kishujaa.
  • 14:16 - 14:17
    Mwaka 1942,
  • 14:19 - 14:21
    shangazi yangu na bibi yangu walikuwa wakiishi Brussels
  • 14:21 - 14:22
    chini ya utawala wa Ujerumani.
  • 14:24 - 14:26
    Walipokea wito
  • 14:26 - 14:30
    kutoka katika mamlaka ya Nazi, kwenda katika stesheni ya reli ya Brussels.
  • 14:32 - 14:35
    Bibi yangu mara moja alitambua kwamba kuna kitu hakipo.
  • 14:37 - 14:39
    Aliwasihi ndugu zake
  • 14:39 - 14:41
    wasiende stesheni ya reli ya Brussels.
  • 14:42 - 14:44
    Ndugu zake walimwambia,
  • 14:45 - 14:48
    "Kama hatutakwenda, kama hatutafanya tulichoambiwa,
  • 14:48 - 14:50
    tutakuwa katika hatari kubwa."
  • 14:51 - 14:53
    Unaweza tabiri nini kilitokea
  • 14:53 - 14:55
    kwa wale ndugu waliokwenda stesheni ya reli ya Brussels.
  • 14:56 - 14:57
    Hawakuonekana tena.
  • 14:58 - 15:00
    Lakini bibi yangu na shangazi yangu,
  • 15:01 - 15:03
    walikwenda katika kijiji kidogo
  • 15:03 - 15:05
    kusini mwa Brussels
  • 15:06 - 15:09
    ambapo walishawahi kwenda likizo muongo mmoja uliopita,
  • 15:09 - 15:13
    na walifikia katika nyumba ya mwanakijiji ambaye ni mkulima,
  • 15:13 - 15:15
    wa Kikatoliki aliyeitwa Monsieur Maurice,
  • 15:16 - 15:18
    na waliomba kuishi pale.
  • 15:19 - 15:21
    na aliwakubalia,
  • 15:21 - 15:22
    na baada ya vita kuisha,
  • 15:23 - 15:27
    Wayahudi 17, niliambiwa, walikuwa wakiishi katika kijiji kile.
  • 15:28 - 15:30
    Na nilipokuwa kijana, nilimuuliza shangazi yangu,
  • 15:30 - 15:32
    "Unaweza nipeleka nikamuone Monsieur Maurice?"
  • 15:33 - 15:37
    Na alisema, "Ndiyo, ninaweza. Bado yupo hai. Twende ukamuone."
  • 15:37 - 15:38
    Hivyo, ilikuwa ni mwaka '83,'84
  • 15:39 - 15:41
    tulikwenda kumuona.
  • 15:41 - 15:44
    Na tuseme, kama kijana tu ningeweza,
  • 15:44 - 15:45
    pale nilipoonana nae,
  • 15:45 - 15:48
    alikuwa ni mwanaume mstaarabu aliye na mvi,
  • 15:48 - 15:50
    Nikamwambia,
  • 15:51 - 15:52
    "Kwanini ulifanya vile?
  • 15:53 - 15:56
    Kwanini ulikubali kuingia katika hatari?"
  • 15:57 - 15:59
    Aliniangalia
  • 15:59 - 16:01
    na akasema, katika lugha ya Kifaransa,
  • 16:01 - 16:03
    "On doit."
  • 16:03 - 16:04
    ikimaanisha "Yatupasa."
  • 16:04 - 16:07
    Ilikuwa ndani yake.
  • 16:07 - 16:08
    Ni asili.
  • 16:08 - 16:13
    Na hoja yangu kwenu inatakiwa halisi na asili ndani yetu, pia.
  • 16:13 - 16:14
    Iambie nafsi yako,
  • 16:15 - 16:18
    hili janga la wakimbizi linaweza simamiwa,
  • 16:18 - 16:19
    lina ufumbuzi,
  • 16:19 - 16:21
    na kila mmoja wetu
  • 16:21 - 16:25
    ana jukumu binafsi la kuhakikisha jambo hili linafanikiwa.
  • 16:25 - 16:29
    Kwa sababu hili jambo ni kuhusu wokozi wetu na thamani yetu
  • 16:29 - 16:32
    vile vile na wokozi wa wakimbizi na maisha yao.
  • 16:32 - 16:34
    Asante sana.
  • 16:34 - 16:37
    (Makofi)
  • 16:45 - 16:48
    Bruno Giussani: David, asante. David Miliband: Asante.
  • 16:48 - 16:50
    BG: Haya ni mapendekezo yenye nguvu
  • 16:50 - 16:53
    na wito wako kwa kila mmoja ni wenye nguvu pia,
  • 16:53 - 16:55
    lakini ninatatizwa na wazo moja, ni hili hapa:
  • 16:55 - 16:59
    umetaja, na haya ni maneno yako,"utawala usio wa kawaida wa Magharibi"
  • 16:59 - 17:01
    ambao umeongoza kwa miaka 60 hivi iliyopita
  • 17:01 - 17:03
    kuhusu majadiliano mazima kuhusu haki za binadamu,
  • 17:03 - 17:06
    hadi kwenye makongamano kuhusu wakimbizi, kadhalika na kadhalika.
  • 17:07 - 17:10
    Uongozi huu ulitokea baada ya mkanganyiko mkubwa
  • 17:10 - 17:14
    na ulitokea katika nafasi ya makubaliano ya kisiasa,
  • 17:14 - 17:16
    na sasa tupo mgawanyiko wa kisiasa.
  • 17:16 - 17:19
    Kiuhalisia, wakimbizi wamekuwa moja ya jambo la mgawanyiko.
  • 17:19 - 17:21
    Kwa hiyo ni wapi uongozi utatokea leo hii?
  • 17:21 - 17:24
    DM: Ninadhani upo sahihi kusema
  • 17:24 - 17:26
    uongozi uliozua vita
  • 17:27 - 17:29
    una hasira tofauti na mwendo tofauti
  • 17:29 - 17:30
    na muonekano tofauti pia
  • 17:30 - 17:33
    kuliko uongozi uliozua amani.
  • 17:34 - 17:37
    Na kwa hiyo jibu langu litakuwa kwamba uongozi unatakiwa kutokea chini,
  • 17:37 - 17:39
    na sio juu.
  • 17:39 - 17:42
    Ninamaanisha, maudhui yanayojirudia ya mkutano wiki hii
  • 17:42 - 17:46
    yamekuwa kuhusu kuleta demokrasia katika nguvu.
  • 17:46 - 17:48
    Na tunatakiwa kulinda demokrasia yetu,
  • 17:48 - 17:51
    lakini pia tunatakiwa amsha demokrasia yetu wenyewe.
  • 17:51 - 17:53
    Na pale watu wanaponiambia,
  • 17:53 - 17:54
    "Kuna upinzani katika suala la wakimbizi,"
  • 17:54 - 17:56
    ninachowaambia ni hiki,
  • 17:56 - 17:58
    "Hapana, kuna matabaka,
  • 17:58 - 17:59
    na kwa wakati huu,
  • 17:59 - 18:01
    wale ambao wanaogofya wanapiga kelele zaidi
  • 18:01 - 18:03
    kuliko wale ambao wenye fahari."
  • 18:03 - 18:07
    Kwa hiyo jibu langu kuhusu swali lako ni kwamba tutadhamini na kuhamasisha
  • 18:07 - 18:08
    na kutoa ujasiri katika uongozi
  • 18:08 - 18:10
    pale tunapoungana.
  • 18:10 - 18:14
    Na ninadhani pale pale ambapo unakuwa katika nafasi ya kutafuta uongozi,
  • 18:14 - 18:15
    unatakiwa kuangalia ndani
  • 18:15 - 18:17
    na kuunganisha jamii yako
  • 18:17 - 18:20
    kujaribu kutengeneza mazingira ya tofauti kwa makazi.
  • 18:20 - 18:22
    BG: Asante, David. Asante kwa kuja TED.
  • 18:22 - 18:26
    (Makofi)
Title:
Mgogoro wa wakimbizi ni kipimo cha utu wetu
Speaker:
David Miliband
Description:

Watu millioni sitini na tano walitolewa katika makazi yao na migogoro na majanga katika mwaka 2016. Huu sio tu ni mgogoro; lakini pia ni kipimo cha kuwa sisi ni nani na tunasimamia nini, anasema David Miliband - kila moja wetu ana jukumu binafsi kutatua hali hii. Katika mazungumzo haya yenye umuhimu wa kipekee kuyaangalia , Miliband anatupa njia za dhahiri za kuwasaidia wakimbizi na kugeuza huruma na kuwawazia wengine kuwa vitendo.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
18:38

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions