Return to Video

Kwanini naongelea kuhusu kuishi na kifafa

  • 0:00 - 0:03
    Nina jambo la kushuhudia.
  • 0:05 - 0:07
    Nimekuwa katika mahusiano
  • 0:08 - 0:10
    tangu nikiwa na miaka 17.
  • 0:11 - 0:15
    Natamani ningeongelea kuhusu vipepeo ndani ya tumbo langu
  • 0:15 - 0:18
    au ramani nilizochora ardhini
  • 0:18 - 0:20
    kila ninapowaza kuhusu uhusiano huu,
  • 0:20 - 0:21
    lakini siwezi.
  • 0:22 - 0:25
    Natamani ningeongelea kuhusu maneno matamu yaliyotamkwa
  • 0:25 - 0:27
    au zawadi nilizowahi kupokea
  • 0:27 - 0:29
    kutokana na uhusiano huu,
  • 0:29 - 0:31
    lakini siwezi.
  • 0:32 - 0:35
    Yote ninayoweza kukwambia ni matokeo,
  • 0:36 - 0:40
    ya kuhusu siku nilizotumia nikijiuliza mfululizo;
  • 0:40 - 0:43
    Kwanini, kwanini, kwanini mimi?
  • 0:45 - 0:48
    Nakumbuka yote haya yalipoanzia.
  • 0:48 - 0:51
    Nilikuwa katika mwaka wangu wa mwisho wa shule ya sekondari,
  • 0:51 - 0:54
    na darasa langu lilikuwa limeshinda katika michezo,
  • 0:54 - 0:59
    hivyo tulikuwa tukiimba na kucheza na kukumbatiana.
  • 0:59 - 1:01
    Nilikwenda kuoga.
  • 1:01 - 1:02
    Kisha nikaenda kupata chakula cha jioni.
  • 1:03 - 1:05
    Na nilipokaa ili nipate chakula,
  • 1:06 - 1:08
    meno yangu yakaanza kugongana,
  • 1:08 - 1:11
    na nikashindwa kuweka kijiko katika mdomo wangu.
  • 1:11 - 1:13
    Nilikimbia katika ofisi ya nesi,
  • 1:13 - 1:16
    na kwa sababu nilikuwa siwezi kuongea, nilinyooshea kidole mdomoni mwangu.
  • 1:17 - 1:19
    Hakuelewa ni jambo gani lililokuwa likitokea,
  • 1:19 - 1:21
    aliniambia nilale
  • 1:21 - 1:22
    ilinisaidia --
  • 1:22 - 1:25
    baada ya dakika chache, kugongana kwa meno kuliacha.
  • 1:25 - 1:29
    Nilitaka kuondoka haraka, kisha akaniambia --
  • 1:29 - 1:33
    Hapana, akisisitiza -- kwamba niende bwenini kulala.
  • 1:34 - 1:37
    Wakati huu nilikuwa mwaka wa mwisho wa elimu yangu ya sekondari,
  • 1:37 - 1:42
    miezi michache tu kabla sijaanza mitihani yangu ya mwisho
  • 1:42 - 1:47
    na siku chache kabla ya kufanya mitihani ambayo kwa hapa Kenya tunaiita "mocks"
  • 1:47 - 1:53
    ambayo dhumuni lake ni kumpima mwanafunzi ni kwa namna gani amejiandaa na mtihani wa mwisho.
  • 1:53 - 1:55
    Hakuna namna ningeweza kulala
  • 1:55 - 1:57
    na kuacha mitihani hii inifanyie mzaha.
  • 1:57 - 2:00
    Nilienda darasani, nikaketi,
  • 2:00 - 2:03
    nikachukua notisi zangu za historia ya Kenya,
  • 2:03 - 2:07
    Nikaanza kusoma, kuhusu miji ya pwani za Kenya,
  • 2:07 - 2:09
    kuhusu mfalme Mekatili wa Menza,
  • 2:09 - 2:14
    mwanamke wa Giriama aliyeongoza watu wake kupinga ukoloni wa Waingereza.
  • 2:15 - 2:18
    Baada ya hapo, bila kutambua chochote,
  • 2:18 - 2:21
    mkono wangu wa kushoto ukaanza kutetemeka,
  • 2:23 - 2:25
    na ikawa kama naweka alama katika karatasi la kufikirika.
  • 2:26 - 2:28
    Ndani na nje,
  • 2:29 - 2:32
    na kila mjongeo, mmoja baada ya mwingine,
  • 2:32 - 2:36
    wanadarasa wenzangu wakaacha kujisomea
  • 2:36 - 2:38
    na wakaanza kunishangaa mimi.
  • 2:39 - 2:41
    Na kujaribu kwa bidii zote kuzuia hali hiyo,
  • 2:41 - 2:43
    lakini sikuweza,
  • 2:43 - 2:45
    kwa sababu ulikuwa na aina yake ya maisha.
  • 2:46 - 2:51
    Kisha, ulipokuwa umehakikisha kwamba kila mtu alikuwa akituangalia,
  • 2:51 - 2:55
    Ukaonyesha rasmi,
  • 2:55 - 2:58
    Kuwa na degedege kwa mara ya kwanza,
  • 2:58 - 3:03
    ambapo ilikuwa ni mwanzo wa mahusiano ambayo yana miaka 15 mpaka sasa.
  • 3:06 - 3:12
    Mpapatiko ni moja dalili ya aina nyingi za kifafa,
  • 3:12 - 3:17
    na kila mpapatiko wowote wa mapema hutakiwa kuchunguzwa na daktari
  • 3:17 - 3:19
    kugundua kama mtu ana kifafa
  • 3:19 - 3:22
    au kama ni dalili ya ugonjwa mwingine.
  • 3:22 - 3:26
    Katika tatizo langu, iligundulika kwamba nilikuwa na kifafa.
  • 3:26 - 3:31
    Nilitumia muda mwingi sana hospitali na nyumbani,
  • 3:31 - 3:34
    na shule nilirudi kufanya mtihani wangu wa mwisho tu.
  • 3:35 - 3:39
    Nilikuwa nikipatwa na mpapatiko katika ya mitihani,
  • 3:39 - 3:41
    lakini nilifanikiwa kupata alama nzuri za kutosha
  • 3:41 - 3:45
    kupata nafasi ya kujiunga na shahada ya sayansi ya takwimu za bima
  • 3:45 - 3:46
    katika chuo cha Nairobi.
  • 3:46 - 3:50
    (Makofi)
  • 3:53 - 3:57
    Kwa bahati mbaya, niliacha chuo nikiwa mwaka wa pili.
  • 3:57 - 4:00
    Sikuwa na uwezo wa kutosha wa kuendana na wenzangu
  • 4:00 - 4:02
    na jamii iliyokuwa inanizunguka.
  • 4:02 - 4:04
    Nilibahatika kupata kazi,
  • 4:05 - 4:10
    lakini nilifukuzwa baada ya kupatwa na mpapatiko nikiwa kazini.
  • 4:11 - 4:15
    Nikajikuta katika mahala
  • 4:15 - 4:18
    ambapo nilikuwa najiuliza kila wakati
  • 4:18 - 4:21
    kwanini suala hili limenitokea mimi.
  • 4:22 - 4:25
    Nimeishi katika kukataa ukweli kwa muda mrefu,
  • 4:25 - 4:32
    na kujikataa huku pengine ni kwa sababu ya mambo ambayo yalitokea,
  • 4:32 - 4:35
    kuacha chuo na kufukuzwa kazi.
  • 4:36 - 4:40
    Au kwa sababu ya vitu nilivyosikia kuhusu kifafa
  • 4:40 - 4:42
    na kuhusu watu wanaoishi na kifafa;
  • 4:42 - 4:45
    kwamba hawawezi kuishi wenyewe
  • 4:45 - 4:47
    na hawawezi kusafiri wakiwa peke yao
  • 4:47 - 4:48
    au hata kupata kazi;
  • 4:49 - 4:51
    Kwamba ni watu walio tofauti,
  • 4:51 - 4:55
    walio na roho ambayo wanatakiwa kuokolewa kutoka hiyo roho.
  • 4:57 - 5:00
    Hivyo, nilipokuwa nikizidi kuwaza kuhusu haya mambo,
  • 5:00 - 5:04
    na ndiyo hali yangu ilikuwa ikinitokea,
  • 5:04 - 5:07
    Niliishi miguu yangu ikiwa inafungwa kamba kwa siku kadhaa,
  • 5:07 - 5:11
    sauti yangu ilikuwa ikififia
  • 5:11 - 5:14
    na katika mwisho wa siku, hivi ndivyo ambavyo ningekuwa.
  • 5:15 - 5:17
    Siku mbili au tatu baada ya mpapatiko,
  • 5:17 - 5:20
    kichwa na mikono yangu vilikuwa bado vinatingishika.
  • 5:22 - 5:24
    Nilijihisi kupotea,
  • 5:25 - 5:27
    kama vile ningepoteza kila kitu,
  • 5:28 - 5:29
    na wakati mwingine,
  • 5:31 - 5:32
    hata shauri la kuishi.
  • 5:42 - 5:43
    (Mguno)
  • 5:49 - 5:51
    Nilikuwa na msongo mkubwa wa mawazo.
  • 5:52 - 5:54
    Nikaanza kuandika,
  • 5:54 - 5:56
    kwa sababu watu waliokuwa wananizunguka hawakuwa na majibu
  • 5:56 - 5:58
    ya maswali niliyokuwa nayo.
  • 5:59 - 6:02
    Kisha nikaandika hofu zangu zote
  • 6:02 - 6:03
    na wasiwasi wangu.
  • 6:04 - 6:08
    Niliandika kuhusu siku zangu nzuri na siku zangu mbaya na zile zilizo mbaya zaidi,
  • 6:08 - 6:10
    kisha nikashirikisha katika blogu.
  • 6:11 - 6:12
    Na kabla ya muda kupita,
  • 6:13 - 6:17
    Nilianza kuonekana na kusikika na watu waliokuwa na kifafa
  • 6:17 - 6:19
    na familia zao,
  • 6:19 - 6:21
    na hata wale ambao hawana ugonjwa huu.
  • 6:22 - 6:26
    Na nikaondoka kutoka kwa yule msichana ambae alikuwa akijiuliza ni kwanini mimi kila wakati mimi
  • 6:26 - 6:29
    na nikawa ambae sio tu najishauri mwenyewe
  • 6:29 - 6:32
    lakini hata kwa wale ambao bado hawajatambua sauti zao.
  • 6:35 - 6:40
    (Makofi)
  • 6:43 - 6:47
    Mpapatiko wangu umepungua mno, kutoka mara mbili hadi tatu kwa siku,
  • 6:47 - 6:50
    na wakati mwingine mara mbili hadi tatu ndani ya mwaka.
  • 6:50 - 6:52
    Nikaendelea --
  • 6:52 - 6:56
    (Makofi)
  • 6:57 - 7:00
    Nikafanikiwa kuajiri watu watano,
  • 7:00 - 7:02
    nilipoanzisha inayofahamika kama taasisi ya kwanza Kenya
  • 7:02 - 7:05
    ya bure kuhusu ushauri wa afya ya akili na kifafa.
  • 7:06 - 7:07
    Na nikasafiri --
  • 7:07 - 7:10
    (Makofi)
  • 7:10 - 7:14
    Nikasafiri kuongelea kuhusu uhusiano wangu,
  • 7:14 - 7:16
    vitu hivi vyote ambavyo niliambiwa
  • 7:16 - 7:21
    kwamba watu wenye kifafa kama mimi hawatoweza kamwe.
  • 7:21 - 7:27
    Kila mwaka, watu takribani asilimia 80 sawa na watu waliopo jijini Nairobi
  • 7:27 - 7:29
    hugundulika kuwa na kifafa
  • 7:29 - 7:31
    dunia nzima.
  • 7:31 - 7:33
    Na ni watu kama mimi.
  • 7:33 - 7:37
    ambao wanapitia hisia za unyanyapaa na kutengwa.
  • 7:39 - 7:42
    Nimeifanya kuwa safari ya maisha yangu
  • 7:42 - 7:45
    kufanya maongezi yaendelee,
  • 7:45 - 7:48
    na bado ninakubaliana na uhusiano wangu
  • 7:48 - 7:51
    Ili watu ambao hawana kifafa
  • 7:51 - 7:55
    wanaweza tambua na kukumbuka kila wakati
  • 7:55 - 7:58
    kwamba hakuna tatizo kuwa pamoja na watu kama sisi.
  • 7:58 - 8:04
    kwa kadiri wanavyodidimiza ukuta wala unyanyapaa na kutengwa,
  • 8:04 - 8:06
    Ya kwamba sisi, kama wao,
  • 8:06 - 8:10
    tunaweza kabiliana na chochote kinachotujia maishani.
  • 8:10 - 8:11
    Asante.
  • 8:11 - 8:16
    (Makofi)
Title:
Kwanini naongelea kuhusu kuishi na kifafa
Speaker:
Sitawa Wafula
Description:

Aliyewahi kubaki nyumbani kutokana na ugonjwa wa kifafa. Sitawa Wafula, ambae ni mhamasishaji wa afya ya akili alipata nguvu kuandika kuhusu ugonjwa wake. Kwa sasa, anahamasisha kwa ajili ya wengine ambao bado hawajatambua sauti zao, akivunja unyanyapaa na kutengwa katika kuongelea ni namna gani inavyokuwa kwa mtu anayeishi na ugonjwa wa kifafa.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
08:29

Swahili subtitles

Revisions