Hujambo, Jina langu ni Suzan Song, Mwelekezi wa Kitengo cha Tiba na Taaluma ya Ugonjwa wa Akili kwa Watoto, Vijana na Familia cha Chuo Kikuu cha George Washington, na Mshauri wa Kulinda Ubinadamu kwa waathiriwa wa uhamishaji wa lazima kote duniani na nchini. Kumekuwa na ongezeko la kipekee la idadi ya wakimbizi kote ulimwenguni, wakiwemo wakimbizi, watafuta makao, wahamiaji wasio halali na watoto walio pweke. Kote ulimwenguni, zaidi ya watu milioni 65 kwa sasa ni wakimbizi kutokana na vita, mateso au mgogoro wa kivita. Kufikia mwanzo mwa 2018, takribani watoto milioni 31 kote ulimwenguni walifanywa wakimbizi kutokana na vurugu na migogoro. Iwapo mitindo hii ya sasa itaendelea, mtu mmoja kati ya watu mia moja atakuwa mkimbizi hivi karibuni. Kwa bahati mbaya, wakimbizi na waathiriwa wengi wa uhamaji wa lazima hawapokei huduma inayohitajika ya afya ya akili. kutokana na umakini wa huduma, ukosefu wa kufikia huduma ya kitaalamu, na shutuma dhidi ya matatizo ya akili.