Makadirio-kukaribisha kwenye mkumi Katika maisha yako ya hesabu, utakutana na hali ambayo itakubidi ukaribishe namba. Na unaweza kujiuliza kwanini? Inatokea katika hali gani? Hii inakuwa katika hali ambayo unajaribu kupata makadirio ya vitu labda una kipimo na unataka kisilingane sawasawa ili kurahisisha vitu. Au hujui kama kipimo ni sahihi kwa kiasi gani. Hivyo hapa tutajadili kukaribisha ni nini. Na tutakaribisha namba hizi 36, 34, 35, 26, na 12. Tunakwenda kuzikaribisha kwenye 10 Na nitakwambia maana yake. Hii maana yake chukua kila namba, na utafute zinazogawanyika kwa 10. je zinazogawanyika kwa 10 ni zipi? 10 mara 0 ni 0, 10 mara 1 ni 10, 20, 30, 40, 50, 60, nakuendelea. Nitaomba usimamishe video, na ukumbuke nilichokwambia, makadirio ya 10 kwa kila namba. Fikiria kuitazama hii zaidi tuchore mstari wa namba hapa. Nitaweka mistari miwili ya namba hapa. Hivyo tuna mistari ya namba hapa. Na tuone wapi hizi alama zitakaa kwenye mstari huu wa namba. Kwanza namba 36 wapi itakaa wapi kwenye huu mstari wa namba? hivyo ni kati ya 30 na 40. na hii alama ndogo ya bluu ni 35 Hivyo 36 ni kubwa zaidi kuliko 53 hivyo 36 itakuwa hapa. Na tukiikuza ni kati ya 30 na 40. Kwhiyo tukisema hii ni 30 na hii ni 40. je 36 itakuwa wapi? Halafu hii ni 35. 36 ni mbele kidogo hivyo 36 itakuwa hapa. Hivyo tukitaka kuikaribisha kwenye makumi Njia mbili za kufanya ni zipi? Nitachukua 36 na kuikaribisha kwenye zinazogawanyika kwa 10 ambayo ni 40. hivyo ningekaribisha mpaka kwenye 40 na ya chini inayogawanyika kwa 10 ni 30. Na inabidi nijue ni namba ipi ipo karibu zaidi. Hivyo ukiangalia hapa unaona. Lakini pia ungeweza sema 36 ni namba nne kufikia 40 na ni 6 kurudi kwenye 30, ni karibu na 40 hivyo tutakaribisha. tutakaribisha mpaka kwenye 40. Hii ndio kukaribisha kwa kuongeza. Sasa tujaribu namba hizi. vipi kuhusu 34? Na naomba usimamishe video. Tafuta namba ambayo utakadiria kwa kuongeza na kwa kupunguza, na ipi iko karibu. 34 iko hapa kwenye namba hii, tukiivuta karibu, 34 iko hapa. Na tuna njia mbili. Zinazogawanyika kwa 10 juu ya 34 zinazogawanyika kwa 10 zaidi ya 34 ni 40. Zinazogawanyika kwa 10 chini ya 34 ni 30. Je ipi iko karibu? Ni nne tu kutoka kwenye 30 na 6 kutoka kwenye 40, ni karibu na 30 Hivyo tutakaribisha kwa kupunguza mpaka 30. Na kumbuka tumekwenda kwenye 30. Na unaweza fikiri tulivyokaribisha kwenye makumi, imeongezeka toka kwenye 3 mpaka 4, kutoka kwenye 30 mpaka kwenye 40. Labda tukikaribisha kwa kupunguza , sehemu ya makumi itapungua kutoka kwenye 30 kwenda 20 ,hapana 30 inagawanyika kwa 10 chini ya 34. Kwahiyo ukikaribisha kwa kupunguza unaenda kwenye zinazogawanyika kwa kumi ila kwenye mamoja itakuwa 0. Sasa tujaribu na hii. Tujaribu kukaribisha namba 35 kwenye makumi. Kabla hatujaifanya, tutazame njia mbili tunazoweza kutumia. Tumeshaziona. 35 iko hapa. Kwenye huu mstari wa namba ni, 35 na tuna njia mbili. 35 tunaweza kukaribisha kwa kuongeza mpaka 40 na kukaribisha kwa kupunguza mpaka 30. Nitashauri usimamishe video hii kidogo inachanganya kwasababu kwenda juu ni tano kurudi chini ni tano. 5 toka kwenye 40 na 5 kwenda kwenye 30 Hivyo wanahesabu waliamua kueleza cha kufanya unapokutana na hii hesabu ambapo una 5 kwenye mamoja. kama una 5 au zaidi kwenye mamoja utakaribisha kwa kuongeza. Hii ndio kanuni yake. Ikiwa 5 au zaidi kwenye mamoja , unakaribisha kwa kuongeza. Hivyo 35 unakaribisha mpaka 40. Tambua, 6 kwenye mamoja ilikuwa tano au zaidi Hivyo kama unakaribisha kwenye makumi, unakaribisha kwa kuongeza mpaka 40. Nne kwenye mamoja sio 5 au zaidi, hivyo unakaribisha kwa kupunguza. Na hii inaleta maana kwenye hizi namba mbili. Tujaribu tuone nini kinatokea kwenye 26. 26, njia ni zipi? kwenye 26 zinazogawanyika kwa 10 kwenda juu ni zipi? na zinazogawanyika kwa 10 kwenda chini ni zipi? Sawa, inayogawanyika kwa 10 kwenda juu ni 30, na kwenda chini ni 20. Hivyo tunakaribisha kwa kuongeza mpaka 30. tunakaribisha kwa kupunguza mpaka 20. kama tunakaribisha kwenye makumi tunaangalia sehemu ya makumi. Hivyo ndivyo tutakavyokaribisha. tutakaribisha kwenye makumi-- lakini tunaangalia kwenye sehemu ya mamoja. Sehemu ya mamoja itaamua. Na tunaona hapa hii ni 5 au zaidi. Au unaweza sema hii ni kubwa kuliko au ni sawasawa na 5 Hivyo tunakaribisha kwa kuongeza. 26 kwenye makumi tunakaribisha kwa kuongeza mpaka 30. Je vipi kuhusu 12? Nadhani unaelewa sasa Sasa tufikirie zinazogawanyika kwa 10 zaidi ya 12. Hivyo tunaweza kukaribisha kwa kuongeza mpaka 20. 12 iko hapa. tunaweza karibisha kwa kuongeza mpaka 20 au kupunguza mpaka 10. kama tunakaribisha kwenye makumi, tutaangalia kwenye mamoja. Tutaangalia kwenye mamoja hapa. Hii ni ndogo kuliko 5. Kwasababu ni ndogo kuliko 5tunakaribisha kwa kupunguza, ambayo inaleta maana kwasababu ni karibu 10 kuliko ilivyo 20. Hivyotunakaribisha kwa kupunguza mpaka 12, utapata 10.