Wakikuomba ulipe kabla ya kukuombea, tafadhali ukimbie.
Huduma ya kiroho haiuzwi.
Ikiwa kuna masharti -
'Kabla sijakuombea, lazima utoe hiki' -
tafadhali kimbia. Jitenganishe.
Hiyo ni bendera kubwa nyekundu kiroho.
Kinachoombewa hakiwezi kulipiwa.
Hakuna kiasi cha pesa kinachoweza kukupa amani ya moyo.
Kuna vitu Mungu pekee anaweza kutoa.
Tukisema lazima utoe pesa kabla ya kupokea maombi,
unaweza kupokea maombi bila amani.
Na mimi ninayekuombea - pia sitakuwa na amani yoyote.
Ninaweza kukuombea ukinilipa, lakini sitakuwa na amani.
Haitaambatana na furaha.
Haitaambatana na kuridhika.
Ni somo watu wa Mungu.
Tafadhali, usifanye kwa sababu ya kukata tamaa,
usifanye hivyo kwa sababu ya ushawishi wa ulimwengu huu
kwenda nje ya viwango vya Mungu katika kutafuta suluhu,
hata kwa mtu anayedai kuwa ni wa Mungu.
Kuwa mwangalifu. Hebu kuwe na busara.
Biblia ndio kiwango chetu.