WEBVTT 00:00:09.280 --> 00:00:12.960 Neema na amani iwe kwenu nyote katika jina kuu la Yesu 00:00:12.960 --> 00:00:20.120 na karibu katika toleo jingine la 'Imani Ni Asili' hapa kwenye TV ya Moyo wa Mungu. 00:00:20.120 --> 00:00:26.000 Leo, nataka kuzungumzia suala ambalo limejitokeza mara nyingi sana 00:00:26.000 --> 00:00:33.960 katika mazungumzo na watu - katika nyakati za maombi, ushauri na kutia moyo. 00:00:33.960 --> 00:00:40.280 Nimeona tu kwamba watu wengi sana leo 00:00:40.280 --> 00:00:47.080 wanaishi maisha yao kupitia lenzi hii ya jana, 00:00:47.080 --> 00:00:49.040 kupitia lenzi ya walivyokuwa - 00:00:49.040 --> 00:00:56.320 mabaya yao ya zamani, makosa, maumivu na uchungu. 00:00:56.320 --> 00:01:02.160 Na kama matokeo ya hili, wengi hujikuta wamenaswa 00:01:02.160 --> 00:01:12.880 katika mzunguko huu mbaya wa hatia na hukumu kwa makosa waliyofanya 00:01:12.880 --> 00:01:18.320 au vilevile mzunguko mbaya wa uchungu na chuki 00:01:18.320 --> 00:01:23.280 juu ya mabaya waliyofanyiwa huko nyuma. 00:01:23.280 --> 00:01:27.240 Na ni hatari sana. 00:01:27.240 --> 00:01:35.840 Watu wa Mungu, hii si chochote ila ni njama ya hila, hila ya kawaida ya shetani 00:01:35.840 --> 00:01:40.880 ili kukutenganisha na Mungu. 00:01:40.880 --> 00:01:45.520 Shetani anafurahia kujadili mambo yako ya nyuma na wewe. 00:01:45.520 --> 00:01:52.840 Anafurahi kukukumbusha juu ya kutofaulu kwako zamani, makosa ya zamani, maumivu ya zamani. 00:01:52.840 --> 00:01:57.800 Kwa sababu hicho ndicho kitu pekee kinachokuunganisha naye. 00:01:57.800 --> 00:02:04.720 Hiyo ndiyo habari pekee ambayo anayo kuhusu wewe - siku zako za nyuma. 00:02:04.720 --> 00:02:11.040 Na shetani atachukua kila njia inayopatikana 00:02:11.040 --> 00:02:19.320 kujaribu na kukuzuia usitende Neno la Mungu sasa. 00:02:19.320 --> 00:02:24.640 Angalia, hajali ikiwa utalichambua tu Neno. 00:02:24.640 --> 00:02:30.640 Haijalishi kama unastaajabia Neno au hata kukubali ukweli wa Neno 00:02:30.640 --> 00:02:35.960 mradi hutendi Neno hilo. 00:02:35.960 --> 00:02:39.480 Hataki utende neno la Mungu! 00:02:39.480 --> 00:02:48.840 Anataka uishi maisha yako kupitia lenzi ya maisha yako ya zamani yasiyofaa, 00:02:48.840 --> 00:02:53.040 kwa wewe kuchuja kila kitu kupitia hiyo, 00:02:53.040 --> 00:03:00.960 ili kulemaza uwezo wako wa kutenda imani muda huu 00:03:00.960 --> 00:03:07.200 na hivyo kuharibu maisha yako ya baadaye. 00:03:07.200 --> 00:03:20.120 Watu wa Mungu, ni hatari kuchukua safari zisizo za lazima hadi jana. 00:03:20.120 --> 00:03:23.840 Ni hatari sana. 00:03:23.840 --> 00:03:30.920 Angalia, siku zako za nyuma haziamui sasa yako 00:03:30.920 --> 00:03:36.040 na haiamui mustakabali wako. 00:03:36.040 --> 00:03:41.440 Unaweza kujifunza kutoka kwenye maisha yako ya zamani bila kuishi katika maisha yako ya zamani. 00:03:41.440 --> 00:03:45.440 Usiishi ndani yake; jifunze kutoka kwake. 00:03:45.440 --> 00:03:54.680 Usiheshimu udanganyifu wa shetani kwa umakini wako - umakini wako wa thamani. 00:03:54.680 --> 00:04:00.400 Kwa sababu makosa yako hayakufafanui wewe. 00:04:00.400 --> 00:04:03.680 Zaburi 37:24 00:04:03.680 --> 00:04:08.920 Narudia - makosa yako hayakufafanui. 00:04:08.920 --> 00:04:13.080 Kwa kweli, yanaweza hata kukuboresha. 00:04:13.080 --> 00:04:21.960 Namaanisha, Mungu anaweza hata kutumia makosa yako kukupeleka mahali 00:04:21.960 --> 00:04:32.640 anapotaka uwe - kulingana na mwitikio wako. 00:04:32.640 --> 00:04:35.320 Jambo kuu liko kwenye mwitikio wako. 00:04:35.320 --> 00:04:37.920 Je, unaitikiaje kwenye kosa hilo? 00:04:37.920 --> 00:04:41.480 Sasa, ngoja nikupe mfano halisi sana. 00:04:41.480 --> 00:04:44.240 Hebu wazia uko safarini mahali fulani. 00:04:44.240 --> 00:04:46.240 Unaenda mahali fulani; unajua unakokwenda. 00:04:46.240 --> 00:04:51.160 Na katika safari hii, ghafla unatambua kuwa uko mahali pasipofaa. 00:04:51.160 --> 00:04:54.160 Umechukua hatua mbaya; umekosa mwelekeo. 00:04:54.160 --> 00:04:56.120 Unafanya nini? 00:04:56.120 --> 00:05:03.000 Unahitaji kurejesha hatua zako na kurudi kwenye mstari. 00:05:03.000 --> 00:05:06.880 Ikiwa unatambua kuwa umeenda katika mwelekeo mbaya, je, unasema tu, 00:05:06.880 --> 00:05:11.120 'Oh sawa, nimechelewa mno! Acha niendelee tu katika njia hii mbaya.' 00:05:11.120 --> 00:05:23.680 Hapana! Unarudi haraka kwenye njia sahihi, rudi kwenye mstari na uendelee na safari yako. 00:05:23.680 --> 00:05:32.320 Watu wa Mungu, katika safari hii ya maisha, 00:05:32.320 --> 00:05:39.320 ukichukua hatua mbaya, unajibuje? 00:05:39.320 --> 00:05:42.480 Je, unaitikiaje? 00:05:42.480 --> 00:05:52.920 Je, unatambua kosa lako, rudia hatua zako na kumkimbilia Mungu kwa toba? 00:05:52.920 --> 00:05:59.680 Au unapinga kujichunguza, 00:05:59.680 --> 00:06:03.200 galagala kwa kujihurumia 00:06:03.200 --> 00:06:16.760 na kuanguka ndani zaidi katika mtandao huo tatanishi wa hatia, lawama na uduni? 00:06:16.760 --> 00:06:24.040 Je, unarudi kwenye mstari au unaenda nje zaidi? 00:06:24.040 --> 00:06:28.160 Chaguo ni lako. 00:06:28.160 --> 00:06:39.760 Kuchagua kuishi katika maisha yako ya zamani ni kuchagua kwenda zaidi nje ya njia. 00:06:39.760 --> 00:06:45.080 Kuanguka katika hatia na hukumu hiyo - unaenda nje zaidi. 00:06:45.080 --> 00:06:47.880 Vivyo hivyo, ikiwa unahalalisha kosa lako 00:06:47.880 --> 00:06:50.560 au unanyosha vidole kushoto, kulia na katikati 00:06:50.560 --> 00:06:57.040 au kutoa visingizio, natoka nje ya njia ya mstari. 00:06:57.040 --> 00:07:01.680 Na jambo la hatari hapa ni kwamba 00:07:01.680 --> 00:07:09.560 kadiri unavyoongeza kukaa kwako katika makosa, 00:07:09.560 --> 00:07:18.840 ndivyo uharibifu zaidi shetani anavyoweza kuuletea moyoni mwako. 00:07:18.840 --> 00:07:27.200 Na shetani anapokuwa na nafasi ndani ya moyo wako. 00:07:27.200 --> 00:07:32.640 uharibifu huo unaweza kuenea kwa urahisi kwenye nyumba yako, 00:07:32.640 --> 00:07:38.520 ndoa, familia, mahusiano na kazi yako. 00:07:38.520 --> 00:07:44.960 Tunasuka mtandao ulioingiliana 00:07:44.960 --> 00:07:52.000 wakati makosa yetu, tunakataa kuondoka. 00:07:52.000 --> 00:07:54.880 Sisemi kwamba hutafanya makosa. 00:07:54.880 --> 00:07:58.000 Kila mtu hufanya makosa katika safari hii. 00:07:58.000 --> 00:08:00.480 Kila mtu hukosa alama. 00:08:00.480 --> 00:08:05.280 Ninamaanisha, angalia tu Biblia, mwongozo wetu, Neno la Mungu - 00:08:05.280 --> 00:08:10.440 wahusika wengi wakuu wa Biblia tunaowasoma. 00:08:10.440 --> 00:08:14.200 Nuhu alipambana na pombe. 00:08:14.200 --> 00:08:16.320 Yakobo alitumia udanganyifu. 00:08:16.320 --> 00:08:19.600 Lutu alipambana na uchu. 00:08:19.600 --> 00:08:25.080 Vipi kuhusu Musa ambaye alipambana na hasira. 00:08:25.080 --> 00:08:31.080 Petro mara nyingi aliingiwa na woga, Tomaso na mashaka. 00:08:31.080 --> 00:08:36.560 Vipi kuhusu Mfalme Daudi, Sulemani, Samsoni - wote walishindwa na tamaa. 00:08:36.560 --> 00:08:44.000 Hakuna mkamilifu katika ulimwengu huu (Warumi 3:10, 23) 00:08:44.000 --> 00:08:51.840 Sisi sote hujikwaa kwa njia nyingi (Yakobo 3:2) 00:08:51.840 --> 00:08:58.600 Katika ulimwengu huu mwovu, kutakuwa na mzozo huo daima, 00:08:58.600 --> 00:09:04.320 ile vita ndani ya moyo wa mwanadamu kati ya mwili na roho. 00:09:04.320 --> 00:09:11.640 Wazo lililo moyoni mwako ni vita utakayokabiliana nayo hadi siku ya mwisho, 00:09:11.640 --> 00:09:15.880 mpaka Yesu atakapokuja - ndivyo vita utakavyokabiliana nayo. 00:09:15.880 --> 00:09:22.320 Kwa hiyo, faraja yangu kwenu leo, watu wa Mungu, ni hii: 00:09:22.320 --> 00:09:30.280 Mara tu unapogundua kuwa umechukua hatua mbaya, 00:09:30.280 --> 00:09:36.040 rudi haraka kwenye mstari. 00:09:36.040 --> 00:09:45.680 Usiongeze muda wa kukaa kwako katika makosa kwa kujitetea kwenye hilo. 00:09:45.680 --> 00:09:54.480 Angalia, kama mtoto wa Mungu, unaweza kujua unapochukua hatua mbaya. 00:09:54.480 --> 00:10:02.920 Vipi? Roho wa Mungu atachochea dhamiri yako kutubu. 00:10:02.920 --> 00:10:07.880 Warumi 9:1, 2 Wakorintho 7:10 00:10:07.880 --> 00:10:14.040 Roho Mtakatifu ataisukuma dhamiri yako kutubu. 00:10:14.040 --> 00:10:25.280 Swali ni - roho yako ni sikivu kiasi gani? 00:10:25.280 --> 00:10:32.760 una haraka kiasi gani kujitetea? 00:10:32.760 --> 00:10:42.960 Kasi ambayo unatambua kosa lako ni sawia 00:10:42.960 --> 00:10:52.680 na kiwango ambacho Neno la Mungu linatawala moyo wako. 00:10:52.680 --> 00:11:03.960 Na kuwa mwangalifu zaidi kwa msukumo wa Roho wa Mungu katika roho yako, 00:11:03.960 --> 00:11:09.960 inakupasa kutumia muda mwingi zaidi miguuni pake, 00:11:09.960 --> 00:11:13.320 muda mwingi mbele zake, 00:11:13.320 --> 00:11:16.160 muda zaidi katika Neno Lake. 00:11:16.160 --> 00:11:22.240 Lazima aongezeke; lazima upungue (Yohana 3:30). 00:11:22.240 --> 00:11:26.400 Kwa sababu yote yanamhusu Yesu; haikuhusu wewe. 00:11:26.400 --> 00:11:31.960 Sio juu ya kustahili kwako kwa sababu hakuna mtu anayestahili. 00:11:31.960 --> 00:11:39.160 Sio juu ya udhaifu wako kwa sababu kila mtu ana udhaifu. 00:11:39.160 --> 00:11:45.200 Yote ni juu ya utayari wako - 00:11:45.200 --> 00:11:49.280 utayari wako wa kukiri kosa lako, 00:11:49.280 --> 00:11:53.160 kuweka kiburi chako kando, 00:11:53.160 --> 00:11:59.040 rudia hatua zako, rudi kwenye mstari na Mungu 00:11:59.040 --> 00:12:03.440 na endelea na safari yako ya imani. 00:12:03.440 --> 00:12:10.520 Kwa sababu si lazima uwe mkamilifu ili uwe mtoto wa Mungu; 00:12:10.520 --> 00:12:14.760 unatakiwa tu uwepo. 00:12:14.760 --> 00:12:18.720 Watu wa Mungu, nitawaacha leo na neno la Maandiko 00:12:18.720 --> 00:12:22.960 kutoka kwa Mtume Paulo katika Warumi 8:1. 00:12:22.960 --> 00:12:35.480 Akasema, Sasa basi, hakuna hukumu ya adhabu 00:12:35.480 --> 00:12:39.000 kwa wale walio katika Kristo Yesu." 00:12:39.000 --> 00:12:44.760 Sasa, Maandiko haya hayatupi msingi wa kuhurumia dhambi, 00:12:44.760 --> 00:12:50.360 kuhalalisha makosa au kuchukua neema kirahisi. Hapana! 00:12:50.360 --> 00:13:00.960 Lakini inasisitiza tu kwamba hatupaswi kuruhusu hatia ya makosa yetu 00:13:00.960 --> 00:13:10.480 kutunyang'anya amani ya pekee inayopatikana katika msamaha wa Kristo. 00:13:10.480 --> 00:13:15.680 Badala ya kosa lako kukutoa mbele za Mungu, 00:13:15.680 --> 00:13:23.800 inapaswa kuwa sababu ya wewe kumkaribia Yeye zaidi. 00:13:23.800 --> 00:13:27.520 Kwa sababu katika maneno ya Nabii T.B. Joshua: 00:13:27.520 --> 00:13:38.640 "Unaweza kujua wewe ni mtoto wa Mungu wakati makosa yako yanapochochea maisha yako ya kiroho." 00:13:38.640 --> 00:13:40.560 Asante, Yesu Kristo. 00:13:40.560 --> 00:13:44.720 Sasa hivi, watu wa Mungu, ni wakati wa maombi. 00:13:51.160 --> 00:13:59.760 Hivi sasa, kwa kila moyo uliochafuliwa na hatia - 00:13:59.760 --> 00:14:05.600 takaswa, katika jina kuu la Yesu Kristo! 00:14:05.600 --> 00:14:10.880 kwa kila roho inayosumbuliwa na hukumu, 00:14:10.880 --> 00:14:18.960 takaswa kwa Damu ya thamani ya Yesu Kristo! 00:14:18.960 --> 00:14:26.680 Damu ya Yesu Kristo inapokusafisha, umetakaswa kwelikweli! 00:14:26.680 --> 00:14:29.120 Takaswa sasa hivi! 00:14:29.120 --> 00:14:38.000 Katika roho yako, katika nafsi yako, katika mwili wako - takaswa! 00:14:38.000 --> 00:14:48.640 Kila roho ya dhiki, utumwa, udhaifu, ndoto mbaya - 00:14:48.640 --> 00:14:53.160 uoshwe kwa Damu ya Yesu Kristo! 00:14:53.160 --> 00:15:03.640 Uoshwe sasa hivi, katika jina kuu la Yesu Kristo! 00:15:03.640 --> 00:15:07.160 Pokea ujasiri! 00:15:07.160 --> 00:15:10.080 Pokea nguvu! 00:15:10.080 --> 00:15:20.160 Pokea usadikisho wa kushikilia msimamo wako katika Kristo! 00:15:20.160 --> 00:15:27.040 Ee Bwana, rekebisha kila moyo mkaidi na utashi. 00:15:27.040 --> 00:15:30.680 Ongoza hatua zinazoenda kombo. 00:15:30.680 --> 00:15:35.520 Osha madoa ya hatia. 00:15:35.520 --> 00:15:41.320 Tusaidie kuona kupitia macho yako. 00:15:41.320 --> 00:15:48.720 Tuvute kwenye uhusiano wa karibu na Wewe 00:15:48.720 --> 00:15:56.560 na utujalie ufahamu mkubwa zaidi wa moyo Wako. 00:15:56.560 --> 00:16:06.000 Katika jina kuu la Yesu Kristo! Amina! 00:16:06.000 --> 00:16:08.280 Asante, Yesu Kristo.