[Script Info] Title: [Events] Format: Layer, Start, End, Style, Name, MarginL, MarginR, MarginV, Effect, Text Dialogue: 0,0:00:09.28,0:00:12.96,Default,,0000,0000,0000,,Neema na amani iwe kwenu nyote katika jina kuu la Yesu Dialogue: 0,0:00:12.96,0:00:20.12,Default,,0000,0000,0000,,na karibu katika toleo jingine la 'Imani Ni Asili' hapa kwenye TV ya Moyo wa Mungu. Dialogue: 0,0:00:20.12,0:00:26.00,Default,,0000,0000,0000,,Leo, nataka kuzungumzia suala ambalo limejitokeza mara nyingi sana Dialogue: 0,0:00:26.00,0:00:33.96,Default,,0000,0000,0000,,katika mazungumzo na watu - katika nyakati za maombi, ushauri na kutia moyo. Dialogue: 0,0:00:33.96,0:00:40.28,Default,,0000,0000,0000,,Nimeona tu kwamba watu wengi sana leo Dialogue: 0,0:00:40.28,0:00:47.08,Default,,0000,0000,0000,,wanaishi maisha yao kupitia lenzi hii ya jana, Dialogue: 0,0:00:47.08,0:00:49.04,Default,,0000,0000,0000,,kupitia lenzi ya walivyokuwa - Dialogue: 0,0:00:49.04,0:00:56.32,Default,,0000,0000,0000,,mabaya yao ya zamani, makosa, maumivu na uchungu. Dialogue: 0,0:00:56.32,0:01:02.16,Default,,0000,0000,0000,,Na kama matokeo ya hili, wengi hujikuta wamenaswa Dialogue: 0,0:01:02.16,0:01:12.88,Default,,0000,0000,0000,,katika mzunguko huu mbaya wa hatia na hukumu kwa makosa waliyofanya Dialogue: 0,0:01:12.88,0:01:18.32,Default,,0000,0000,0000,,au vilevile mzunguko mbaya wa uchungu na chuki Dialogue: 0,0:01:18.32,0:01:23.28,Default,,0000,0000,0000,,juu ya mabaya waliyofanyiwa huko nyuma. Dialogue: 0,0:01:23.28,0:01:27.24,Default,,0000,0000,0000,,Na ni hatari sana. Dialogue: 0,0:01:27.24,0:01:35.84,Default,,0000,0000,0000,,Watu wa Mungu, hii si chochote ila ni njama ya hila, hila ya kawaida ya shetani Dialogue: 0,0:01:35.84,0:01:40.88,Default,,0000,0000,0000,,ili kukutenganisha na Mungu. Dialogue: 0,0:01:40.88,0:01:45.52,Default,,0000,0000,0000,,Shetani anafurahia kujadili mambo yako ya nyuma na wewe. Dialogue: 0,0:01:45.52,0:01:52.84,Default,,0000,0000,0000,,Anafurahi kukukumbusha juu ya kutofaulu kwako zamani, makosa ya zamani, maumivu ya zamani. Dialogue: 0,0:01:52.84,0:01:57.80,Default,,0000,0000,0000,,Kwa sababu hicho ndicho kitu pekee kinachokuunganisha naye. Dialogue: 0,0:01:57.80,0:02:04.72,Default,,0000,0000,0000,,Hiyo ndiyo habari pekee ambayo anayo kuhusu wewe - siku zako za nyuma. Dialogue: 0,0:02:04.72,0:02:11.04,Default,,0000,0000,0000,,Na shetani atachukua kila njia inayopatikana Dialogue: 0,0:02:11.04,0:02:19.32,Default,,0000,0000,0000,,kujaribu na kukuzuia usitende Neno la Mungu sasa. Dialogue: 0,0:02:19.32,0:02:24.64,Default,,0000,0000,0000,,Angalia, hajali ikiwa utalichambua tu Neno. Dialogue: 0,0:02:24.64,0:02:30.64,Default,,0000,0000,0000,,Haijalishi kama unastaajabia Neno au hata kukubali ukweli wa Neno Dialogue: 0,0:02:30.64,0:02:35.96,Default,,0000,0000,0000,,mradi hutendi Neno hilo. Dialogue: 0,0:02:35.96,0:02:39.48,Default,,0000,0000,0000,,Hataki utende neno la Mungu! Dialogue: 0,0:02:39.48,0:02:48.84,Default,,0000,0000,0000,,Anataka uishi maisha yako kupitia lenzi ya maisha yako ya zamani yasiyofaa, Dialogue: 0,0:02:48.84,0:02:53.04,Default,,0000,0000,0000,,kwa wewe kuchuja kila kitu kupitia hiyo, Dialogue: 0,0:02:53.04,0:03:00.96,Default,,0000,0000,0000,,ili kulemaza uwezo wako wa kutenda imani muda huu Dialogue: 0,0:03:00.96,0:03:07.20,Default,,0000,0000,0000,,na hivyo kuharibu maisha yako ya baadaye. Dialogue: 0,0:03:07.20,0:03:20.12,Default,,0000,0000,0000,,Watu wa Mungu, ni hatari kuchukua safari zisizo za lazima hadi jana. Dialogue: 0,0:03:20.12,0:03:23.84,Default,,0000,0000,0000,,Ni hatari sana. Dialogue: 0,0:03:23.84,0:03:30.92,Default,,0000,0000,0000,,Angalia, siku zako za nyuma haziamui sasa yako Dialogue: 0,0:03:30.92,0:03:36.04,Default,,0000,0000,0000,,na haiamui mustakabali wako. Dialogue: 0,0:03:36.04,0:03:41.44,Default,,0000,0000,0000,,Unaweza kujifunza kutoka kwenye maisha yako ya zamani bila kuishi katika maisha yako ya zamani. Dialogue: 0,0:03:41.44,0:03:45.44,Default,,0000,0000,0000,,Usiishi ndani yake; jifunze kutoka kwake. Dialogue: 0,0:03:45.44,0:03:54.68,Default,,0000,0000,0000,,Usiheshimu udanganyifu wa shetani kwa umakini wako - umakini wako wa thamani. Dialogue: 0,0:03:54.68,0:04:00.40,Default,,0000,0000,0000,,Kwa sababu makosa yako hayakufafanui wewe. Dialogue: 0,0:04:00.40,0:04:03.68,Default,,0000,0000,0000,,Zaburi 37:24 Dialogue: 0,0:04:03.68,0:04:08.92,Default,,0000,0000,0000,,Narudia - makosa yako hayakufafanui. Dialogue: 0,0:04:08.92,0:04:13.08,Default,,0000,0000,0000,,Kwa kweli, yanaweza hata kukuboresha. Dialogue: 0,0:04:13.08,0:04:21.96,Default,,0000,0000,0000,,Namaanisha, Mungu anaweza hata kutumia makosa yako kukupeleka mahali Dialogue: 0,0:04:21.96,0:04:32.64,Default,,0000,0000,0000,,anapotaka uwe - kulingana na mwitikio wako. Dialogue: 0,0:04:32.64,0:04:35.32,Default,,0000,0000,0000,,Jambo kuu liko kwenye mwitikio wako. Dialogue: 0,0:04:35.32,0:04:37.92,Default,,0000,0000,0000,,Je, unaitikiaje kwenye kosa hilo? Dialogue: 0,0:04:37.92,0:04:41.48,Default,,0000,0000,0000,,Sasa, ngoja nikupe mfano halisi sana. Dialogue: 0,0:04:41.48,0:04:44.24,Default,,0000,0000,0000,,Hebu wazia uko safarini mahali fulani. Dialogue: 0,0:04:44.24,0:04:46.24,Default,,0000,0000,0000,,Unaenda mahali fulani; unajua unakokwenda. Dialogue: 0,0:04:46.24,0:04:51.16,Default,,0000,0000,0000,,Na katika safari hii, ghafla unatambua kuwa uko mahali pasipofaa. Dialogue: 0,0:04:51.16,0:04:54.16,Default,,0000,0000,0000,,Umechukua hatua mbaya; umekosa mwelekeo. Dialogue: 0,0:04:54.16,0:04:56.12,Default,,0000,0000,0000,,Unafanya nini? Dialogue: 0,0:04:56.12,0:05:03.00,Default,,0000,0000,0000,,Unahitaji kurejesha hatua zako na kurudi kwenye mstari. Dialogue: 0,0:05:03.00,0:05:06.88,Default,,0000,0000,0000,,Ikiwa unatambua kuwa umeenda katika mwelekeo mbaya, je, unasema tu, Dialogue: 0,0:05:06.88,0:05:11.12,Default,,0000,0000,0000,,'Oh sawa, nimechelewa mno! Acha niendelee tu katika njia hii mbaya.' Dialogue: 0,0:05:11.12,0:05:23.68,Default,,0000,0000,0000,,Hapana! Unarudi haraka kwenye njia sahihi, rudi kwenye mstari na uendelee na safari yako. Dialogue: 0,0:05:23.68,0:05:32.32,Default,,0000,0000,0000,,Watu wa Mungu, katika safari hii ya maisha, Dialogue: 0,0:05:32.32,0:05:39.32,Default,,0000,0000,0000,,ukichukua hatua mbaya, unajibuje? Dialogue: 0,0:05:39.32,0:05:42.48,Default,,0000,0000,0000,,Je, unaitikiaje? Dialogue: 0,0:05:42.48,0:05:52.92,Default,,0000,0000,0000,,Je, unatambua kosa lako, rudia hatua zako na kumkimbilia Mungu kwa toba? Dialogue: 0,0:05:52.92,0:05:59.68,Default,,0000,0000,0000,,Au unapinga kujichunguza, Dialogue: 0,0:05:59.68,0:06:03.20,Default,,0000,0000,0000,,galagala kwa kujihurumia Dialogue: 0,0:06:03.20,0:06:16.76,Default,,0000,0000,0000,,na kuanguka ndani zaidi katika mtandao huo tatanishi wa hatia, lawama na uduni? Dialogue: 0,0:06:16.76,0:06:24.04,Default,,0000,0000,0000,,Je, unarudi kwenye mstari au unaenda nje zaidi? Dialogue: 0,0:06:24.04,0:06:28.16,Default,,0000,0000,0000,,Chaguo ni lako. Dialogue: 0,0:06:28.16,0:06:39.76,Default,,0000,0000,0000,,Kuchagua kuishi katika maisha yako ya zamani ni kuchagua kwenda zaidi nje ya njia. Dialogue: 0,0:06:39.76,0:06:45.08,Default,,0000,0000,0000,,Kuanguka katika hatia na hukumu hiyo - unaenda nje zaidi. Dialogue: 0,0:06:45.08,0:06:47.88,Default,,0000,0000,0000,,Vivyo hivyo, ikiwa unahalalisha kosa lako Dialogue: 0,0:06:47.88,0:06:50.56,Default,,0000,0000,0000,,au unanyosha vidole kushoto, kulia na katikati Dialogue: 0,0:06:50.56,0:06:57.04,Default,,0000,0000,0000,,au kutoa visingizio, natoka nje ya njia ya mstari. Dialogue: 0,0:06:57.04,0:07:01.68,Default,,0000,0000,0000,,Na jambo la hatari hapa ni kwamba Dialogue: 0,0:07:01.68,0:07:09.56,Default,,0000,0000,0000,,kadiri unavyoongeza kukaa kwako katika makosa, Dialogue: 0,0:07:09.56,0:07:18.84,Default,,0000,0000,0000,,ndivyo uharibifu zaidi shetani anavyoweza kuuletea moyoni mwako. Dialogue: 0,0:07:18.84,0:07:27.20,Default,,0000,0000,0000,,Na shetani anapokuwa na nafasi ndani ya moyo wako. Dialogue: 0,0:07:27.20,0:07:32.64,Default,,0000,0000,0000,,uharibifu huo unaweza kuenea kwa urahisi kwenye nyumba yako, Dialogue: 0,0:07:32.64,0:07:38.52,Default,,0000,0000,0000,,ndoa, familia, mahusiano na kazi yako. Dialogue: 0,0:07:38.52,0:07:44.96,Default,,0000,0000,0000,,Tunasuka mtandao ulioingiliana Dialogue: 0,0:07:44.96,0:07:52.00,Default,,0000,0000,0000,,wakati makosa yetu, tunakataa kuondoka. Dialogue: 0,0:07:52.00,0:07:54.88,Default,,0000,0000,0000,,Sisemi kwamba hutafanya makosa. Dialogue: 0,0:07:54.88,0:07:58.00,Default,,0000,0000,0000,,Kila mtu hufanya makosa katika safari hii. Dialogue: 0,0:07:58.00,0:08:00.48,Default,,0000,0000,0000,,Kila mtu hukosa alama. Dialogue: 0,0:08:00.48,0:08:05.28,Default,,0000,0000,0000,,Ninamaanisha, angalia tu Biblia, mwongozo wetu, Neno la Mungu - Dialogue: 0,0:08:05.28,0:08:10.44,Default,,0000,0000,0000,,wahusika wengi wakuu wa Biblia tunaowasoma. Dialogue: 0,0:08:10.44,0:08:14.20,Default,,0000,0000,0000,,Nuhu alipambana na pombe. Dialogue: 0,0:08:14.20,0:08:16.32,Default,,0000,0000,0000,,Yakobo alitumia udanganyifu. Dialogue: 0,0:08:16.32,0:08:19.60,Default,,0000,0000,0000,,Lutu alipambana na uchu. Dialogue: 0,0:08:19.60,0:08:25.08,Default,,0000,0000,0000,,Vipi kuhusu Musa ambaye alipambana na hasira. Dialogue: 0,0:08:25.08,0:08:31.08,Default,,0000,0000,0000,,Petro mara nyingi aliingiwa na woga, Tomaso na mashaka. Dialogue: 0,0:08:31.08,0:08:36.56,Default,,0000,0000,0000,,Vipi kuhusu Mfalme Daudi, Sulemani, Samsoni - wote walishindwa na tamaa. Dialogue: 0,0:08:36.56,0:08:44.00,Default,,0000,0000,0000,,Hakuna mkamilifu katika ulimwengu huu (Warumi 3:10, 23) Dialogue: 0,0:08:44.00,0:08:51.84,Default,,0000,0000,0000,,Sisi sote hujikwaa kwa njia nyingi (Yakobo 3:2) Dialogue: 0,0:08:51.84,0:08:58.60,Default,,0000,0000,0000,,Katika ulimwengu huu mwovu, kutakuwa na mzozo huo daima, Dialogue: 0,0:08:58.60,0:09:04.32,Default,,0000,0000,0000,,ile vita ndani ya moyo wa mwanadamu kati ya mwili na roho. Dialogue: 0,0:09:04.32,0:09:11.64,Default,,0000,0000,0000,,Wazo lililo moyoni mwako ni vita utakayokabiliana nayo hadi siku ya mwisho, Dialogue: 0,0:09:11.64,0:09:15.88,Default,,0000,0000,0000,,mpaka Yesu atakapokuja - ndivyo vita utakavyokabiliana nayo. Dialogue: 0,0:09:15.88,0:09:22.32,Default,,0000,0000,0000,,Kwa hiyo, faraja yangu kwenu leo, watu wa Mungu, ni hii: Dialogue: 0,0:09:22.32,0:09:30.28,Default,,0000,0000,0000,,Mara tu unapogundua kuwa umechukua hatua mbaya, Dialogue: 0,0:09:30.28,0:09:36.04,Default,,0000,0000,0000,,rudi haraka kwenye mstari. Dialogue: 0,0:09:36.04,0:09:45.68,Default,,0000,0000,0000,,Usiongeze muda wa kukaa kwako katika makosa kwa kujitetea kwenye hilo. Dialogue: 0,0:09:45.68,0:09:54.48,Default,,0000,0000,0000,,Angalia, kama mtoto wa Mungu, unaweza kujua unapochukua hatua mbaya. Dialogue: 0,0:09:54.48,0:10:02.92,Default,,0000,0000,0000,,Vipi? Roho wa Mungu atachochea dhamiri yako kutubu. Dialogue: 0,0:10:02.92,0:10:07.88,Default,,0000,0000,0000,,Warumi 9:1, 2 Wakorintho 7:10 Dialogue: 0,0:10:07.88,0:10:14.04,Default,,0000,0000,0000,,Roho Mtakatifu ataisukuma dhamiri yako kutubu. Dialogue: 0,0:10:14.04,0:10:25.28,Default,,0000,0000,0000,,Swali ni - roho yako ni sikivu kiasi gani? Dialogue: 0,0:10:25.28,0:10:32.76,Default,,0000,0000,0000,,una haraka kiasi gani kujitetea? Dialogue: 0,0:10:32.76,0:10:42.96,Default,,0000,0000,0000,,Kasi ambayo unatambua kosa lako ni sawia Dialogue: 0,0:10:42.96,0:10:52.68,Default,,0000,0000,0000,,na kiwango ambacho Neno la Mungu linatawala moyo wako. Dialogue: 0,0:10:52.68,0:11:03.96,Default,,0000,0000,0000,,Na kuwa mwangalifu zaidi kwa msukumo wa Roho wa Mungu katika roho yako, Dialogue: 0,0:11:03.96,0:11:09.96,Default,,0000,0000,0000,,inakupasa kutumia muda mwingi zaidi miguuni pake, Dialogue: 0,0:11:09.96,0:11:13.32,Default,,0000,0000,0000,,muda mwingi mbele zake, Dialogue: 0,0:11:13.32,0:11:16.16,Default,,0000,0000,0000,,muda zaidi katika Neno Lake. Dialogue: 0,0:11:16.16,0:11:22.24,Default,,0000,0000,0000,,Lazima aongezeke; lazima upungue (Yohana 3:30). Dialogue: 0,0:11:22.24,0:11:26.40,Default,,0000,0000,0000,,Kwa sababu yote yanamhusu Yesu; haikuhusu wewe. Dialogue: 0,0:11:26.40,0:11:31.96,Default,,0000,0000,0000,,Sio juu ya kustahili kwako kwa sababu hakuna mtu anayestahili. Dialogue: 0,0:11:31.96,0:11:39.16,Default,,0000,0000,0000,,Sio juu ya udhaifu wako kwa sababu kila mtu ana udhaifu. Dialogue: 0,0:11:39.16,0:11:45.20,Default,,0000,0000,0000,,Yote ni juu ya utayari wako - Dialogue: 0,0:11:45.20,0:11:49.28,Default,,0000,0000,0000,,utayari wako wa kukiri kosa lako, Dialogue: 0,0:11:49.28,0:11:53.16,Default,,0000,0000,0000,,kuweka kiburi chako kando, Dialogue: 0,0:11:53.16,0:11:59.04,Default,,0000,0000,0000,,rudia hatua zako, rudi kwenye mstari na Mungu Dialogue: 0,0:11:59.04,0:12:03.44,Default,,0000,0000,0000,,na endelea na safari yako ya imani. Dialogue: 0,0:12:03.44,0:12:10.52,Default,,0000,0000,0000,,Kwa sababu si lazima uwe mkamilifu ili uwe mtoto wa Mungu; Dialogue: 0,0:12:10.52,0:12:14.76,Default,,0000,0000,0000,,unatakiwa tu uwepo. Dialogue: 0,0:12:14.76,0:12:18.72,Default,,0000,0000,0000,,Watu wa Mungu, nitawaacha leo na neno la Maandiko Dialogue: 0,0:12:18.72,0:12:22.96,Default,,0000,0000,0000,,kutoka kwa Mtume Paulo katika Warumi 8:1. Dialogue: 0,0:12:22.96,0:12:35.48,Default,,0000,0000,0000,,Akasema, Sasa basi, hakuna hukumu ya adhabu Dialogue: 0,0:12:35.48,0:12:39.00,Default,,0000,0000,0000,,kwa wale walio katika Kristo Yesu." Dialogue: 0,0:12:39.00,0:12:44.76,Default,,0000,0000,0000,,Sasa, Maandiko haya hayatupi msingi wa kuhurumia dhambi, Dialogue: 0,0:12:44.76,0:12:50.36,Default,,0000,0000,0000,,kuhalalisha makosa au kuchukua neema kirahisi. Hapana! Dialogue: 0,0:12:50.36,0:13:00.96,Default,,0000,0000,0000,,Lakini inasisitiza tu kwamba hatupaswi kuruhusu hatia ya makosa yetu Dialogue: 0,0:13:00.96,0:13:10.48,Default,,0000,0000,0000,,kutunyang'anya amani ya pekee inayopatikana katika msamaha wa Kristo. Dialogue: 0,0:13:10.48,0:13:15.68,Default,,0000,0000,0000,,Badala ya kosa lako kukutoa mbele za Mungu, Dialogue: 0,0:13:15.68,0:13:23.80,Default,,0000,0000,0000,,inapaswa kuwa sababu ya wewe kumkaribia Yeye zaidi. Dialogue: 0,0:13:23.80,0:13:27.52,Default,,0000,0000,0000,,Kwa sababu katika maneno ya Nabii T.B. Joshua: Dialogue: 0,0:13:27.52,0:13:38.64,Default,,0000,0000,0000,,"Unaweza kujua wewe ni mtoto wa Mungu wakati makosa yako yanapochochea maisha yako ya kiroho." Dialogue: 0,0:13:38.64,0:13:40.56,Default,,0000,0000,0000,,Asante, Yesu Kristo. Dialogue: 0,0:13:40.56,0:13:44.72,Default,,0000,0000,0000,,Sasa hivi, watu wa Mungu, ni wakati wa maombi. Dialogue: 0,0:13:51.16,0:13:59.76,Default,,0000,0000,0000,,Hivi sasa, kwa kila moyo uliochafuliwa na hatia - Dialogue: 0,0:13:59.76,0:14:05.60,Default,,0000,0000,0000,,takaswa, katika jina kuu la Yesu Kristo! Dialogue: 0,0:14:05.60,0:14:10.88,Default,,0000,0000,0000,,kwa kila roho inayosumbuliwa na hukumu, Dialogue: 0,0:14:10.88,0:14:18.96,Default,,0000,0000,0000,,takaswa kwa Damu ya thamani ya Yesu Kristo! Dialogue: 0,0:14:18.96,0:14:26.68,Default,,0000,0000,0000,,Damu ya Yesu Kristo inapokusafisha, umetakaswa kwelikweli! Dialogue: 0,0:14:26.68,0:14:29.12,Default,,0000,0000,0000,,Takaswa sasa hivi! Dialogue: 0,0:14:29.12,0:14:38.00,Default,,0000,0000,0000,,Katika roho yako, katika nafsi yako, katika mwili wako - takaswa! Dialogue: 0,0:14:38.00,0:14:48.64,Default,,0000,0000,0000,,Kila roho ya dhiki, utumwa, udhaifu, ndoto mbaya - Dialogue: 0,0:14:48.64,0:14:53.16,Default,,0000,0000,0000,,uoshwe kwa Damu ya Yesu Kristo! Dialogue: 0,0:14:53.16,0:15:03.64,Default,,0000,0000,0000,,Uoshwe sasa hivi, katika jina kuu la Yesu Kristo! Dialogue: 0,0:15:03.64,0:15:07.16,Default,,0000,0000,0000,,Pokea ujasiri! Dialogue: 0,0:15:07.16,0:15:10.08,Default,,0000,0000,0000,,Pokea nguvu! Dialogue: 0,0:15:10.08,0:15:20.16,Default,,0000,0000,0000,,Pokea usadikisho wa kushikilia msimamo wako katika Kristo! Dialogue: 0,0:15:20.16,0:15:27.04,Default,,0000,0000,0000,,Ee Bwana, rekebisha kila moyo mkaidi na utashi. Dialogue: 0,0:15:27.04,0:15:30.68,Default,,0000,0000,0000,,Ongoza hatua zinazoenda kombo. Dialogue: 0,0:15:30.68,0:15:35.52,Default,,0000,0000,0000,,Osha madoa ya hatia. Dialogue: 0,0:15:35.52,0:15:41.32,Default,,0000,0000,0000,,Tusaidie kuona kupitia macho yako. Dialogue: 0,0:15:41.32,0:15:48.72,Default,,0000,0000,0000,,Tuvute kwenye uhusiano wa karibu na Wewe Dialogue: 0,0:15:48.72,0:15:56.56,Default,,0000,0000,0000,,na utujalie ufahamu mkubwa zaidi wa moyo Wako. Dialogue: 0,0:15:56.56,0:16:06.00,Default,,0000,0000,0000,,Katika jina kuu la Yesu Kristo! Amina! Dialogue: 0,0:16:06.00,0:16:08.28,Default,,0000,0000,0000,,Asante, Yesu Kristo.