1 00:00:09,280 --> 00:00:12,960 Neema na amani iwe kwenu nyote katika jina kuu la Yesu 2 00:00:12,960 --> 00:00:20,120 na karibu katika toleo jingine la 'Imani Ni Asili' hapa kwenye TV ya Moyo wa Mungu. 3 00:00:20,120 --> 00:00:26,000 Leo, nataka kuzungumzia suala ambalo limejitokeza mara nyingi sana 4 00:00:26,000 --> 00:00:33,960 katika mazungumzo na watu - katika nyakati za maombi, ushauri na kutia moyo. 5 00:00:33,960 --> 00:00:40,280 Nimeona tu kwamba watu wengi sana leo 6 00:00:40,280 --> 00:00:47,080 wanaishi maisha yao kupitia lenzi hii ya jana, 7 00:00:47,080 --> 00:00:49,040 kupitia lenzi ya walivyokuwa - 8 00:00:49,040 --> 00:00:56,320 mabaya yao ya zamani, makosa, maumivu na uchungu. 9 00:00:56,320 --> 00:01:02,160 Na kama matokeo ya hili, wengi hujikuta wamenaswa 10 00:01:02,160 --> 00:01:12,880 katika mzunguko huu mbaya wa hatia na hukumu kwa makosa waliyofanya 11 00:01:12,880 --> 00:01:18,320 au vilevile mzunguko mbaya wa uchungu na chuki 12 00:01:18,320 --> 00:01:23,280 juu ya mabaya waliyofanyiwa huko nyuma. 13 00:01:23,280 --> 00:01:27,240 Na ni hatari sana. 14 00:01:27,240 --> 00:01:35,840 Watu wa Mungu, hii si chochote ila ni njama ya hila, hila ya kawaida ya shetani 15 00:01:35,840 --> 00:01:40,880 ili kukutenganisha na Mungu. 16 00:01:40,880 --> 00:01:45,520 Shetani anafurahia kujadili mambo yako ya nyuma na wewe. 17 00:01:45,520 --> 00:01:52,840 Anafurahi kukukumbusha juu ya kutofaulu kwako zamani, makosa ya zamani, maumivu ya zamani. 18 00:01:52,840 --> 00:01:57,800 Kwa sababu hicho ndicho kitu pekee kinachokuunganisha naye. 19 00:01:57,800 --> 00:02:04,720 Hiyo ndiyo habari pekee ambayo anayo kuhusu wewe - siku zako za nyuma. 20 00:02:04,720 --> 00:02:11,040 Na shetani atachukua kila njia inayopatikana 21 00:02:11,040 --> 00:02:19,320 kujaribu na kukuzuia usitende Neno la Mungu sasa. 22 00:02:19,320 --> 00:02:24,640 Angalia, hajali ikiwa utalichambua tu Neno. 23 00:02:24,640 --> 00:02:30,640 Haijalishi kama unastaajabia Neno au hata kukubali ukweli wa Neno 24 00:02:30,640 --> 00:02:35,960 mradi hutendi Neno hilo. 25 00:02:35,960 --> 00:02:39,480 Hataki utende neno la Mungu! 26 00:02:39,480 --> 00:02:48,840 Anataka uishi maisha yako kupitia lenzi ya maisha yako ya zamani yasiyofaa, 27 00:02:48,840 --> 00:02:53,040 kwa wewe kuchuja kila kitu kupitia hiyo, 28 00:02:53,040 --> 00:03:00,960 ili kulemaza uwezo wako wa kutenda imani muda huu 29 00:03:00,960 --> 00:03:07,200 na hivyo kuharibu maisha yako ya baadaye. 30 00:03:07,200 --> 00:03:20,120 Watu wa Mungu, ni hatari kuchukua safari zisizo za lazima hadi jana. 31 00:03:20,120 --> 00:03:23,840 Ni hatari sana. 32 00:03:23,840 --> 00:03:30,920 Angalia, siku zako za nyuma haziamui sasa yako 33 00:03:30,920 --> 00:03:36,040 na haiamui mustakabali wako. 34 00:03:36,040 --> 00:03:41,440 Unaweza kujifunza kutoka kwenye maisha yako ya zamani bila kuishi katika maisha yako ya zamani. 35 00:03:41,440 --> 00:03:45,440 Usiishi ndani yake; jifunze kutoka kwake. 36 00:03:45,440 --> 00:03:54,680 Usiheshimu udanganyifu wa shetani kwa umakini wako - umakini wako wa thamani. 37 00:03:54,680 --> 00:04:00,400 Kwa sababu makosa yako hayakufafanui wewe. 38 00:04:00,400 --> 00:04:03,680 Zaburi 37:24 39 00:04:03,680 --> 00:04:08,920 Narudia - makosa yako hayakufafanui. 40 00:04:08,920 --> 00:04:13,080 Kwa kweli, yanaweza hata kukuboresha. 41 00:04:13,080 --> 00:04:21,960 Namaanisha, Mungu anaweza hata kutumia makosa yako kukupeleka mahali 42 00:04:21,960 --> 00:04:32,640 anapotaka uwe - kulingana na mwitikio wako. 43 00:04:32,640 --> 00:04:35,320 Jambo kuu liko kwenye mwitikio wako. 44 00:04:35,320 --> 00:04:37,920 Je, unaitikiaje kwenye kosa hilo? 45 00:04:37,920 --> 00:04:41,480 Sasa, ngoja nikupe mfano halisi sana. 46 00:04:41,480 --> 00:04:44,240 Hebu wazia uko safarini mahali fulani. 47 00:04:44,240 --> 00:04:46,240 Unaenda mahali fulani; unajua unakokwenda. 48 00:04:46,240 --> 00:04:51,160 Na katika safari hii, ghafla unatambua kuwa uko mahali pasipofaa. 49 00:04:51,160 --> 00:04:54,160 Umechukua hatua mbaya; umekosa mwelekeo. 50 00:04:54,160 --> 00:04:56,120 Unafanya nini? 51 00:04:56,120 --> 00:05:03,000 Unahitaji kurejesha hatua zako na kurudi kwenye mstari. 52 00:05:03,000 --> 00:05:06,880 Ikiwa unatambua kuwa umeenda katika mwelekeo mbaya, je, unasema tu, 53 00:05:06,880 --> 00:05:11,120 'Oh sawa, nimechelewa mno! Acha niendelee tu katika njia hii mbaya.' 54 00:05:11,120 --> 00:05:23,680 Hapana! Unarudi haraka kwenye njia sahihi, rudi kwenye mstari na uendelee na safari yako. 55 00:05:23,680 --> 00:05:32,320 Watu wa Mungu, katika safari hii ya maisha, 56 00:05:32,320 --> 00:05:39,320 ukichukua hatua mbaya, unajibuje? 57 00:05:39,320 --> 00:05:42,480 Je, unaitikiaje? 58 00:05:42,480 --> 00:05:52,920 Je, unatambua kosa lako, rudia hatua zako na kumkimbilia Mungu kwa toba? 59 00:05:52,920 --> 00:05:59,680 Au unapinga kujichunguza, 60 00:05:59,680 --> 00:06:03,200 galagala kwa kujihurumia 61 00:06:03,200 --> 00:06:16,760 na kuanguka ndani zaidi katika mtandao huo tatanishi wa hatia, lawama na uduni? 62 00:06:16,760 --> 00:06:24,040 Je, unarudi kwenye mstari au unaenda nje zaidi? 63 00:06:24,040 --> 00:06:28,160 Chaguo ni lako. 64 00:06:28,160 --> 00:06:39,760 Kuchagua kuishi katika maisha yako ya zamani ni kuchagua kwenda zaidi nje ya njia. 65 00:06:39,760 --> 00:06:45,080 Kuanguka katika hatia na hukumu hiyo - unaenda nje zaidi. 66 00:06:45,080 --> 00:06:47,880 Vivyo hivyo, ikiwa unahalalisha kosa lako 67 00:06:47,880 --> 00:06:50,560 au unanyosha vidole kushoto, kulia na katikati 68 00:06:50,560 --> 00:06:57,040 au kutoa visingizio, natoka nje ya njia ya mstari. 69 00:06:57,040 --> 00:07:01,680 Na jambo la hatari hapa ni kwamba 70 00:07:01,680 --> 00:07:09,560 kadiri unavyoongeza kukaa kwako katika makosa, 71 00:07:09,560 --> 00:07:18,840 ndivyo uharibifu zaidi shetani anavyoweza kuuletea moyoni mwako. 72 00:07:18,840 --> 00:07:27,200 Na shetani anapokuwa na nafasi ndani ya moyo wako. 73 00:07:27,200 --> 00:07:32,640 uharibifu huo unaweza kuenea kwa urahisi kwenye nyumba yako, 74 00:07:32,640 --> 00:07:38,520 ndoa, familia, mahusiano na kazi yako. 75 00:07:38,520 --> 00:07:44,960 Tunasuka mtandao ulioingiliana 76 00:07:44,960 --> 00:07:52,000 wakati makosa yetu, tunakataa kuondoka. 77 00:07:52,000 --> 00:07:54,880 Sisemi kwamba hutafanya makosa. 78 00:07:54,880 --> 00:07:58,000 Kila mtu hufanya makosa katika safari hii. 79 00:07:58,000 --> 00:08:00,480 Kila mtu hukosa alama. 80 00:08:00,480 --> 00:08:05,280 Ninamaanisha, angalia tu Biblia, mwongozo wetu, Neno la Mungu - 81 00:08:05,280 --> 00:08:10,440 wahusika wengi wakuu wa Biblia tunaowasoma. 82 00:08:10,440 --> 00:08:14,200 Nuhu alipambana na pombe. 83 00:08:14,200 --> 00:08:16,320 Yakobo alitumia udanganyifu. 84 00:08:16,320 --> 00:08:19,600 Lutu alipambana na uchu. 85 00:08:19,600 --> 00:08:25,080 Vipi kuhusu Musa ambaye alipambana na hasira. 86 00:08:25,080 --> 00:08:31,080 Petro mara nyingi aliingiwa na woga, Tomaso na mashaka. 87 00:08:31,080 --> 00:08:36,560 Vipi kuhusu Mfalme Daudi, Sulemani, Samsoni - wote walishindwa na tamaa. 88 00:08:36,560 --> 00:08:44,000 Hakuna mkamilifu katika ulimwengu huu (Warumi 3:10, 23) 89 00:08:44,000 --> 00:08:51,840 Sisi sote hujikwaa kwa njia nyingi (Yakobo 3:2) 90 00:08:51,840 --> 00:08:58,600 Katika ulimwengu huu mwovu, kutakuwa na mzozo huo daima, 91 00:08:58,600 --> 00:09:04,320 ile vita ndani ya moyo wa mwanadamu kati ya mwili na roho. 92 00:09:04,320 --> 00:09:11,640 Wazo lililo moyoni mwako ni vita utakayokabiliana nayo hadi siku ya mwisho, 93 00:09:11,640 --> 00:09:15,880 mpaka Yesu atakapokuja - ndivyo vita utakavyokabiliana nayo. 94 00:09:15,880 --> 00:09:22,320 Kwa hiyo, faraja yangu kwenu leo, watu wa Mungu, ni hii: 95 00:09:22,320 --> 00:09:30,280 Mara tu unapogundua kuwa umechukua hatua mbaya, 96 00:09:30,280 --> 00:09:36,040 rudi haraka kwenye mstari. 97 00:09:36,040 --> 00:09:45,680 Usiongeze muda wa kukaa kwako katika makosa kwa kujitetea kwenye hilo. 98 00:09:45,680 --> 00:09:54,480 Angalia, kama mtoto wa Mungu, unaweza kujua unapochukua hatua mbaya. 99 00:09:54,480 --> 00:10:02,920 Vipi? Roho wa Mungu atachochea dhamiri yako kutubu. 100 00:10:02,920 --> 00:10:07,880 Warumi 9:1, 2 Wakorintho 7:10 101 00:10:07,880 --> 00:10:14,040 Roho Mtakatifu ataisukuma dhamiri yako kutubu. 102 00:10:14,040 --> 00:10:25,280 Swali ni - roho yako ni sikivu kiasi gani? 103 00:10:25,280 --> 00:10:32,760 una haraka kiasi gani kujitetea? 104 00:10:32,760 --> 00:10:42,960 Kasi ambayo unatambua kosa lako ni sawia 105 00:10:42,960 --> 00:10:52,680 na kiwango ambacho Neno la Mungu linatawala moyo wako. 106 00:10:52,680 --> 00:11:03,960 Na kuwa mwangalifu zaidi kwa msukumo wa Roho wa Mungu katika roho yako, 107 00:11:03,960 --> 00:11:09,960 inakupasa kutumia muda mwingi zaidi miguuni pake, 108 00:11:09,960 --> 00:11:13,320 muda mwingi mbele zake, 109 00:11:13,320 --> 00:11:16,160 muda zaidi katika Neno Lake. 110 00:11:16,160 --> 00:11:22,240 Lazima aongezeke; lazima upungue (Yohana 3:30). 111 00:11:22,240 --> 00:11:26,400 Kwa sababu yote yanamhusu Yesu; haikuhusu wewe. 112 00:11:26,400 --> 00:11:31,960 Sio juu ya kustahili kwako kwa sababu hakuna mtu anayestahili. 113 00:11:31,960 --> 00:11:39,160 Sio juu ya udhaifu wako kwa sababu kila mtu ana udhaifu. 114 00:11:39,160 --> 00:11:45,200 Yote ni juu ya utayari wako - 115 00:11:45,200 --> 00:11:49,280 utayari wako wa kukiri kosa lako, 116 00:11:49,280 --> 00:11:53,160 kuweka kiburi chako kando, 117 00:11:53,160 --> 00:11:59,040 rudia hatua zako, rudi kwenye mstari na Mungu 118 00:11:59,040 --> 00:12:03,440 na endelea na safari yako ya imani. 119 00:12:03,440 --> 00:12:10,520 Kwa sababu si lazima uwe mkamilifu ili uwe mtoto wa Mungu; 120 00:12:10,520 --> 00:12:14,760 unatakiwa tu uwepo. 121 00:12:14,760 --> 00:12:18,720 Watu wa Mungu, nitawaacha leo na neno la Maandiko 122 00:12:18,720 --> 00:12:22,960 kutoka kwa Mtume Paulo katika Warumi 8:1. 123 00:12:22,960 --> 00:12:35,480 Akasema, Sasa basi, hakuna hukumu ya adhabu 124 00:12:35,480 --> 00:12:39,000 kwa wale walio katika Kristo Yesu." 125 00:12:39,000 --> 00:12:44,760 Sasa, Maandiko haya hayatupi msingi wa kuhurumia dhambi, 126 00:12:44,760 --> 00:12:50,360 kuhalalisha makosa au kuchukua neema kirahisi. Hapana! 127 00:12:50,360 --> 00:13:00,960 Lakini inasisitiza tu kwamba hatupaswi kuruhusu hatia ya makosa yetu 128 00:13:00,960 --> 00:13:10,480 kutunyang'anya amani ya pekee inayopatikana katika msamaha wa Kristo. 129 00:13:10,480 --> 00:13:15,680 Badala ya kosa lako kukutoa mbele za Mungu, 130 00:13:15,680 --> 00:13:23,800 inapaswa kuwa sababu ya wewe kumkaribia Yeye zaidi. 131 00:13:23,800 --> 00:13:27,520 Kwa sababu katika maneno ya Nabii T.B. Joshua: 132 00:13:27,520 --> 00:13:38,640 "Unaweza kujua wewe ni mtoto wa Mungu wakati makosa yako yanapochochea maisha yako ya kiroho." 133 00:13:38,640 --> 00:13:40,560 Asante, Yesu Kristo. 134 00:13:40,560 --> 00:13:44,720 Sasa hivi, watu wa Mungu, ni wakati wa maombi. 135 00:13:51,160 --> 00:13:59,760 Hivi sasa, kwa kila moyo uliochafuliwa na hatia - 136 00:13:59,760 --> 00:14:05,600 takaswa, katika jina kuu la Yesu Kristo! 137 00:14:05,600 --> 00:14:10,880 kwa kila roho inayosumbuliwa na hukumu, 138 00:14:10,880 --> 00:14:18,960 takaswa kwa Damu ya thamani ya Yesu Kristo! 139 00:14:18,960 --> 00:14:26,680 Damu ya Yesu Kristo inapokusafisha, umetakaswa kwelikweli! 140 00:14:26,680 --> 00:14:29,120 Takaswa sasa hivi! 141 00:14:29,120 --> 00:14:38,000 Katika roho yako, katika nafsi yako, katika mwili wako - takaswa! 142 00:14:38,000 --> 00:14:48,640 Kila roho ya dhiki, utumwa, udhaifu, ndoto mbaya - 143 00:14:48,640 --> 00:14:53,160 uoshwe kwa Damu ya Yesu Kristo! 144 00:14:53,160 --> 00:15:03,640 Uoshwe sasa hivi, katika jina kuu la Yesu Kristo! 145 00:15:03,640 --> 00:15:07,160 Pokea ujasiri! 146 00:15:07,160 --> 00:15:10,080 Pokea nguvu! 147 00:15:10,080 --> 00:15:20,160 Pokea usadikisho wa kushikilia msimamo wako katika Kristo! 148 00:15:20,160 --> 00:15:27,040 Ee Bwana, rekebisha kila moyo mkaidi na utashi. 149 00:15:27,040 --> 00:15:30,680 Ongoza hatua zinazoenda kombo. 150 00:15:30,680 --> 00:15:35,520 Osha madoa ya hatia. 151 00:15:35,520 --> 00:15:41,320 Tusaidie kuona kupitia macho yako. 152 00:15:41,320 --> 00:15:48,720 Tuvute kwenye uhusiano wa karibu na Wewe 153 00:15:48,720 --> 00:15:56,560 na utujalie ufahamu mkubwa zaidi wa moyo Wako. 154 00:15:56,560 --> 00:16:06,000 Katika jina kuu la Yesu Kristo! Amina! 155 00:16:06,000 --> 00:16:08,280 Asante, Yesu Kristo.