[Mnamo Januari ya mwaka 2020,
Christian Happi na Pardis Sabeti waliwasilisha wazo lenye uthubutu]
[Sentinel: Mfumo wa ilani ya mapema katika kutambua na kufuatilia mlipuko wa gonjwa lijalo]
[Hivi ni namna utavyofanya kazi ...]
Christian Happi: Kiashiria ni mfumo wa ilani ya mapema iliyo amilifu katika kukinzana na magonjwa yanayoenea sana.
Inajengwa na misingi mikuu mitatu.
Pardis Sabeti: Msingi wa kwanza ni Utambuzi.
Mimi na Christian tumekuwa tukitafiti pamoja magonjwa ya kuambukizwa
duniani kote kwa miongo miwili.
Tumekuwa tukitumia mfululizo wa jenomu.
Tukizisoma taarifa timilifu za vinasaba vya vijidudu,
inatusaidia kutambua virusi, hata vile ambavyo hatujawahi kuviona kabla,
kuvifuatilia pale vinaposambaa
na kuangazia mabadiliko yake mapya.
Na sasa tukiwa na teknolojia yenye uwezo mkubwa wa kuziboresha chembe za urithi(jeni) iitwayo CRISPR,
tunaweza kutumia taarifa hizi za kinasaba
kutengeneza vipimo vya utambuzi vilivyo sahihi kwa vijidudu aina zote.
CH: Moja ya nyenzo hizi zinafahamika kama SHERLOCK.
Inaweza kutumika kutambua virusi vinavyotambulika katika vijikaratasi.
Ni nafuu mno,
na wafanyakazi wa afya walio mstari wa mbele wanaweza tumia SHERLOCK
Kutambua virusi vinavyojulikana au vile ambavyo ni tishio
ndani ya saa moja.
PS: Nyenzo nyingine ni CARMEN.
Inahitaji maabara, lakini inaweza kupima mamia ya virusi kwa wakati mmoja.
Hivyo wafanyakazi wa maabara wanaweza pima sampuli za wagonjwa
kutambua aina nyingi za virusi
ndani ya siku moja.
Msingi wetu wa pili ni Ungana.
Kumuunganisha kila mmoja na kushirikishana taarifa
kote katika jamii ya afya ya umma.
Katika magonjwa mengi ya mlipuko,
wafanyakazi wa hospitali hushirikishana taarifa kupitia nyaraka za karatasi.
Hii hufanya ufatiliaji wa taarifa katika nafasi na nyakati
na upatikanaji wa huduma
kuwa mgumu sana.
Hivyo tunatengeneza mfumo wa kimtandao na programu za simu
ambazo zinawaunganisha wafanyakazi wa afya,
waliopo zahanati, timu za afya umma -- kila mmoja --
na kuwawezesha kuingiza taarifa,
kufanya tathmini, kushirikishana vidokezo
na kutengeneza mpango wa kuweza kuchukua hatua
katika wakati sahihi.
CH: Msingi wetu wa tatu ni Uwezeshaji.
Mfumo wa uangalizi wa magonjwa ya mlipuko unaweza fanikiwa
kama tutawawezesha wafanyakazi wa afya walio mstari wa mbele
kuhudumia jamii.
Inahitaji mafunzo mengi sana.
Mimi na Pardis tunalitambua hilo.
Tumetumia miaka kumi
tukiwafunza mamia ya wanasayansi wadogo na wafanyakazi wa zanahati barani Afrika.
Katika miaka mitano ijayo, tutaweza kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya wengine takribani 1,000
katika kutumia mfumo wa Kiashiria
na kuwawezesha pia kufundisha wafanyakazi wenzao.
Namna hii, tutaweza kuboresha mfumo halisi wa afya
na kuweza tumia uangalizi wa kina katika masuala ya kitabibu.
[Tangu kuwakilisha mpango wao wa Uthubutu katika TED, ulimwengu umebadilika ...]
Briar Goldberg: Tupo hapa, tunarekodi hili tukio.
Ni tarehe 7 mwezi Aprili, 2020,
na kwa uhakika, tupo katika tabu ya hili gonjwa ambalo ni janga la ulimwengu
linalosababishwa na virusi vipya vya corona.
Nyinyi wawili mmekuwa mkifanya kazi pamoja siku zote,
na mlikuwa pamoja kwa juhudi
katika janga la Ebola mwaka 2014.
Mnalitazamaje hili jambo?
CH: Miaka sita baada ya mlipuko wa Ebola,
tumekumbana na janga lingine,
na tupo katika wakati, ambao kwamba, hatujajifunza mengi kuhusu janga lililopita.
Na hivyo, kiukweli, kwangu mimi, inanivunja moyo.
PS: Ninadhani janga hili limetuonyesha ni namna gani hatukujiandaa
duniani kote.
Christian na washirika wetu pamoja tulikuwa na vikagua magonjwa katika hospitali zetu
nchini Nigeria, Sierra Leone na Senegal mapema mwezi Februari.
Majimbo mengi nchini Marekani hayakuwa navyo mpaka baadaye.
Inatueleza kwamba wote tupo pamoja katika hili,
na wote tupo nyuma .
BG: Hivyo, huu mfumo wa Kiashiria ni mzuri,
lakini nafahamu swali ambalo lipo akilini mwa kila mtu:
Namna gani huu mfumo unasaidia sasa hivi?
PS: Unajua, tumeelezea Kiashiria kama mfumo wa kuondokana na magonjwa yanayoenea sana,
na hapa tupo katika moja ya magonjwa hayo.
Lakini kilicho kikubwa ni kwamba, nyenzo zilezile unazohitaji
kuondokana na gonjwa linaloenea
ni zilezile unazohitaji kuondokana nalo.
Na hivyo teknolojia ambazo tumeziainisha --
Vipimo vyote vya awali vya uchaguzi,
utambuzi na ufatiliaji wa virusi vinavyobadilika,
na utumiaji wa programu za simu --
ni muhimu mno.
CH: Kwetu sisi, ni vita.
Kimsingi tumejidhatiti katika ratiba ya masaa 24
ili kuweza kutoa majibu,
na inatuhitaji sisi kufanya kazi bila kupoteza muda.
Hivyo ni nyakati yenye changamoto sana.
Tupo mbali na familia.
Angalau nina wasaha wa kuiona familia yangu leo,
na kisha nina uhakika kesho ninarudi tena kwenye kazi.
Katika maabara yangu, tumetengeneza mfululizo wa kwanza wa jenomu ya COVID-19
katika bara la Afrika,
na hilo lilifanyika ndani ya masaaa 48.
Haya ni mapinduzi yanayotokea Afrika
na kisha kufanya taarifa hizi kupatikana katika jamii ya masuala ya afya ulimwenguni
ili kuona virusi vya Afrika vinaonekana katika namna gani.
Ninaamini kwa kutumia teknolojia na maarifa
na kisha kushirikisha taarifa,
tunaweza fanya vizuri na kuweza kulishinda gonjwa.
PS: Wazo zima la Sentinel
ni katika kusimama wote kwa pamoja kulindana.
Wote tunatazama.
Kila mmoja wetu ni mlinzi.
Kila mmoja wetu, anaweza tambua kipi kinachofanya sisi kuumwa,
na kuweza kushirikisha jamii nzima taarifa hizo.
Na nadhani hichi ndicho kitu ninachohitaji kiukweli,
ni kwa wote kusimama kulindana
na kutazamiana pamoja.
[Dr. Pardis Sabeti na Dr. Christian Happi]
[Wanasayansi wenye ustadi.
Washirika wenye moyo.
Mashujaa wa ulimwengu.]