Return to Video

Kutambua magonjwa mapema, tuongee lugha ya siri ya bakteria

  • 0:02 - 0:03
    Hauwajui.
  • 0:04 - 0:05
    Hauwaoni.
  • 0:06 - 0:08
    Lakini daima wapo wanazunguka,
  • 0:09 - 0:11
    wananong'oneza,
  • 0:11 - 0:13
    wakitengeneza mipango ya siri,
  • 0:14 - 0:17
    wakijenga jeshi la mamilioni ya wanajeshi.
  • 0:19 - 0:21
    Na wanapoamua kushambulia,
  • 0:21 - 0:24
    wanashambulia kwa wakati mmoja.
  • 0:27 - 0:29
    Ninaongelea kuhusu bakteria.
  • 0:29 - 0:30
    (Kicheko)
  • 0:30 - 0:33
    Mlidhani ninaongelea kuhusu nani?
  • 0:34 - 0:38
    Bakteria wanaishi kwenye jamii
    kama tu binadamu.
  • 0:38 - 0:39
    Wana familia,
  • 0:39 - 0:40
    wanaongea,
  • 0:40 - 0:42
    na wanapanga shughuli zao.
  • 0:42 - 0:45
    Na kama tu binadamu, wanahila, waongo,
  • 0:45 - 0:47
    na wengine hata wanadanganyana wenyewe.
  • 0:48 - 0:52
    Je kama nikikuambia kua tunaweza
    kusikiliza mazungumzo ya bakteria
  • 0:52 - 0:56
    na kutafsiri taarifa zao za siri
    kuwa lugha ya binadamu?
  • 0:56 - 1:01
    Na kama je nikiwaambia kuwa kutafsiri
    mazungumzo ya bakteria kutaokoa maisha?
  • 1:03 - 1:04
    Nina PhD ya nanofizikia,
  • 1:04 - 1:09
    na nimetumia teknolojia ya nano kuunda
    chombo cha kutafsiri cha muda halisi
  • 1:09 - 1:11
    kinachoweza kupeleleza kwenye jamii
    za bakteria
  • 1:11 - 1:14
    na kutupa rekodi za nini
    bakteria wanafanya.
  • 1:16 - 1:18
    Bakteria wanaishi kila sehemu.
  • 1:18 - 1:20
    Wako kwenye udongo, kwenye samani zetu
  • 1:20 - 1:21
    na ndani ya miili yetu.
  • 1:22 - 1:27
    Ki ukweli, asilimia 90 ya seli zote hai
    kwenye huu ukumbi ni bakteria.
  • 1:28 - 1:30
    Baadhi ya bakteria ni wazuri
    kwetu;
  • 1:30 - 1:33
    wanatusaidia kumeng'enya chakula
    au kutengeneza dawa.
  • 1:33 - 1:35
    Na baadhi ya bakteria na wabaya kwetu:
  • 1:35 - 1:37
    wanasababisha magonjwa na kifo.
  • 1:38 - 1:40
    Kushirikisha kazi zote bakteria
    walizonazo,
  • 1:40 - 1:42
    wanatakiwa wawe na uwezo wa
    kupanga,
  • 1:42 - 1:44
    na wanafanya hivyo kama tu sisi
    binadamu --
  • 1:44 - 1:46
    kwa mawasiliano.
  • 1:47 - 1:48
    Lakini badala ya kutumia
    maneno,
  • 1:48 - 1:51
    wanatumia molekuli za ishara
    kuwasiliana wenyewe kwa wenyewe.
  • 1:52 - 1:53
    Bakteria wanapokuwa wachche,
  • 1:53 - 1:56
    molekuli za ishara zinatiririka nje,
  • 1:56 - 1:59
    kama kelele za mtu peke yake
    jangwani.
  • 2:00 - 2:04
    Lakini kukiwa na bakteria wengi,
    molekuli za ishara zinajikusanya,
  • 2:04 - 2:07
    na bakteria wanaanza kuhisi kuwa
    hawapo peke yao.
  • 2:07 - 2:09
    Wanasikilizana wenyewe.
  • 2:09 - 2:12
    Kwa njia hii, wanapima
    wako wangapi
  • 2:12 - 2:16
    na wanapokuwa wengi wa kutosha
    kuanzisha hatua mpya.
  • 2:17 - 2:20
    Na pale molekuli za ishara zinafika
    kizingiti flani,
  • 2:20 - 2:24
    bakteria wote wanahisi kwa mara moja
    kua wanahitaji kutenda
  • 2:24 - 2:25
    kwa tendo hilo hilo.
  • 2:26 - 2:30
    Hivyo mazungumzo ya bakteria yanakuwa
    na mwanzo na jibu,
  • 2:30 - 2:33
    uzalishaji wa molekuli
    na majibu yake.
  • 2:35 - 2:38
    Kwenye utafiti wangu, nimelenga kupeleleza
    kwenye jamii za bakteria
  • 2:38 - 2:40
    ndani ya mwili wa binadamu.
  • 2:40 - 2:42
    Inafanyaje kazi?
  • 2:42 - 2:44
    Tunasampuli kutoka kwa mgonjwa.
  • 2:44 - 2:47
    Inaweza kuwa ni sampuli ya damu au mate.
  • 2:47 - 2:50
    Tunapiga elektroni ndani ya sampuli,
  • 2:50 - 2:54
    elektroni zitaingilia na molekuli
    zozote za mazungumzo zilizopo,
  • 2:54 - 2:56
    na huu muingiliano utatupa
    taarifa
  • 2:56 - 2:58
    ya aina ya bakteria,
  • 2:58 - 3:00
    aina ya mawasiliano
  • 3:00 - 3:02
    na kiasi gani bakteria wanazungumza.
  • 3:04 - 3:07
    Lakini inakuaje pale
    bakteria wakizungumza?
  • 3:08 - 3:12
    Kabla sijaunda chombo cha kutafsiri,
  • 3:12 - 3:15
    dhana yangu ya kwanza ilikua bakteria
    watakua na lugha ya halisi,
  • 3:15 - 3:19
    kama vichanga ambao bado hawajaunda
    maneno na sentensi.
  • 3:19 - 3:22
    Wanapocheka, wanafuraha;
    wanapolia, wanahuzuni.
  • 3:22 - 3:23
    Rahisi kama hivyo.
  • 3:24 - 3:28
    Lakini bakteria walionekana kutokuwa
    karibu na halisi kama nilivyodhani.
  • 3:29 - 3:31
    Molekuli sio tu molekuli.
  • 3:31 - 3:34
    Inaweza kumaanisha vitu tofauti
    kulingana na muktadha,
  • 3:34 - 3:37
    kama tu vilio vya watoto
    vinavyomaanisha vitu tofauti:
  • 3:37 - 3:39
    saa nyingine mtoto ana njaa,
  • 3:39 - 3:40
    saa nyingine amelowa,
  • 3:40 - 3:42
    saa nyingine ameumia au anaogopa.
  • 3:42 - 3:45
    Wazazi wanajua jinsi ya kusoma hivi vilio.
  • 3:46 - 3:48
    Na kua chombo kizuri cha kutafsiri,
  • 3:48 - 3:51
    kinatakiwa kiwe na uwezo wa kusoma
    molekuli za ishara
  • 3:51 - 3:55
    na kuzitafsiri
    kulingana na muktadha.
  • 3:55 - 3:57
    Na nani anajua?
  • 3:57 - 3:59
    Labda Tafsiri ya Google inaweza
    kuiptisha hii.
  • 3:59 - 4:01
    (Kicheko)
  • 4:02 - 4:04
    Hebu niwape mfano.
  • 4:04 - 4:08
    Nimeleta baadhi ya taarifa za bakteria
    zinazoweza kuwa ngumu kuelewa
  • 4:08 - 4:09
    kama hauna mafunzo,
  • 4:09 - 4:10
    lakini jaribu kuangalia.
  • 4:12 - 4:13
    (Kicheko)
  • 4:15 - 4:18
    Hii ni familia ya bakteria yeye furaha
    ambayo imemshambulia mgonjwa.
  • 4:20 - 4:22
    Wacha tuwaite familia ya Montague.
  • 4:24 - 4:27
    Wanatumia wote rasilimali,
    wanazaliana, wanakua.
  • 4:28 - 4:30
    Siku moja, wanapata mgeni mpya,
  • 4:33 - 4:35
    familia ya bakteria Capulet.
  • 4:35 - 4:36
    (Kicheko)
  • 4:36 - 4:39
    Kila kitu ni sawa,
    alimradi wanafanya kazi kwa pamoja.
  • 4:40 - 4:43
    Lakini kitu kisichopangwa kinatokea.
  • 4:44 - 4:49
    Romeo wa Montague anakua na mahusiano
    na Juliet wa Capulet.
  • 4:49 - 4:50
    (Kicheko)
  • 4:51 - 4:54
    Na ndio, wanagawiana chembe za urithi.
  • 4:54 - 4:56
    (Kicheko)
  • 4:58 - 5:01
    Sasa, uhamisho wa kinasaba unaweza
    kuwa hatari kwa wakina Montague
  • 5:01 - 5:05
    waliokuwa na matarajio ya kuwa familia
    pekee kwenye mgonjwa waliomshambulia,
  • 5:05 - 5:07
    kugawana chembe za urithi
    kunachangia
  • 5:07 - 5:10
    kwa wakina Capulet kutengeneza
    kinga kwa dawa.
  • 5:12 - 5:16
    Hivyo wakina Montague wanaanza kuongea
    kwa ndani kuondoa hii familia nyingine
  • 5:16 - 5:18
    kwa kutoa molekuli hii.
  • 5:19 - 5:20
    (Kicheko)
  • 5:21 - 5:22
    Na kwa maelezo:
  • 5:22 - 5:24
    [Hebu turatibu shambulizi.]
  • 5:24 - 5:25
    (Kicheko)
  • 5:26 - 5:27
    Hebu turatibu shambulizi.
  • 5:29 - 5:32
    Na kila mtu mara moja akaitikia
  • 5:32 - 5:37
    kwa kutoa sumu
    itakayoua ile familia nyingine.
  • 5:37 - 5:38
    [Ondoa!]
  • 5:40 - 5:42
    (Kicheko)
  • 5:43 - 5:48
    Wakina Capulet wakajibu kwa
    kuita shambulizi la kujibu.
  • 5:48 - 5:49
    [Shambulia!]
  • 5:49 - 5:50
    Na wakawa na vita.
  • 5:52 - 5:57
    Hii ni video ya bakteria wa ukweli
    wakipigana na viumbe kama upanga,
  • 5:57 - 5:58
    ambapo wanajaribu kuuana
  • 5:58 - 6:01
    kwa kuchomana kihalisi
    na kupasuana wenyewe.
  • 6:03 - 6:07
    Familia ya yeyote atakayeshinda hii vita
    anakuwa bakteria mkuu.
  • 6:08 - 6:12
    Hivyo ninachoweza kufanya ni kuchunguza
    mazungumzo ya bakteria
  • 6:12 - 6:14
    yanayopelekea tabia
    tofauti za kwa pamoja
  • 6:14 - 6:15
    kama ugomvi mliyouona.
  • 6:16 - 6:19
    Na nilichofanya ni kupeleleza
    kwenye jamii za bakteria
  • 6:19 - 6:21
    ndani ya mwili wa binadamu
  • 6:21 - 6:22
    kwenye wagonjwa hospitalini.
  • 6:23 - 6:25
    Nilifuatilia wagonjwa 62 kwenye jaribio,
  • 6:25 - 6:29
    ambapo nilipima sampuli ya mgonjwa
    kwa aina moja ya shambulizi,
  • 6:29 - 6:32
    bila kujua majibu ya
    vipimo vya kawaida.
  • 6:32 - 6:37
    Basi, kwenye upimaji wa bakteria,
  • 6:37 - 6:39
    sampuli inasambazwa kwenye kisahani,
  • 6:39 - 6:42
    na kama bakteria watakua ndani ya siku
    tano,
  • 6:42 - 6:44
    mgonjwa anagunduliwa kama ameathirika.
  • 6:46 - 6:49
    Nilipomaliza utafiti na
    kulinganisha majibu ya chombo
  • 6:49 - 6:52
    na vipimo vya kawaida
    na vipimo vya kuhakikisha,
  • 6:52 - 6:53
    nilishtuka.
  • 6:53 - 6:57
    Ilikua inashangaza zaidi
    kuliko nilivyowahi kutarajia.
  • 6:58 - 7:00
    Ila kabla sijawaambia
    nini chombo kilionyesha,
  • 7:00 - 7:03
    ningependa kuwaambia kuhusu
    mgonjwa mahsusi niliomfuatilia,
  • 7:03 - 7:04
    binti mdogo.
  • 7:05 - 7:06
    Alikua na cystic fibrosis,
  • 7:06 - 7:10
    ugonjwa wa kurithi uliofanya mapafu yake
    kuathiriwa kirahisi na bakteria.
  • 7:11 - 7:13
    Huyu binti hakua sehemu ya
    majaribio.
  • 7:13 - 7:16
    Nilimfuatilia kwa sababu nilijua
    kutoka kwenye taarifa zake
  • 7:16 - 7:18
    kua hakuwahi kupata mashambulizi
    kabla.
  • 7:19 - 7:22
    Mara moja kwa mwezi, huyu binti
    alienda hospitali
  • 7:22 - 7:24
    kuweka sampuli ya kohozi
    ambayo alitemea kwenye kikombe.
  • 7:25 - 7:28
    Hii sampuli ilisafirishwa kwa
    uchunguzi wa bakteria
  • 7:28 - 7:30
    huko maabara kuu
  • 7:30 - 7:33
    ili madaktari watende haraka
    iwapi wangekuta shambulizi.
  • 7:34 - 7:37
    Iliniruhusu mimi kupima chombo
    changu kwa sampuli zake pia.
  • 7:37 - 7:41
    Miezi miwili ya mwanzo nilipima
    sampuli zake, hakukua na kitu.
  • 7:42 - 7:43
    Lakini mwezi wa tatu,
  • 7:43 - 7:46
    Niligundua mazungumzo ya
    bakteria kwenye sampuli yake.
  • 7:46 - 7:50
    Bakteria walikua wanashirikiana
    kuharibu tishu ya pafu lake.
  • 7:51 - 7:55
    Lakini vipimo vya kawaida
    havikuonyesha bakteria kabisa.
  • 7:56 - 7:58
    Nilipima tena mwezi ujao,
  • 7:58 - 8:01
    na niliona kua yale mazungumzo ya
    bakteria yamekua makali zaidi.
  • 8:02 - 8:05
    Bado, vipimo vya kawaida
    havikuonyesha chochote.
  • 8:06 - 8:10
    Utafiti wangu ukaisha, lakini nusu mwaka
    baadae, nikafuatilia hali yake
  • 8:10 - 8:13
    kuona kama bakteria niliowajua
    pekee walipotea
  • 8:13 - 8:15
    bila muingilio wa tiba.
  • 8:16 - 8:18
    Hawakupotea.
  • 8:18 - 8:21
    Yule binti sasa alikua amegundulika
    na mashambulio makali
  • 8:21 - 8:22
    ya bakteria wabaya.
  • 8:24 - 8:28
    Walikua ni wale wale bakteria
    chombo changu kiligundua kabla.
  • 8:29 - 8:31
    Na licha ya ukali wa
    dawa za kutibu,
  • 8:31 - 8:34
    ilikua inashindikana
    kuondoa mashambulizi.
  • 8:35 - 8:38
    Madaktari waliona kua asingeweza
    kufikia miaka ya 20.
  • 8:40 - 8:43
    Nilipopima kwenye sampuli ya binti huyu,
  • 8:43 - 8:45
    kifaa changu kilikua kwenye
    hatua za mwanzo.
  • 8:45 - 8:47
    Sikujua hata
    kama njia yangu ilifanya kazi kabisa,
  • 8:47 - 8:50
    hivyo nikawa na makubaliano
    na madaktari
  • 8:50 - 8:52
    kutowaambia chombo changu
    kilichoonyesha
  • 8:52 - 8:54
    ili kutokuharibu matibabu yao.
  • 8:54 - 8:57
    Hivyo nilipoona haya majibu
    ambayo hata hayakuwa yamehakikishwa,
  • 8:57 - 8:58
    sikudhubutu kusema
  • 8:58 - 9:01
    ka sababu kutibu mgonjwa
    bila mashambulizi halisi
  • 9:01 - 9:04
    pia ina matokeo mabaya
    kwa mgonjwa.
  • 9:05 - 9:07
    Lakini sasa tunajua bora,
  • 9:07 - 9:10
    na kuna wavulana na wasichana wadogo
    wengi bado wanaweza kuokolewa
  • 9:11 - 9:15
    kwa sababu, bahati mbaya,
    hii hali inatokea mara nyingi.
  • 9:15 - 9:16
    Wagonjwa wanaathirika,
  • 9:16 - 9:20
    bakteria kwa namna flani hawaonekani
    kwenye vipimo vya kawaida,
  • 9:20 - 9:24
    na ghafla, maambukizi yanatokea
    ndani ya mgojwa na dalili kali.
  • 9:24 - 9:26
    Na kwenye mda huo, tayari tumechelewa.
  • 9:27 - 9:31
    Majibu ya kushangaza ya
    wagonjwa 62 niliowafuatilia
  • 9:31 - 9:33
    yalikua chombo changu kilishika
    mazungumzo ya bakteria
  • 9:33 - 9:36
    kwa zaidi ya nusu ya sampuli za wagonjwa
  • 9:36 - 9:39
    ambao walikua wamegundulika bila kitu
    kwa njia za upimaji za kawaida.
  • 9:39 - 9:43
    Kwa maneno mengine, zaidi ya nusu ya
    hawa wagonjwa walirudi nyumbani wakiwaza
  • 9:43 - 9:45
    kua wako huru na maambukizi,
  • 9:45 - 9:48
    japokuwa kihalisi walibeba
    bakteria hatari.
  • 9:49 - 9:52
    Ndani ya wagonjwa waliopimwa vibaya,
  • 9:52 - 9:55
    bakteria walikuwa wanaandaa shambulizi
    la kuambatanishwa.
  • 9:56 - 9:57
    Walikua wananong'onezana.
  • 9:58 - 10:00
    Ninachoita "mnong'ono wa bakteria"
  • 10:00 - 10:03
    ni bakteria ambao njia za kawaida
    za upimjai haziwezi kuona.
  • 10:03 - 10:07
    Mpaka sasa, ni chombo cha kutafsiri tu
    kinachoweza kudaka hao wanong'onezaji.
  • 10:08 - 10:12
    Ninaamini kua mda uliopo ambao
    bakteria bado wananong'onezana
  • 10:12 - 10:15
    ni nafasi nzuri ya matibabu
    ya malengo.
  • 10:16 - 10:19
    Kama yule binti angekua ametibiwwa
    kwenye kuu mda wenye nafasi,
  • 10:19 - 10:21
    ingekua inawezekana kuua
    bakteria
  • 10:21 - 10:23
    kwenye hatua yao ya mwanzo,
  • 10:23 - 10:25
    kabla maambukizi kuwa nje ya uwezo.
  • 10:27 - 10:31
    Nilichopitia na huyu binti mdogo
    kumenifanya niamue kufanya ninachoweza
  • 10:31 - 10:33
    kusukuma hii teknolojia kwenye hospitali.
  • 10:34 - 10:35
    Pamoja na madaktari,
  • 10:35 - 10:38
    tayari ninafanya kazi kutumia
    hiki kifaa kwenye kliniki
  • 10:38 - 10:40
    kutambua maambukizi ya kwanza.
  • 10:41 - 10:45
    Japo bado haijajulikana jinsi
    madaktari watatibu wagonjwa
  • 10:45 - 10:46
    kwenye kipindi cha mnong'ono,
  • 10:46 - 10:50
    hiki kifaa kinaweza kusaidia madaktari
    kuwa makini na wagonjwa kwenye hatari.
  • 10:51 - 10:54
    Kinaweza kuwasaidia kuhakikisha
    kama tiba imefanya kazi au la,
  • 10:54 - 10:57
    na inaweza kusaidia kujibu maswali rahisi:
  • 10:57 - 10:58
    Mgonjwa ana mashambulizi?
  • 10:58 - 11:00
    Na bakteria wako wanapanga nini?
  • 11:01 - 11:03
    Bakteria wanaongea,
  • 11:03 - 11:05
    wanatengeneza mipango ya siri,
  • 11:05 - 11:08
    na wanatumiana taarifa za siri.
  • 11:08 - 11:11
    Lakini sio tu kuawaangalia wenyewe
    wakinong'onezana,
  • 11:11 - 11:13
    sisi sote tunaweza kujifunza lugha ya siri
  • 11:13 - 11:16
    na kua wenyewe wanong'onezi wa bakteria.
  • 11:17 - 11:19
    Na, kama bakteria wangesema,
  • 11:20 - 11:23
    "3-oxo-C12-aniline."
  • 11:24 - 11:25
    (Kicheko)
  • 11:25 - 11:26
    (Makofi)
  • 11:26 - 11:27
    Asanteni.
Title:
Kutambua magonjwa mapema, tuongee lugha ya siri ya bakteria
Speaker:
Fatima AlZahra'a Alatraktchi
Description:

Bakteria "wanaongea" pamoja, wakituma taarifa za kemikali kuunda mashambulizi. Je kama tungesikiliza wanachosema? Mnanofizikia Fatima AlZahra's Alatraktchi ameunda kifaa cha kupeleleza mazungumzo ya bakteria na kutafsiri mazungumzo yao ya siri kwenda lugha ya binadamu. Kazi yake inaweza kuandaa njia ya ugunduzi wa mapema wa ugonjwa -- kabla hata hatujaumwa.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
11:41

Swahili subtitles

Revisions