Kwanini unapaswa kusoma Flannery O'Connor? - Iseult Gillespie
-
0:06 - 0:11Bibi muongeaji na mhalifu anayezurura
wakizozana katika barabara chafu. -
0:11 - 0:15Muuza Biblia anampeleka mwanafalsafa
mwenye mguu mmoja bandani. -
0:15 - 0:20Fundi anaesafiri anamfundisha mwanamke
kiziwi neno lake la kwanza shambani. -
0:20 - 0:23Kutoka shambani kwake vijijini Georgia,
-
0:23 - 0:25akizungukwa na kundi la ndege wa kufugwa,
-
0:25 - 0:28Flannery O'Connor aliandika simulizi
za waliotengwa, -
0:28 - 0:31wavamizi na wasioleweka waliunda
dunia aliyoifahamu vizuri: -
0:32 - 0:33Marekani Kusini.
-
0:34 - 0:35Alichapisha riwaya mbili,
-
0:35 - 0:38lakini anajulikana zaidi
kwa simulizi zake fupi, -
0:38 - 0:43ambazo zilichunguza maisha ya mji mdogo kwa
lugha kali, na ucheshi usio wa kawaida, -
0:43 - 0:45na mazingira ya kufurahisha yenye karaha.
-
0:45 - 0:49Kwenye muda wake wa ziada O'Connor
alichora katuni, -
0:49 - 0:51na uandishi wake pia
umejaa masihara. -
0:51 - 0:56Kwenye simulizi zake, mama na sura
"pana na ya upole kama kabichi", -
0:57 - 1:00mwanaume ana nguvu sana kama "dekio la
sakafuni", -
1:00 - 1:03na mwili wa mwanamke mmoja
una umbo kama "chombo cha kuzika". -
1:04 - 1:07Majina ya wahusika wake yamejawa ujanja.
-
1:07 - 1:10Chukulia simulizi "Maisha Unayoyaokoa
Yanaweza Kuwa ya Kwako", -
1:10 - 1:13ambapo mtembezi mwenye mkono mmoja
Tom Shiftlet anaenda kwenye maisha -
1:13 - 1:16ya ajuza mmoja aitwae Lucynell Crater
-
1:16 - 1:18na binti yake ambaye ni kiziwi na bubu.
-
1:18 - 1:20Japo mama Carter anajiamini,
-
1:20 - 1:22nyumba yake iliyojitenga inaanguka.
-
1:22 - 1:25Mwanzoni, tunaweza kushuku nia za Shiflet
-
1:25 - 1:27alipojitolea kusaidia kwenye nyumba,
-
1:27 - 1:30lakini O'Connor anaenda kuonyesha
kuwa yule ajuza ni -
1:30 - 1:33mjanja kama mgeni wake asiotarajiwa-
-
1:33 - 1:36na kutikisa mategemeo ya msomaji
kuhusu nani ana faida zaidi. -
1:36 - 1:38Kwa O'Connor, hamna somo lililokuwa
na kizuizi. -
1:39 - 1:41Japo alikuwa ni Mkatoliki aliyejitoa,
-
1:41 - 1:43hakuogopa kufuatilia uwezekano
-
1:43 - 1:45wa mawazo mema na tabia isiyo njema,
-
1:45 - 1:47inayokuwepo kwa mtu mmoja.
-
1:47 - 1:49Kwenye riwaya yake ya Wajeuri
Wanaiondolea Mbali, -
1:49 - 1:53mhusika mkuu anatingwa na mawazo
ya kuwa mtu wa Mungu - -
1:53 - 1:56lakini pia anawasha moto na kuua.
-
1:56 - 2:00Kitabu kinaanza na nabii amaesita
akiwa kwenye nafasi yenye utata: -
2:00 - 2:04"Mjomba wa Francis Marion Tarwater
alikua amekufa kwa nusu siku tu -
2:04 - 2:08pale huyo mvulana alipolewa sana akashindwa
kumalizia kuchimba kaburi lake". -
2:08 - 2:12Hii inamuacha mpita njia "kuvuta
mwili kutoka kwenye meza ya chai -
2:12 - 2:14ambapo ulikuwa umekaa bado na
kuuzika [...] -
2:14 - 2:16na udongo wa kutosha kwa juu
kuzuia mbwa kuufukua". -
2:17 - 2:19Japokuwa siasa zake bado ni za kulumbana,
-
2:19 - 2:23bunilizi ya O'Connor inaweza pia
kulinganishwa na ubaguzi wa Kusini. -
2:23 - 2:26Kwenye "Kila Kinachopanda Lazima
Kikutane", -
2:26 - 2:29anaelezea mvulana anayechukizwa
na upendeleo wa mama yake. -
2:29 - 2:32Lakini simulizi inaelezea kuwa
ana mapungufu yake -
2:32 - 2:34na inasema kwamba kuyagundua mabaya tu
-
2:34 - 2:37haitetei tabia yake kutokuthibitiwa.
-
2:37 - 2:40Hata O'Connor anavyochunguza
mambo potofu ya ubinadamu, -
2:40 - 2:43anaacha mlango wa ukombozi wazi kidogo.
-
2:43 - 2:45Kwenye "Mwanaume Mzuri ni Mgumu Kupata",
-
2:45 - 2:49anamkomboa ajuza anayeteseka kwa
kumsamehe mshitakiwa aliyekubuhu, -
2:49 - 2:51hata anavyoikaribia familia yake.
-
2:52 - 2:55Japo tunaweza kushtushwa na malipo
anayolipa huyu mama kusamehewa, -
2:55 - 2:57tunalazimika kukabiliana na
yanayoendelea kwenye mda -
2:57 - 3:00tunapoweza kuzingatia kuwa
ukatili au ubaya. -
3:00 - 3:03Uwezo wa O'Connor wa ajabu
-
3:03 - 3:06na tafiti zake za kujitenga na
ushirikina wa Kusini -
3:06 - 3:10ulimpelekea kutambuliwa kama
mwandishi wa Kigothi wa Kusini. -
3:10 - 3:12Lakini kazi yake ilisogea kupita
tabia za kijinga kabisa -
3:12 - 3:15na za kutisha zilizohusishwa
na huo mtindo -
3:15 - 3:18kuvumbua tofauti na mchanganyiko
wa tabia za binadamu. -
3:18 - 3:21Alijua baadhi ya hii tofauti
ilileta karaha, -
3:21 - 3:23na kuwa hadithi zake zingekuwa
na ladha inayohitajika - -
3:23 - 3:26lakini alisikia raha kuwachanganya
wasomaji wake, -
3:26 - 3:29O'Connor alikufa kwa lupus akiwa
na miaka 39, -
3:29 - 3:33baada ya ugonjwa kumweka shambani mwake
Georgia kwa miaka kumi na mbili. -
3:34 - 3:35Kwenye miaka hiyo,
-
3:35 - 3:37aliandika kazi zake nyingi
alizokuwa akiwaza. -
3:37 - 3:40Uwezo wake wa kuhama kati ya
maudhi na uvumbuzi -
3:40 - 3:45unaendelea kuvutia wasomaji kwenye
dunia yake ya kufikirika isiyoisha. -
3:45 - 3:47Kama mhusika Tom Shirlet anavyosema,
-
3:47 - 3:49mwili ni "kama nyumba:
-
3:49 - 3:51haiendi popote,
-
3:51 - 3:54lakini roho, mwanamke,
ni kama gari moto: -
3:54 - 3:56daima lipo kwenye mwendo".
- Title:
- Kwanini unapaswa kusoma Flannery O'Connor? - Iseult Gillespie
- Speaker:
- Iseult Gillespie
- Description:
-
Angalia somo zima: https://ed.ted.com/lessons/why-should-you-read-flannery-o-connor-iseult-gillespie
Flannery O'Connor aliandika simulizi za waliotengwa, wavamizi na wahangaikaji kwenye dunia aliyoijua vizuri: Marekani ya Kusini. Alikuwa ni mkufunzi wa sanaa ya kila kitu, lakini kazi yake ilipita mambo yote ya kijinga na ya kuogopesha kuvumbua tofauti na mchanganyiko wa tabia za binadamu. Iseult Gillespie anadadafua jinsi kazi za O'Connor zinazidi kuwavutia wasomaji miaka mingi baadae.
Somo na Iseult Gillespie, ikiongozwa na Anton Bogaty.
- Video Language:
- English
- Team:
- closed TED
- Project:
- TED-Ed
- Duration:
- 03:56
Nelson Simfukwe approved Swahili subtitles for Why should you read Flannery O’Connor? - Iseult Gillespie | ||
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for Why should you read Flannery O’Connor? - Iseult Gillespie | ||
Doris Mangalu accepted Swahili subtitles for Why should you read Flannery O’Connor? - Iseult Gillespie | ||
Doris Mangalu edited Swahili subtitles for Why should you read Flannery O’Connor? - Iseult Gillespie | ||
Doris Mangalu edited Swahili subtitles for Why should you read Flannery O’Connor? - Iseult Gillespie | ||
Julieth Mbeyella edited Swahili subtitles for Why should you read Flannery O’Connor? - Iseult Gillespie | ||
Julieth Mbeyella edited Swahili subtitles for Why should you read Flannery O’Connor? - Iseult Gillespie | ||
Julieth Mbeyella edited Swahili subtitles for Why should you read Flannery O’Connor? - Iseult Gillespie |