Return to Video

Kufanya yasiyowezekana, kuishinda hofu| Dan Meyer | TEDxMaastricht

  • 0:08 - 0:10
    Asante
  • 0:16 - 0:21
    Palikuwa na mfalme nchini India, Maharaja
    na siku yake ya kuzaliwa ilitolewa amri
  • 0:21 - 0:24
    kwamba machifu wote walete
    zawadi kwa mfalme.
  • 0:24 - 0:28
    Wengine wakaleta hariri bora,
    wengine wakaleta panga maridadi,
  • 0:28 - 0:29
    wengine dhahabu
  • 0:29 - 0:33
    mwisho wa mstari alikuja akitembea
    mzee mdogo mwenye makunyanzi
  • 0:33 - 0:37
    ambaye alitembea kutoka kijijini kwake
    kwa safari ya siku nyingi kando ya bahari.
  • 0:37 - 0:41
    alipokuwa akisogea mwana mfalme akauliza,
    'Umemletea zawadi gani Mfalme?'
  • 0:41 - 0:45
    Na mzee yule taratibu sana
    akakunjua mkono wake kuonyesha
  • 0:45 - 0:50
    kombe la baharini zuri sana, lenye makoa
    ya zambarau na njano,nyekundu na bluu.
  • 0:50 - 0:51
    Na mwana Mfalme akasema,
  • 0:51 - 0:54
    "Hiyo si zawadi kwa Mfalme!
    Ni zawadi gani hiyo?"
  • 0:55 - 0:57
    Mzee yule akamwangalia taratibu
    na kusema
  • 0:58 - 1:01
    "Kutembea mwendo mrefu.. ni sehemu
    ya zawadi"
  • 1:01 - 1:03
    (Kicheko)
  • 1:03 - 1:06
    Baada ya muda mfupi,
    Nitawapa zawadi,
  • 1:06 - 1:08
    zawadi niaminiyo
    ni zawadi inayostahili kuenezwa.
  • 1:08 - 1:10
    Ila kabla ya hayo, ngoja niwachukue
  • 1:10 - 1:12
    kwenye mwendo wangu mrefu.
  • 1:12 - 1:14
    Kama wengi wenu,
  • 1:14 - 1:15
    Nilianza maisha kama mtoto mdogo.
  • 1:15 - 1:17
    Wangapi kati yenu
    mlianza maisha kama mtoto ?
  • 1:17 - 1:19
    Aliyezaliwa mchanga?
  • 1:19 - 1:20
    Karibia nusu yenu.. Sawa
  • 1:21 - 1:22
    (Kicheko)
  • 1:22 - 1:25
    Na mliobakia, vipi?
    Mlizaliwa mkiwa watu wazima?
  • 1:25 - 1:28
    Ama kweli, nataka kukutana na mama zenu!
  • 1:28 - 1:29
    Ongelea yasiyowezekana!
  • 1:31 - 1:35
    Nikiwa mtoto mdogo, siku zote nilipendezwa
    kufanya mambo yasiyowezekana
  • 1:36 - 1:39
    Leo ni siku ambayo nimekuwa nikiitarajia
    kwa miaka mingi,
  • 1:39 - 1:41
    kwa sababu leo ni siku ambayo
    nitajaribu
  • 1:41 - 1:44
    kufanya yasiyowezekana
    mbele ya macho yenu
  • 1:44 - 1:45
    Hapahapa TEDxMaastrich
  • 1:46 - 1:48
    Nitaanza
  • 1:49 - 1:51
    Kwa kuonyesha mwisho wake:
  • 1:51 - 1:53
    Na nitawathibitishia kwamba
  • 1:53 - 1:55
    yasiyowezekana siyo hayawezekani
  • 1:55 - 1:58
    Na nitamalizia kwa kuwapa
    zawadi yenye kustahili kuieneza:
  • 1:58 - 2:01
    Nitawaonyesha kwamba unaweza
    kufanya yasiyowezekana maishani mwako.
  • 2:03 - 2:05
    katika kutafuta kufanya yasiyowezekana,
    nimegundua kuna
  • 2:05 - 2:08
    mambo mawili yanayofanana
    kati ya watu duniani.
  • 2:08 - 2:10
    Kila mtu ana hofu,
  • 2:10 - 2:12
    na kila mtu ana ndoto.
  • 2:13 - 2:18
    Katika kutafuta kufanya yasiyowezekana
    nimegundua kuna vitu vitatu
  • 2:18 - 2:20
    ambavyo nimevifanya miaka mingi ambavyo
  • 2:20 - 2:23
    vimenisababishia kufanya yasiyowezekana:
  • 2:24 - 2:27
    Mchezo wa mpira wa kuchenga au "Trefball"
  • 2:27 - 2:28
    Superman,
  • 2:28 - 2:29
    na Mbu
  • 2:29 - 2:31
    Hayo ni maneno yangu matatu makuu.
  • 2:31 - 2:34
    Mmeshajua kwanini nafanya
    yasiyowezekana maishani mwangu
  • 2:34 - 2:36
    Hivyo nitawachukua katika safari
    yangu, ya mwendo mrefu
  • 2:36 - 2:39
    kutoka kwenye hofu hadi ndoto
  • 2:39 - 2:41
    kutoka kwenye maneno hadi panga,
  • 2:41 - 2:43
    Kutoka Mpira wa kuchenga
  • 2:43 - 2:44
    hadi Superman
  • 2:44 - 2:45
    hadi kwa Mbu
  • 2:46 - 2:47
    Na ninatumaini kuwaonyesha
  • 2:47 - 2:50
    unawezaje kufanya yasiyo
    wezekana maishani mwako
  • 2:52 - 2:55
    Oktoba 4, mwaka 2007.
  • 2:56 - 2:58
    Moyo wangu ulienda mbio,
    magoti yangu yalitetema
  • 2:58 - 2:59
    nilipokuwa napanda jukwaani
  • 2:59 - 3:01
    kwenye ukumbi wa Sanders
  • 3:01 - 3:03
    Chuo cha Harvard kupokea
  • 3:03 - 3:06
    Tuzo ya Ig Nobel katika Utabibu
  • 3:06 - 3:09
    kwa kushiriki kuandika ikisiri
    ya utafiti wa kitabibu
  • 3:09 - 3:10
    ulioitwa "Kumeza Upanga...
  • 3:10 - 3:12
    ...na Athari zake"
  • 3:12 - 3:13
    (Kicheko)
  • 3:14 - 3:18
    Ilichapishwa kwenye jarida dogo
    ambalo sikuwahi kulisoma kabla,
  • 3:18 - 3:20
    Jarida la Kitabibu la Uingereza.
  • 3:21 - 3:25
    Na kwangu, hiyo ilikuwa ndoto
    isiyowezekana kuwa kweli,
  • 3:25 - 3:28
    ilikuwa ni mshangao usiotegemewa
    kwa mtu kama mimi,
  • 3:28 - 3:31
    ilikuwa ni heshima ambayo sitaweza kusahau
  • 3:31 - 3:35
    Lakini haikuwa sehemu ya kubwa ya
    kukumbuka maishani mwangu.
  • 3:36 - 3:38
    Mnamo Oktoba 4, mwaka 1967
  • 3:38 - 3:40
    kijana mwoga, mwenye aibu, mwembamba
  • 3:41 - 3:43
    aliteseka na hofu kubwa kupita kiasi.
  • 3:43 - 3:46
    Alipojiandaa kupanda jukwaani,
  • 3:46 - 3:47
    moyo wake ulienda mbio,
  • 3:48 - 3:49
    magoti yake yalikuwa yakitetemeka.
  • 3:50 - 3:52
    Alikwenda kufungua kinywa chake kuongea,
  • 3:56 - 3:58
    maneno hayakuweza kutoka.
  • 3:58 - 4:00
    Alisimama akitetemeka na kutoa machozi.
  • 4:01 - 4:02
    Alipooza kwa mshtuko wa ghafla,
  • 4:02 - 4:04
    alipatwa fadhaa kwa hofu.
  • 4:04 - 4:06
    huyu kijana mwoga, mwenye aibu, mwembamba
  • 4:06 - 4:08
    alitesekana na hofu kubwa kupita kiasi.
  • 4:09 - 4:10
    Alikuwa na hofu ya giza,
  • 4:11 - 4:12
    hofu ya vimo virefu,
  • 4:12 - 4:13
    hofu ya buibui na nyoka ...
  • 4:13 - 4:15
    Kuna yeyote anayeogopa buibui na nyoka?
  • 4:15 - 4:17
    Naam, wachache wenu ...
  • 4:17 - 4:19
    Alikuwa na hofu ya maji na papa ...
  • 4:19 - 4:22
    Hofu ya madaktari na manesi na madaktari
    wa meno,
  • 4:22 - 4:25
    na sindano na kutobolewa na vitu vya
    ncha kali.
  • 4:25 - 4:27
    Lakini zaidi ya chochote,
    alikuwa na hofu ya
  • 4:27 - 4:28
    watu
  • 4:29 - 4:32
    Huyo kijana mwoga,mwenye aibu na mwembamba
  • 4:32 - 4:33
    alikuwa mimi.
  • 4:33 - 4:36
    Nilikuwa na hofu ya kushindwa na
    kukataliwa,
  • 4:37 - 4:40
    kutojithamini, kujiona duni,
  • 4:40 - 4:43
    na kitu ambacho hata hatukujua
    unaweza kujiandikisha kwa siku hizo:
  • 4:43 - 4:45
    ugonjwa wa hofu ya ukaribu na watu.
  • 4:45 - 4:49
    Kwa sababu nilikuwa na hofu, waonevu
    walinitania na kunipiga.
  • 4:49 - 4:52
    Walinicheka na kuniita majina,
    Hawakuniruhusu kucheza nao
  • 4:52 - 4:54
    michezo ya aina yoyote.
  • 4:55 - 4:58
    Ah, kulikuwa na mchezo mmoja
    walikuwa wakiruhusu kucheza kwenye ...
  • 4:58 - 4:59
    Mpira wa kuchenga -
  • 5:00 - 5:01
    na sikuwa mchengaji nzuri.
  • 5:02 - 5:04
    Waonevu waliita jina langu,
  • 5:04 - 5:06
    na nilipoangalia
    niliona mipira myekundu ya kukwepa
  • 5:06 - 5:08
    ikivurumishwa usoni wangu kwa kasi kubwa
  • 5:08 - 5:10
    bam, bam, bam!
  • 5:11 - 5:13
    Ninakumbuka siku nyingi
    nikirudi nyumbani kutoka shule,
  • 5:13 - 5:18
    uso wangu ulikuwa mwekundu ukichonyota,
    masikio yangu yalikuwa mekundu yakivuma.
  • 5:18 - 5:21
    Macho yangu yalichoma kwa machozi,
  • 5:21 - 5:24
    na maneno yao yalichoma masikioni mwangu.
  • 5:24 - 5:25
    Na yeyote aliyesema,
  • 5:25 - 5:29
    "Fimbo na mawe vyaweza kunivunja mifupa,
    bali maneno hayatoniumiza kamwe "...
  • 5:29 - 5:30
    Ni uongo.
  • 5:30 - 5:32
    Maneno huweza kukata kama kisu.
  • 5:32 - 5:34
    Maneno huweza kupenya kama upanga.
  • 5:34 - 5:36
    Maneno huwezafanya majeraha yenye kina
  • 5:36 - 5:38
    yasiweze kuonekana.
  • 5:38 - 5:41
    Hivyo nilikuwa na hofu.
    Na maneno yalikuwa adui yangu mkubwa.
  • 5:41 - 5:42
    Bado ni adui yangu.
  • 5:43 - 5:45
    Lakini pia nilikuwa na ndoto.
  • 5:45 - 5:48
    Nilienda nyumbani
    na kutorokea kwenye futuhi za Superman
  • 5:48 - 5:50
    na nilisoma futuhi za Superman
  • 5:50 - 5:53
    na niliota kutaka kuwa shujaa mkubwa
    kama Superman.
  • 5:53 - 5:56
    Nilitaka kupigania kweli na haki,
  • 5:56 - 5:59
    Nilitaka kupambana dhidi ya
    wahalifu na mahasimu,
  • 5:59 - 6:03
    Nilitaka kupaa duniani kote
    kufanya vitendo vya ujasiri kuokoa maisha.
  • 6:03 - 6:06
    Nilikuwa pia navutiwa mno
    na vitu vilivyokuwa kweli.
  • 6:06 - 6:09
    Nilisoma kitabu cha Rekodi za Dunia za Guiness
    na kitabu cha Ripley kiitwacho Amini au Usiamini.
  • 6:09 - 6:13
    Yeyote kati yenu amewahi kusoma kitabu cha Rekodi za Dunia za Guinness au kitabu cha Ripley?
  • 6:13 - 6:14
    Navipenda vitabu hivi!
  • 6:14 - 6:16
    Niliona watu wafanyao ujasiri halisia.
  • 6:16 - 6:18
    Nikasema, Nataka kufanya hivyo.
  • 6:18 - 6:19
    Ikiwa waonevu hawataniruhusu
  • 6:19 - 6:21
    kucheza katika michezo yao yoyote,
  • 6:21 - 6:23
    Nataka kufanya maajabu, ujasiri halisi.
  • 6:23 - 6:27
    Nataka kufanya kitu cha kusifika
    ambacho hao waonevu hawawezi kufanya.
  • 6:27 - 6:29
    Nataka kupata kusudi langu na wito wangu,
  • 6:29 - 6:31
    Nataka kujua kuwa maisha yangu yana maana,
  • 6:31 - 6:33
    Nataka kufanya kitu cha kushangaza
    kubadili ulimwengu;
  • 6:33 - 6:37
    Ninataka kuthibitisha
    yasiyowezekana sio hayawezekani.
  • 6:38 - 6:40
    Kupeleka mbele miaka 10 -
  • 6:40 - 6:43
    Ilikuwa wiki kabla ya kutimiza miaka 21.
  • 6:43 - 6:47
    Mambo mawili yalitokea kwa siku moja
    ambayo yangebadilisha maisha yangu milele.
  • 6:47 - 6:49
    Nilikuwa nikiishi Tamil Nadu, India Kusini
  • 6:50 - 6:51
    Nilikuwa mmishonari huko,
  • 6:51 - 6:53
    na mshauri wangu, rafiki yangu aliniuliza,
  • 6:53 - 6:55
    "Je, una Thromu, Daniel?"
  • 6:55 - 6:57
    Na nikasema, "Thromu?
    Thromu ni nini? "
  • 6:57 - 7:00
    Alisema, "Thromu ni malengo makuu ya
    maisha.
  • 7:00 - 7:05
    Ni muunganiko
    wa ndoto na malengo, kama ungeweza
  • 7:05 - 7:07
    kufanya chochote unachotaka,
    kwenda popote unapotaka
  • 7:07 - 7:08
    kuwa mtu yeyote unayetaka,
  • 7:08 - 7:10
    ungekwenda wapi?
    Ungefanya nini?
  • 7:10 - 7:11
    Ungekuwa nani?
  • 7:11 - 7:14
    Nikasema, "Siwezi kufanya hivyo!
    Naogopa sana! Naogopa mengi mno! "
  • 7:14 - 7:18
    Usiku huo nilichukua mkeka wangu wa mchele
    juu ya paa la ghorofa,
  • 7:18 - 7:19
    nikautandika chini ya nyota,
  • 7:19 - 7:22
    na kuangalia popo wakiwashambulia mbu.
  • 7:22 - 7:26
    Na yote niliyofikiria ilikuwa thromu,
    na ndoto na malengo,
  • 7:26 - 7:28
    na wale washujaaji wenye mipira ya kuchenga.
  • 7:29 - 7:31
    Masaa machache baadaye niliamka.
  • 7:31 - 7:34
    Moyo wangu ulienda mbio,
    magoti yangu yakitetemeka.
  • 7:34 - 7:36
    Safari hii haikuwa na hofu.
  • 7:36 - 7:38
    Mwili wangu wote ulitikisika.
  • 7:38 - 7:40
    Na kwa siku tano zilizofuata
  • 7:40 - 7:44
    Nilipoteza na kurudisha fahamu,
    kitandani nikipigania maisha yangu.
  • 7:44 - 7:48
    Ubongo wangu ulikuwa unawaka
    na homa ya malaria yenye jotoridi la 105.
  • 7:48 - 7:52
    Na kila fahamu ziliponirudia,
    nilichowaza ilikuwa kuhusu thromu.
  • 7:52 - 7:54
    Niliwaza
    "Nataka kufanya nini na maisha yangu?"
  • 7:54 - 7:56
    Hatimaye, usiku kabla
    sijafikisha miaka 21,
  • 7:56 - 7:58
    katika wakati wa kuelewa,
  • 7:58 - 8:00
    Nilikuja kutambua:
  • 8:00 - 8:02
    Nilitambua kwamba yule mbu mdogo,
  • 8:03 - 8:05
    Anofelesi Stefensi,
  • 8:05 - 8:07
    yule mbu mdogo
  • 8:07 - 8:08
    aliye na uzito chini ya mikrogramu 5
  • 8:08 - 8:10
    chini ya punje ya chumvi,
  • 8:10 - 8:13
    anaweza kuangusha
    mtu wa ratili 170, mtu wa kilo 80,
  • 8:13 - 8:15
    Niligundua kwamba alikuwa hasimu wangu.
  • 8:15 - 8:17
    Kisha nikagundua,
    hapana, hapana, sio mbu,
  • 8:17 - 8:19
    Ni vimelea vidogo
    ndani ya mbu,
  • 8:19 - 8:23
    Plasmodium Falciparum,
    ambao huua zaidi ya watu milioni kwa mwaka
  • 8:24 - 8:26
    Kisha nikagundua
    Hapana, hapana, tena ni ndogo zaidi,
  • 8:26 - 8:29
    lakini kwangu, ilionekana kubwa zaidi.
  • 8:29 - 8:30
    Niligundua,
  • 8:30 - 8:31
    hofu ilikuwa hasimu yangu,
  • 8:31 - 8:32
    vimelea yangu,
  • 8:32 - 8:35
    vilivyonitia ulemavu
    na kunipooza mimi maisha yangu yote.
  • 8:35 - 8:38
    Unajua, kuna tofauti
    kati ya hatari na hofu.
  • 8:38 - 8:40
    Hatari ni halisi.
  • 8:40 - 8:42
    Hofu ni hiari.
  • 8:42 - 8:44
    Na nikagundua kuwa nina hiari:
  • 8:44 - 8:48
    Aidha niishi kwa hofu,
    na kufa katika kushindwa usiku ule,
  • 8:49 - 8:52
    au ningeweza kuua hofu yangu,
    na ningeweza
  • 8:52 - 8:56
    kufikia ndoto zangu,
    Ningeweza kuthubutu kuishi maisha.
  • 8:57 - 9:00
    Na unajua, kuna kitu kuhusu
    kuwa kwenye kitanda cha mauti
  • 9:00 - 9:04
    na kukabiliwa na kifo ambacho haswa
    kinakufanya utake kweli kuishi maisha.
  • 9:04 - 9:07
    Nikagundua kuwa kila mtu hufa,
    si kila mtu huishi.
  • 9:08 - 9:10
    Ni katika kufa ndio sisi tunaishi.
  • 9:10 - 9:12
    Unajua, wakati unapojifunza kufa,
  • 9:12 - 9:13
    unajifunza kweli kuishi.
  • 9:13 - 9:15
    Kwa hiyo nikaamua nitaenda kubadilisha
  • 9:15 - 9:16
    hadithi yangu usiku huo.
  • 9:17 - 9:18
    Sikutaka kufa.
  • 9:18 - 9:20
    Hivyo nikafanya sala ndogo, nikasema,
  • 9:20 - 9:22
    "Mungu, ukiniruhusu niishi
    nifikishe miaka 21,
  • 9:22 - 9:25
    Sitaruhusu hofu
    itawale maisha yangu tena.
  • 9:25 - 9:27
    Nitaziweka hofu zangu kifoni,
  • 9:27 - 9:30
    Nitaenda kuzifikia ndoto zangu,
  • 9:30 - 9:31
    Ninataka kubadilisha mtazamo wangu,
  • 9:31 - 9:34
    Nataka kufanya kitu cha ajabu
    na maisha yangu,
  • 9:34 - 9:36
    Nataka kupata kusudi langu na wito wangu,
  • 9:36 - 9:39
    Ninataka kujua kuwa yasiyowezekana
    si hayawezekani. "
  • 9:39 - 9:43
    Sitawaambia kama nilinusurika usiku ule;
    Nitawaacha mfikirie.
  • 9:43 - 9:44
    (Kicheko)
  • 9:44 - 9:47
    Lakini usiku huo niliandika orodha
    ya Thromu zangu 10 za kwanza:
  • 9:47 - 9:50
    Niliamua nilitaka
    kutembelea mabara makubwa
  • 9:50 - 9:52
    kutembelea Maajabu 7 ya Dunia
  • 9:52 - 9:53
    kujifunza lugha nyingi,
  • 9:53 - 9:55
    kuishi kwenye kisiwa kitupu,
  • 9:55 - 9:56
    kuishi kwenye meli baharini,
  • 9:56 - 9:59
    kuishi na kabila la Wahindi
    katika Amazon,
  • 9:59 - 10:01
    kupanda hadi juu
    ya mlima mrefu kuliko yote Sweden,
  • 10:01 - 10:03
    Nilitaka kuona mawio Mlima Everest,
  • 10:03 - 10:05
    kufanya kazi na biashara ya muziki
    Nashville,
  • 10:05 - 10:07
    Nilitaka kufanya kazi ya sarakasi,
  • 10:07 - 10:09
    na nilitaka kuruka nje ya ndege.
  • 10:09 - 10:12
    Zaidi ya miaka ishirini iliyofuata,
    Nilitimiza thromu hizo kwa wingi.
  • 10:12 - 10:15
    Kila wakati niliondoa
    thromu kwenye orodha yangu,
  • 10:15 - 10:18
    Niliongeza 5 au 10 zaidi kwenye orodha
    na orodha yangu iliendelea kukua.
  • 10:19 - 10:23
    Kwa miaka saba iliyofuata, niliishi
    kwenye kisiwa kidogo katika Bahamas
  • 10:23 - 10:25
    kwa karibu miaka saba
  • 10:25 - 10:27
    katika kibanda cha makuti,
  • 10:29 - 10:34
    nikiwinda papa na taa wa kula,
    nikiwa mtu pekee kwenye kisiwa,
  • 10:34 - 10:36
    nikiwa nimevaa msuli,
  • 10:37 - 10:39
    na nikajifunza kuogelea na papa.
  • 10:39 - 10:41
    Na kutoka huko, nikahamia Mexico,
  • 10:41 - 10:45
    na kisha nikasafiri
    kwa bonde la Mto Amazon nchini Ecuador,
  • 10:45 - 10:48
    Pujo Pongo Ecuador,
    niliishi na kabila moja huko,
  • 10:48 - 10:52
    na kidogo kidogo nilianza kuongeza
    kujiamini kwa thromu zangu tu.
  • 10:52 - 10:55
    Nilihamia biashara ya muziki Nashville,
    kisha Sweden,
  • 10:55 - 10:58
    nikahamia Stockholm,
    kufanyakazi katika biashara ya muziki,
  • 10:58 - 11:02
    ambapo nilipanda kilele cha Ml. Kebnekaise
    juu ya mzunguko wa Arctic.
  • 11:03 - 11:05
    Nilijifunza udamisi,
  • 11:05 - 11:06
    na viinimacho,
  • 11:06 - 11:07
    na kutembea kama ngongoti,
  • 11:07 - 11:10
    kuendesha baiskeli kwa tairi moja,
    kula moto, kula kioo.
  • 11:10 - 11:14
    Mwaka 1997 nilisikia kuna
    wameza panga wasiozidi kumi na mbili
  • 11:14 - 11:15
    na nikasema, "Inabidi kufanya hivyo!"
  • 11:15 - 11:18
    Nilikutana na mmeza panga,
    na nikamwomba vidokezo.
  • 11:18 - 11:20
    Akasema, "Naam, nitakupa vidokezo 2:
  • 11:20 - 11:22
    Namba 1: Ni hatari sana,
  • 11:22 - 11:24
    Watu wamekufa wakifanya hivi.
  • 11:24 - 11:25
    Namba 2:
  • 11:25 - 11:26
    Usijaribu! "
  • 11:26 - 11:28
    (Kicheko)
  • 11:28 - 11:30
    Basi nikaiongeza kwenye orodha ya thromu.
  • 11:30 - 11:33
    Na nikafanya mazoezi
    mara 10 hadi 12 kwa siku, kila siku
  • 11:34 - 11:35
    kwa miaka minne.
  • 11:35 - 11:37
    Sasa nilipigia hesabu hizo...
  • 11:37 - 11:40
    4 x 365 [x 12]
  • 11:40 - 11:43
    Ilikuwa karibu 13,000
    majaribio yasiyofanikiwa
  • 11:43 - 11:45
    kabla sijatia panga langu wa kwanza
    chini koo mwaka 2001.
  • 11:46 - 11:48
    Wakati huo nikaweka thromu
  • 11:48 - 11:51
    kuwa mtaalamu wa ulimwengu
    kwa kumeza panga.
  • 11:51 - 11:54
    Basi nilitafuta kila kitabu,
    gazeti, makala ya gazeti,
  • 11:54 - 11:58
    kila ripoti ya kitabibu,
    Nilijifunza fiziolojia, anatomia,
  • 11:58 - 12:00
    Niliongea na madaktari na manesi,
  • 12:00 - 12:02
    niliwakutanisha wameza panga wote
    pamoja
  • 12:02 - 12:04
    kwenye Shirikisho la Wameza Panga
    Kimataifa,
  • 12:04 - 12:06
    nikafanya ikisiri miaka 2
    ya utafiti kitabibu
  • 12:06 - 12:09
    kuhusu Umezaji wa Panga na athari zake
  • 12:09 - 12:11
    iliyochapishwa
    katika Jarida la Kitabibu Uingereza.
  • 12:11 - 12:12
    (Kicheko)
  • 12:12 - 12:13
    Asanteni.
  • 12:13 - 12:18
    (Makofi)
  • 12:18 - 12:22
    Na nilijifunza mambo ya kuvutia sana
    kuhusu umezaji wa panga.
  • 12:22 - 12:25
    Vitu vingine ambavyo haujawahi kufikiria
    kabla, hutasahau baada ya usiku huu.
  • 12:25 - 12:29
    Wakati utakapoenda nyumbani, na unakata
    steki yako na kisu chako
  • 12:29 - 12:32
    au panga, au "bestek" zako,
    utafikiri juu ya hili ...
  • 12:34 - 12:37
    Nilijifunza kwamba umezaji panga
    ulianzia India -
  • 12:37 - 12:40
    mahali nilipona kwa mara ya kwanza
    nikiwa kijana wa miaka 20 -
  • 12:40 - 12:42
    karibu miaka 4000 ya kale, karibu 2000 BC.
  • 12:42 - 12:46
    Zaidi ya miaka 150 iliyopita,
    wameza panga walitumika
  • 12:46 - 12:47
    katika medani za sayansi na kitabibu
  • 12:47 - 12:51
    ili kusaidia kuunda
    endoskopia imara mwaka 1868
  • 12:51 - 12:54
    wakiwa na Dk. Adolf Kussmaul wa Freiburg, Ujerumani
  • 12:54 - 12:57
    Mnamo 1906, elektrokadiogramu huko Wales,
  • 12:57 - 13:00
    kujifunza matatizo ya kumeza,
    na mmeng'enyo wa chakula,
  • 13:00 - 13:02
    aina ya bronkoskopia, .
  • 13:02 - 13:04
    Lakini zaidi ya miaka 150 iliyopita,
  • 13:04 - 13:08
    tunajua mamia ya madhara
    na vifo kadhaa ...
  • 13:08 - 13:15
    Hii ni endoskopia imara
    iliyoanzishwa na Dk. Adolph Kussmaul.
  • 13:15 - 13:19
    Lakini tuligundua kuwa kulikuwa na
    Vifo 29 zaidi ya miaka 150 iliyopita.
  • 13:19 - 13:22
    pamoja na mmezaji panga huko London
    aliyetoboa moyo wake kwa panga
  • 13:23 - 13:25
    Tulijifunza pia kuwa kuna kesi tatu hadi nane za
  • 13:25 - 13:28
    madhara mkubwa ya umezaji panga
    kila mwaka.
  • 13:28 - 13:30
    Najua kwa sababu mimi hupata simu.
  • 13:30 - 13:31
    Nilikuwa na wawili,
  • 13:31 - 13:34
    mmoja kutoka Sweden, na kutoka Orlando
    wiki chache zilizopita,
  • 13:34 - 13:37
    wamezaji panga waliopo hospitalini
    kutokana na madhara.
  • 13:37 - 13:39
    Kwa hiyo ni hatari sana.
  • 13:39 - 13:42
    Jambo jingine nililojifunza ni kuwa
    kumeza panga huchukua
  • 13:42 - 13:44
    miaka 2 hadi miaka 10
    kujifunza jinsi ya kumeza panga
  • 13:44 - 13:46
    kwa watu wengi.
  • 13:46 - 13:48
    Lakini ugunduzi unaovutia sana
    Nilijifunza ilikuwa
  • 13:48 - 13:51
    jinsi wameza panga wanavyojifunza
    kufanya yasiyowezekana.
  • 13:51 - 13:53
    Nami nitawapa siri ndogo:
  • 13:54 - 13:58
    Usizingatie kwenye asilimia 99.9
    kuwa haiwezekani.
  • 13:58 - 14:02
    Unazingatia hiyo 1% ambayo inawezekana,
    na fikiria jinsi ya kufanya iwezeikane
  • 14:03 - 14:06
    Sasa napenda kukupeleka kwenye safari
    ndani ya akili ya mmeza panga.
  • 14:06 - 14:09
    Ili kumeza panga,
    inahitaji akili itafakari jambo,
  • 14:09 - 14:12
    uzingativu wa hali ya juu,
    kuonyesha ufasaha ili
  • 14:12 - 14:16
    kutenganisha viungo vya ndani vya mwili
    na kushinda vitendo hiari mwilini
  • 14:16 - 14:20
    kupitia njia ya ubongo iliyoimarishwa,
    kupitia marido ya kumbukumbu ya misuli
  • 14:20 - 14:24
    kwa mazoezi ya makusudi
    zaidi ya mara 10,000.
  • 14:24 - 14:28
    Sasa ngoja niwasafirishe kidogo
    ndani ya mwili wa mmeza panga
  • 14:28 - 14:30
    Ili kumeza panga,
  • 14:30 - 14:32
    Lazima niteleze panga juu ya ulimi wangu,
  • 14:32 - 14:35
    nizuie kutaka kutapika
    kwenye shingo ya umio,
  • 14:35 - 14:38
    zungusha mgeuko wa nyuzi 90
    chini ya gegedu ya ulimi,
  • 14:38 - 14:41
    pitia kwenye msuli juu ya kilinda umio,
  • 14:41 - 14:43
    zuia vitendohiari vya tumbo,
  • 14:43 - 14:44
    telezea makali kwenye shimo la kifua
  • 14:44 - 14:46
    kati ya mapafu.
  • 14:46 - 14:48
    Katika hatua hii,
  • 14:48 - 14:50
    Lazma kweli nisukume moyo wangu pembeni.
  • 14:50 - 14:52
    Ikiwa utaangalia kwa makini,
  • 14:52 - 14:54
    unawezaona moyo ukidunda kwa panga langu
  • 14:54 - 14:56
    kwa sababu linaegemea moyo
  • 14:56 - 14:59
    ikitenganishwa na karibu thumuni ya inchi
    ya tishu ya umio.
  • 14:59 - 15:01
    Hicho sio kitu unaweza kudanganya.
  • 15:01 - 15:03
    Kisha hutelezesha
    kupita mfupa wa kifua,
  • 15:03 - 15:06
    kupita kilinda umio,
    chini ndani ya tumbo,
  • 15:06 - 15:09
    zuia vitendohiari ndani ya tumbo
    njia yote hadi kwenye mbuti.
  • 15:09 - 15:10
    Rahisi sana.
  • 15:10 - 15:11
    (Kicheko)
  • 15:11 - 15:13
    Kama ningetakiwa kwenda zaidi ya hapo,
  • 15:13 - 15:18
    hadi kufikia mirija yangu ya mayai.
    mirija ya mayai! (Kidachi)
  • 15:18 - 15:21
    Wanaume, mnaweza kuwauliza wake zenu
    kuhusu hiyo baadaye ...
  • 15:22 - 15:24
    Watu huniuliza, wanasema,
  • 15:24 - 15:27
    "lazima kuchukua ujasiri mwingi
    ili kuhatarisha maisha yako,
  • 15:27 - 15:29
    kusogeza moyo wako,
    na kumeza panga ... "
  • 15:29 - 15:30
    Hapana. Kinachofanya ujasiri halisi
  • 15:30 - 15:33
    ni kwa yule kijana mwoga, mwenye aibu,
    mwembamba
  • 15:33 - 15:36
    kwa kuhatarisha kushindwa na kukataliwa,
  • 15:36 - 15:37
    kufungua moyo wake,
  • 15:37 - 15:38
    na kumeza kiburi chake
  • 15:38 - 15:41
    na kusimama hapa mbele
    ya kundi la watu asiowafahamu kabisa
  • 15:41 - 15:44
    na kukuambia hadithi yake
    kuhusu hofu na ndoto zake,
  • 15:44 - 15:48
    kwa hatarisha kumwaga habari zake,
    vyote kihalisia na kitamathali.
  • 15:48 - 15:49
    Unaona - asante.
  • 15:49 - 15:54
    (Makofi)
  • 15:54 - 15:56
    Unaona, jambo la kustaajabisha sana ni
  • 15:56 - 15:59
    Nimetaka kufanya mambo
    ya kusifika maishani mwangu
  • 15:59 - 16:00
    na sasa nimesifika.
  • 16:00 - 16:03
    Lakini jambo la kusifika haswa
    sio kwamba ninaweza kumeza
  • 16:03 - 16:05
    panga 21 kwa mara moja,
  • 16:08 - 16:10
    au futi 20 chini ya maji kwenye tanki
    la papa 88 na taa
  • 16:10 - 16:12
    kwa kitabu cha Amini au Usiamini,
  • 16:14 - 16:18
    au kuchowa hadi kuwa mwekundu nyuzi 1500
    kwa Watu jasiri wa Stan Lee
  • 16:18 - 16:19
    kama "Mtu wa Chuma"
  • 16:20 - 16:22
    na yule jamaa alikuwa moto!
  • 16:22 - 16:25
    Au kuvuta gari kwa upanga kwa Ripley,
  • 16:25 - 16:26
    au Guinness,
  • 16:26 - 16:29
    au kufikia fainali za
    shindano la vipaji Marekani,
  • 16:29 - 16:32
    au kushinda 2007
    tuzo ya Ig Nobel katika Utabibu.
  • 16:32 - 16:34
    La, hilo sio
    jambo la kusifika sana.
  • 16:34 - 16:36
    Hivyo ndio watu wanafikiria.
    La, la, la. Sio hivyo.
  • 16:36 - 16:38
    Jambo la kusifika sana
  • 16:38 - 16:41
    ni Mungu angemchukua kijana,
    mwoga, mwenye aibu mwembamba
  • 16:41 - 16:42
    aliyehofia vimo virefu,
  • 16:42 - 16:44
    aliyehofia ya maji na papa,
  • 16:44 - 16:46
    na madaktari na manesi
    na sindano na vyenye ncha kali
  • 16:46 - 16:48
    na kuzungumza na watu
  • 16:48 - 16:50
    na sasa ananifanya
    nipae duniani kote
  • 16:50 - 16:51
    katika kina cha futi 30,000
  • 16:51 - 16:54
    kumeza vitu vya ncha
    chini ya maji ya tanki ya papa,
  • 16:54 - 16:57
    na kuzungumza na madaktari na wauguzi
    na hadhira kama ninyi duniani
  • 16:57 - 17:00
    Hilo ni jambo la kustaajabu sana kwangu.
  • 17:00 - 17:01
    Nimetaka kufanya mambo yasiyowezekana -
  • 17:01 - 17:02
    Asante.
  • 17:02 - 17:04
    (Makofi)
  • 17:04 - 17:05
    Asante.
  • 17:06 - 17:09
    (Makofi)
  • 17:10 - 17:13
    Sikuzote nilitaka kufanya yasiyowezekana,
    na sasa nimeweza.
  • 17:13 - 17:16
    Nilitaka kufanya kitu cha kusifika
    maishani na kubadilisha ulimwengu,
  • 17:16 - 17:17
    na sasa nimeweza.
  • 17:17 - 17:20
    Siku zote nilitaka kupaa duniani kote
    kufanya vitendo vigumu
  • 17:20 - 17:21
    na kuokoa maisha, sasa nimeweza.
  • 17:21 - 17:23
    Na unajua nini?
  • 17:23 - 17:26
    Bado kuna sehemu ndogo
    ya ndoto kubwa ya yule mtoto mdogo
  • 17:26 - 17:27
    ndani kabisa.
  • 17:30 - 17:36
    (Kicheko) (Makofi)
  • 17:37 - 17:40
    Na unajua, sikuzote nilitaka kupata
    kusudi langu na wito wangu,
  • 17:40 - 17:42
    na sasa nimepata.
  • 17:42 - 17:43
    Lakini nadhani nini?
  • 17:43 - 17:46
    Si kwa panga,
    sio unavyofikiria, si kwa nguvu zangu.
  • 17:46 - 17:49
    Ni kwa udhaifu wangu, maneno yangu.
  • 17:49 - 17:51
    Kusudi langu na wito
    ni kubadili ulimwengu
  • 17:51 - 17:52
    kwa kukata kupitia hofu,
  • 17:52 - 17:55
    upanga mmoja kwa wakati, neno moja
    kwa wakati,
  • 17:55 - 17:57
    kisu moja kwa wakati, maisha kwa wakati,
  • 17:58 - 18:00
    kuhamasisha watu kuwa mashujaa
  • 18:00 - 18:02
    na kufanya yasiyowezekana maishani mwao.
  • 18:02 - 18:05
    Kusudi langu ni kusaidia wengine
    kupata yao.
  • 18:05 - 18:06
    La kwako ni lipi?
  • 18:06 - 18:07
    Nini kusudi lako?
  • 18:07 - 18:09
    Uliwekwa kufanya nini hapa?
  • 18:09 - 18:12
    Naamini sisi wote
    tumeitwa kuwa mashujaa.
  • 18:12 - 18:14
    Nguvu yako kubwa ni nini?
  • 18:15 - 18:18
    Kati ya idadi ya watu duniani
    ya watu zaidi ya bilioni 7,
  • 18:18 - 18:20
    kuna wameza upanga
    wachache sana
  • 18:20 - 18:22
    waliobakia duniani kote leo,
  • 18:22 - 18:23
    lakini kuna wewe mmoja.
  • 18:23 - 18:24
    Wewe ni wa pekee.
  • 18:24 - 18:26
    Hadithi yako ni nini?
  • 18:26 - 18:28
    Nini kinakufanya uwe tofauti?
  • 18:28 - 18:29
    Simulia hadithi yako,
  • 18:29 - 18:32
    hata kama sauti yako ni nyembamba
    na inatetemeka.
  • 18:32 - 18:33
    Je, thromu zako ni nini?
  • 18:33 - 18:36
    kama ungefanya chochote,
    kuwa yeyote, kwenda popote -
  • 18:36 - 18:37
    Ungefanya nini?
    Ungekwenda wapi?
  • 18:37 - 18:38
    Ungefanya nini?
  • 18:38 - 18:40
    Unataka kufanya nini na maisha yako?
  • 18:40 - 18:42
    Nini ndoto zako kubwa?
  • 18:42 - 18:44
    Nini ndoto zako kubwa ulipokuwa mdogo?
    Fikiria tena
  • 18:44 - 18:46
    Nina uhakika hii haikuwa hivyo, si ndiyo?
  • 18:46 - 18:48
    Nini zilikuwa ndoto zako
    kuu
  • 18:48 - 18:50
    ulizofikiri zilikuwa ajabu sana
    na zisizoeleweka?
  • 18:50 - 18:54
    Hakika hii inafanya ndoto zako zisionekane
    za ajabu tena, sivyo?
  • 18:55 - 18:57
    Upanga wako ni nini?
  • 18:57 - 18:59
    Kila mmoja wenu ana upanga,
  • 18:59 - 19:01
    upanga wa pande mbili wa hofu na ndoto.
  • 19:01 - 19:04
    Meza upanga wako, chochote utachokuwa.
  • 19:04 - 19:06
    Fuata ndoto zako, mabibi na mabwana,
  • 19:06 - 19:09
    Hujachelewa sana kuwa
    chochote unataka kuwa.
  • 19:10 - 19:13
    Kwa wale waonevu na mipira ya kukwepa,
    wale watoto waliodhani
  • 19:13 - 19:15
    kuwa sitaweza kufanya yasiyowezekana,
  • 19:15 - 19:18
    Nina kitu kimoja tu cha kuwaambia:
  • 19:18 - 19:19
    Asanteni.
  • 19:19 - 19:22
    Kwa sababu kama si kwa wahalifu,
    tusingekuwa kuwa na mashujaa.
  • 19:23 - 19:27
    Nipo hapa kuthibitisha
    yasiyowezekana si hayawezekani.
  • 19:28 - 19:32
    Hii ni hatari sana,
    Inaweza kuniua.
  • 19:32 - 19:34
    Natumaini mtafurahia.
  • 19:34 - 19:35
    (Kicheko)
  • 19:36 - 19:39
    Nitahitaji msaada wenu kwenye hili.
  • 19:47 - 19:48
    Hadhira:Mbili, tatu.
  • 19:48 - 19:52
    Dan Meyer:La, la, la. Nahitaji msaada wenu
    kwenye kuhesabu, nyote, sawa?
  • 19:52 - 19:53
    (Vicheko)
  • 19:53 - 19:56
    Kama unajua maneno? Sawa?
    Hesabu na mimi. Tayari?
  • 19:56 - 19:57
    Moja.
  • 19:57 - 19:58
    Mbili.
  • 19:58 - 19:59
    Tatu.
  • 19:59 - 20:01
    La, hiyo ni 2, lakini mmeelewa
  • 20:07 - 20:08
    Hadhira: Moja.
  • 20:08 - 20:09
    Mbili.
  • 20:09 - 20:10
    Tatu.
  • 20:11 - 20:13
    (Vuta pumzi)
  • 20:14 - 20:16
    (Makofi)
  • 20:16 - 20:17
    DM: Ndiyo!
  • 20:17 - 20:23
    (Makofi) (Kushangilia)
  • 20:23 - 20:25
    Asanteni sana.
  • 20:25 - 20:29
    Asante, asante, asante.
    Asante kutoka kina cha moyo wangu
  • 20:29 - 20:31
    Kweli, asante
    kutoka chini ya tumbo langu.
  • 20:32 - 20:35
    Niliwaambia nimekuja hapa kufanya
    yasiyowezekana, na sasa nimeweza.
  • 20:35 - 20:38
    Ila hii haikuwa isiyowezekana.
    Ninafanya hivi kila siku.
  • 20:38 - 20:43
    Kitu kisichowezekana ilikuwa yule mwoga,
    mwenye aibu mwembamba kukabili hofu zake
  • 20:43 - 20:45
    kusimama hapa kwenye jukwaa la [TEDx],
  • 20:45 - 20:47
    na kubadilisha dunia,
    neno moja kwa wakati,
  • 20:47 - 20:49
    upanga kwa wakati, maisha kwa wakati.
  • 20:49 - 20:52
    kama nimekufanya ufikiri kwa njia mpya,
    kama nimekufanya uamini
  • 20:52 - 20:54
    yasiyowekana si hayawezekani,
  • 20:54 - 20:58
    ikiwa nimekufanya uelewe kuwa waweza
    fanya yasiyowezekana maishani mwako,
  • 20:58 - 21:01
    basi kazi yangu imekwisha,
    na yako ndiyo kwanza imeanza.
  • 21:01 - 21:04
    Usiache kuwa na ndoto. Usiache kuamini.
  • 21:05 - 21:06
    Asanteni kwa kuniamini
  • 21:06 - 21:08
    na asanteni kuwa sehemu
    ya ndoto yangu.
  • 21:08 - 21:10
    Hii ni zawadi kwenu:
  • 21:10 - 21:11
    Yasiyowezekana si ...
  • 21:11 - 21:13
    Hadhira: Hayawezekani.
  • 21:13 - 21:15
    Mwendo mrefu ni sehemu ya zawadi.
  • 21:15 - 21:20
    (Makofi)
  • 21:20 - 21:21
    Asanteni.
  • 21:21 - 21:25
    (Makofi)
  • 21:26 - 21:28
    (Kushangilia)
  • 21:28 - 21:31
    Mwenyeji: Asante, Dan Meyer, wow!
Title:
Kufanya yasiyowezekana, kuishinda hofu| Dan Meyer | TEDxMaastricht
Description:

Umewahi kutaka kuwa shujaa na kufanya yasiyowezekana? Dan Meyer anaamini haijalishi tuna hofu kiasi gani au kiasi gani ndoto zetu hazitimiziki, kila mmoja ana uwezo wa kuwa shujaa, kufanya yasiyowezekana na kuubadilisha ulimwengu. Mkurugenzi wa shirika la msaada ya kuwasaidia watoto yatima nchini Kazakhstan, Dan anasimulia jinsi alivyoishinda hofu, ugonjwa wa hofu ya ukaribu na watu na unyanyaswaji akiwa mtoto na kufanya maajabu, na kuwa mshindani wa fainali wa shindano la vipaji la Marekani, kushinda Tuzo ya Nobel ya 2007 katika Utabibu huko Harvard , na kuwa mmiliki wa rekodi ya dunia 39x katika sanaa ya Kumeza Upanga - na shauku ya kutoa msukumo kwa watu kufanya yasiyowezekana katika maisha YAO.

Katika mazungumzo yake ya kwanza TED talk, Dan anaichukua hadhira kwenye safari yake ndefu kutokea kwenye hofu kupita kiasi hadi mambo ya kijasiri kupita kiasi, mwoga kwa mshika rekodi ya dunia, mkosaji kwa mshindi wa Tuzo ya Nobel na mkataji tamaa wa mshindani wa fainali wa shindano la Vipaji Marekani. Dan anaelezea sayansi nyuma ya sanaa ya kale ya umezaji wa upanga, na kuelekezea uchunguzi wake katika ujasiri wa kishujaa, kudhibiti kushindwa na mipaka ya mwili wa binadamu kufanya yasiyowezekana na kuibadilisha dunia. Na anatuelezea dondoo za jinsi ya kuishinda hofu kufanya yasiyowezekana maishani MWAKO!
Mjadala huu ulitolewa kwenye mihadhara ya ndani ya TEDx, iliyoandaliwa kibinafsi mbali na makongamano ya TED.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDxTalks
Duration:
21:38

Swahili subtitles

Revisions