Njia isiyo na mwiko kuongelea kuhusu siku za hedhi
-
0:01 - 0:02Siku.
-
0:02 - 0:03Damu.
-
0:04 - 0:05Hedhi.
-
0:05 - 0:07Uchafu.
-
0:07 - 0:09Siri.
-
0:09 - 0:10Kuficha.
-
0:10 - 0:12Kwanini?
-
0:13 - 0:15Utaratibu asilia kibaolojia
-
0:15 - 0:18ambao kila msichana na mwanamke
anapitia kila mwezi -
0:19 - 0:21kwa karibia nusu ya maisha yake.
-
0:21 - 0:23Jambo ambalo ni la umuhimu mkubwa sana
-
0:23 - 0:28kiasi kwamba kupona na uenezwaji
wa spishi zetu unautegemea. -
0:28 - 0:30Bado tunauchukulia kama mwiko.
-
0:31 - 0:34Tunajisikia ugumu
na fedheha kuliongelea. -
0:36 - 0:38Nilipopata siku zangu mara ya kwanza,
-
0:38 - 0:40Niliambiwa nifanye iwe
siri nisiwaambie wengine-- -
0:41 - 0:43hata kwa baba yangu au kaka.
-
0:44 - 0:46Baadaye wakati hili somo
limejitokeza vitabuni mwetu, -
0:46 - 0:49mwalimu wetu wa baolojia aliiruka mada.
-
0:49 - 0:51(Kicheko)
-
0:52 - 0:54Nilijifunza nini kutokana na hili?
-
0:54 - 0:58Nilijifunza kwamba
ni fedheha mno kuongelea jambo hili. -
0:58 - 1:01Nilijifunza kufedheshwa na mwili wangu.
-
1:01 - 1:04Nilijifunza kutokufahamu siku zangu
-
1:04 - 1:06ili kuweza kubaki na heshima.
-
1:06 - 1:08Utafiti katika sehemu mbalimbali India
-
1:08 - 1:13waonyesha wasichana watatu kati ya kumi
hawafahamu kuhusu hedhi -
1:13 - 1:15wakati wa siku zao za kwanza.
-
1:15 - 1:17Na baadhi ya sehemu za Rajasthan
-
1:17 - 1:22hii namba ni kubwa kama wasichana tisa
kati ya kumi kutokufahamu -
1:23 - 1:24Unaweza kushangazwa kujua
-
1:24 - 1:27kwamba wasichana wengi
nilioongea nao, -
1:27 - 1:31waliokuwa hawajui kuhusu siku zao
wakati wa hedhi zao za kwanza -
1:31 - 1:33walifikiria kuwa wana saratani ya damu
-
1:33 - 1:35na watakufa muda sio mrefu.
-
1:37 - 1:40Usafi wa hedhi
ni kipengele muhimu cha hatari -
1:40 - 1:42kwa maambukizi wa mfumo wa via vya uzazi.
-
1:43 - 1:46Lakini India, ni asilimia 12 tu
ya wasichana na wanawake -
1:46 - 1:50wanaweza kupata njia za usafi
wa kumudu siku zao. -
1:51 - 1:52Ukifanya mahesabu,
-
1:52 - 1:57asilimia 88 ya wasichana na wanawake
hutumia njia zisizo salama kwa siku zao. -
1:57 - 1:59Nilikuwa mmoja wao.
-
2:00 - 2:03Nilikulia kwenye mji mdogo
uitwao Garhwa, jimbo la Jharkhand, -
2:03 - 2:06ambako hata kununua pedi
ilichukuliwa kama fedheha. -
2:07 - 2:09Sasa nilipoanza kupata siku zangu,
-
2:09 - 2:11Nilianza kutumia matambara.
-
2:13 - 2:15Baada ya kila matumizi
niliyafua na kuyatumia tena. -
2:15 - 2:16Lakini kuyahifadhi,
-
2:17 - 2:19Niliyaficha na kuyaweka
sehemu yenye giza na unyevu -
2:19 - 2:22ilikwamba mtu asijue
kuwa niko kwenye hedhi. -
2:23 - 2:25Kwa kuyarudia kufua
matambara yalikuja kuwa magumu, -
2:25 - 2:28na mara nyingi nilipata upele
na maambukizi kwa kuyatumia. -
2:29 - 2:33Niliyavaa kwa muda wa miaka mitano
hadi nilipohama ule mji. -
2:36 - 2:38Suala lingine
ambalo siku zilileta maishani mwangu -
2:38 - 2:40lile la kuwekewa mipaka kijamii
-
2:40 - 2:45iliyowekwa kwa wasichana wetu
na wanawake wakiwa kwenye siku zao. -
2:45 - 2:47Nafikiri wote lazma mtakuwa mnajua,
-
2:47 - 2:50lakini bado nitaelezea
kwa wale wachache wasiojua. -
2:51 - 2:53Sikuruhusiwa kula au kugusa vitu vichachu.
-
2:54 - 2:59Sikuruhusiwa kukaa kwenye sofa
au kitandani mwa ndugu wa familia. -
2:59 - 3:01Nilitakiwa kufua mashuka
kila baada ya siku zangu, -
3:01 - 3:03hata kama hazikuchafuka kwa madoa.
-
3:03 - 3:05Nilichukuliwa kama najisi
-
3:05 - 3:10na kukatazwa kuabudu au kugusa
kitu chochote chenye umuhimu kidini. -
3:11 - 3:13Ulikutana na matangazo nje ya misikiti
-
3:13 - 3:16kukataza wasichana
na wanawake walio kwenye hedhi. -
3:17 - 3:18Chakuchekesha,
-
3:18 - 3:21wakati wote ni wanawake watu wazima
-
3:21 - 3:26ndio walioweka vizuizi hivyo
kwa wasichana wadogo katika familia. -
3:26 - 3:31hata hivyo, wamekua
wakikubali vizuizi hivyo kama desturi. -
3:31 - 3:34Na katika kukosekana kwa kuingiliwa,
-
3:34 - 3:36ni imani potofu na kutoeleweka
-
3:36 - 3:38kunakoenezwa
kizazi hata kizazi. -
3:39 - 3:41Kwa miaka nilyofanyia kazi
taaluma hii, -
3:41 - 3:43Nimeshakutana na hadithi
-
3:43 - 3:46ambapo wasichana walitakiwa kula
na kuosha vyombo vyao kwa kutengwa. -
3:46 - 3:49Hawakuruhusiwa
kuoga wakati wa siku zao, -
3:49 - 3:53na katika nyumba nyingine walitengwa
hata na ndugu wengine wa familia. -
3:54 - 3:57Kiasi cha asilimia 85 za wasichana
na wanawake India -
3:57 - 4:03walifuata moja au zaidi ya masharti
ya mila kwenye siku zao kila mwezi. -
4:03 - 4:05Unafikiria hii inafanya nini
-
4:05 - 4:08katika kujithamini
na kujiamini kwa msichana mdogo? -
4:09 - 4:11Kiwewe cha kisaikolojia
ambacho hili huumiza, -
4:11 - 4:14kuathiri haiba yake,
-
4:14 - 4:16utendaji wake kimasomo
-
4:16 - 4:20na kila kipengele cha ukuaji
katika miaka ya awali ya uumbaji wake? -
4:22 - 4:26Nilifuata kwa bidii masharti haya yote
ya kimila kwa miaka 13, -
4:26 - 4:29hadi mjadala na mshirika mwenzangu, Tuhin,
-
4:29 - 4:31ulipobadilisha mtazamo wangu
kuhusu hedhi milele. -
4:32 - 4:38Mwaka 2009, mimi na Tuhin tulikuwa
tunasoma stashada katika ubunifu. -
4:38 - 4:39Tukapendana
-
4:39 - 4:42na nilikuwa huru
kujadiliana naye kuhusu siku zangu. -
4:43 - 4:45Tuhin alijua kidogo kuhusu siku.
-
4:46 - 4:48(Kicheko)
-
4:52 - 4:55Alishangazwa kujua kwamba
wasichana hupata maumivu makali -
4:55 - 4:57na hutokwa damu kila mwezi.
-
4:57 - 4:59(Kicheko)
-
4:59 - 5:00Ndio.
-
5:01 - 5:02Alishtushwa kabisa kujua
-
5:02 - 5:07kuhusu vizuizi vinavyowekwa kwa
wasichana na wanawake walio kwenye hedhi -
5:08 - 5:10na familia pamoja na jamii zao wenyewe.
-
5:10 - 5:12Ili kuweza kunisaidia na maumivu yangu,
-
5:12 - 5:16alikwenda kwenye mtandao wa intaneti
kujifunza kuhusu hedhi. -
5:17 - 5:18Aliponielezea alichojifunza,
-
5:18 - 5:21Niligundua ufahamu mdogo
nilionao kuhusu hedhi, -
5:22 - 5:25na vitu vingi nilivyoamini
vilikuja kuwa ni imani potofu, -
5:26 - 5:28Ndipo nilipojiuliza:
-
5:28 - 5:30kama sisi, tumesoma vizuri hivi,
-
5:30 - 5:32tumefundishwa vibaya kuhusu hedhi,
-
5:32 - 5:36kutakuwa na mamilioni ya wasichana huko
nje waliofundishwa vibaya, pia. -
5:38 - 5:39Kusoma--
-
5:39 - 5:41kuelewa tatizo vizuri,
-
5:41 - 5:45Nilifanya utafiti wa mwaka mmoja kujifunza
ukosefu wa ufahamu kuhusu hedhi -
5:45 - 5:47na chanzo chake nyuma yake.
-
5:48 - 5:50Wakati kiujumla inaaminika
-
5:50 - 5:56kwamba kutokufahamu hedhi na
kuelewa vibaya ni tatizo la vijijini, -
5:56 - 5:57katika utafiti wangu,
-
5:57 - 6:00Niligundua kwamba
ni tatizo la mijini pia. -
6:00 - 6:04Na lipo kwa daraja la walioelimika
mijini, pia. -
6:05 - 6:08Wakati naongea na wazazi wengi
pamoja na waalimu, -
6:08 - 6:13Niligundua kuwa wengi wao walitaka
kuelimisha wasichana kuhusu siku zao -
6:13 - 6:16kabla hawajaanza
kupata mzunguko wao wa hedhi. -
6:17 - 6:18Na--
-
6:18 - 6:22lakini wenyewe walikosa
njia stahiki. -
6:22 - 6:23Na kwavile ni mwiko,
-
6:23 - 6:26wanajisikia kusita
na fedheha kuongelea jambo hilo. -
6:27 - 6:31Wasichana siku hizi hupata siku zao
wakiwa darasa la sita na la saba, -
6:31 - 6:33lakini mtaala wetu wa elimu
-
6:33 - 6:37hufundisha wasichana kuhusu siku zao
darasa la nane na la tisa tu. -
6:38 - 6:39na kwa vile ni mwiko,
-
6:40 - 6:43waalimu bado
wanairuka mada. -
6:45 - 6:49Hivyo shule haziwafundishi
wasichana kuhusu siku zao, -
6:49 - 6:51wazazi hawazungumzii jambo hilo.
-
6:51 - 6:53Wasichana wanaenda wapi?
-
6:54 - 6:57Miongo miwili iliyopita na sasa--
-
6:57 - 6:58hakuna kilichobadilika.
-
7:00 - 7:03Nilimshirikisha Tuhin matokeo yangu
na tulijiuliza -
7:03 - 7:05Itakuwaje tukianzisha kitu
-
7:05 - 7:09ambacho kitasaidia wasichana kuelewa
kuhusu hedhi wao wenyewe -- -
7:09 - 7:13Kitu ambacho kitawasaidia
wazazi na waalimu -
7:13 - 7:16kuongelea kuhusu siku za hedhi
kwa raha kwa wasichana wadogo? -
7:18 - 7:19Wakati wa utafiti wangu,
-
7:19 - 7:21Nilikuwa nakusanya hadithi nyingi.
-
7:21 - 7:26Hizi ni hadithi za mambo waliyopitia
wasichana kipindi cha siku zao. -
7:27 - 7:30Hadithi hizi zitawafanya wasichana
wawe wadadisi na kuvutiwa -
7:30 - 7:34katika kuongea kuhusu hedhi
ndani ya watu wao wa karibu. -
7:34 - 7:35Hicho ndio tulichotaka.
-
7:36 - 7:39Tulitaka kitu ambacho
kingewafanya wasichana wawe wadadisi -
7:39 - 7:41na kuwasukuma kujifunza.
-
7:41 - 7:44Tulitaka kutumia hadithi hizi
kufundisha wasichana kuhusu siku zao. -
7:45 - 7:48Hivyo tukaamua kutengeneza kitabu
cha vikatuni -
7:48 - 7:52ambapo wahusika wa katuni
wataigiza hadithi hizi -
7:52 - 7:56na kuwaelimisha wasichana kuhusu hedhi
kwa njia ya kufurahisha na kuwashirikisha. -
7:56 - 7:59Kuwasilisha wasichana
katika hatua zao tofauti za kubalehe, -
7:59 - 8:01tunao wahusika watatu.
-
8:02 - 8:05Pinki, ambaye hajapata siku zake bado,
-
8:05 - 8:08Jiya anayepata siku zake
wakati wa simulizi za kitabu -
8:08 - 8:12na Mira ambaye tayari
amekuwa akipata siku zake. -
8:12 - 8:14Kuna mhusika wa nne, Priya Didi.
-
8:14 - 8:18Kupitia yeye, wasichana wanakuja kujua
kuhusu vipengele kadhaa vya ukuaji -
8:18 - 8:19na kusimamia usafi wa hedhi.
-
8:20 - 8:22Utengenezaji kitabu,
ulitumia umakini -
8:22 - 8:26hakuna katika vielelezo ambavyo
vilikuwa na pingamizi lolote -
8:26 - 8:28na hiyo ni nyeti kitamaduni.
-
8:29 - 8:33Wakati wa majaribio ya sampuli ya awali
tuligundua wasichana wakilipenda kitabu. -
8:33 - 8:34Walikuwa na hamu ya kukisoma
-
8:34 - 8:37na kujua zaidi na zaidi
kuhusu siku zao wao wenyewe. -
8:38 - 8:41Wazazi na waalimu walikuwa
hawaoni shida kuongea kuhusu siku -
8:41 - 8:43kwa wasichana wadogo kutumia kitabu
-
8:43 - 8:46na wakati mwingine hata wavulana
walivutiwa kukisoma. -
8:46 - 8:48(Kicheko)
-
8:48 - 8:50(Makofi)
-
8:52 - 8:56Kitabu cha vikatu kilisaidia
katika kujenga mazingira -
8:56 - 8:58ambapo itasimamisha hedhi kuwa mwiko.
-
8:59 - 9:03Wengi wa waliojitolea walichukua hii
sampuli ya awali kuelimisha wasichana -
9:03 - 9:07na kufanya warsha za kuelimisha hedhi
katika majimbo matano tofauti India. -
9:07 - 9:10na mmoja wa waliojitolea alitumia
sampuli hii kuelimisha watawa vijana -
9:10 - 9:12na aliipeleka kwenye nyumba ya utawa
Ladakh. -
9:12 - 9:16Tulitengeneza toleo la mwisho la kitabu,
tukakiita "Menstrupedia Comic" -
9:16 - 9:19na kukizindua Septemba mwaka jana.
-
9:19 - 9:20Na mpaka sasa,
-
9:21 - 9:25zaidi ya wasichana 4,000 wameelimika
kwa kutumia kitabu India na -- -
9:25 - 9:28(Makofi)
-
9:28 - 9:29Asanteni.
-
9:29 - 9:31(Makofi)
-
9:34 - 9:36na nchi nyingine 10.
-
9:37 - 9:40Mara kwa mara tunakitafsiri kitabu
katika lugha tofauti -
9:40 - 9:43Na kushirikiana na mashirika ya ndani
nchi -
9:43 - 9:46na kufanya hiki kitabu kipatikane
katika nchi tofauti. -
9:46 - 9:49Mashule 15 katika sehemu tofauti India
-
9:49 - 9:52yamekifanya kitabu hiki
kuwa sehemu ya mtaala wa shule zao -
9:52 - 9:54kufundisha wasichana kuhusu hedhi.
-
9:54 - 9:56(Makofi)
-
10:00 - 10:06Nafurahishwa kuona jinsi wanaojitolea,
-
10:06 - 10:10watu binafsi, wazazi
waalimu, wakuu wa mashule -
10:10 - 10:11wamekutana pamoja
-
10:11 - 10:16na kufanya msukumo huu wa ufahamishaji
wa hedhi kwa jamii zao, -
10:16 - 10:19wamehakikisha wasichana wanajifunza
kuhusu siku zao katika umri sahihi -
10:19 - 10:22na kusaidia katika kuvunja mwiko huu
-
10:23 - 10:27Ninaota maisha ya mbele
ambapo hedhi sio laana, -
10:27 - 10:29sio ugonjwa,
-
10:29 - 10:31ila ni mabadiliko katika
maisha ya msichana. -
10:32 - 10:33Na ninge --
-
10:33 - 10:35(Makofi)
-
10:38 - 10:39Na ningependa kumalizia hii
-
10:39 - 10:43kwa ombi dogo
kwa wazazi wote hapa. -
10:43 - 10:44Wapendwa wazazi,
-
10:45 - 10:47kama mtakuwa mnafedheheshwa na hedhi
-
10:47 - 10:50na mabinti zenu watafedheheshwa, pia.
-
10:50 - 10:52Hivyo tafadhali muwe na mtazamo chanya
katika siku. -
10:52 - 10:53(Kicheko)
-
10:53 - 10:55Asanteni.
-
10:55 - 10:57(Makofi)
- Title:
- Njia isiyo na mwiko kuongelea kuhusu siku za hedhi
- Speaker:
- Aditi Gupta
- Description:
-
Ni kweli: kuongelea kuhusu hedhi kunafanya watu wengi wakose raha. Na mwiko huo una matokeo yake: nchini India, wasichana watatu kati ya 10 hawajui hata hedhi ni nini wakati wa siku zao za kwanza, na masharti ya mila yanayohusiana na siku za hedhi yanaleta uharibifu kisaikolojia kwa wasichana. Kukua katika mwiko huu mwenyewe, Aditi Gupta alijua anataka kusaidia wasichana, wazazi, waalimu kuzungumzia kuhusu siku za hedhi kwa raha bila aibu. Anatushirikisha alivyofanya.
- Video Language:
- English
- Team:
- closed TED
- Project:
- TEDTalks
- Duration:
- 11:10
Joachim Mangilima approved Swahili subtitles for A taboo-free way to talk about periods | ||
Joachim Mangilima accepted Swahili subtitles for A taboo-free way to talk about periods | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for A taboo-free way to talk about periods | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for A taboo-free way to talk about periods | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for A taboo-free way to talk about periods | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for A taboo-free way to talk about periods | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for A taboo-free way to talk about periods | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for A taboo-free way to talk about periods |