Return to Video

Nguvu inayoponya katika kusoma

  • 0:01 - 0:06
    Ninataka kuzungumza namna kusoma
    kunavyoweza kubadilisha maisha yetu
  • 0:06 - 0:09
    na kuhusu mipaka ya mabadiliko hayo
  • 0:10 - 0:14
    Ninataka kuzungumza na wewe namna kusoma
    kunavyoweza kutupa ulimwengu wa ushirika
  • 0:14 - 0:17
    wa muunganiko wenye nguvu wa kibinadamu
  • 0:18 - 0:21
    pia namna ambavyo muunganiko huo
    ni sehemu tu mara zote
  • 0:21 - 0:26
    Kusoma mwisho wa siku ni kitendo cha
    upweke na kisicho cha kawaida.
  • 0:28 - 0:30
    Muandishi aliyebadilisha maisha yangu
  • 0:30 - 0:35
    Ni mmarekani mweusi na mwandishi
    wa riwaya James Baldwin
  • 0:35 - 0:38
    Wakati ninakuwa katika eneo la
    Magharibi mwa Michigan miaka ya 1980,
  • 0:38 - 0:42
    hakukuwa na wamarekani wenye asili ya asia
    wengi wanaoandika kuhusu mabadiliko ya kijamii
  • 0:43 - 0:47
    Na ndio maana nilimgeukia James Baldwin
  • 0:47 - 0:51
    kama namna ya kuliziba hili ombwe,
    kama namna ya kuwamakini na rangi
  • 0:52 - 0:56
    lakini haswa kwa sababu nilifahamu
    mimi sikuwa mmarekani mweusi,
  • 0:56 - 1:00
    Pia nilisikia kupata changamoto na
    kuthibitishwa na maneno yake.
  • 1:00 - 1:03
    Hasusani maneno haya:
  • 1:03 - 1:07
    "Ni watu huria walio na mitazamo sahihi,
  • 1:07 - 1:09
    lakini hawana misimamo halisi.
  • 1:10 - 1:14
    pale ambapo vipande vipo chini
    na unawategemea kuleta matokeo,
  • 1:14 - 1:17
    na huenda hawako hapo kwa namna fulani".
  • 1:17 - 1:19
    Hawako hapo kwa namna fulani.
  • 1:19 - 1:22
    Nikayachukua hayo maneno nikitafakari.
  • 1:22 - 1:23
    Nijiweke wapi?
  • 1:24 - 1:27
    Nilikwenda kwenye delta ya Mississippi,
  • 1:27 - 1:30
    mojawapo ya maeneo masikini sana ya
    Marekani.
  • 1:30 - 1:33
    Hii ni sehemu ambayo imejengwa
    na historia yenye nguvu.
  • 1:33 - 1:38
    Katika mwaka wa 1960, Wamarekani weusi
    walijitoa maisha yao kupigania Elimu,
  • 1:38 - 1:40
    kupigania haki ya kupiga kura.
  • 1:41 - 1:43
    Nilitaka kuwa sehemu ya badiliko hilo,
  • 1:43 - 1:47
    kuwasaidia vijana wadogo wamalize shule
    na kujiunga na vyuo.
  • 1:48 - 1:51
    Nilipoenda kwenye Delta ya Mississipi,
  • 1:51 - 1:53
    Palikuwa ni mahali duni bado,
  • 1:53 - 1:55
    bado pametengwa,
  • 1:55 - 1:58
    Bado panahitaji mabadiliko ya kasi.
  • 1:59 - 2:02
    Shule yangu, pale nilipokuwa nasoma,
  • 2:02 - 2:07
    haikuwa na maktaba, hakuna mshauri,
  • 2:07 - 2:10
    lakini ilikuwa na afisa wa polisi.
  • 2:10 - 2:12
    Nusu ya walimu walikuwa ni mbadala
  • 2:12 - 2:14
    na wanafunzi walipoingia kwenye ugomvi,
  • 2:14 - 2:18
    Shule iliwapeleka kwenye jela ya
    mahali hapo.
  • 2:20 - 2:23
    Hii ndiyo shule nilipokutana na Patrick.
  • 2:23 - 2:28
    Alikuwa na miaka 15 na alikamatwa mara
    mbili, alikuwa darasa la nane.
  • 2:28 - 2:31
    Alikuwa ni mkimya na mndani,
  • 2:31 - 2:34
    ni kama kila wakati alikuwa mwenye mawazo.
  • 2:34 - 2:36
    Na alichukia kuona wengine wakipigana.
  • 2:38 - 2:41
    Nilimuona mara moja akiruka kati ya
    mabinti wawili walipokuwa wakipigana
  • 2:41 - 2:44
    Na akajikuta akidondoka na kuanguka chini.
  • 2:45 - 2:48
    Patrick alikuwa na tatizo moja.
  • 2:48 - 2:50
    Hakuwa akifika shuleni.
  • 2:51 - 2:54
    Alisema kuwa shule wakati mwingine humfanya kuwa na msongo
  • 2:54 - 2:57
    Sababu wanafunzi hupigana mara zote na
    walimu wanaondoka.
  • 2:58 - 3:04
    Lakini pia, mama yake anafanya kazi mbili
    na huwa anachoka kuweza kumfanya aje shule.
  • 3:04 - 3:07
    Hivyo nikafanya iwe kazi yangu
    kumfanya awe anakuja shule.
  • 3:07 - 3:11
    Na sababu nilikuwa na wazimu na miaka 22
    na mwenye bidii ya matumaini
  • 3:11 - 3:13
    Njia yangu ilikuwa ni
    kwenda nyumbani kwao
  • 3:13 - 3:16
    na kusema "Eti, kwanini hauji
    shuleni?"
  • 3:17 - 3:18
    Na njia hii ilifanya kazi,
  • 3:18 - 3:21
    akaanza kuja shuleni kila siku.
  • 3:21 - 3:23
    Na akaanza kufanikiwa katika darasa langu.
  • 3:23 - 3:26
    Aliandika mashairi,
    alisoma vitabu.
  • 3:27 - 3:29
    Alikuja shuleni kila siku.
  • 3:31 - 3:33
    takriban muda ule ule
  • 3:33 - 3:35
    Nilipogundua namna ya kushirikiana
    na Patrick,
  • 3:35 - 3:37
    Nilikwenda shule ya sheria Harvard.
  • 3:40 - 3:43
    Nilikutana tena na swali hili,
    nijiweke wapi,
  • 3:43 - 3:45
    niuweke wapi mwili wangu?
  • 3:45 - 3:48
    Na nikawaza mwenyewe
  • 3:48 - 3:52
    Kuwa Mississipi Delta
    ni mahali ambapo watu wenye fedha,
  • 3:52 - 3:54
    watu wenye fursa,
  • 3:54 - 3:55
    watu hao huondoka.
  • 3:56 - 3:57
    Na watu wanaobakia
  • 3:57 - 4:00
    ni watu ambao hawana fursa ya kuondoka.
  • 4:01 - 4:03
    Sikutaka kuwa mtu anayeondoka.
  • 4:03 - 4:05
    Nilitaka kuwa mtu anayebakia.
  • 4:06 - 4:09
    Kwa upande mwingine, nilikuwa mpweke
    na mchovu.
  • 4:09 - 4:13
    Na hivyo nilijishawishi mwenyewe
    kuwa ninaweza kufanya mabadiliko
  • 4:14 - 4:18
    Kwa kiasi kikubwa kama ningekuwa
    na shahada yenye heshima ya sheria.
  • 4:20 - 4:21
    Hivyo nikaondoka.
  • 4:23 - 4:24
    Miaka mitatu baadaye,
  • 4:24 - 4:27
    Nilipokaribia kuhitimu
    shule ya sheria,
  • 4:27 - 4:29
    rafiki yangu alinipigia simu
  • 4:29 - 4:33
    na kuniambia kuwa Patrick
    amepigana na kuua mtu.
  • 4:35 - 4:37
    Nilitaharuki.
  • 4:37 - 4:40
    Sehemu ya mimi haikuamini,
  • 4:40 - 4:43
    na sehemu ya mimi pia iliamini kuwa
    ni kweli.
  • 4:44 - 4:46
    Nilisafiri kwenda kumuona Patrick.
  • 4:47 - 4:49
    Nilimtembelea gerezani.
  • 4:51 - 4:54
    Na aliniambia kuwa ilikuwa kweli.
  • 4:54 - 4:57
    Ya kwamba ameua mtu.
  • 4:57 - 4:59
    Na asingependa kuzungumzia suala hilo.
  • 5:00 - 5:02
    Nilimuuliza nini kiliendelea kuhusu shule
  • 5:02 - 5:06
    na akasema aliacha shule mwaka mooja
    baada ya mimi kuondoka.
  • 5:06 - 5:09
    Na alitaka kuniambia kuhusu kitu kingine
  • 5:09 - 5:12
    Alitazama chini akasema
    ya kwamba amepata mtoto wa kike
  • 5:12 - 5:14
    ambaye ndiye kwanza amezaliwa.
  • 5:14 - 5:16
    Na anahisi kuwa amemuangusha binti yake.
  • 5:19 - 5:22
    Hivyo ndivyo ilivyokuwa, mazungumzo yetu
    yalikuwa ya haraka na mabaya.
  • 5:23 - 5:28
    Nilipotoka nje ya gereza,
    sauti ndani yangu iliniambia,
  • 5:28 - 5:30
    "Rudi.
  • 5:30 - 5:33
    Usiporudi sasa, hutarudi kamwe".
  • 5:36 - 5:40
    Hivyo nikahitimu shule ya sheria na
    nikarudi.
  • 5:41 - 5:43
    Nikarudi kumuona Patrick,
  • 5:43 - 5:46
    Nikarudi kuona kama ninaweza kumsaidia
    na kesi yake ya sheria.
  • 5:47 - 5:50
    Muda huu,
    nilipomuona kwa mara ya pili,
  • 5:50 - 5:53
    Nilidhani nina hili wazo zuri,
    nikamwambia,
  • 5:53 - 5:56
    "Hey, Patrick, kwanini usiandike barua
    kwa binti yako,
  • 5:56 - 6:00
    ili uweze kumuweka katika
    fikra zako?"
  • 6:00 - 6:04
    Nikampatia kalamu na
    kipande cha karatasi,
  • 6:04 - 6:05
    na akaanza kuandika.
  • 6:07 - 6:09
    Lakini nilipoiona karatasi aliyonipatia,
  • 6:09 - 6:11
    Nilipigwa na butwaa.
  • 6:13 - 6:15
    Sikuutambua mwandiko wake,
  • 6:15 - 6:18
    alikuwa amefanya makosa
    machache ya matamshi.
  • 6:19 - 6:22
    na nikawaza mwenyewe kama mwalimu,
  • 6:22 - 6:25
    Ninafahamu ya kuwa mwanafunzi
    anaweza kufanya vizuri kwa kasi
  • 6:25 - 6:28
    Kwa muda mfupi sana,
  • 6:28 - 6:32
    lakini sikuwahi kuwaza kuwa mwanafunzi
    anaweza kurudi nyuma kwa kasi.
  • 6:34 - 6:36
    kilichoniumiza zaidi,
  • 6:36 - 6:39
    ni kuona kile alichokiandika
    kwa binti yake.
  • 6:40 - 6:41
    aliandika,
  • 6:41 - 6:45
    "Ninasikitika kwa makosa yangu,
    ninasikitika kutokuwa pamoja nawe."
  • 6:46 - 6:49
    Na hiki ndicho alichojisikia
    anataka kusema naye.
  • 6:50 - 6:55
    Nikajiuliza ni namna gani ninaweza
    kumshawishi kuwa anaweza kumwambia zaidi,
  • 6:55 - 6:58
    ile sehemu yake ambayo
    hahitaji kuomba radhi kwayo.
  • 6:59 - 7:00
    Nilitaka yeye ajisikie
  • 7:00 - 7:04
    kuwa anakitu cha thamani
    kumshirikisha binti yake.
  • 7:06 - 7:09
    Kwa kila siku kwa miezi saba iliyofuatia,
  • 7:09 - 7:12
    Nilimtembelea na kumpelekea vitabu.
  • 7:12 - 7:16
    Mkoba wangu uligeuka kuwa maktaba ndogo.
  • 7:16 - 7:18
    Nilimpelekea James Baldwin,
  • 7:18 - 7:23
    Nilipeleka Walt Whitman, C.S.Lewis.
  • 7:23 - 7:28
    Nilileta vitabu vya mwongozo wa miti,
    wa ndege,
  • 7:28 - 7:31
    na kitabu alichotokea kukipenda zaidi,
    kamusi.
  • 7:32 - 7:33
    Kwa baadhi ya siku,
  • 7:33 - 7:37
    tulikaa kimya kwa masaa,
    wote wawili tukisoma.
  • 7:38 - 7:40
    Na siku nyingine,
  • 7:40 - 7:43
    tulisoma pamoja,
    tulisoma mashairi.
  • 7:44 - 7:47
    tulianza kwa kusoma haikus,
    mamia ya haikus,
  • 7:47 - 7:50
    ni kito rahisi na danganyifu.
  • 7:50 - 7:53
    Na ningemuuliza,
    "Nishirikishe haiku zako unazozipenda".
  • 7:53 - 7:56
    Na baadhi yake ni za kufurahisha sana.
  • 7:56 - 7:58
    Kuna hii ya Issa:
  • 7:58 - 8:02
    "Usijali, buibui,
    ninaweka nyumba kikawaida."
  • 8:03 - 8:07
    Na hii: "Nimelala nusu ya siku,
    na hakuna aliyeniadhibu!"
  • 8:09 - 8:13
    Na hii nyingine ya kuvutia, inayohusu
    siku ya kwanza barafu ilipodondoka,
  • 8:13 - 8:18
    "Kulungu wakilamba baridi ya kwanza
    kutoka kwenye koti la kila mmoja wao."
  • 8:19 - 8:22
    Kuna kitu cha ajabu na cha kuvutia
  • 8:22 - 8:25
    kuhusu namna shairi linavyoonekana.
  • 8:25 - 8:30
    Nafasi ya shairi ni muhimu
    kama maneno yenyewe.
  • 8:31 - 8:34
    Tunasoma shairi hili lililoandikwa na
    W.S.Merwin,
  • 8:34 - 8:38
    ambalo aliliandika baada ya kumuona
    mkewe akifanya kazi kwenye bustani
  • 8:38 - 8:42
    na akakumbuka kuwa wataishi maisha
    yao yote yaliyobaki wakiwa pamoja.
  • 8:43 - 8:46
    "Wacha nifikiri kuwa tutakuja tena
  • 8:46 - 8:49
    tutakapotaka na itakuwa wakati wa masika
  • 8:49 - 8:52
    hatutakuwa na umri mkubwa
    kuliko tulivyowahi kuwa
  • 8:52 - 8:56
    na majonzi yatakuwa mepesi kama
    mawingu ya mapema
  • 8:56 - 9:00
    ambayo kwayo asubuhi
    huja yenyewe taratibu"
  • 9:00 - 9:03
    Nikamuuliza Patrick mstari alioupenda
    zaidi ni upi, na akasema
  • 9:03 - 9:07
    "Hatutakuwa na umri mkubwa
    kuliko tulivyokuwa."
  • 9:08 - 9:13
    Alisema inamkumbusha
    mahali ambapo muda husimama,
  • 9:13 - 9:16
    pale ambapo muda haumaanishi
    kitu chochote.
  • 9:16 - 9:18
    Na nikamuuliza kama amewahi kuwa
    na mahali pa jinsi hiyo.
  • 9:18 - 9:20
    pale ambapo muda hudumu milele.
  • 9:20 - 9:22
    Na akasema, "Mama yangu".
  • 9:24 - 9:28
    Na pale unaposoma shairi
    pamoja na mtu mwingine,
  • 9:28 - 9:30
    shairi hubadilika katika maana.
  • 9:31 - 9:36
    Kwa sababu huwa la kibinafsi kwa mtu huyo,
    huwa la kibinafsi kwako.
  • 9:38 - 9:40
    Halafu tulisoma vitabu,
    tulisoma vitabu vingi sana,
  • 9:40 - 9:43
    tulisoma kumbukumbu za Frederick Douglass,
  • 9:43 - 9:47
    Mtumwa wa Marekani aliyejifunza mwenyewe
    kusoma na kuandika
  • 9:47 - 9:50
    na aliyetoroka na kuwa huru
    sababu ya kuelimika kwake.
  • 9:52 - 9:55
    Nimekua nikimfikiria Frederick Douglass
    kama shujaa
  • 9:55 - 9:58
    na niliiona hii simulizi kama
    iliyojaa matumaini na yenye kuinua
  • 9:59 - 10:02
    Lakini kitabu hiki kilimuweka Patrick
    katika hofu.
  • 10:03 - 10:08
    Alibakia katika simulizi aliyoielezea
    Douglass jinsi ambavyo, katika Christmas,
  • 10:08 - 10:11
    Mabwana waliwapa watumwa jini(pombe kali)
  • 10:11 - 10:15
    kama namna ya kuwaaminisha kuwa
    hawawezi kuumudu uhuru.
  • 10:15 - 10:17
    Kwa sababu watumwa waliweweseka
    katika mashamba.
  • 10:20 - 10:22
    Patrick alisema anajifananisha na hili.
  • 10:22 - 10:26
    Alisema kuwa kuna watu gerezani ambao,
    kama watumwa,
  • 10:26 - 10:28
    hawataki kuwaza juu ya hali zao,
  • 10:28 - 10:30
    kwa sababu inawaumiza sana.
  • 10:30 - 10:32
    Inaumiza sana kuwaza mambo ya nyuma,
  • 10:32 - 10:35
    inaumiza sana kuwaza
    kuhusu umbali gani tunapaswa kwenda.
  • 10:37 - 10:40
    Mstari alioupenda sana ulikuwa huu:
  • 10:40 - 10:43
    "Chochote kile, bila kujali chochote,
    kujiondoa katika kuwaza!
  • 10:44 - 10:49
    Ilikuwa ni huku kuwaza kusiko koma kuhusu
    hali yangu ndiko kunako kipa mateso."
  • 10:50 - 10:54
    Patrick alisema Douglass alikuwa jasiri
    kuandika, ili aendelee kuwaza.
  • 10:55 - 11:01
    Lakini Patrick hakufahamu kuwa alionekana
    kufanana sana na Douglass kwangu.
  • 11:01 - 11:04
    Namna alivyoendelea kusoma,
    ijapokuwa ilimuweka katika hofu.
  • 11:05 - 11:08
    Alimaliza kitabu kabla yangu,
  • 11:08 - 11:12
    akisoma katika ngazi za
    zege zisizo na taa.
  • 11:14 - 11:16
    Halafu tukaendelea kusoma mojawapo
    ya vitabu ninavyovipenda,
  • 11:16 - 11:19
    Cha Marilynne Robinson's "Gilead,"
  • 11:19 - 11:23
    ambayo ni barua endelevu kutoka
    kwa baba kwenda kwa mwanae.
  • 11:23 - 11:25
    Alipenda mstari huu:
  • 11:25 - 11:27
    "Ninaandika hii kwa sehemu kukuambia
  • 11:27 - 11:31
    ya kwamba kama umewahi kujiuliza
    kile umekifanya katika maisha yako...
  • 11:31 - 11:33
    umekuwa neema ya Mungu kwangu,
  • 11:33 - 11:36
    muujiza, kitu ambacho ni zaidi
    ya muujiza."
  • 11:37 - 11:43
    Kitu kimoja kuhusu hii lugha,
    upendo wake, subira yake, sauti yake,
  • 11:43 - 11:46
    iliamsha shauku ya Patrick katika kuandika.
  • 11:46 - 11:49
    Na alijaza daftari kwa daftari
  • 11:49 - 11:53
    na barua kwenda kwa binti yake.
  • 11:53 - 11:56
    katika barua hizi nzuri na imara,
  • 11:56 - 12:02
    alijiwazia yeye na binti yake
    wakipanda mtumbwi katika mto Mississipi
  • 12:02 - 12:05
    Alijiwazia yeye na binti yake
    wakipata vijito vya milimani
  • 12:05 - 12:07
    vikiwa na maji masafi bila kasoro.
  • 12:08 - 12:10
    Nilipomtazama Patrick akiandika,
  • 12:11 - 12:13
    Nilijiwazia mwenyewe,
  • 12:13 - 12:15
    na sasa ninawaulizeni nyote,
  • 12:16 - 12:21
    ni wangapi wenu mmewahi kuandika barua
    kwa mtu unayehisi umemwangusha?
  • 12:22 - 12:27
    Ni rahisi sana
    kuwaweka hao watu nje ya fikra zako.
  • 12:28 - 12:33
    Lakini Patrick alijitokeza kila siku,
    akimkabili binti yake,
  • 12:33 - 12:36
    akijiwajibisha kwake,
  • 12:36 - 12:39
    neno kwa neno kwa umakini wa hali ya juu.
  • 12:42 - 12:45
    Ningependa katika maisha yangu binafsi
  • 12:46 - 12:49
    kujiweka katika hatari kwa namna hiyo.
  • 12:49 - 12:53
    Kwa sababu hatari hiyo inadhihirisha
    nguvu za moyo wa mtu.
  • 12:57 - 13:01
    Ngoja nirudi hatua moja nyuma na niulize
    swali ambalo linaleta wasiwasi.
  • 13:01 - 13:04
    Mimi ni nani kusimulia simulizi hii,
    hii simulizi ya Patrick?
  • 13:06 - 13:09
    Patrick ndiye aliyeishi kwenye
    maumivu haya
  • 13:09 - 13:13
    na mimi sijawahi kukaa na njaa hata
    kwa siku moja kwenye maisha yangu
  • 13:15 - 13:17
    Ninawaza sana kuhusu swali hili,
  • 13:17 - 13:21
    lakini ninachotaka kusema ni kuwa hii
    simulizi sio tu kuhusu Patrick.
  • 13:21 - 13:22
    Inatuhusu sisi,
  • 13:22 - 13:25
    ni kuhusu tofauti kati yetu.
  • 13:26 - 13:27
    Ulimwengu wa vingi
  • 13:28 - 13:32
    ambao Patrick na wazazi wake
    na mababu zake
  • 13:32 - 13:34
    hawajawahi kuuona.
  • 13:34 - 13:37
    Katika simulizi hii, mimi ninawakilisha
    huo ulimwengu wa vingi.
  • 13:38 - 13:42
    Na katika kueleza simulizi hii
    sikutaka kujificha mwenyewe.
  • 13:42 - 13:44
    Kuficha nguvu ambazo ninazo.
  • 13:45 - 13:49
    Katika kueleza simulizi hii,
    ninataka kuifichua nguvu hiyo
  • 13:49 - 13:51
    halafu kuuliza,
  • 13:51 - 13:54
    tunawezaje kuipunguza
    umbali kati yetu?
  • 13:56 - 14:00
    Kusoma ni njia mojawapo ya kuipunguza
    hiyo nafasi.
  • 14:00 - 14:04
    Kunatuma ulimwengu wa ukimya
    ambao tunaweza kuushiriki pamoja,
  • 14:04 - 14:07
    ambao tunaweza kuushiriki kwa usawa.
  • 14:08 - 14:12
    Inawezekana unajiuliza sasa kuwa
    ni nini kilitokea kwa Patrick.
  • 14:12 - 14:13
    Je kusoma kuliokoa maisha yake?
  • 14:15 - 14:17
    Kuliyaokoa na hakukuyaokoa.
  • 14:18 - 14:21
    Patrick alipotoka gerezani,
  • 14:21 - 14:23
    safari yake ilikuwa ya maumivu.
  • 14:24 - 14:28
    Waajiri hawakumkubali kwa sababu
    ya historia yake,
  • 14:28 - 14:31
    rafiki yake mpenzi, mama yake,
    alifariki katika umri wa miaka 43
  • 14:31 - 14:33
    kwa ugonjwa wa moyo na kisukari.
  • 14:33 - 14:36
    Alikuwa hana pa kuishi,
    amekuwa hana chakula.
  • 14:38 - 14:43
    Kwa hiyo watu wanasema mengi kuhusu kusoma
    ambayo kwangu ninahisi wanazidisha chumvi.
  • 14:44 - 14:48
    Uwezo wa kusoma haukumzuia yeye
    asitengwe na jamii.
  • 14:48 - 14:50
    Hakukumzuia mama yake asifariki.
  • 14:52 - 14:54
    Kwa hiyo kusoma kunaweza kufanya nini?
  • 14:55 - 14:59
    Nina majibu machache ninapomalizia leo.
  • 15:01 - 15:03
    Kusoma kulibadili utu wake wa ndani
  • 15:05 - 15:08
    kwa mambo yaliyofichika na uwezo wa
    kuwaza kwa picha.
  • 15:08 - 15:09
    kwa uzuri.
  • 15:10 - 15:15
    Kusoma kulimpa taswira zilizompa furaha:
  • 15:15 - 15:21
    milima, bahari, kulungu, theluji.
  • 15:21 - 15:25
    Maneno yenye ladha ya ulimwengu huru
    na halisi.
  • 15:28 - 15:31
    Kusoma kulimpa lugha kwa yale aliyopoteza.
  • 15:31 - 15:36
    Ni jinsi gani yalivyo mazuri haya maneno
    kutoka kwa mshairi Derek Walcott?
  • 15:36 - 15:38
    Patrick alilikariri hili shairi.
  • 15:38 - 15:40
    "Siku ambazo nilizishikilia,
  • 15:40 - 15:42
    siku ambazo nilizipoteza,
  • 15:42 - 15:46
    siku ambazo zinakuwa kupitiliza,
    kama mabinti,
  • 15:46 - 15:48
    mikono yangu inayoshikilia."
  • 15:49 - 15:52
    Kusoma kulimfundisha ujasiri wake
    mwenyewe.
  • 15:52 - 15:55
    Kumbuka kwamba aliendelea kusoma
    Frederick Douglass,
  • 15:55 - 15:57
    ijapokuwa ilikuwa ya kuumiza.
  • 15:57 - 16:01
    Aliendelea kuwa makini,
    ijapokuwa kuwa makini kunauma.
  • 16:02 - 16:05
    Kusoma ni aina ya kutafakari,
  • 16:05 - 16:09
    ndio maana ni vigumu sana kusoma
    kwa sababu tunataka kutafakari.
  • 16:09 - 16:13
    Na Patrick alichagua kutafakari,
    badala ya kutokutafakari.
  • 16:16 - 16:20
    Na mwishoni, kusoma kulimpa lugha
    ya kuongea na binti yake.
  • 16:21 - 16:25
    Kusoma kulimpa shauku ya kutaka kuandika.
  • 16:25 - 16:29
    Muunganiko kati ya kusoma na
    kuandika ni wenye nguvu sana.
  • 16:29 - 16:31
    Tunapoanza kusoma,
  • 16:31 - 16:33
    tunaanza kupata maneno.
  • 16:34 - 16:39
    Na alipata maneno ya kutafakari
    wao wawili wakiwa pamoja.
  • 16:39 - 16:40
    Alipata maneno
  • 16:42 - 16:44
    ya kumwelezea ni namna gani anampenda.
  • 16:46 - 16:50
    Kusoma pia kulibadilisha
    mahusiano baina yetu.
  • 16:50 - 16:52
    Kunatupa nyakati za kuwa karibu,
  • 16:52 - 16:55
    kuweza kuona zaidi ya mitazamo yetu.
  • 16:55 - 16:58
    Na kusoma kulichukua mahusiano ya
    kutokuwa sawa
  • 16:58 - 17:00
    na kulitupa usawa wa muda mfupi.
  • 17:02 - 17:05
    Ukikutana na mtu kama msomaji,
  • 17:05 - 17:07
    unakutana naye kwa mara ya kwanza,
  • 17:07 - 17:09
    kwa upya kabisa.
  • 17:10 - 17:13
    Hakuna namna unaweza kufahamu mstari
    anaoupenda sana ni upi.
  • 17:14 - 17:18
    Ni kumbukumbu zipi na huzuni zipi za
    siri alizonazo.
  • 17:19 - 17:23
    Na unakutana na sitara ya hali ya juu
    ya utu wake wa ndani.
  • 17:24 - 17:27
    Na halafu unaanza kushangaa,
    "Eti,utu wangu wa ndani umejengwa na nini?
  • 17:27 - 17:30
    Ni kitu gani nilichonacho cha thamani
    cha kumshirikisha mwingine?"
  • 17:33 - 17:34
    Ninataka kufunga
  • 17:36 - 17:40
    kwa mistari yangu ninayoipenda
    kutoka kwa barua za Patrick kwa bintiye.
  • 17:41 - 17:44
    "Mto una kivuli kwenye baadhi ya maeneo
  • 17:44 - 17:47
    lakini mwanga unaangaza
    kupitia mianya ya miti...
  • 17:47 - 17:51
    Kwenye baadhi ya matawi
    muliberi nyingi zimening'inia.
  • 17:51 - 17:54
    Unanyoosha mkono wako
    ili uweze kuyachukua baadhi".
  • 17:56 - 17:58
    Na barua hii ya upendo, anapoandika,
  • 17:58 - 18:03
    "Fumba macho yako na usikilize
    sauti ya maneno.
  • 18:03 - 18:05
    Ninafahamu shairi hili kwa moyo
  • 18:05 - 18:08
    na ningependa pia wewe ulifahamu."
  • 18:09 - 18:11
    Ninawashukuruni nyote.
  • 18:11 - 18:14
    (Makofi)
Title:
Nguvu inayoponya katika kusoma
Speaker:
Michelle Kuo
Description:

Kusoma na kuandika vinaweza kuwa vitendo vya ujasiri vinavyotuleta karibu na watu wengine na karibu na nafsi zetu pia. Mwandishi Michelle Kuo anashirikisha namna ambavyo kufundisha stadi za kusoma kwa wanafunzi wake kule Mississippi Delta kulivyofunua nguvu ya daraja la maneno yaliyoandikwa-- pamoja na mipaka ya nguvu hiyo.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
18:27
Nelson Simfukwe approved Swahili subtitles for The healing power of reading
Nelson Simfukwe accepted Swahili subtitles for The healing power of reading
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for The healing power of reading
Miriam Loivotoki Elisha edited Swahili subtitles for The healing power of reading
Miriam Loivotoki Elisha edited Swahili subtitles for The healing power of reading
Miriam Loivotoki Elisha edited Swahili subtitles for The healing power of reading
Miriam Loivotoki Elisha edited Swahili subtitles for The healing power of reading
Miriam Loivotoki Elisha edited Swahili subtitles for The healing power of reading
Show all

Swahili subtitles

Revisions